Azam kuibomoa Yanga tena 99%. Bangala mali ya Azam FC

Lakini Morrison mlimrudisha, au umesahau?
 
Amshukuru Rais kumuokoa otherwise yeye pamoja na wapambe wake kama nyie msingemsaidia chochote kwa maana alikuwa mdomoni mwa mamba!
Siyo kwamba ni Yanga ingeenda kuadhirika tena huko CAS? We umeona wapi timu inayoendeshwa kwa weledi inamng'ang'ania mchezaji tena wa bei rahisi kisa kumkomoa
 
Kwa nini wachezaji hawataki kuchezea Yanga?
Kwahiyo wanaochezea Yanga ni majini?

Mbona huwa hamumuulizi Chama swali kama hili akianzaga kuwajambisha?

Yanga ni kubwa kuliko mtu yeyote yule, hata GSM siyo mkubwa mbele ya Yanga ndio sembuse mchezaji?mudathir na Sure boy wamekwenda Yanga wakitokea timu gani?
 
Siyo kwamba ni Yanga ingeenda kuadhirika tena huko CAS? We umeona wapi timu inayoendeshwa kwa weledi inamng'ang'ania mchezaji tena wa bei rahisi kisa kumkomoa
Ingeenda kuadhirika kwa kipi labda ebu tupe mrejesho wa mkataba wake ulkuwaje
 
Mpira biashara
Bangala hakuwa na msimu mzuru + nidhamu yake
Kocha Nabi alipendekeza aachwe
Kwakuwa azam wamejaa kwenye mfumo yanga amepiga hela safi
Hakuna mchezaji asiyeuzwa.
Huu ndo uweledi sio uhuni aliyofanya feitoto nadhani Bangala ametoa somo na ameheshimu mkataba akauvunja kwa utaratibu na sasa ameenda azam

Me kama shabiki wa yanga namtakia kila la heri huko azam
 
Kumbe na wewe ni half empty glass, Pyramids imefanya biashara na Yanga ndio inammiliki Mayele.

Kwa sasa Mayele akienda Pyramids wamiliki ni Pyramids siyo Yanga Tena.

Agent siyo mmiliki wa mchezaji.
Mkuu usipoteze muda wako bure kuwaelezea vijana wa mangungu jambo linaloeleweka kwa kila mtu mwenye akili timamu, iyo ajenda ya kwamba mayele anamilikiwa na sijui nani wameiset wao wazee wa kuongeza sifuri, inaonekana kuna jambo linawasumbua vichwani mwao juu ya mauzo ya mayele
 
Hata mechi ya fainal kule algeria nilishangaa sana dickson job ndo alicheza namba sita huku bangala akiwa bench na hata sub hakuingia jamaa kiwango kilishuka labda akiwa azam apambane kipande
 
Hizo habari anazitoaga bin kazumari yule jamaa ana majungu kupita maelezo
 
Kwa sababu akili hawana wameshindwa kuchukuwa Yanick Bangala kiurahisi tu na walikuwa wanamwitaji.

Wangekuwa na Inonga na kiungo mkabaji Bangala angewasaidia sana hizi international games.

Lakini badala ya kujikita kwenye mambo ya msingi wao wamekalia umbea tu, wacha Azzam wamchukuwe.

Note kwa usajili wa Azzam Simba wajitaidi wawepo kwenye top four, maana ushindani wa ubingwa utakuwa ni kati ya Yanga na Azzam, Simba na Singida wapambane nafasi ya tatu.
 
Azam Wamchukue Na Djuma Shaban, Tuwape Banda Kwa Mkopo

Wale Makipa wao 2 wakigeni ni Mapazia tuuu wawaache
 
Ada ya Feisal uliiona wapi
 
Bangala ndiyo alikuwa wa kwanza kuonyesha haitaki Yanga. Alilionyesha hilo uwanjani kwa mgomo baridi na akaja kulisema kwa mdomo wake. Mchezaji aliyekuwa MVP misimu miwili iliyopita unamuuzaje 100M?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…