AZAM MEDIA tafuteni njia nzuri za kurecord mechi katika uwanja wa UHURU, angle mnazo-record ni za ovyo

AZAM MEDIA tafuteni njia nzuri za kurecord mechi katika uwanja wa UHURU, angle mnazo-record ni za ovyo

Mechi zote zinazochezwa uhuru hawaruhusiwi kuweka main camera juu kwa sababu ya eneo la jeshi kuwa pale, kwahy hata ukashtaki FIFA hakuna hukumu yoyote Azam TV watapewa.



Na ishu ni main camera na sio camera zote, uwanja wa uhuru ukitumia main camera unaona hadi nje ya uwanja ambapo ndio kuna kambi ya jeshi lakini pale kwa mkapa main camera haionyeshi kambi ya jeshi kutokana na location na miundombinu ya uwanja wa mkapa.
 
Mara kadhaa nimekuwa nikifuatilia matangazo yenu mubashara kutoka uwanja wa UHURU na kuangalia angles mnazorikodi mechi kwa camera zenu na kugundua kuwa hazimpi mtazamaji wa matangazo yenu ya mpira katika uwanja wa uhuru uwezo wa kuona mechi vizuri.

Wito wangu kwa kampuni ya AZAM MEDIA ni kuwa muongeze idadi ya camera katika uwanja wa UHURU na pia mjitahidi kuweka camera zitakazorikodi kutoka juu ili tuuone uwanja katika ukubwa wake kama mechi za EPL na ligi nyingine barani ulaya.

Leo hii nadhani idadi ya camera zinazotumika kurecord matangazo mubashara ya mechi kati ya Simba dhidi ya Kagera Sugar hazizidi tatu na hakuna camera ya juu hata moja.
Hovyo sana, tena Bora hapo Uhuru. Mechi za mikoani tena ambazo timu tatu zile hazihusiki ndio balaa. Ni kama wamechoka au wanachukulia poa tu, Kwa ujumla wamepunguza usiriasi.
 
Mechi zote zinazochezwa uhuru hawaruhusiwi kuweka main camera juu kwa sababu ya eneo la jeshi kuwa pale, kwahy hata ukashtaki FIFA hakuna hukumu yoyote Azam TV watapewa.



Na ishu ni main camera na sio camera zote, uwanja wa uhuru ukitumia main camera unaona hadi nje ya uwanja ambapo ndio kuna kambi ya jeshi lakini pale kwa mkapa main camera haionyeshi kambi ya jeshi kutokana na location na miundombinu ya uwanja wa mkapa.
Na ndio kinawatesa Azam hicho ,shots moja tu ya main camera imeondoa show yote ya mpira
 
Hili tumeshalisema sana na kwa mtazamo wangu kisingizio cha jeshi bado hakina mashiko kwa sababu kwanza kuna upande ule wa pili wenye jukwaa chakavu wanaweza weka main camera, lakini pia hata upande huo huo wanaoutimia sasa hata wakiweka juu halafu cameraman wakapewa maelekezo kwamba wasipige shoti za nje ya uwanja sioni shida yoyote. Ukikaa juu ukafocus kwenye pitch hauwezi ona nje.

Kibaya zaidi kwenye huo uwanja ni pitch yake. Wachezaji wanacheza kama wanacheza kwenye sakafu, mpira unadundadunda na hatari za majeruhi ni kubwa zaidi na hili pia tumeshalilalamikia sana na leo Benchikha kalisema. Kama Chamazi imeshindikana, Simba ihamie hata Zanzibar kucheza mechi zake zote za nyumbani za NBC.
 
Production ya mechi zote duniani ukiondoa wide angle lazima mechi ionekane mbaya ndio maana camera inayoonyesha wide inaitwa main camera au no. 1 camera.
Yes,Mkuu nalijua hilo vzr sana nimelielezea juu huko , maana uwanja wa uhuru nishawahi fanya production hapo miaka ya nyuma ,main tulikua tunaweka juu , enzi za Tamasha la michezo
 
Hili tumeshalisema sana na kwa mtazamo wangu kisingizio cha jeshi bado hakina mashiko kwa sababu kwanza kuna upande ule wa pili wenye jukwaa chakavu wanaweza weka main camera, lakini pia hata upande huo huo wanaoutimia sasa hata wakiweka juu halafu cameraman wakapewa maelekezo kwamba wasipige shoti za nje ya uwanja sioni shida yoyote. Ukikaa juu ukafocus kwenye pitch hauwezi ona nje.

Kibaya zaidi kwenye huo uwanja ni pitch yake. Wachezaji wanacheza kama wanacheza kwenye sakafu, mpira unadundadunda na hatari za majeruhi ni kubwa zaidi na hili pia tumeshalilalamikia sana na leo Benchikha kalisema. Kama Chamazi imeshindikana, Simba ihamie hata Zanzibar kucheza mechi zake zote za nyumbani za NBC.
Hata mm jeshi natakaa maana Nishafanya na ITV live hapo Main camera tulifunga juu jukwaani
 
Yaani ni hovyo hovyo,unaangalia mpira na mivitu mingine ambayo sio ya muhimu,mm nafikiri Simba nao wanazingua kutaka kutumia uwanja huu ktk mechi zao....
 
Hata mm jeshi natakaa maana Nishafanya na ITV live hapo Main camera tulifunga juu jukwaani
Mi nadhani Azam wanafanya kusudi. Yaani hata ukiacha main camera, camera za pembeni walipoziweka zinashindwa kuonyesha offside. Unaona kabisa mechi za Uhuru wanafanya kama kutimiza wajibu tu.

Sijui mkataba unasemaje kwenye haki za timu mwenyeji kuhakikisha na kudai matangazo yake yana quality maana hata kama timu haipati kitu, inaathiri kwenye kuweka kumbukumbu nzuri za mechi zake.
 
Back
Top Bottom