Awamu ya Tano iliua UDART, hili tuliseme wazi si kumung'unya maneno

Huwezi kumtoa mwekezaji na kuvunja mkataba kama huna vigezo. Mwisho wa siku serikali itashitakiwa na kumlipa fidia mwekezaji kitu ambacho ni hasara kwa mlipa kodi. Dawa ni kumbana mwekezaji atimize wajibu wake, kama akishindwa ndio unapata sababu ya kuufuta mkataba.
 
Kumbe kuna watu walikuwa wanaomba jamaa atawale milele ili waendelee kupiga pesa
 
Haya mkuu nimekuelewa
 
Kutokana na mahesabu ya mradi UDART za 2013, gharama ya tiketi ya Mbezi- Kivukoni - Mbezi (round trip) ilipaswa kuwa Tsh 3,000 au Tsh 1,500 kwa safari ya kwenda tu.

Hiyo ndiyo bei inayoweza kulipa ghharama za uwekezaji, gharama za uendeshaji na riba za Benki.

Mradi ulipoanza ulianza kwa Serikali kuingiza Siasa ndipo UDART wakaambiwa wa charge Tsh 1,300 kwa round trip au Tsh 650/= kwa trip ya kwenda tu.

Gharama kubwa sana ya kuendesha UDART iko kwenye Workshop (Karakana). Karakana siyo revenue centre kama yalivyo mabasi, instead yenyewe ni cost centre. Inakula tu na haizalishi.

Hiyo tofauti ya Tsh 3,000 ya kwenye upembuzi yakinifu na ile Tsh 1,300 ya Serikali ambayo imelazimisha ni Tsh 1,700.
Kwa hiyo kila abiria wa Mwendokasi anakokwenda Kariakoo na kurudi anatengeneza hasara ya Tsh 1,700.
Na hapo ndipo inaonekana mradi hauwezi kugomboa magari 70 ambayo yako TPA kuanzia mwaka 2019 yakisubiri yasamehewe Custom duty na Excise tax. Vile vile ndiyo chanzo cha kushindwa kununua magari mapya.

TUSITAFUTE MCHAWI, SERIKALI NDIYO CHANZO CHA KUDORORA KWA UDART
 
wezi waliiba hata kwa nyerere

ngozi laana hii, wallahi Tarrahi
Kwakweli inafikirisha sana. Jinsi Magufuli alivyojipambanua kulinda mali za umma akateua wazalendo kila mahali na sasa haya ndio matokeo kila mradi. Hii ngozi kweli imelaaniwa.
 
Mungu katuokoa sana.
 
Hayati aliamini yeye anaweza kila kitu. Hata hii miradi alikuwa anasimamia kutokea Ikulu. Matokeo yake ndio haya katuachia majanga kila mahala.

Sasa kama mimi waziri nipo rais anaruka anaenda kukagua vitu ambavyo vipo chini yangu bila hata kunishirikisha si mwisho naacha tu afuatilie yeye mwenyewe kila kitu.
 
Wivu tu waliona vijana wa kitanzania wanapata sana. Sasa tiketi zinakatwa kutokea nyumbani kama zile za pantoni za wakati ule.
 
Mkuu unadandia treni kwa mbele, hujui post imetoka wapi.
 
Mkuu unadandia treni kwa mbele, hujui post imetoka wapi.
Hizi ni page chache sana kwa ufahamu wangu. Najua sana, na naweza kutabiri thinking yako. Tungekuwa tunaonana usoni, ningeweza ku-judge hata intelligence yako. Mammals' instinct!
 
Hizi ni page chache sana kwa ufahamu wangu. Najua sana, na naweza kutabiri thinking yako. Tungekuwa tunaonana usoni, ningeweza ku-judge hata intelligence yako. Mammals' instinct!
Okay genius
 
Mkuu mtu aliyeweza kuwekeza hata laki moja na akafanya biashara kwa faida, anakuzidi kiakili kwa mbali sana hata kama una PhD.
Mfanyabiashara anafikiria ALL scenarios to make money.
Nyie watu wa kunyoosha mkono kila mwisho wa mwezi mna mataizo sana.

Tatizo kubwa ni kufikiri kuwa mfanyabiashara yupo hapo ili nyie mliokaa vitini mle na kuota vitambi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…