Azam TV Limited yaingia mkataba wa kuonesha Matangazo ya Ligi Kuu kwa miaka 10. Mshindi misimu mitatu ijayo kulamba bonus Tsh 500m

Hizo billion 200+ azam wana uwezo wa kurecover ndani ya miezi miwili hadi mitatu, baaada ya hapo wataendelea kupiga tu hadi 2032.

Waliotia hii saini wachunguzwe na takukuru
Hii ni tender yeye kashinda na hakuna kampuni yoyote TZ wakushindana na Azam na league yetu washukuru walichopata tusianze kujiona kama tumekuwa EPL na zaidi hakuna kampuni inaingia mkataba kwenda kupata hasara lengo ni faida kamtoe Azam halafu tuone wakuja nani TBC, hao hata mechi za nje tu ZBC wanawashinda.
 
Heshima kwako mkuu kwa data.

Hata tukienda na hiyo 1.1m na tua assume azam pekee ana 500k na kati ya hao 500k ni 300k tu ndio wanaolipia soka...bado azam anapata faida na hili deal linatakiwa kupunguzwa urefu maana linaua ubunifu na kuongezeka masirahi ndani ya muda mfupi....
 
Commercials ...
 
Pamoja na hesabu nzuri, kuna haja ya kurekebisha takwimu.
View attachment 1797134
Japokuwa takwimu ni za Desemba 2020 bdo kuweka makadirio ya ving'amuzi 1,000,000 ni makisio makubwa sana.

Ni kweli mkuu...lakini hujajiuliza growth rate ya soko la ving'amuzi vya azam itakayokuwa influenced na uoneshaji wa soka....na hiyo growth rate ni dynamic as it changes yearly, umewaza hicho?

Point yetu ni kuwa..kwa namna moja ama nyingineaazam anapata faida ndio maana hata kaamua kuwekeza, lakini pia anapata/atapata faida kubwa kuliko thamani ya mkataba..ni either mkataba ufupishwe au thamani yake iongezwe.
 
Mkuu hii point yako itengeneze vizuri then tuma kwenye ma group ya whatsap na kule instagram ili kila mtu ajue kiundani sio kupiga makofi huku tukinyonywa.

Sent from my SM-A260F using JamiiForums mobile app
Hii ni tender sio uteuzi tu wao wametoa offer hiyo wameshinda hii league iko hivi leo sababu ya Azam wame ibrand walikuwa wapi kabla ya Azam? Leo hii Azam ukimtoa biashara yake haiwezi kufa labda faida yake itapungua lakini VPL nani atakayewapa pesa hiyo? Bidding hakuna mjadala umetangaza tender anayeshinda ku meet vigezo anapewa. Azam anahitaji VPL na VPL wanahitaji Azam. Faida ni dhumuni la biashara hilo na ujue kuna operating cost pia hapo faida sio dhambi.
 
Ishu inakuja wamekaa na vilabu kukubaliana huo mkataba?
 
Pamoja na maelezo yako je nini maana ya tender? kuna tender unaweka kiwango au unaweka masharti ya mtu kupeleka tender ikubaliwe iwe commercial na technical wao wameshinda kama ni close tender hakuna mjadala fair masuala ya faida hayawahusu TFF hayo ni ya Azam maana ukitaka kujuwa faida na je wakijakusema tumepata hasara. Bidding ni fair process haina mjadala hayo ya tender miaka 10 au 3 au sijui 5 ni ya TFF sio Azam.
 
Hesabu nzuri, lkn tujiulize kuna media nyingine imeshindana na Azam? Ambacho sikubaliani nacho ni huo mkataba wa miaka 10. Ni muda mrefu sana.

Vv
 
Waoneshe epl
 
Kila nikikusoma napata shida AZAM wame offer kiwango hicho kama wao sasa labda ungejiuliza wa pili katoa offer ngapi? hapo ndio tungelinganisha wao kama kampuni nia yao kufanya biashara kutengeneza faida sio kutoa sadaka kwa vilabu vya Tanzania hii ni biashara. Point yako ya miaka 5 au sijui ifupishwe sawa ila hiyo sio kazi ya Azam ni TFF wametoa tender na masharti yake ndio maana Azam kaja na hiyo number ingekuwa TFF wamtoa tender ya miaka 5 Azam angekuja na number nyingine kabisa sio kiwango hichi. Hatujawa EPL sisi kugombaniwa hii ni league ya hapa Bongo na uwekezaji wa mwanzo ni mkubwa kama vifaa sasa hakuna mtu mpya atakuja kusema anunue vifaa vyote aanze upya kwa kutegemea VPL na mkataba wa miaka 5 hakuna. Azam kaanza taratibu nafikia watu wote Tanzania wamekuwa number one bidhaa wanaweza kuifikisha kwa ufasaha. Mo kanunua team nzima maisha kwa Billion 20 watu kimyaa. Hi ndio thamani ya Simba na kwa Tanzania ni Simba na Yanga tu. Umekuja na malalamiko lakini hakuna solution zaidi ya kusema thamani iongezwe hii ni Tender kashinda muhimu kuangalia nani wa pili na kiasi gani katoa offer kama yupo. Vunja bei alitoa sijui Billion 2 kashinda na Simba walisema wapili alikuwa chini sana sasa atakuja mtu atasema Vunja bei atauza sana jezi billion 2 ndogo atapata faida kubwa, yes yeye anatafuta faida sasa kusema Azam atafaidikia sana ndio na lengo lao kufaidikia wewe kakupa chako ulichoridhia mwenyewe na kutangaza. Sioni point katika hili unless uje uniambie mchakato haukuwa wa Tender hapo nitakubaliana na wewe.
 

kwanza nawapa hongera azam lakini pia mpaka sasa mwenye vifaa bora vya kuonyesha mechi za bongo kiukweli ni azam, hata star times walijaribu lakini walishindwa! tuseme ni mwanzo mzuri, najua yapo maoni mengi ila tuwape mda
 
nimekupata mkuu..kiukweli sitaki kuzungumzia kama tender ilitangazwa ama la maana sijui kama ilitangazwa..sina coment kwenye swala la tender mkuu.
 

point nzuri, voda wenyewe wanatoa mil 80 kwa mwaka
 
Hizo billion 200+ azam wana uwezo wa kurecover ndani ya miezi miwili hadi mitatu, baaada ya hapo wataendelea kupiga tu hadi 2032.

Waliotia hii saini wachunguzwe na takukuru

bil 200+ kwa mda gan eti πŸ˜‚ πŸ˜‚ πŸ˜‚ πŸ˜‚ πŸ˜‚
 
Bado demand ya timu ni kubwa kuliko uwekezaj wa Azam. Kwa miaka 3 ijayo hiyo 500ml haitakuw naa thaman kubwa kam ilivo sasaiv.

Cha kufanya ili kuokoa soka la bongo Kampuni zenye uwezo (AZAM MO GSM) zingekaa chini na TFF kuona ni namna gani wanawezi saidia vilabu vidogo. Just imagine nafasi ya 5 atapokea 65ml haitoshi hata kwa nauli ya msimu mzma.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…