Atheists wana mtindio wa ubongo

Mungu hajatoa hiyo idhini na hakuna hukumu aliyotoa.
Lakini si ndiye aliyeumba ulimwengu huu wenye matetemeko ambayo yanaua hadi watoto wasio na hatia?

Ye hakuliona hilo kuwa litaweza kutokea?

Kwakua ni mjuzi wote na akaliona, kwanini hakulizuia?

Kama aliliona na hakulizuia akaliacha litokee, utasemaje hakutoa idhini?
 
Wameonewa na nani na kwa nini?
Na Mungu ambaye ameumba ulimwengu wenye matetemeko ambayo umedai yanaua watu kwa makosa ya ujenzi mbovu

Kwasababu yeye ni mwema muda wote, kwanini aruhusu watoto wadogo wasio na hatia wafe kikatili kwenye jambo ambalo hawahusiki nalo?
 
Mpaka sasa hakuna aliyethibitisha Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote yupo.

Kwa sababu Mungu huyo hayupo.

Kama unabisha, thibitisha Mungu huyo yupo.
 
Ni kama mtu akuulize ni nani alianzisha lugha ya kiingereza? Si rahisi kumjua ila utajua ni wapi lugha ili anzia..
Lugha ni tofauti na suala la dini kijana, jifunze kutofautisha vitu. Lugha haianzishwi bali ni umbile ambalo mwanadamu amumbwa nalo. Ndiyo maana lugha ni katika vitu vilivyo umbwa na Allah.
 
Shida husomi, hizo Zina watu wake na waasisi wake, hakuna dini ambayo haina muasisi kijana.

Wasomo wameandika vitabu kibao kuhusu hizo dini na waasisi wake.
 
Njaa unaweza kuthibitisha. Unaweza kujua imetokana na nn na namna ya kuizuia. Maumivu nayo ivoivo.... na Mungu?

Sent using Jamii Forums mobile app
Maana yake kuwepo kwa kitu Fulani si lazima ukione, Bali zipo ishara za kuonyesha ya kuwa kitu hicho kipo.

Hata Leo wewe unaamini uwepo lakini, nacho ni kitu hiki, lakini huioni ila Kuna ishara zinazo onyesha uwepo wa akili.

Swali langu la msingi ni kuwa kwako wewe uthibitisho una sifa gani ili uitwe uthibitisho. Nakuuliza tena sababu umeonyesha una ufahamu mdogo sana juu ya kitu na uthibitisho.
 
Ulimwengu hauna mabaya na wala hauruhusu mabaya. Ubaya unao binadamu kwa kutumia akili zake vibaya.

Mungu alikupa akili za kutosha ili zitumike vizuri kuwiana na mazingira yetu. Akili ni kila kitu.

Ukitumia akili vizuri, hautathirika na jambo lolote lile unaloliita baya.
 
Lugha ni tofauti na suala la dini kijana, jifunze kutofautisha vitu. Lugha haianzishwi bali ni umbile ambalo mwanadamu amumbwa nalo. Ndiyo maana lugha ni katika vitu vilivyo umbwa na Allah.
Duh...
Unabishia ukweli yani. Ukisoma mada ya huu uzi afu ukiangalia na participants, ni kinyume chake

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama ulimwengu hauruhusu mabaya, kivipi katika ulimwengu usioruhusu mabaya iwezekane binadamu kufanya mabaya kutumia akili zake?
 
Nimejibu hapo; inategemea unathibitisha nn
Vitu visivyo onekana tunaweza vithibitisha kwa kuvipima. Sasa ukimuuliza muamini athibitishe kuhusu mungu wake kua yupo anaanza kukupa mistari kutoka kwenye kitabu. Yani huo ndio uthibitisho pekee! [emoji2365]

Afu mbaya zaidi nyie waamini wenyew mnapingana kuhusu mungu wa nani ni wa kweli...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Lugha ni tofauti na suala la dini kijana, jifunze kutofautisha vitu. Lugha haianzishwi bali ni umbile ambalo mwanadamu amumbwa nalo. Ndiyo maana lugha ni katika vitu vilivyo umbwa na Allah.
Pia allah kama anatengeneza lugha tungekua hatuna haja ya kujifunza. Tungezaliwa tunaijua basi. Ila mbona lugha zimezid kuongezeka huku nyingine zikipotea?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama ulimwengu hauruhusu mabaya, kivipi katika ulimwengu usioruhusu mabaya iwezekane binadamu kufanya mabaya kutumia akili zake?
Mabaya yanafanyika kwa sababu ya matumizi mabaya ya akili zetu. Tungetumia vizuri, tusingepata mabaya.

Ulimwengu haudhibiti akili za binadamu. Kwa hiyo hauwezi kuingilia kati matendo yetu.

Ulimwengu hauhitaji maarifa ya kuishi na binadamu, bali binadamu tunahitaji kutumia akili ya kuishi katika ulimwengu huu.
 
Unaelewa kwamba ulimwengu ungekuwa hauruhusu mabaya, isingewezekana kwa namna yeyote ile akili ya mtu kufanya mabaya?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…