Awamu ya 4 wafugaji (mostly wasukuma) waliondolewa bonde la Usangu na kupelekwa Lindi. Kwanini iwe nongwa kwa wamasai wa Loliondo?

Sexless

JF-Expert Member
Joined
Mar 11, 2017
Posts
23,683
Reaction score
55,898
Kuna kelele nyingi sana kufuatia dhamira njema ya serikali ya kuwaondoa wamasai kwenye pori tengefu la Loliondo.

Kwanini wamasai wa Loliondo wanataka wawe na special treatment nchi hii?

Awamu ya 4 iliwaondoa wafugaji maeneo ya bonde la Usangu, Ihefu, na Ujiji lkn hakuna aliyepiga kelele. Why??
 
..Wamaasai kwa maelfu ya miaka wamekuwa wakiishi na wanyama huko Ngorongoro na serikali ndiyo iliyowafuata na kuamua kuanzisha hifadhi ya wanyama.

..Wasukuma wao walitoka makwao Usukumani na kwenda kuvamia bonde la Usangu, Ihefu, wakiwa na mifugo, na sio wenyeji wa eneo hilo.

..Kinachotakiwa kufanya ni kutoa ELIMU kwa Wamaasai ili wakubali kuhama na kwenda maeneo mengine na kutoa nafasi kwa serikali kutumia eneo lao kwa ajili ya utalii.
 
Ngorongoro kuna NGOs zaidi ya elfu ajira zao zikitegemea wamasai. NGOs zingine makao makuu yakiwa Arusha. Wanakula kuku kwa mrija Arusha, Loliondo wanaenda tu kazini kupiga piga za wanyonge ili ripoti ziende kwa donors zikionesha hali ngumu ya wenyeji.

Wamasai wakiondolewa hizo NGOs zitakula wapi? Mbunge wa Ngorongoro atawakilisha nini? Wakenya watafugia wapi ng'ombe zao kwa kisingizio cha Masai hana border? Zaidi Wakenya wanategemea Loliondo kama chanzo cha nyama nzuri ambayo pamoja matumizi ya ndani ya nchi yao lakini pia husafirisha nje ya Kenya kama Kenyan product.

Ngorongoro mambo yameingiliana sana, kelele zote unazosikia ni maslahi binafsi wala si huduma kwa wamasai.
Wamasai wahamishwe mara moja kukata mirija ya Wakenya. Ni ujinga nchi kutumiwa vibaya na Kenyan petty bourgeoisis Na Kwa madharau hao hao Wakenya wamekimbilia mahakamani kuweka pingamizi. Worse enough mahakama walizoenda Jaji anaitwa Nyachae, mkenya mwenzao. Kweli? Hapana, inatosha sasa.
 
Wewe umeongea UHALISIA ULIVYO.

Ukiachana na sisi MASHABIKI wa ONLINE, WANAHARAKATI na WANASIASA UCHWARA ambao siku zoye husimama na aliye tofauti na SERIKALI.

Pale WAPIGA KELELE wengi ULAJI wao UKO HAPO.
 
sababu za kuwaondoa wasukuma na wamasai zinafanana?
au umesimuliwa tu hujui sababu ya wasukuma kuondolewa sangu?
sangu ni chanzo cha maji ya mto ruaha ambayo inaingiza maji mtera/kidatu uwepo wao ktk chanzo cha maji ulifanya mto ruaha ukakauka na ikatishia kilimo cha mpunga pia.
 
Wewe umeongea UHALISIA ULIVYO.

Ukiachana na sisi MASHABIKI wa ONLINE, WANAHARAKATI na WANASIASA UCHWARA ambao siku zoye husimama na aliye tofauti na SERIKALI.

Pale WAPIGA KELELE wengi ULAJI wao UKO HAPO.
Wacha Serikali iende polepole, Wakenya watakaa tu. Wasituchezee pamoja na wanaharakati uchwara.
 
Walipohamishwa wasukumwa hapakuwa na kelele eneo hilo anataka kupewa mjomba, kwanini Loliondo na Ngorongoro kelele za kuwahamisha wamasai huibuka tu pale waswahili wa Pwani wanapoingia ikulu?
 
sexless hivi unajua wamasai ni sehemu ya ecology ya mbugani
 
Tena hawa wanabembelezwa sana sijui kwa nini
Najua ilitakiwa wote wawe treated same ila wale wa mapori ya Kaliuwa huko kuna wengine mmh pole yao
Wengine waliondolewa sehemu nyingi kwa mtutu na kuitwa wavamizi ila walifuta machozi na maisha yakaendelea

Leo tunaona hawa nguvu inayowekwa eti mpaka kushtaki kwa waume zao wazungu

Ila wale waliokuwa wanaonewa na kupigwa awamu ile Hakuna aliethubutu kubinua mdomo
 
na wai ni nation park hawatakiwi kuhama..
 
Kwa kuongeza sio wasukuma tu waliohamishwa, Kuna kata ya msangaji yote ilihamishwa na vijiji vyake, vijiji vya nje ya msangaji Ikoga walihamishwa. Kwahiyo sio wasukuma tu Kuna wasangu maelfu walihamishwa mwaka 2007-2009
 
Sasa kama ishu ni kuishi miaka mingi mahali ndio hoja, itakuwa hoja dhaifu sana
Yaani kama kuna kitu kina maslahi ya taifa kipo hatarani watu wasiondolewe kisa wameishi hapo muda mrefu

Watu wamehamishwa kupisha miradi ya migodi, gesi barabara, bandari n.k na walikuwa muda mrefu hayo maeneo
 
Tanzania halina mwenye kwao
 
Ficha umbumbu wako pori tengefu la Loliondo Kuna vyanzo vya maji na mito ni vijito vinyoenda Serengeti na Ngorongo na mazilia ya Nyumbu wanaohama hama kati ya Kenya na Tz
Utalii unaingiza fedha nyingi za kigeni kuliko mpunga wa Ihefu
 
Utawasikia wakenya wanasema Tanzania shamba la bibi,imekula kwao sasa
 

..sisemi wasihamishwe.

..napendekeza waelimishwe na kushawishiwa kuhama.

..naona kama serikali imekurupuka na ndio maana kuna mzozo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…