AZAM MEDIA tafuteni njia nzuri za kurecord mechi katika uwanja wa UHURU, angle mnazo-record ni za ovyo

AZAM MEDIA tafuteni njia nzuri za kurecord mechi katika uwanja wa UHURU, angle mnazo-record ni za ovyo

Sifahamu walikuwa wanatumia aina gani ya Kamera au angle ambayo kamera husika ilikuwa inachukua live coverage ya mechi hii.Ukweli ni kwamba "live coverage" ya mechi ya Simba dhidi ya Kagera Sugar ni moja kati ya "live coverage" za hovyo. Nimelazimika kuingalia hii mechi kupitia Azam kwa kuwa sikuwa na mbadala wa "live coverage"ya hii mechi.
 
Mi nadhani Azam wanafanya kusudi. Yaani hata ukiacha main camera, camera za pembeni walipoziweka zinashindwa kuonyesha offside. Unaona kabisa mechi za Uhuru wanafanya kama kutimiza wajibu tu.

Sijui mkataba unasemaje kwenye haki za timu mwenyeji kuhakikisha na kudai matangazo yake yana quality maana hata kama timu haipati kitu, inaathiri kwenye kuweka kumbukumbu nzuri za mechi zake.
Umegusia mkataba na quality, hii kitu muhimu sana tena sana ,sijui kama walikumbuka ,picha za mechi za simba ktk uwanja wa uhuru zitakua zinaboa tu kutazma ,huoni maumbo ya mfumo wa timu
 
Umegusia mkataba na quality, hii kitu muhimu sana tena sana ,sijui kama walikumbuka ,picha za mechi za simba ktk uwanja wa uhuru zitakua zinaboa tu kutazma ,huoni maumbo ya mfumo wa timu
Binafsi hili suala nimewahi kulipigia kelele sana, angalia post hizo chini. Nadhani kuna namna ambayo kitengo cha habari cha Simba kinatakiwa kuimarishwa zaidi ili moja ya maeneo yao iwe ni kuhakikisha matangazo ya mechi zake ndani ya Azam yana quality nzuri kuanzia kwenye picha, sauti, wachambuzi na watangazaji. Tumekuwa tunasema management ya Simba haina watu wa kutosha kiasi kwamba mambo mengi ikiwemo kama hili wanashindwa kuyafanyia kazi.

Jana nilipokuwa nafuatilia gemu ya Yanga, nilikuwa nasikia mahaba ya kupitiliza kwa timu ya Yanga kutoka kwa mtangazaji Baraka Mpenja na hii siyo mara ya kwanza kuliona hili.

Jana alikuwa anatoa kauli kama "upande wa pili nao watakuwa wakienda chooni wanasema Yanga kweli anapiga mpira mwingi" na kauli aliyokuwa anairudia mara nyingi ni "huu ni mpira wa kitabuni, siyo mpira wa papatu papatu". Ulikuwa unawalenga kina nani kwa kauli hizo?

Viongozi wa Simba nao waamke, hali iliyokuwepo msimu uliopita ya kuishi kinyonge haitaifikisha hii timu popote. Karibia media zote sasa hivi ziko kwenye payroll ili kuichafua Simba. Mnaweza kuyaona haya mambo ni madogo ila media ina nguvu sana inaweza kuupamba uongo hadi ukaonekana kweli.

Azam kiujumla ni kama wamekuwa na bifu na Simba ndiyo maana wanasimba wengi wanafurahi mnapofanya vibaya. Uwanjani mnaikamia Simba halafu Yanga wanajipigia wanavyotaka.

Mechi zinazochezwa uwanja wa Uhuru hawafanyi coverage nzuri, Camera ya muhimu inawekwa chini na muda wote unaona kwanza mabenchi na nguzo kabla haujawaona wachezaji waliopo uwanjani. Mechi za mikoani hawaweki camera za kuonyesha offside, matokeo yake minong'ono kuwa Simba inabebwa na marefa inakuwa na nguvu bila ushahidi wa kutosha. Inabidi wawepo watu ndani ya Simba kuhakikisha mechi zake hasa zile za nyumbani zinatangazwa ipasavyo.

Kwa ujinga huu ndiyo maana wengine ikifika makundi tu ya CAF tunaswitch DSTV. Watangazaji wa nje wanatoa facts siyo mahaba binafsi na pia hawatangazi mpira kama wako redioni.

Nimemaliza.
Hivi kwa nini kwenye uwanja wa Uhuru Azam wasiwe wanaweka camera zao upande ule wa pili? Upande wanaoweka camera ziko chini sana.

Wapi nimesema hivyo? Watangaze na waonyeshe mpira kwa weledi. Mechi za uwanja wa Uhuru mpira hautazamiki huwa tunajilazimisha tu
 
Mtoa mada tuko pamoja.
Azam utafikiri kituo kimeanza leo kuonesha mipira,aibu sanaa
 
Simba ikatae kucheza mechi zake ktk uwanja wa Uhuru, ni bora kuchezea CHAMAZI kwa bakhresa. Uwanja wa uhuru una pitch mbaya ina vijiwe vijiwe vidogo kama changarawe, mchezaji akianguka ni rahisi kuumia
 
DAH yaani nmechek mpira yaani hata hauvutii kabisa shots za hovyo kabisa , mpira ukipigwa ukasogea karibu na main camera na mabench ya wachezaji wa akiba utafikiri wachezaji
wanapita ndani ya makaravati barabaran na kutokea upand wa pili,,unaona kabisa kichwa cha onana kina mkinga hadi baleke kule mbele
 
Washa sema uwanja wa Uhuru upo karibu na jeshi hawaruhusu kutumia drone footage,
Kwani kuna umbali gani kutoka uhuru hadi kwa mkapa? Pale uhuru hakuna sehemu ya kukaa mpiga picha kutokana na jukwaa kuu lilivyo
 
Mi nadhani Azam wanafanya kusudi. Yaani hata ukiacha main camera, camera za pembeni walipoziweka zinashindwa kuonyesha offside. Unaona kabisa mechi za Uhuru wanafanya kama kutimiza wajibu tu.

Sijui mkataba unasemaje kwenye haki za timu mwenyeji kuhakikisha na kudai matangazo yake yana quality maana hata kama timu haipati kitu, inaathiri kwenye kuweka kumbukumbu nzuri za mechi zake.
Mm naona kabla ya kusema wanafanya kusudi em jiulize n kwann iwe n kwenye uwanja wa uhuru tuu, je kuna kitu wanafaidika wakifanya hvy.? Jibu n hapana, Mm nadhani wakulaumiwa n jeshi pale mana eneo lake halionekani kwa ukubwa hvy mpaka kusababisha Production ya mechi kuwa mbaya.
Kingine naona umezngumzia camera za offside, bila shaka kama unajua maana ya camera ya offside bc unajua umuhimu wa main camera, daima popote pale duniani kwenye Production ya mpira huwezi kutumia offside camera kuwa main camera.
 
Mm naona kabla ya kusema wanafanya kusudi em jiulize n kwann iwe n kwenye uwanja wa uhuru tuu, je kuna kitu wanafaidika wakifanya hvy.? Jibu n hapana, Mm nadhani wakulaumiwa n jeshi pale mana eneo lake halionekani kwa ukubwa hvy mpaka kusababisha Production ya mechi kuwa mbaya.
Kingine naona umezngumzia camera za offside, bila shaka kama unajua maana ya camera ya offside bc unajua umuhimu wa main camera, daima popote pale duniani kwenye Production ya mpira huwezi kutumia offside camera kuwa main camera.
Mimi sijasema camera za offside ndiyo zitumike kama main camera. Camera za pembeni zilikuwepo kwa ajili ya kuchukua matukio ya pembeni ikiwemo offside ila kuna tukio moja ambalo Mohammed Hussein aliitiwa offside, camera haikuwa positioned kulichukua kwa usahihi hadi mtangazaji naye akashangaa maana katika marudio, mwanzo camera ilikata eneo ambalo isingeweza kuonyesha hiyo offside ilipo, ila ilipokuja kusogea ikaonyesha MH alipokuwa bado kuna wachezaji wengine wa Kagera upande wa goli lao na kuifanya ile kutokuwa offside. Mtangazaji akabaki kuguna tu. Ndiyo maana wengine tunapata tafsiri kuwa kuna ulipuaji wa kazi maana kama ni mfuatiliaji utajua production uwanja wa uhuru inakuwaga chini kwa maeneo mengi.

Vilevile narudia kusema, vipi wakiamua kuweka main camera upande huu wa pili wenye jukwaa chakavu, au na huku wamekatazwa maana huku ukikaa kwenye ngazi za juu kabisa nadhani kwanza unakuwa juu zaidi halafu unakuwa hauna makorokoro mengine kama nguzo za bendera zinazoziba camera.

Screen Shot 2023-12-15 at 11.47.52 PM.png


Ila vilevile kuna sababu nyingi za kutotumia huo uwanja, hilo la camera ni mojawapo tu. Ona mabenchi ya ufundi, yaani unamlipa kocha milioni 80 kuja kumkalisha sehemu kama hii?

Screen Shot 2023-12-15 at 11.52.28 PM.png
 
Mimi sijasema camera za offside ndiyo zitumike kama main camera. Camera za pembeni zilikuwepo kwa ajili ya kuchukua matukio ya pembeni ikiwemo offside ila kuna tukio moja ambalo Mohammed Hussein aliitiwa offside, camera haikuwa positioned kulichukua kwa usahihi hadi mtangazaji naye akashangaa maana katika marudio, mwanzo camera ilikata eneo ambalo isingeweza kuonyesha hiyo offside ilipo, ila ilipokuja kusogea ikaonyesha MH alipokuwa bado kuna wachezaji wengine wa Kagera upande wa goli lao na kuifanya ile kutokuwa offside. Mtangazaji akabaki kuguna tu. Ndiyo maana wengine tunapata tafsiri kuwa kuna ulipuaji wa kazi maana kama ni mfuatiliaji utajua production uwanja wa uhuru inakuwaga chini kwa maeneo mengi.

Vilevile narudia kusema, vipi wakiamua kuweka main camera upande huu wa pili wenye jukwaa chakavu, au na huku wamekatazwa maana huku ukikaa kwenye ngazi za juu kabisa nadhani kwanza unakuwa juu zaidi halafu unakuwa hauna makorokoro mengine kama nguzo za bendera zinazoziba camera.

View attachment 2843650

Ila vilevile kuna sababu nyingi za kutotumia huo uwanja, hilo la camera ni mojawapo tu. Ona mabenchi ya ufundi, yaani unamlipa kocha milioni 80 kuja kumkalisha sehemu kama hii?

View attachment 2843649
Mm n camera operator Na Najua production Namna zinazofanywa, binafsi hua nikiangalia video yoyote ile hua naangalia pia kwa jicho la camera operator.

Sasa ukiangalia production zote za mpira kote duniani zinazofanywa utagundua kuwa Main camera zote zinakuwa upande wa lango kuu wa wachezaji wanapoingilia (Main Gate) Na Kwenye production zote za mpira main camera hua ni mbili zinazofanya kazi tofauti ambazo ndio hizo lazima ziwe upande wa lango kuu, kwa wenzetu hua na camera nyingi ambazo zinaweza kuwa kwenye mzunguko wote wa uwanja yani nyuzi 360 za uwanja na zote zikatumika lkn bado main camera zile mbili ni lazima utazikuta zipo upande wa lango kuu na asilimia 80 ya camera zote bado zitakuwa upande wa main gate (kombe la dunia la 2022 kuna mahali nilisoma wanasema kulikuwa na camera 33,sina uhakika 😂)
Nadhani wanafanya hv ili kuziba pengo la ule lango kuu na kuacha mashabiki ndio waonekane na ndio mana kwenye main camera ni lazima utaona na mashabiki.

Hivyo haiwezekani camera kuwa upande wa Jukwaa kule kulikochakaa, ila serikali nao dah yani kweli wanashindwa kupiga rangi uwanja 😂

Nimejibu kulingana na experience yangu kama camera operator
 
Ule uwanja unamilikiwa na jeshi siyo wa serikali direct wenye huo uwanja ndiyo wameweka masharti hayo kuwa kamera za juu (zaidi juu ya jukwaa kuu wanakokaa viongozi) hawaruhusu wapiga picha kule kwasababu wanazojua wao wenye uwanja. Suala hili limeshawahi kutolewa ufafanuzi na azam tv
 
Mm n camera operator Na Najua production Namna zinazofanywa, binafsi hua nikiangalia video yoyote ile hua naangalia pia kwa jicho la camera operator.

Sasa ukiangalia production zote za mpira kote duniani zinazofanywa utagundua kuwa Main camera zote zinakuwa upande wa lango kuu wa wachezaji wanapoingilia (Main Gate) Na Kwenye production zote za mpira main camera hua ni mbili zinazofanya kazi tofauti ambazo ndio hizo lazima ziwe upande wa lango kuu, kwa wenzetu hua na camera nyingi ambazo zinaweza kuwa kwenye mzunguko wote wa uwanja yani nyuzi 360 za uwanja na zote zikatumika lkn bado main camera zile mbili ni lazima utazikuta zipo upande wa lango kuu na asilimia 80 ya camera zote bado zitakuwa upande wa main gate (kombe la dunia la 2022 kuna mahali nilisoma wanasema kulikuwa na camera 33,sina uhakika 😂)
Nadhani wanafanya hv ili kuziba pengo la ule lango kuu na kuacha mashabiki ndio waonekane na ndio mana kwenye main camera ni lazima utaona na mashabiki.

Hivyo haiwezekani camera kuwa upande wa Jukwaa kule kulikochakaa, ila serikali nao dah yani kweli wanashindwa kupiga rangi uwanja 😂

Nimejibu kulingana na experience yangu kama camera operator
Kuna production nyingi za mpira ambazo camera kuu inaweza kuangalia hiyo unaita lango kuu huku ikiangalia mabenchi ya wachezaji na hii ni kuanzia Ulaya hadi hapa Africa. Kuangalia lango kuu hakuna umuhimu wowote katika production. Camera za mechi hata ziwe nyingi kiasi gani, zile muhimu zinazoonyesha muendelezo wa mechi zinatakiwa kuwa nyuzi 180 na siyo 360. Camera za ziada nje ya hapo zinatumika kuonyesha matukio mengine ya ndani au nje ya uwanja lakini siyo ya muendelezo wa mechi.

Kwa hapa Africa najaribu kukumbuka ila kuna mechi ambayo camera kuu ilikuwa inaangalia lango kuu waliloingilia na kutoka wachezaji ingawa mabenchi yalikuwa upande wa camera kuu. Benchi la ufundi na wachezaji wa akiba walivuka katikati ya uwanja kwenda kwenye mabenchi yao. Inawezekana ilikuwa Simba na Horoya kule kwao.

Halafu hiyo sababu uliyoisema ya kuonyesha mashabiki, ukiangalia uwanja wa Uhuru camera zingekaa kule kwenye jukwaa chakavu ukiacha sababu hizi tunazoongelea hapa lakini hata kwa muonekano tu, picha zingependeza zaidi maana mashabiki wengi katika uwanja ule wanakuwa jukwaa kuu tena lenye viti kwa hiyo lile jukwaa chakavu ambalo halivutii kwa macho halafu lina mashabiki wachache halitaonekana.
 
Achana na hiyo, kuna kitu kingine unakuta camera ilikuwa inaonesha subject fulani, halafu ghafla camera ina move haraka sana kuelekezwa kwingine utafikiri mshika camera anajua anaangalia peke yake kiasi ambacho inamlazimu mchanganya picha aihame hiyo shot haraka sana.

Kitu kama hiki huwa sioni kwa live coverage za wenzetu hata ligi ya south africa hapo achana na ulaya, unakuta camera ina-rotate taratibu kiasi mtazamaji unaona kila inachochukua.
 
Kuna mechi moja simba walicheza na Geita, Geita wakapata goli lakini refa akalikataa kuwa mshambuliaji alimsukuma Kapombe. Picha za marudio wakionyesha mara unaona Kapombe hajaguswa lakini wakirudia unaona Kapombe kaguswa. Kumbe Azam waliweka Camera mbili moja kwenye goli la Geita nyingine kwenye goli la simba na ndio zilikuwa zinaleta utata. Ikiwa mikoani ni balaa zaidi. Azam badala ya kuweka taa kwenye viwanja wangeongeza kamera ukichukulia kuweka taa sio kazi yao.
 
Swala lilishatolewa ufafanuzi ni mambo ya JWTZ, lakini nachojiuliza ni kwanini Simba walichagua huu uwanja maana hata pitch yenyewe ni artificial turf ambayo ishachoka. Anyways tuseme walikua hawajui but now washajua kila kitu kwanini wasiombe kubadilisha uwanja maana taratibu zinaruhusu
 
Back
Top Bottom