Bi zandile
JF-Expert Member
- Sep 12, 2024
- 301
- 856
Kaka zangu chukueni hii....
Unapozama kwenye himaya ya mwanamke, ukiibuka pale lazima kuna kitu unaondoka nacho.
Waweza kuchukua baraka au mikosi na nuksi kwa huyo mwanamke.
Kuna mwanamke, mke mwema aliyeandaliwa na Mungu mwenyewe kwa ajili yako, huyo mke mwema ukizama kwake tu unajikuta unafanikiwa na vitu vinatembea na kusonga mbele.
Kuna mwanamke mwingine hakuandaliwa kwa ajili yako ukizama tu kwake kwa tamaa zako za kimwili kisha ukaanzisha naye mahusiano ya kimapenzi utajikuta umepigwa pin ghafla vitu vinaanza kukwama, kila kitu kinavurugika.
Umepewa mke mwema halafu hutulii kwa mkeo, kila siku unahangaika na wanawake ambao hawakuandaliwa na Mungu kwa ajili yako. Kwa nini kujiangamiza?
Hebu tulia na mkeo uliyepewa na Mungu, acha kuonja onja wanawake wa wengine, kumbuka sex ni jambo la kiroho sana, ikiwalala hao wasio wako basi unakuwa umeunganishwa na roho chafu ambapo zitakuandama daima, na hayo maangamizi yanakuwa ni yako peke yako.
Kisima cha MKEO ndiyo kisima cha baraka zote kwako, umheshimu mkeo na utabarikiwa. .
Kwa wale ambao hamjaoa tumieni akili zenu vizuri kwa kujiepusha na uzinzi, oeni mtulie na wake zenu.
Mit 6:32
Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa; Afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake.
Unapozama kwenye himaya ya mwanamke, ukiibuka pale lazima kuna kitu unaondoka nacho.
Waweza kuchukua baraka au mikosi na nuksi kwa huyo mwanamke.
Kuna mwanamke, mke mwema aliyeandaliwa na Mungu mwenyewe kwa ajili yako, huyo mke mwema ukizama kwake tu unajikuta unafanikiwa na vitu vinatembea na kusonga mbele.
Kuna mwanamke mwingine hakuandaliwa kwa ajili yako ukizama tu kwake kwa tamaa zako za kimwili kisha ukaanzisha naye mahusiano ya kimapenzi utajikuta umepigwa pin ghafla vitu vinaanza kukwama, kila kitu kinavurugika.
Umepewa mke mwema halafu hutulii kwa mkeo, kila siku unahangaika na wanawake ambao hawakuandaliwa na Mungu kwa ajili yako. Kwa nini kujiangamiza?
Hebu tulia na mkeo uliyepewa na Mungu, acha kuonja onja wanawake wa wengine, kumbuka sex ni jambo la kiroho sana, ikiwalala hao wasio wako basi unakuwa umeunganishwa na roho chafu ambapo zitakuandama daima, na hayo maangamizi yanakuwa ni yako peke yako.
Kisima cha MKEO ndiyo kisima cha baraka zote kwako, umheshimu mkeo na utabarikiwa. .
Kwa wale ambao hamjaoa tumieni akili zenu vizuri kwa kujiepusha na uzinzi, oeni mtulie na wake zenu.
Mit 6:32
Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa; Afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake.