ATCL shusheni bei ili mtengeneze soko kubwa la ndani, kwa namna hii mtapata faida. Kumbukeni the higher the price...

Mkuu hapo umenena hawa jamaa walewa sifa kwa kuwa hawana mshindani na hapo ndio tunakumbuka air daladala yetu Fastjet ambayo ilituwezesha wazazi wetu vikongwe kuwapandisha ndege kwenda Muhimbili kutibiwa hadi mbeki 3 pia tuliwapandisha FJ kwa nauli ya laki moja sasa hawa wanataka kupata faida asilimia 100, naamini bila ya mwendazake hili shirika litakuwa ICU kama hawajabadili hizo nauli,weka nauli nafuu sababu hii ni budget airline ujaze hata mbuzi kwenye cabin, ndio maana akina Lusinde Kibajaji,Musukuma wanawadharau hawa wasomi wetu,wanashindwa kufikiri na kuangalia mazingira.
 
Tatizo moja kubwa ninaloliona ATCL ni kushindwa kutumia opportunity za kwenye CARGO. Wangeweza kuuza cargo space kuleta nyama kutoka Mwanza au Arusha kwa ngombe/mbuzi waliokuwa washachinjwa tayari na kufika Dar saa 7 au 8 usiku (1am or 2am). Na wafanye hivyo kwa bidhaa nyengime pia zenye bei kama vile Garlic kuna wakati inafika 7000/kg kwa sababu ya uhaba wa logistic, hata samaki kama Sato na Sangara. Wangeweza.kugenerate 20,000 kwenye cargo per trip kwa ndege kubwa.
 
Kwani sasa hivi wanazo ngapi mkuu? Kuna muda zinafika hadi tano. Ungefanya kautafiti kidogo kabla ya kuleta uzi.
Tano? Acha upuuzi. Kupata tatu kwa siku nadra, sisi tunataka kila siku ndege ijae na tripu ziwe zaidi ya nne. Huo nimekuwekea mfano tu
 
Tano? Acha upuuzi. Kupata tatu kwa siku nadra, sisi tunataka kila siku ndege ijae na tripu ziwe zaidi ya nne. Huo nimekuwekea mfano tu
Hatutaki mfano ila uhalisia, ninakupa facts. Shida unaongea kwa hisia. Fanya utafiti hata kidogo.

Kesho tarehe 19.04.2021
Mwanza - Dar es Salaam Air Tanzania wana ndege tano.

Source:
 
Umekariri madesa unatuletea mchanganyiko hapa. Nani kakwambia usafiri wa ndege ni luxury?
Mbona fastjet alikuwa anajaza ndege siku 2 kabla wakati precision yeye zake zilikuwa hazijai mapema?
Hitaji la mtu ni kusafiri kutoka point A kwenda B. Gharama kubwa zinafanya achague kuchelewa kwa bus ili aepuke gharama kubwa za ndege
 
Ila mfano wako haukuwa Sawa kuutumia kwenye mada tajwa mfano wa chumvi na bei ya nauli ya ndege wapinawapi
 
Kwani sasa hivi wanazo ngapi mkuu? Kuna muda zinafika hadi tano. Ungefanya kautafiti kidogo kabla ya kuleta uzi.
Tano? Acha upuuzi. Kupata tatu kwa siku nadra, sisi tunataka kila siku ndege ijae na tripu ziwe zaidi ya nne. Huo nimekuwekea mfano tu
 
Nyankurungu2020 unajifanyaga kipanga, huyu amekukomesha na ukanjanja wako wa kisimbe. Rudi shule
 
nenda kwenye tovuti yao ipo... andika vitu ambavyo una uhakika navyo.
Ahaaa, nafikiri hukuelewa ninacho maanisha. Kaa kimya kama hujui. Mpaka sasa wanahudumia watu 60000 kwa mwezi ni soko dogo sana kwa hapa Tanzania. Hivyo panua ubongo wako uweze kuelewa.
 
Ahaaa, nafikiri hukuelewa ninacho maanisha. Kaa kimya kama hujui. Mpaka sasa wanahudumia watu 60000 kwa mwezi ni soko dogo sana kwa hapa Tanzania. Hivyo panua ubongo wako uweze kuelewa.
Umeandika usichokijua. Unajiaibisha.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…