Aziniye na mwanamke hujiangamiza mwenyewe

Aziniye na mwanamke hujiangamiza mwenyewe

Bi zandile

JF-Expert Member
Joined
Sep 12, 2024
Posts
301
Reaction score
856
Kaka zangu chukueni hii....

Unapozama kwenye himaya ya mwanamke, ukiibuka pale lazima kuna kitu unaondoka nacho.

Waweza kuchukua baraka au mikosi na nuksi kwa huyo mwanamke.

Kuna mwanamke, mke mwema aliyeandaliwa na Mungu mwenyewe kwa ajili yako, huyo mke mwema ukizama kwake tu unajikuta unafanikiwa na vitu vinatembea na kusonga mbele.

Kuna mwanamke mwingine hakuandaliwa kwa ajili yako ukizama tu kwake kwa tamaa zako za kimwili kisha ukaanzisha naye mahusiano ya kimapenzi utajikuta umepigwa pin ghafla vitu vinaanza kukwama, kila kitu kinavurugika.

Umepewa mke mwema halafu hutulii kwa mkeo, kila siku unahangaika na wanawake ambao hawakuandaliwa na Mungu kwa ajili yako. Kwa nini kujiangamiza?

Hebu tulia na mkeo uliyepewa na Mungu, acha kuonja onja wanawake wa wengine, kumbuka sex ni jambo la kiroho sana, ikiwalala hao wasio wako basi unakuwa umeunganishwa na roho chafu ambapo zitakuandama daima, na hayo maangamizi yanakuwa ni yako peke yako.

Kisima cha MKEO ndiyo kisima cha baraka zote kwako, umheshimu mkeo na utabarikiwa. .

Kwa wale ambao hamjaoa tumieni akili zenu vizuri kwa kujiepusha na uzinzi, oeni mtulie na wake zenu.

Mit 6:32
Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa; Afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake.
 
Hivi ni kwanini mnaandikaga ujinga huu?

Dini ndio zinafundisha huu upuuzi?

Kwa mwanamke utajiangamiza kwa factor zifuatazo,

1)Utaanza kuhudumia kwa kutoa pesa hivyo kufilisika.
2)Utakuwa bize na mahusiano na hivyo kupoteza muda mwingi wa kufocus na kufanya kazi.
3)Unaweza kuambukizwa magonjwa, kumaliza pesa kujitibia, au ukapata magonjwa yasiyotibika na hivyo kufa mapema.

Enyi waafrika wenzangu kizazi cha nyoka, hivi ni nani aliewaroga?

Kwa nini mnaamini vitu vya kipuuzi namna hiyo?
 
Kaka zangu chukueni hii....

Unapozama kwenye himaya ya mwanamke, ukiibuka pale lazima kuna kitu unaondoka nacho.

Waweza kuchukua baraka au mikosi na nuksi kwa huyo mwanamke.

Kuna mwanamke, mke mwema aliyeandaliwa na Mungu mwenyewe kwa ajili yako, huyo mke mwema ukizama kwake tu unajikuta unafanikiwa na vitu vinatembea na kusonga mbele.

Kuna mwanamke mwingine hakuandaliwa kwa ajili yako ukizama tu kwake kwa tamaa zako za kimwili kisha ukaanzisha naye mahusiano ya kimapenzi utajikuta umepigwa pin ghafla vitu vinaanza kukwama, kila kitu kinavurugika.

Umepewa mke mwema halafu hutulii kwa mkeo, kila siku unahangaika na wanawake ambao hawakuandaliwa na Mungu kwa ajili yako. Kwa nini kujiangamiza?

Hebu tulia na mkeo uliyepewa na Mungu, acha kuonja onja wanawake wa wengine, kumbuka sex ni jambo la kiroho sana, ikiwalala hao wasio wako basi unakuwa umeunganishwa na roho chafu ambapo zitakuandama daima, na hayo maangamizi yanakuwa ni yako peke yako.

Kisima cha MKEO ndiyo kisima cha baraka zote kwako, umheshimu mkeo na utabarikiwa. .

Kwa wale ambao hamjaoa tumieni akili zenu vizuri kwa kujiepusha na uzinzi, oeni mtulie na wake zenu.

Mit 6:32
Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa; Afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake.
Hivi mzinzi huwa ni mwanaume tu?
 
Hii ina apply tz tuu...ukienda ulaya hukuti hii kitu.
Watu wanazini na wana prosper sasa hapo sijui mtutupa sababu gani mtoa mada
Mtoa mada ana zile imani za kishamba kabisa zilizopitwa na wakati.

Hawa ni watu ambao, chanzo cha maarifa yao ni kanisani ama msikitini tu.

Hawatafuti maarifa nje ya hapo.

Wanacholishwa na wachungaji au mashehe ndio wanameza hicho hicho, na mara nyingi wanalishwa matango pori.

P didy kazini na kila mwanamke maarufu unaemjua, net worthy yake ni 1 bilion USD.


Hizo ni takribani trillioni tatu za kitanzania.

Ukikuta mwanaume mwenye hela hafanyi ngono na watu mbalimbali huyo atakuwa na matatizo ya nguvu za kiume.

Matajiri wanafanya umalaya wa ajabu, na hawajawahi kupata hiyo mikosi anayoisema mtoa mada.
 
Nikajua ni wanaume tu ndo wanaamini kwamba wanawake wana mikosi kumbe hadi nyie wenyewe mnaamini?

Kwa mantiki yako hakuna ndoa ingewahi kuvunjika ndoa, ukioa mambo yako yote yanaenda sawa sio?
Mleta mada kafundishwa hayo kwny dini.

Dini, hasa hasa huu uislamu na ukristo zima zimetungwa na wanaume hivyo zina mfumo dume.

Zinajaribu kumuonea na kumkandamiza mwanamke kwa kila namna.

Wanawake walioko kwny hizo dini wanakaririshwa hayo na wanayaamini.
 
Back
Top Bottom