Awamu ya Tano iliua UDART, hili tuliseme wazi si kumung'unya maneno

Awamu ya Tano iliua UDART, hili tuliseme wazi si kumung'unya maneno

Haha, uzi wako ulikuwa sio wa kuongelea matatizo ya mwendo kasi ila ni kunyoosha vidole utawala wa awamu ya tano.

Kama mwekezaji alikuwa anajuwa kigezo chake ni faida, kwanini alitaka kwenda kinyume na mkataba kwa kupandisha nauli wakati hakuna viashiria vyovyote vilivyo support upandishaji wa nauli? Bei ya mafuta ilikuwa ile ile, thamani ya shilingi haikubadilika sana, mfumuko wa bei ulikuwa unazidi kushuka, maishahara haikupanda. Kama sio ulafi na ubinafsi ni nini?
Inaonekana huna hata ABC ya biashara. Unafahamu aliwekeza kiasi gani? Profit margin projections ilikuwa kiasi gani? Na alipoanza kuuendesha mradi, kulikuwa na tofauti gani kati ya projections na mapato halisi?

Unapotaka kuanzisha mradi, kuna projections za gharama za uwekezaji, uendeshaji na mapato. Mradi ukianza, unakutana na uhalisia. Yawezekana kwenye uhalisia, gharama halisi za uendeshaji na mapato halisi ya biashara, vikawa na tofauti kubwa na projections. Lazima ufanye review. Na kwenye review, kuna items ambazo utakuwa huna uwezo wa kuzibadili, kama vile bei ya mafuta, kodi, bei za vipuli, n.k. Hivyo unabakia na maeneo machache sana ya kufanyia marekebisho, zaidi ni kwenye nauli.

Huwezi kusema hakukuwa na mabadiliko ya gharama wakati hujui kama toka mwanzo alikuwa anaendesha kwa faida au hasara.
 
Lakini si ni kampuni binafsi ndio ilikuwa na mamlaka ya kuendesha UDART kulingana na makubaliano ya mkataba? Sasa taasisi ya rais itaingiliaje uendeshaji bila ya kuwa na sababu za msingi? Serikali inatakiwa kuingilia pale tu inapoonekana kampuni inaendeshwa shughuli zake kinyume na makubaliano.
Hiyo unayoisema huwa ipo kama Serikali ikiwa inaongozwa na wenye busara.

Lakini mkipata kiongozi asiye na busara, nani ana msuli wa kuizuia serikali inachotaka kufanya, hata kama ni kuvuruga na kufuta mkataba wenyewe?
 
You must be crazy and misinformed! Usijiandikie tu! Haya ndo yanayochotwa na wabunge na baadhi ya wana JF wasiokuwa na uelewa na kuwapotosha.
Hapakuwa na mwekezaji mwenye mtaji bali mtu tapeli na mwizi. Serikali ilidai hisa zake na zile za jiji. Iliidai UDA yake iliyochotwa kitapeli, sasa ulitaka aachiwe wizi wa wazi? Andikeni kama wenye uelewa na siyo mashabiki wa watu washenzi tu!
Kudai sawa. Kudai halafu mshindwe kuendesha hata kidogo walichokuwa mlichokuwa mkipata kwa kodi hola sasa, sasa huu si upuuzi.
 
Tatizo kubwa si hilo.

Tatizo ni kutaka kulazimisha serikali kufanya biashara ambazo haiwezi, pamoja na "kuwafanyizia" wafanyabiasgara wazalendo.
Pamoja na yote hayo, magu hakupenda kuona watanzani wote tunaishi kwa raha na kumiliki njia za uchumi.
Haijawahi tokea maji yakapand mlima, ndivyo ilivyotabia ya pesa, haiezi toka kwa masikini kwenda kwa tajiri

Pesa hutoka kwa tajiri kwenda kwa masikini
Magu kakomba pesa za majiri, kaua biashara zao akidhani anawakomoa hao kumbe huku kajambani tuna Hali mbaya kuliko
 
Uzuri sisi wengine tupo humu JF kitambo na akili zetu ni zile zile hatuendi na upepo. Soma huu uzi na comments zake alafu umpe JPM heshima yake.



Mkuu Asante sana shida humu wengi ni waropokaji tuu!
 
Uache siasa za changa la macho, Serikali ya JPM ndiyo imeua utendaji wa UDART.

Barabara za UDART kweli ni mali ya serikali lakini mradi wa mabasi mwendo kasi ulikuwa toka mwanzo ni mradi binafsi (private investment) uliowekezwa na mtanzania, Nd Kisenha.

Serikali ilifanya kila njia kumnyima pumzi mwekezaji huyu wa UDART. Alipoagiza mabasi alinyimwa katakata kuyatoa bandarini mpaka hela yote ipatikane kulipa kodi.

Huku ni kukosa ushirikiano kwa muwekezaji, ambapo wale wa kigeni hupewa Tax Holiday au Mkataba maalum kwa malipo ya kodi kubwa.

Hii ingewezesha huduma iendelee, biashara iendelee na kodi ilipwe. Hili ni kosa, maana serikali haikuwa na msaada wowote kwa muwekezaji.

Pili, tunasikia tetesi kuwa sasa UDART ni mali ya Serikali maana baada ya Nd Kusenha kufunguliwa madai ya Uhujumu uchumi, kwawaida ya modus operadi ya Awamu ya 5kwa wafanyabiashara, serikali imejimilikisha uendeshaji.

Serikali zote toka Awamu ya kwanza hadi nafikiri Mwinyi (miaka zaidi ya33) mfupa wa DMT (Dra es Salaam Motor Transport) na UDA (Usafiri Dar es Salaam), ziliwashinda.

Sasa sijui Awamu ya 5 ndio wangeweza Kuendesha UDART?

Mbaya zaidi serikali inaua moyo wa wazalendo kuingia miradi mikubwa kiuwekezaji, kinyume cha wanachoongea majukwaani. Ziara ya Waziri Mkuu Majaliwa kwa UDART kweli sioni mantiki yake zaidi ya kusema Serikali imachukua na kuanza mradi huu on a false start.

Sana sana ni kujikosha kwa wananchi kwa failures za serikali yenyewe, kusaidia wazalendo kuwekeza nchini mwao.

Umeandika usicho kijua! Hahahaha
 
Mkuu Asante sana shida humu wengi ni waropokaji tuu!
Ndio maana hawawezi ku refer huo uzi utawaumbua. Watu wanaofanya mambo kwa malengo fulani hufikiri kila wakati wanaweza kutwist mambo kirahisi tu.
 
Inaonekana huna hata ABC ya biashara. Unafahamu aliwekeza kiasi gani? Profit margin projections ilikuwa kiasi gani? Na alipoanza kuuendesha mradi, kulikuwa na tofauti gani kati ya projections na mapato halisi?

Unapotaka kuanzisha mradi, kuna projections za gharama za uwekezaji, uendeshaji na mapato. Mradi ukianza, unakutana na uhalisia. Yawezekana kwenye uhalisia, gharama halisi za uendeshaji na mapato halisi ya biashara, vikawa na tofauti kubwa na projections. Lazima ufanye review. Na kwenye review, kuna items ambazo utakuwa huna uwezo wa kuzibadili, kama vile bei ya mafuta, kodi, bei za vipuli, n.k. Hivyo unabakia na maeneo machache sana ya kufanyia marekebisho, zaidi ni kwenye nauli.

Huwezi kusema hakukuwa na mabadiliko ya gharama wakati hujui kama toka mwanzo alikuwa anaendesha kwa faida au hasara.
Ndio umuhimu wa kusoma na kuelewa mkataba. Unapoweka tender na kaweka bei ya chini ili tu ushinde tender na kutegemea uta negisiate mbeleni, ni wewe ndio itakuja kuumia.

Simon group was a not best fit to run this company, they haven't run any public service company before and their not willing to put down a substantial investment.
 
Acha kupotosha wewe,

Ukweli ni kwamba huyo marehemu ndiye alikuwa anapiga. Ubabe wake ulikuwa ni zuga tu na uhuni wake. Marehemu amepiga hela ndefu Sana mfano alitumia 1.2 trillion kununua ndege by cash ambapo alilipwa 10% ya hiyo hela ,unafikiri ni sh ngapi?

Yeye alikuwa ni mwizi Namba 1 wa nchi hii.

Usijifanye hujui wakati unajua acha kudemka.
Waruhusu pawepo na private investors kama 3 hivi kwenye UDART. Miundo mbinu ni ya serikali lakini mabasi yawe ya wawekezaji binafsi. Wakiruhusu hili kutakuwa na ushindani na efficiency itaongezeka kwa 100%
 
Hayo unayotoa ni mawazo tegemezi ya mtu anayeshindwa kufikiri nje ya box.
Ati mtu hajawahi kuendesha mradi kama huo duniani!
My foot!
Nyie bongolala mmejiaminisha kuwa hamuwezi kitu mpaka mzungu awatie boost.

Mtaamka lini?
Mtimanyongo wenu unaua ari ya uwekezaji wa Watanzania.
Mfanyabiashara akiwekeza kigezo lazima kiwe faida na gharama za uendeshaji.
Walioajiriwa huwa hawajui hii fact.
Wewe ukienda hospitali una tatizo linahitaji upasuaji wakikuambia atakayekupasua hana elimu na ujuzi wa upasuaji..utakubali?
Kila fani inahitaji elimu, ujuzi, maarifa na uzoefu ili angalau kuwa na uhakika wa kufanikiwa, Kisena hakuwa na uwezo kurun sekta ya usafirishaji...tuache ubabaishaji na umachinga kwny kila jambo..kifupi hakustahili!
 
Acha kupotosha wewe,

Ukweli ni kwamba huyo marehemu ndiye alikuwa anapiga. Ubabe wake ulikuwa ni zuga tu na uhuni wake. Marehemu amepiga hela ndefu Sana mfano alitumia 1.2 trillion kununua ndege by cash ambapo alilipwa 10% ya hiyo hela ,unafikiri ni sh ngapi?

Yeye alikuwa ni mwizi Namba 1 wa nchi hii.

Usijifanye hujui wakati unajua acha kudemka.
Weka ushahidi hapa kuwa alilipwa 10% na sio kubwabwaja hapa
 
Uache siasa za changa la macho, Serikali ya JPM ndiyo imeua utendaji wa UDART.

Barabara za UDART kweli ni mali ya serikali lakini mradi wa mabasi mwendo kasi ulikuwa toka mwanzo ni mradi binafsi (private investment) uliowekezwa na mtanzania, Nd Kisenha.

Serikali ilifanya kila njia kumnyima pumzi mwekezaji huyu wa UDART. Alipoagiza mabasi alinyimwa katakata kuyatoa bandarini mpaka hela yote ipatikane kulipa kodi.

Huku ni kukosa ushirikiano kwa muwekezaji, ambapo wale wa kigeni hupewa Tax Holiday au Mkataba maalum kwa malipo ya kodi kubwa.

Hii ingewezesha huduma iendelee, biashara iendelee na kodi ilipwe. Hili ni kosa, maana serikali haikuwa na msaada wowote kwa muwekezaji.

Pili, tunasikia tetesi kuwa sasa UDART ni mali ya Serikali maana baada ya Nd Kusenha kufunguliwa madai ya Uhujumu uchumi, kwawaida ya modus operadi ya Awamu ya 5kwa wafanyabiashara, serikali imejimilikisha uendeshaji.

Serikali zote toka Awamu ya kwanza hadi nafikiri Mwinyi (miaka zaidi ya33) mfupa wa DMT (Dra es Salaam Motor Transport) na UDA (Usafiri Dar es Salaam), ziliwashinda.

Sasa sijui Awamu ya 5 ndio wangeweza Kuendesha UDART?

Mbaya zaidi serikali inaua moyo wa wazalendo kuingia miradi mikubwa kiuwekezaji, kinyume cha wanachoongea majukwaani. Ziara ya Waziri Mkuu Majaliwa kwa UDART kweli sioni mantiki yake zaidi ya kusema Serikali imachukua na kuanza mradi huu on a false start.

Sana sana ni kujikosha kwa wananchi kwa failures za serikali yenyewe, kusaidia wazalendo kuwekeza nchini mwao.
Awamu ya Tano imeboresha UDART,makusanyo ya UDART makubwa sana MABASI ya UDART barabarani ni Mengi Hakuna Malalamiko ya Wananchi Kabisa
 
Kisena aliwekwa kama chambo tu. Ile kampuni ya SIMON GROUP ina wahusika wengi sana wakubwa, akiwepo Profesa Kapuya na Marehemu Idd Simba. Kuna vigogo kadhaa wamo mle. Ukipekua humu JF kuna mada inayoongelea SIMON GROUP, utayaona mengi sana
Kwani Watanzania wakiungana na kufanya biashara nyie wakodoa macho wa maofisini mnatafuta visingizio vya kuchafua biashara.
Stupid idea! UNajua kwa nini tunawasaka watu wa money laundering duniani kote?
unawasaka wewe na nani.
Mtu anafanya biashara vizuri tu, akiweka benki zinatafunwa na TRA.
Akiweka nyumbani money laundering!
 
Pamoja na yote hayo, magu hakupenda kuona watanzani wote tunaishi kwa raha na kumiliki njia za uchumi.
Haijawahi tokea maji yakapand mlima, ndivyo ilivyotabia ya pesa, haiezi toka kwa masikini kwenda kwa tajiri

Pesa hutoka kwa tajiri kwenda kwa masikini
Magu kakomba pesa za majiri, kaua biashara zao akidhani anawakomoa hao kumbe huku kajambani tuna Hali mbaya kuliko
Kweli mkuu
Huo ni ukweli usiopingika.
 
Acha kupotosha wewe,

Ukweli ni kwamba huyo marehemu ndiye alikuwa anapiga. Ubabe wake ulikuwa ni zuga tu na uhuni wake. Marehemu amepiga hela ndefu Sana mfano alitumia 1.2 trillion kununua ndege by cash ambapo alilipwa 10% ya hiyo hela ,unafikiri ni sh ngapi?

Yeye alikuwa ni mwizi Namba 1 wa nchi hii.

Usijifanye hujui wakati unajua acha kudemka.
ujinga mwingine huu acha kumsingizia marehemu wizi.
 
Back
Top Bottom