Azam Pesa: Huduma mpya ya kifedha

Azam Pesa: Huduma mpya ya kifedha

Hii huduma ina makato yeyote kwenda kwa Mtandao host?

Mfano Tigo, nikiingia kwenye menu ya AzamPesa watanikata salio?
Hapana. Hakuna gharama yeyote utakayokatwa kwa ku'access' menu ya AzamPesa katika mtandao wowote. Ni bure.
Na je gharama za kutuma na kutoa Pesa zikoje?
Gharama za kutuma na kutoa pesa ni chini kulinganisha huduma nyinginezo za kifedha
Na kitu gani hasa nitanufaika nacho kwenye AzamPesa ambacho kwenye Mpesa sikipati? Hasa kama situmii King'amuzi cha Azam?
Gharama za kutuma na kupokea zipo chini na nafuu kuliko huduma zingine
 
Tofauti ya hii huduma na SARAFU ni nini?
Sarafu ni huduma ya kutuma na kupokea malipo ya huduma na bidhaa.

Sarafu inahitaji kuunganisha account zako za benki na mfumo wa Sarafu. AzamPesa haihitaji taarifa zako za kibenki.

Sarafu inakuhitaji uwe na Application maalum. AzamPesa inahitaji namba yako ya simu pekee na kuunganishwa.

Karibu!.
 
Hapana. Hakuna gharama yeyote utakayokatwa kwa ku'access' menu ya AzamPesa katika mtandao wowote. Ni bure.

Gharama za kutuma na kutoa pesa ni chini kulinganisha huduma nyinginezo za kifedha

Gharama za kutuma na kupokea zipo chini na nafuu kuliko huduma zingine
Weka makato yake tuone apa mfano kutuma laki moja na kutoa wanakata shs ngap?????.......na je tozo za serikali ipo umo kwenye azampesa.

Sent from my SM-A260F using JamiiForums mobile app
 
Kwa mawakala nini wafanye ili waweze kusajiliwa kuwa mawakala wa AZAM PESA?.
Ili kuwa wakala wa AzamPesa, fika katika kibanda cha kusajili wateja wa kawaida wa AzamPesa.

Muombe akuelekeze kwa Wakala Mkuu wa AzamPesa. Ukifika, atakusajili kwanza kama mteja wa kawaida. Kisha atakupa form ya kujaza ukiambatanisha na vifuatavyo:
1. TIN NUMBER
2. LESENI YA BIASHARA
3.KITAMBULISHO CHA NIDA.

Ukishajaza na kusaini kukubaliana na vigezo na masharti, utamuachia Wakala Mkuu.

Naye atazikusanya na kuscan, zitatumwa kwetu. Tutakuandalia TILL number pamoja na vifaa vinginevyo.

Kisha, kumfikishia wakala Mkuu ambaye naye atakupigia simu ukafate documents zako tayari kama Wakala wa kawaida wa AzamPesa.

Karibu.
 
Kingine sio huduma inaanza baada ya muda inapotea tena.

Sent from my SM-A260F using JamiiForums mobile app
Nikuhakikishie;

Ndiyo, huduma huanzishwa ili kuleta tija kwa jamii. Lakini pia, kampuni hujiwekea malengo kupitia utoaji wa huduma hiyo.

Kampuni itakapoona huduma hiyo haina tija na huleta hasara, basi huifunga na kuipotezea.

Lakini, wataalamu na washauri wa 'Bakhresa Group' wameshafanya tafiti na kujihakikishia kuwa AzamPesa italeta mapinduzi katika huduma za kifedha. Hivyo kwa namna yeyote, haitoweza kupotea.

Karibu kuwa mteja wa AzamPesa.
 
Weka makato yake tuone apa mfano kutuma laki moja na kutoa wanakata shs ngap?????.......na je tozo za serikali ipo umo kwenye azampesa.

Sent from my SM-A260F using JamiiForums mobile app
Nitaweka 'sheet' yenye gharama za kutuma na kutoa pesa kwa wateja wa AzamPesa.

Ndiyo, tozo za serikali ni takwa la kisheria. Hivyo AzamPesa haina 'exception' ya kutojumuisha tozo za Kiserikali.
 
Ili kuwa wakala wa AzamPesa, fika katika kibanda cha kusajili wateja wa kawaida wa AzamPesa.

Muombe akuelekeze kwa Wakala Mkuu wa AzamPesa. Ukifika, atakusajili kwanza kama mteja wa kawaida. Kisha atakupa form ya kujaza ukiambatanisha na vifuatavyo:
1. TIN NUMBER
2. LESENI YA BIASHARA
3.KITAMBULISHO CHA NIDA.

Ukishajaza na kusaini kukubaliana na vigezo na masharti, utamuachia Wakala Mkuu.

Naye atazikusanya na kuscan, zitatumwa kwetu. Tutakuandalia TILL number pamoja na vifaa vinginevyo.

Kisha, kumfikishia wakala Mkuu ambaye naye atakupigia simu ukafate documents zako tayari kama Wakala wa kawaida wa AzamPesa.

Karibu.
1.kuna mawakala wengine wapo mikoani tena vijijini mfano wakala yupo matombo morogoro vijijini.
2.kuna wakala ana namba ya nida ila kitambulisho bado hajapata.

Sent from my SM-A260F using JamiiForums mobile app
 
Nitaweka 'sheet' yenye gharama za kutuma na kutoa pesa kwa wateja wa AzamPesa.

Ndiyo, tozo za serikali ni takwa la kisheria. Hivyo AzamPesa haina 'exception' ya kutojumuisha tozo za Kiserikali.
Pia unaweza kutuma pesa kwenda mtandao washindani????......mfano kutuma pesa kutoka azampesa kwenda Tigo pesa au airtel money

Sent from my SM-A260F using JamiiForums mobile app
 
Kampuni kubwa na iliyoenea katika nchi ya Tanzania pamoja na nchi jirani 'Bakhresa Group' imeleta sokoni huduma mpya ya kifedha ijulikanayo kama 'Azam Pesa'.

Huduma hii ni kama zilivyo huduma nyinginezo za M-Pesa, Airtel Money, Tigo Pesa and the like.

Ili kuielewa zaidi huduma hii, nitaenda katika mtindo wa Maswali na kisha majibu.

Je, Azam wameanzisha mtandao wao wa simu?
Hapana. Azam bado hawajaanzisha mtandao wao kama zilivyo kampuni kadhaa za mawasiliano hapa nchini.

Bali AzamPesa wameingia makubaliano na baadhi ya mitandao kwa ajili ya kuwezesha upatikanaji wa huduma kupitia line za mitandao hiyo.

Mpaka sasa AzamPesa wameshakubaliana na Tigo, Airtel na Zantel. Hivyo huduma hii inapatikana katika line za mitandao tajwa.

Vodacom, Halotel na mitandao mingine bado wapo kwenye mazungumzo. Watakapokubaliana basi huduma hii itawezeshwa katika line hizo.

Je, huduma hi inahusika
na nini?
Kama ilivyo huduma zingine, huduma hii inahusika na;
1.Kutuma Pesa
2.Kutoa Pesa
3.Kulipia bili
4.Kulipia bidhaa za Azam

Je, huduma hii imeanza kufanya kazi?
Ndiyo, huduma hii imeshaanza kufanya kazi kwa wateja wote waliosajiliwa.

Je, najiungaje na huduma hii?
Fika katika duka la wakala na uweze kusajiliwa. Kinachohitajika ni namba yako ya simu pamoja na namba yako ya NIDA. Ndani ya dakika mbili tayari utakuwa umeshasajiliwa kuwa mteja wa AzamPesa.

Je, huduma naweza kupata vifurushi 'bundles' maalum vya Azam?
Hapana. Kama ambavyo nilijwishaeleza hapo juu kwamba Azam bado hawajaanzisha mtandao wao hivyo swala la vifurushi linabakia kuwa maamuzi ya mtandao husika.

Je, huduma hii naipata wapi?
Huduma hii inapatikana katika mikoa yote Tanzania. Ijapokuwa bado haijatapakaa kila mahali lakini upatikanaji wake katika maeneo mengi ya miji ni uhakika.

Je, menu 'ussd' ya AzamPesa ni ngapi?
Baada ya kusajiliwa, utabadili namba ya siri. Hivyo utabonyeza *150*08# na kuweza kupata huduma ya AzamPesa.

Kama una swali lolote kuhusiana na huduma za AzamPesa, basi karibu.

Wasalaam.
Kwa style hii mtawapata wachache sana.maswali ni mengi kuliko majibu.kuna faida/uzuri gani wa kujiunga na hiyo azampesa badala ya kutumia tigo pesa ya kawaida? Au hii ni sawa na Nala ile yule mtoto wa Fenandes?

Maswali ni mengi mkuu
 
Back
Top Bottom