Mathayo Fungo
JF-Expert Member
- Nov 13, 2018
- 319
- 511
Nimekutana nayo hii mwananchi eti! Mpaka nimeshangaaaManeno ya Diamond mwenyewe
"
- Naomba nisisitize kuwa Siku ya jana tareh 16 | 12 Mimi Nasibu Abdul Juma Issaack, na nilokuwa Nasafiri nao Tokea Mwanza Sikuchelewa ndege Kabisa..Nilifika Muda Sawia kama Usafiri wa ndege za ndani unavyotaka, na kulidhihirisha hilo.. nikiwa niko pale kuna hata Abiria wengine waliingia nusu saa baadae, tena nikiwepo nimesimama palepale... na mmoja ya watu waloingia nikiwepo nimesimama ni @Harmonize_tz ... kilichotokea ni kuwa Mmoja ya watu wenye dhamana pale, siti zetu aliziuza kwa abilia wa fastjet...kwa Abiria watalii wazungu, na Walichokuwa hawajajua pia waliwauzia na baadhi ya Watu ambao ni wafanyakazi wetu wa Wasafi Media...Na Kuthibitisha tena kuwa hatukuchelewa, alikuja tena Mtu wa Air Tanzania na Kutuambia kuwa Siti zimebaki Mbili...Hivyo Tuchague watu wawili tu wasafiri.... kama kweli tulichelewa, sasa Hao wawili, sasa wangewezaje ingia??? tukasema hatuwezi safiri wawili lazima tuwe wote kama tulivyokata... hivyo ni dhahiri kuwa hatukuchelewa....ila kutokana na Ndege nyingi za kuja mwanza zilicancel Trip zao, ikiwepo Fastjet hivyo Tickets zikawa ni Dili sana na ndio yote kutokea....
USHAURI tu kwa Ndugu zetu walopewa dhamana ya Kuliendesha shirika letu la Air Tanzania....tutambue kuwa Mh Rais, Pamoja na Serikali nzima kwa Ujumla imepambana Usiku na Mchana, imeamua kujinyima na kujitoa kwa hali na mali ili kuhakikisha Watanzania nasi tunakuwa na Ndege zetu, kwa kuamini kuwa Licha tu ya kuingiza kipato, lakini Uwepo wa Air Tanzania ni Heshima na fahari kwenye nchi Yetu....Hivyo tunaomba Mzisimamie Vizuri....na nikiwa kama Mtanzania Mzalendo Mwenye akili Timamu, siwezi tu kukurupuka kusema jambo kwani ni jukumu langu kuhakikisha nalilinda shirika
hili, nalitangaza na kuwasifia wanapopatia lakini pia ni jukumu langu kuwaambia Mnapokosea ili mfanye marekebisho na AirTanzania kuwa shirika bora Duniani na kuipa sifa Nchi yetu... hivyo nikiwa kama Mtanzania mwenye uchungu siwezi kuona mtu alopewa dhamana ya Kuzisimamia ndege hizo anafanya vitu tofauti halaf eti nikakaa kimya...Ni sawa na Kumvunja moyo Mh Raisi na Serikali nzima kwa juhudi zake hizi... hivyo Mlopewa Dhamana tunaomba Muwe Makini, na kusimamia vyema ili tusitie doa kwenye ndege zetu.."
.
Nasubiria kauli ya AirTanzania .
Sitoshangaa kama wiki itaisha bila Mkurugenzi wa ATCL kutenguliwa maana uenda huu mchezo anaujua! Haiwezekani watu wanalalamika namna hii dizaini kama wakisubiri nani aanze tu! alafu hapohapo Mkurugenzi amemjibu Mond kuwa kachelewa wakati mwenyewe kaeleza kuwa walikutwa siti zimeuzwa na zimebaki 2
- lemutuz_superbrand
LIVE HARD TALK: Naomba kutoa mchango wangu kuhusu you guys Shirika la Ndege Air Tanzania ...YOU ARE HORRIBLE and SUPER NIGHTMARE ...mambo mnayoyafanya ni Aibu tupu I mean Jumamosi nimeruka na ndege yenu Drimlaina to Mwanza na nimerudi nayo jana Usiku ...Rais Magufuli kwa nia njema kabisa kainunulia Taifa hii ndege ili isaidie kumaliza tatizo la Usafiri ...Ndege ni Kubwa nzuri na Safi lakini tatizo nyingi handlers aidha hamna uzoefu au ni WAZEMBE WA AJABU SANA ....Marubani wapo vizuri na kukata tiketi hapa Dar hakuna tatizo ....Tatizo linaanzia Uwanja wa Ndege Dar kwenye kusafiri hakuna mpangilio mizuri yaani kuanzia mistari ya ku Check in ni kama unapanda Dala dala yaani kweli mnashindwa hata kuwapanga Abiria kistaarabu kama mashirika mengine? ...hapo mpo jirani na Emirates hamuwaoni wao wanayoyafanya? ....kuanzia Check in ni usumbufu mtupu Joto watoto wanalia hakuna Air Conditons Abiria 262 mnagombea ku Check in bila utaratibu maalum ...sasa ukifika juu ndio kabisa Tangazo linasema sasa ndege ipo tayari kuondoka boom abiria wote 262 mnaanza kugombea kuingia kupitia kamlango kadogo sana Kina Mama wenye watoto, Vilema, Wazee, kama daladala ....ok mashirika yote ya ndege Duniani watu wa Business na First Class wanaingia kwa mpango tofauti lakini sio hii ndege yaani jana na juzi niliona Wazungu Watalii wanavyolalamika ...jana tulipokuwa tunatoka Mwanza tukaambiwa abiria wote ni lazima tupitie Mlango mmoja wa Nyuma Horrible halafu ndege ndani Chafu tayari hata usafi unawapa taabu ....na hata mkiwauliza Crew wenu jana niliwapa maneno mazito sana kuhusu huu uzembe wa ajabu sana ...Rais alisema anataka Watalii watumie ndege zetu naomba niwaambie kwa hizo tabia zenu Watalii watakodi magari hata mimi nikiwa Mtalii siwezi nikarudia kupitia bughudha kama zile za Jana na Juzi ....Juhudi zote za Mheshimiwa Rais mnazivuruga kwa Uzembe tu hakuna lolote ni INCOMPETENCE na UZEMBE ....ni Wakati muafaka Rais akawaondoa wote au mrudi kwenye Training ...ok guys NIMEANDIKA NILIYOYAONA KWA MACHO YANGU so ambayo sijayaandika SIKUYAONA! ...MUNGU AIBARIKI TANZANIA! AMEN! - @lemutuz_superbrand
WAFANYAKAZI WA ATCL NA TEAM KIBA TULIZENI VISHUNDU KWANZA SERIKALI IPO KWENYE UCHUNGUZIHuyo dogo anatoa wapi uthubutu wa kulichafua shirika letu la ndege kwa uzembe wake mwenyewe wa kuchelewa mda?!
Kuna nani nyuma yake hadi anakuwa na UTHUBUTU WA KIWANGO KILE KULITUHUMU /KULICHAFUA SHIRIKA ILHALI POPOTE DUNIANI MTU ANAYE CHELEWA NDEGE huwa haimusubiri?!
Huyo dogo/jipu lileeni tu.Ipo siku kwa PAPARA zale na MAJIVUNO yake atakuja kuichafua zaidi nchi kwa matamanio ya KIJINGA!
Kwa kitendo kile SHIRIKA LA NDEGE WAMPELEKE MAHAKAMANI HARAKA KWA KULICHAFUA SHIRIKA KWA UZEMBE WAKE!
Ficha ujinga wako na nimekustahi kwa mda!WAFANYAKAZI WA ATCL NA TEAM KIBA TULIZENI VISHUNDU KWANZA SERIKALI IPO KWENYE UCHUNGUZI
NI LAZIMA MSHIKISHWE ADABU, MMESHAZOEA KUFANYA KAZI KWA MAZOEA SAFARI HII MTAISOMA NAMBA
Na wewe unakera na mpira kwenye thread za watu. Fungua thread yako special ndo uweke haya mambo maana kama ni issue za mpira trust me watu hapa tupo vizuri na latest news, huhitaji kutukumbushia.Droo kamili:
Manchester United v PSG
Schalke v Manchester City
Atletico Madrid v Juventus
Tottenham v Borussia Dortmund
Lyon v Barcelona
Roma v Porto
Ajax v Real Madrid
Liverpool v Bayern Munich
Mechi za kwanza zitachezwa 12-13 na 19-20 Februari, na mechi za marudiano 5-6 na 12-13 Machi, 2019.
nguvu ya mtandao vs brand boss!!Hivi hili suala ATCL wangeamua kukaa kimya wangepata tabu gani? Kuzingua wamezingua ila naona kama wamelipa uzito saaaana kupitiliza katika harakati za kujisafisha. . . .hadi tuite press aiseee. Basi sawa
Mbona huyo wa Mwanza 2014 alihamishiwa Arusha airport.Hii ishu sio ya ATCL. Ni ya Airport ya Mwanza. Niliwahi kufika pale dk 40 kabla ndege kuondoka, ikabidi nitoe rushwa ya elfu 10 ili niruhusiwe kuingia. Hii ilikuwa mwaka 2014.
Huu ni mchezo wa muda mrefu.
Mamlaka ya viwanja vya ndege inabidi imuondoe bosi wa uwanja wa Mwanza, atupwe airport ya Singida huko kwa kushindwa kudhibiti uozo huu.
Narudia tena. Wenye makosa wanaweza wasiwe ATCL bali mamlaka ya uwanja wa Mza.
Msanii wenu mshamba tu kwani hajui muda wa kufika airport. Local flight unatakiwa saa moja kabla ya kuruka. International flights ni masaa 2 kabla. Yeye anadhani muda huu umewekwa na wasanii wen zake. Na safari zote za nje hajaelimika tu. Kweli mtu wa Mbagala huyu.Yaa kumbuka huyu ni msanii nje ya kwamba ni mwananchi kama wengne but fikiria kama alikuwa anaenda kuperforrm mkoa mmja impact yake ingekuwaje nk
Kuna jukwaa la sports, walioliweka sio kwamba hawakuwa na akli timamu...unatia waswas uwezo wako wa akli kwa kuleta taarifa sahihi kwnye jukwaa lisilo sahihi na thread isiyo sahihi.....Droo kamili:
Manchester United v PSG
Schalke v Manchester City
Atletico Madrid v Juventus
Tottenham v Borussia Dortmund
Lyon v Barcelona
Roma v Porto
Ajax v Real Madrid
Liverpool v Bayern Munich
Mechi za kwanza zitachezwa 12-13 na 19-20 Februari, na mechi za marudiano 5-6 na 12-13 Machi, 2019.
Unamuombea uhamisho mama wa watu jamaniHii ishu sio ya ATCL. Ni ya Airport ya Mwanza. Niliwahi kufika pale dk 40 kabla ndege kuondoka, ikabidi nitoe rushwa ya elfu 10 ili niruhusiwe kuingia. Hii ilikuwa mwaka 2014.
Huu ni mchezo wa muda mrefu.
Mamlaka ya viwanja vya ndege inabidi imuondoe bosi wa uwanja wa Mwanza, atupwe airport ya Singida huko kwa kushindwa kudhibiti uozo huu.
Narudia tena. Wenye makosa wanaweza wasiwe ATCL bali mamlaka ya uwanja wa Mza.