Ayatullah Khamenei: Israel itazabwa kibao usoni

Ayatullah Khamenei: Israel itazabwa kibao usoni

Malaria 2

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2023
Posts
6,846
Reaction score
10,288
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Ali Khamenei amesema utawala wa Kizayuni wa Israel utazabwa kibao usoni kutokana na shambulio lake dhidi ya majengo ya ubalozi mdogo wa Iran katika mji mkuu wa Syria, mapema wiki hii.

Katika hotuba yake kwa maafisa wa utawala wa Iran na matawi mengine ya serikali jioni ya jana Jumatano, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu alisema shambulio hilo halitaweza kuinusuru Israel huko Gaza ambako imekuwa ikiendesha vita kwa karibu miezi sita dhidi ya Wapalestina.

"Juhudi za mfamaji za utawala wa Kizayuni kama ulivyofanya huko Syria hazitauepusha kushindwa. Bila shaka utazabwa kibao kwa hatua hii,” amesema Kiongozi Muadhamu.

Ayatullah Khamenei amesisitiza kuwa hakuna uwezekano wa kuwaokoa Wazayuni kutoka kwenye mtego walionasa ndani yake na kuongeza kuwa: Utawala wa Kizayuni utazidi kuwa dhaifu siku baada ya siku na kukaribia kudidimia na kuangamizwa, na tunatumai kuwa vijana wetu wataiona siku ambapo Quds Tukufu itakuwa katika milki ya Waislamu wakiswali hapo na ulimwengu wa Kiislamu utasherehekea kuangamizwa kwa utawala huo ghasibu."

Amesema maandamano yaliyopangwa kwa ajili ya Siku ya Kimataifa ya Quds mwaka huu ambayo yataadhimishwa tarehe 5 Aprili katika Ijumaa ya mwisho ya mwezi mtukufu wa Ramadhani, yatawakusanya watetezi wa Palestina sio tu katika nchi za Kiislamu bali pia katika nchi zisizo za Kiislamu ambazo zimekuwa zikipigania kukomesha uvamizi wa Israel dhidi ya Gaza.

"Siku ya Quds mwaka huu itakuwa uasi wa kimataifa dhidi ya utawala ghasibu wa Israel," amesema Kiongozi Muadhamu.
 
Hawa Iran mikwala na Rumberere nyiiiiiiingi hivi Israel ilipo piga ubarozi wa Iran kuna tamko lolote walitoa?

Wacha maneno weka mziki by darasa.
 
Ayatollah anaongea kwa kukata tamaa haswaa,maana anajua uwezo wa kuwapiga Israel hana,anaishia kujipa matumaini hewa eti ipo siku itaangamizwa.
 
Hakuna nchi duniani inayoweza kuishinda Israel katika medani ya kivita, Russia, China, Iran, Marekani, Uingereza, Ujerumani, Ufaransa, Turkey na dunia yote ya kiarabu ni mashahidi wa ukweli huo.
 
Vita ya maneno inatisha ila uhalisia unaongea. Walikua wamelala wapi hadi ubalozi unagongwa.
 
Why waliugeuza ubalozi kuwa CP ya kijeshi?oops hapa kwetu kusini majeshi ya SADC yameamua kufunga virago na kuondoka,vita imewashinda
 
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Ali Khamenei amesema utawala wa Kizayuni wa Israel utazabwa kibao usoni kutokana na shambulio lake dhidi ya majengo ya ubalozi mdogo wa Iran katika mji mkuu wa Syria, mapema wiki hii.

Katika hotuba yake kwa maafisa wa utawala wa Iran na matawi mengine ya serikali jioni ya jana Jumatano, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu alisema shambulio hilo halitaweza kuinusuru Israel huko Gaza ambako imekuwa ikiendesha vita kwa karibu miezi sita dhidi ya Wapalestina.

"Juhudi za mfamaji za utawala wa Kizayuni kama ulivyofanya huko Syria hazitauepusha kushindwa. Bila shaka utazabwa kibao kwa hatua hii,” amesema Kiongozi Muadhamu.

Ayatullah Khamenei amesisitiza kuwa hakuna uwezekano wa kuwaokoa Wazayuni kutoka kwenye mtego walionasa ndani yake na kuongeza kuwa: Utawala wa Kizayuni utazidi kuwa dhaifu siku baada ya siku na kukaribia kudidimia na kuangamizwa, na tunatumai kuwa vijana wetu wataiona siku ambapo Quds Tukufu itakuwa katika milki ya Waislamu wakiswali hapo na ulimwengu wa Kiislamu utasherehekea kuangamizwa kwa utawala huo ghasibu."

Amesema maandamano yaliyopangwa kwa ajili ya Siku ya Kimataifa ya Quds mwaka huu ambayo yataadhimishwa tarehe 5 Aprili katika Ijumaa ya mwisho ya mwezi mtukufu wa Ramadhani, yatawakusanya watetezi wa Palestina sio tu katika nchi za Kiislamu bali pia katika nchi zisizo za Kiislamu ambazo zimekuwa zikipigania kukomesha uvamizi wa Israel dhidi ya Gaza.

"Siku ya Quds mwaka huu itakuwa uasi wa kimataifa dhidi ya utawala ghasibu wa Israel," amesema Kiongozi Muadhamu.
Wacha weee mwarabu mtarajiwa!
 
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Ali Khamenei amesema utawala wa Kizayuni wa Israel utazabwa kibao usoni kutokana na shambulio lake dhidi ya majengo ya ubalozi mdogo wa Iran katika mji mkuu wa Syria, mapema wiki hii.

Katika hotuba yake kwa maafisa wa utawala wa Iran na matawi mengine ya serikali jioni ya jana Jumatano, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu alisema shambulio hilo halitaweza kuinusuru Israel huko Gaza ambako imekuwa ikiendesha vita kwa karibu miezi sita dhidi ya Wapalestina.

"Juhudi za mfamaji za utawala wa Kizayuni kama ulivyofanya huko Syria hazitauepusha kushindwa. Bila shaka utazabwa kibao kwa hatua hii,” amesema Kiongozi Muadhamu.

Ayatullah Khamenei amesisitiza kuwa hakuna uwezekano wa kuwaokoa Wazayuni kutoka kwenye mtego walionasa ndani yake na kuongeza kuwa: Utawala wa Kizayuni utazidi kuwa dhaifu siku baada ya siku na kukaribia kudidimia na kuangamizwa, na tunatumai kuwa vijana wetu wataiona siku ambapo Quds Tukufu itakuwa katika milki ya Waislamu wakiswali hapo na ulimwengu wa Kiislamu utasherehekea kuangamizwa kwa utawala huo ghasibu."

Amesema maandamano yaliyopangwa kwa ajili ya Siku ya Kimataifa ya Quds mwaka huu ambayo yataadhimishwa tarehe 5 Aprili katika Ijumaa ya mwisho ya mwezi mtukufu wa Ramadhani, yatawakusanya watetezi wa Palestina sio tu katika nchi za Kiislamu bali pia katika nchi zisizo za Kiislamu ambazo zimekuwa zikipigania kukomesha uvamizi wa Israel dhidi ya Gaza.

"Siku ya Quds mwaka huu itakuwa uasi wa kimataifa dhidi ya utawala ghasibu wa Israel," amesema Kiongozi Muadhamu.
Safi wapigwe banzi la uso
 
Back
Top Bottom