Azam Media waomba Radhi kwa wadau wa mpira kwa kurusha interview ya Mahojiano na aliyekua mchezaji wa Yanga Sc Fiston kalala Mayele

Mbu Mbu mbu kwenye ubora wenu .......

Unaelewa ethics za media....haitakiwi kutoa habari ambazo Zina kandamoza one side ....
 
Nadhani kwa watu wasio na taaluma ya habari kama wewe wanaweza kuja na hoja ya namna hii, lakini kiukweli kwa hatua hii Azam wako sahihi.

Mahojiano ya Mayele yalirushwa bila kukidhi mahitaji ya kitaaluma, kwa kuwa baadhi ya mambo yaliyosemwa na Mayele yalikuwa ni tuhuma.

Kwa mujibu wa taaluma ya habari, kila tuhuma ni lazima anayetuhumiwa apewe nafasi ya kujitetea/ kujieleza juu ya tuhuma zake.

Usipofanya hivyo, habari husika huwa ni kashfa kwa aliyetuhumiwa na hivyo ana nafasi kubwa ya kushinda kesi ya kudai fidia mahakamani.

Hivyo, Yanga walionewa na Azam Media kwa makosa ya uhariri wa habari ile, na njia pekee ya kujiokoa ilikuwa ni kuomba radhi.

Ova
 
Azam waanche mchezo na rangi za kijani na njano.
 
Yanga walitafuta hiyo nafasi ya kujitetea?
 
Kwani kuna chombo kipi cha habari kilocho huru kweli kweli?
 
Yanga walitafuta hiyo nafasi ya kujitetea?
Kwa mujibu wa taaluma, media yenye hiyo habari ndiyo inatakiwa kumpa/ kumtafuta Yanga ili kumpa hiyo nafasi ya kujitetea ili ikamilishe habari yake.

Kitaaluma, habari ya mahojiano ya Mayele ilikuwa haijakamilika, hivyo haikuwa na sifa ya kutumiwa kama habari.

Ova
 
Hapo inatakiwa kwanza walipe athari waliyopata Yanga
Na kile kiasi walichopata kwa kuwachafua yanga basi wawape yanga
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…