Azam mlichonga njia mbovu kumpata Feisal, sasa kibao kimewageukia muachieni pia Prince Dube akatafute maisha kwingine!

Fei kukosea taratibu unaona sio kesi sababu ni kwetu huku mpira wetu wa hovyo hovyo na taratibu hazifuatwi ila mbele Fei alikuwa anakula ban moja ya maana hata ya kufungiwa nusu msimu.Ila taratibu zingefuata hata zile kesi za TFF zilikuwa zinatosha kumwadhibu Fei kwa ban na fine.

Nimekutolea mifano Caisedo yule alionesha nio ya kuondoka,Brighton waliweka dau lao wazi?Sio kwamba mchezaji anataka kuondoka ,then timu uhusika ndio iweke dau in a public,vip kama kuna timu zinamtaka zaidi ya dau hilo.

Ndio maana timu hupenda kuzialika club zinazo mtaka zije mezani (kama mnada) so bado Yanga hawa kukosea sababu walikuwa wapo ndani ya taratibu. Angalia biashara iliyofanyika kwa Mudrik,Caisedo na Rice na walivyopiga hela ndefu....... so Yanga walikuwa wapo sawa.
 
Timu nzima ndio inaweza kuvunja mkataba. Ila hiyo Club itatengeneza fedha za kutosha.

Unadhani wachezaji ni watiifu kwa mkataba sababu sheria haziwaruhusu kuvunja? Ni watiifu kwa sababu ya gharama za kuvunja mkataba.
 
Sasa mkuu Yanga wangesema Fei kakosea utaratibu tunamshtaki tulipwe fidia au afungiwe still wangekuwa sawa.

Hoja yangu ni kuwa Yanga hawakuwa wazi ni nini wanataka exactly kwa Fei kama Azam walivyofanya.

Haiwezekani mchezaji hana nidhamu, hayupo kambini na still katika option mnazompa ipo ya kuongezewa mshahara. Sijui kama unanielewa?
Sawa, haya yote unayoyaeleza still hayamzuii mchezaji iwapo yeye mwenyewe atataka kuvunja mkataba wake kisha yeye akale signing fee kama mchezaji huru.
 
Sasa Dube dau lake 750m,yy anataka kuvunja mkataba,Je ikitokea hamna timu yenye kulipa hiyo fedha? Huoni kama wanamkomoa.

Sasa kwa nini Fei alikuwa hataki kukaa kikao na Yanga?

Ujue unapoitwa kwenye kikao sometimes hata dau linaweza kuwa dogo,mfano Kapteni wa Arsenal,mfungaji bora wa EPL ,aliondoka Arsenal kwa hela ndogo sana Pound mil 25 na alilazimisha kuondoka.
 
Reactions: Tsh
Kama mkataba unasema thamani ni dola hizo na hakuna atakayetoa Dube hana namna. Kashindwa yeye hajanyimwa kuvunja mkataba wake.
Sasa akifanya kama rafiki yako FEI. Dube aondoke kambini na akatae majukumu yake ya kucheza just kama alivyofanya Fei, mtafanyaje?
 
We mbona unatumia hisia sana, vikao vinakaa kwenye kuingia mkataba lakini kwenye kutoka sio lazima kukaa kikako, kuna unilateral termination tena bila sababu jambo la msingi ni kulipa fidia tu basi. Hata Neymar alifanya hivyo hivyo, unaweka mzigo tu na barua kwaheri
 
Sasa Dube dau lake 750m,yy anataka kuvunja mkataba,Je ikitokea hamna timu yenye kulipa hiyo fedha? Huoni kama wanamkomoa.
Mkuu, mpira ni biashara. Suala la ukubwa wa 750m inategemeana na thamani ya mkataba. Dube ametaka kuondoka. Kaambiwa wazi alipe kiasi gani, kama anaona si sawa atashtaki, kama anaona ni sawa ila hawezi kulipa atasubiri mkataba uishe.
Sasa kwa nini Fei alikuwa hataki kukaa kikao na Yanga?
Hilo ni suala la Fei. Yeye ndo anajua la muhimu mwakilishi wake alikuwa yupo tayari kukaa chini haikuwa lazima Fei kuwepo.
Ujue unapoitwa kwenye kikao sometimes hata dau linaweza kuwa dogo,mfano Kapteni wa Arsenal,mfungaji bora wa EPL ,aliondoka Arsenal kwa hela ndogo sana Pound mil 25 na alilazimisha kuondoka.
Mkuu, upo sawa. Ila Fei hakutaka kabisa kuonana nao na alikuwa yupo tayari kurudi mtaani. Alichofanywa hatujui, anajua mwenyewe.
 
Sasa akifanya kama rafiki yako FEI. Dube aondoke kambini na akatae majukumu yake ya kucheza just kama alivyofanya Fei, mtafanyaje?
Azam itamshtaki ilipwe fidia. Mbona swali jepesi sana boss?

Yanga wao tulikuwa hatujui hata wanataka nini, mara wampe ofa ya mshahara mpya, mara wamwambie amalizie mkataba, mara waseme timu inayomtaka ije. Mchezaji kakosea taratibu, hayupo kambini, hana nidhamu mnataka nini kutoka kwake zaidi ya fedha au kumshtaki? Mnasema wazi tunataka pesa kiasi hichi uondoke au tunakushtaki. Simple.
 
Sawa hao wawakilishi wake je walikuja au waliomba appointment na Yanga wakakataliwa?
 
Unaonekana sio mtu wa mpira, wewe unazani mpira unaendeshwa kama unavyo endesha biashara zako. Naymer yule ana timu ya watu ipo nyuma yake kila anacho kifanya kaa ukijua kafuata taratibu.
 
Mama Kizimkazi aingilie kati amalize kama alivyomaliza kwa Fei.
 
Sawa hao wawakilishi wake je walikuja au waliomba appointment na Yanga wakakataliwa?
Umesahau mahojiano ya mwakilishi wa Fei na barua alizoandika kuhusu Fei?

Kwa mtazamo wangu, Fei ana jeuri na viongozi wa Yanga wakataka kumuonyesha kuwa wenyewe ni wakubwa sana kumshinda ndo maana lile suala likawa vile.

Fei angeshapotea iwapo raisi asingeingilia maana hiyo kesi huko nje mpaka hukumu itoke huenda kiwango kingesoma -ve na Fei alikuwa yupo tayari sababu ana jeuri.
 
We jamaa usikute ndo FEI kabisa
 
Reactions: Tsh
Sasa barua ndio kukutana? Nilikuwa naomba barua moja wapo na tena intvw aliyo ifanya clouds imemexpose sana Fei na timu yake,sijasikia wakisema kwamba waliomba kukutana na Yanga tena kwa barua rasmi.

Vip wewe kwa mtizamo wako Dube akose timu ya kutoa 750m na amue kususa kama alivyofanya Fei,ina maana Azam watalaumiwa kwa kumkomoa na kushusha kiwango chake? Maana busara za mama kwa Dube hazipo.

So wewe kwa mtizamo wako ni sawa mpira wetu ukaachana na sheria na taratibu na kufuata hekima na busara....... za wanasiasa wenye hadhi kubwa?
 
Ila izo mil 700 za kuvunja mkataba ni za kuchora au? Alijisemea nabiimeja bongo hata mchezaji wa mil 200 hayupo mana hino ela y a kuvunja mkataba wa dube unanunua mtu wa maana kabisa
 
Ndio maisha yalivyo, Yanga Acheni nogwa...

Azam hawana Mpango wa Kumng'ang'ania Dube kama Yanga walivyofanya kwa Fei toto....!
yanga walifanyaje? si walienda hadi kushitaki ili apate haki yake lkn walishindwa? Tff waalijua fika kuwa mwanzo huu sio mwema kwa soka letu ndiio maana mara mbili zote fei anashindwa
 
Kwani dube nae aliwekwa nje na kambi? Scenario mbili tofauti..
 
Taratibu zifatwe, hata kama Azam walikosea mwanzo isiwe sababu ya wao kuhujumiwa. Ili iwe fundisho Azam wakomae nae hadi matakwa ya mkataba yatekelezwe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…