Azam FC 1-2 Yanga SC|| Uwanja wa Chamazi|| NBC Premier League

Azam FC 1-2 Yanga SC|| Uwanja wa Chamazi|| NBC Premier League

Huko kuna mchezaji wetu Abra kadabra lazima tumsapoti
Endelea kuwa support,ni muhimu sana,huku ukitetema
IMG-20220406-WA0001.jpg
 
Mwananchi hashikiki huu Msimu[emoji91]
.
Mayele anawika Chamazi Complex tena Mbele ya Prince Dube akiwa haonekani kabisa. Huyu Mkongo misimu Miwili ligi ya Kongo aliibuka na kiatu na mwingine akiwa nafasi ila sioni kama katika hii ligi kwa huu Moto kuna Mtu anaweza mzuia kubeba Ng'ombe zaidi ya wawili alionao kabla ya kupewa kiatu cha ufungaji bora. MAN ON FIRE [emoji91] [emoji1430][emoji460]
.
Hii sio Bahati mbaya heshima kubwa kwa Usajili wa Yanga hongera kwa ufanisi wa Benchi la ufundi la Yanga . Sio rahisi kumfunga Azam Fc aliye katika ubora huu ndani ya kiwanja tena akiwa full huku wewe ukiwa huna key players wa 3 .
.
Sureboy mtoto wa mzee Aboubakar Sureboy Senior katika dimba alilozoea dhidi ya mpinzani aliyemlea miaka 13 na akawaonyesha ukubwa wake dimbani kwa ladha eneo la kiungo.
.
Kadi yake ya 3 ya Mchezo na kweli atakksa mchezo mmoja wa Azam Sports cup Federation hivyo mechi ya April 30 dhidi ya Mtani atakuwepo huku ikiwa Yanga Sc inatimiza Mwaka na Siku 5 bila kupoteza mchezo wowote wa ligi Kuu.
.
WAITE TU PRESS [emoji16]
.
Mwisho wa Siku Yanga Sc walikubali kukimbia zaidi kuliko mpinzani kiwanjani wakaamua kuonyesha Spirit na Character ya timu kubwa na inayotaka Ubingwa.
.
Deserving Win na alama 51 kibindoni akiwa kileleni kwa Alama 14 zaidi ya mtani wake.
.
KWELI MPIRA UNADUNDA ILA HUU MLIMA NI MREFU MNO WAJOMBA TUWE WAKWELI.
 
Leo kutakuwa na Mtanange wa Kukata na Shoka kati Azam Fc na Yanga SC.
.
Wakuu mechi hii itaanza majira ya saa 2:15 usiku Uwanja wa Chamazi Complex.
.
Tunajua ugumu wa game hii ya leo Ukizingati timu hizi zinapokutana hupigwa mpira wa nguvu sana.
.
Azam FC ni Mwenyeji wa Mchezo wa Leo Dhidi ya Yanga.
.
Huku Team Ya Yanga ikiwakosa Wachezaji wake kama Feisal Salum, Bangala, Aucho nk.

==================================

YANGA YAIFUNGA AZAM FC 2-1, YAFIKISHA POINTI 51

Yanga wameendelea kujiimarisha katika kilele cha Ligi Kuu Bara baada ya kupata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Azam FC kwenye Uwanja wa Azam Complex, Aprili 6, 2022.

Yanga imepata mabao yake kupitia wa Djuma Shaban kwa njia ya penati na Fiston Mayele, bao la Azam FC limefungwa na Rodgers Kola.

Yanga imefikisha pointi 51 wakati Azam FC imebaki na pointi 28 katika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa Ligi.
Nafasi ya kwanza ana point 51 halafu nafasi ya tatu ana point 28!!!? Hii league haina usawa kabisa bora ifutwe tuu[emoji23]
 
Prince Dube majeraha yamemuondoa kabisa katika ramani ya mpira wa miguu. Bila shaka anahitaji muda zaidi kurudi kwenye kiwango chake cha awali.

Kiufupi hana tofauti na Balama Mapinduzi. Vipaji wanavyo, ila ndiyo hivyo tena. Majeraha yamewarudisha nyuma.
 
Hivi tunamtazama mayele kwenye kisimbuzi kimoja na kibuda denis kweli?

tff waliangalie hili sio siri.
 
Back
Top Bottom