Maximo anatakiwa kuwatambua wadau wa soka na kuhakikisha maslahi ya wadau yanatimia, sasa wachezaji ni wadau na wana maslahi pia cocher ni zaidi ya mwalimu sasa Maximo ana behave kama mwalimu wakati anapewa vinaja awacoach.
Si sahihi kusema mafanikio ya stars yanaletwa na Maximo, yeye ni mdau mmoja wapo katika kundi la wadau na hakubali na lawama pia. huyo Jk aliyemleta analaumiwa kila kukicha ndio itakuwa Maximo bwana, amebwagwa Big Phil wakati timu ni ya Tatu katika msimamo. Lakini wabongo tunaambiwa tulidhike na kufungwa, kudroo na kushinda game moja hata kama tuna mtazamo tofauti hii haipo mpira unanoga kama kuna wanao pinga, sio siasa kusema ndio mzee kila siku.
Kwa mazingira ya sasa Tanzania inastahili kuwa mbali zaidi ya ilipo, hata ushindi wenyewe sio predictable kama zilivyo timu za wenzetu. Ukilinganisha na majirani zetu sisi ndio tumewekeza zaidi katika timu ya taifa na hata ligi kuu, tunawazidi hata kenya katika matumizi wakati uchumi wetu ni mdogo lakini kiwango chetu ndio cha chini. tukisema mnalinganisha na miaka 18 iliyopita tena mnafunika hata historia kwamba mashindano yale ya mwaka 1982 ilikuwa CHAN ya ukweli sio hii ya wachezaji wa ndani.
Lakini mnakuwa wakali mkiambiwa bongo bado, si tunaona wakicheza sifa hazikutosha kutupeleka nusu fainali na Afrika mashariki ndio tumechezea kichapo hata cha wasomali. Pesa inayoenda stars ni nyingi kuliko kinachopatikana huko, uliza hata zambia wametumia ngapi ndio mjue Tanzania wanapiga hela na kugombana. Kama bangi wachezaji wengi wa kibongo wanakula jani na sio kigezo cha mwalimu kuchuniana na wachezaji kama vipi si awafukuze yeye si ndio kawaita anaogopa nini sasa.