Taarifa zilizotangazwa jana katika kikao cha ndani ya management hasa kitengo cha sports ni kuwa Azam haitarusha mechi hata moja ya ligi kuu baada ya Vodacom kutoendelea na udhamini kisha kuchukuliwa na wauza pombe TBL ambapo Policy ya Azam ni kutorusha aina yoyote ya pombe.
pia kikao hicho kimetoa pendekezo la kuiondoa timu ya Azam katika ligi hiyo.
Pole wenye vingamuzi vya azam
View attachment 811392
[HASHTAG]#OFFICIAL[/HASHTAG]
KAMPUNI ya Azam TV imesema kwamba itaendedelea kuuheshimu na kuutekeleza mkataba wa kuonyesha mechi za Ligi Kuu ya Bara kulingana na mabukubaliano yao na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).
>>Katika mahojiano maalum leo, Mkurugenzi wa Azam TV, Yussuf Bakhresa amesema kwamba wataendelea kuonyesha mechi za Ligi Kuu chini ya udhamini wa kampuni yoyote kulingana na makubaliano yao na TFF.
“Jukumu letu ni kuonyesha mechi za Ligi Kuu, hilo tutaendelea kulitekeleza kama ambavyo tumekuwa tukifanya miaka yote. Na zaidi ninachoweza kusema ni kwamba watazamaji wetu watarajie mambo mazuri zaidi,”amesema Bakhresa akizungumza kwa simu kutoka Dubai jioni hii.
>>Bakhresa amesema kwamba wamekuwa wakipokea maoni mbalimbali kutoka kwa wadau juu ya mapungufu kadhaa katika uonyeshaji wa mechi za Ligi Kuu na nyingine nyingi na wakati wote wamekuwa wakiyafanyia kazi.
“Hadi sasa tunaridhishwa na kiwango chetu, lakini tumekuwa tukipokea maoni juu ya mapungufu madogo madogo na tumekuwa tukiyafanyia kazi. Na tutaendelea kuyafanyia kazi kwa lengo la kuhakikisha tunawafikishia watazamaji wetu matangazo bora kabisa,”.
Katika hatua nyingine, Bakhresa pia amesema kwamba wamefurahishwa na mafanikio ya klabu ya Azam FC inayoshiriki Ligi Kuu ya Bara kwa kutwaa ubingwa wa Kombe la Kagame kwa mara ya pili mfululizo.
>>Bakhresa amesema kwamba hayo ni matunda ya uwekezaji wao mzuri katika timu, lakini pia kushiriki Ligi Kuu nzuri yenye ushindani. “Azam FC itakuwa na maandalizi mazuri kabla ya msimu mpya wa Ligi Kuu, lengo ni kuhakikisha inafanya vizuri na kutwaa ubingwa kwa mara ya pili mfululizo,”amesema Bakhresa.
*PotiphaJonathan*