Aziz Ali wa Gerezani na Mtoni Dar es Salaam

Aziz Ali wa Gerezani na Mtoni Dar es Salaam

Shukrani ya punda ni mateke. FaizaFoxy kasoma nje ya nchi toka shule ya msingi hadi chuo, yote kwa fadhila alizotendewa baba yake na Mwalimu Nyerere, lakini tazama anavyomkejeli Mwalimu humu!
Gagnija:

Kwa hiyo Nyerere aliyesoma kwa fadhila za mkoloni alitakiwa asiwadharau wazungu.

Elimu aliyotoa Nyerere haikuwa na msisimko wowote wa kiakili. Tulifundishwa hili tuamini na sio kuwa na uhuru wa mawazo.

Anyway tuendelee na mjadala
 
Huyo mzee atawadanganya nyie wavivu Wa kusoma na kufanya utafiti.. Cha ajabu hata maneno ya Nyerere anayapinga, wasio husika anaweweka kwenye historia yake.. Wapigania Uhuru wapo kihistoria hadi Uingereza wana tambua kuna hadi wazungu wahindi walisaidia Uhuru hawataji hapa anazumgumzia Aziz Ali ambae hamna kitu Kazi zake za misikiti... Asidamganye watu kitu kuna wajuu zake Aziz tunawafahamu pia.
Mbona hakuna sehemu alipo sema aziz Ali alipigania Uhuru
 
Ili kuleta ushindani tupien hizo zilizobalance tusome jaman, tatizo liko wapi kwan jamni, unajua hapa mleta thread anaizungumzia dar kwa asilimia kubwa, na hiii ikumbukwe ni miji ambayo asilimia kubwa ni waislam.
Basi tutoe aziz ally tuandike Peter ili tubalance, kingine humu wanaobisha zaid ni wale wa mikoani
Gpeg7g0cg34d2eewewd2eeew23rr8ggg
 
Gagnija,
Nimekuta katika maktaba yangu nyumba ya Kleist Sykes aliyojenga
1942 na nyumba hii ikajakuwa kitovu cha harakati za kupinga ukoloni
katika miaka ya 1950s wakati mwanae Abdul alipokuwa anaishi hapo:

2016%2B-%2B1


Hiyo hapo juu kulia katika gazeti ndiyo ilikuwa nyumba ya Abdul Sykes aliyoishi
na Nyerere 1954 nyumba hii ilikuwa Mtaa wa Stanley na Sikukuu.
Ndugu Mohamed Said:

Nadhani watanzania tumenyimwa haki ya elimu ya kufikiri. Tungekuwa na elimu ya kufikiri basi tungeitrndea historia ya nchi yetu haki.

Hapa nina hoja za kuiangalia upya historia ya Tanganyika.

1. Hivi tulikuwa homogeneous kama koloni? Kwa mtazamo wangu hatukuwa homogeneous. Hivyo mitazamo mbalimbali ya kudai haki na uhuru ilikuwepo. Kwanini tuna mtazamo mmoja tu?

2. Hivi kulikuwa hakuna watanzania wenye mwamko kabla ya 1954? Wakati nchi zote za kiafrika zilikuwa kwenye harakati kwanini watanganyika wasubiri mpaka Nyerere arudi?

3. Ukisoma historia ya mwingereza kwenye makoloni, suala la kutoa uhuru lilikuwepo mezani kabla 1954. Haiwezekani watanganyika wachangamke miaka ya 50. Je kulikuwa na maandalizi gani ya kuwapa watanganyika uhuru?

4. Inaonyesha baada ya uhuru mchango wa watanzania wenye uwezo wa kipesa ulifutwa delibarately kwenye historia. Kwa mfano tunaambiwa kuwa wananchi walichanga pesa kumpeleka Nyerere Umoja wa Mataifa. Fununu zilizokuwepo ni kuwa watu wachache walijitolea. Kwanini historia haitaki kukubali mchango huu?
 
Mbona hakuna sehemu alipo sema aziz Ali alipigania Uhuru
Mkuu ungejua ajenda zake ungeelewa... Huyo ni mmoja Wa watu anaotaka kuwaweka katika history ya Uhuru yaani anaanzia kwenye kizazi cha kwanza hadi cha mwisho.
 
Gagnija:

Kwa hiyo Nyerere aliyesoma kwa fadhila za mkoloni alitakiwa asiwadharau wazungu.

Elimu aliyotoa Nyerere haikuwa na msisimko wowote wa kiakili. Tulifundishwa hili tuamini na sio kuwa na uhuru wa mawazo.

Anyway tuendelee na mjadala
Elimu aliyotoa Nyerere haikuwa na msisimko wowote wa kiakili, Kweli?! Mohamed Said ni product ya elimu hiyohiyo, itakuwa matusi kwake kufikiri alitoka pale Mlimani bila uhuru wa mawazo. Sikuwahi kufikiri kuwa haya yangeandikwa na mtu kama wewe.

Fadhila niliyojaribu kueleza kwa baba yake Faiza ni sawa na ile aliyopewa Wasira miaka ya mwanzo ya 80 kwenda kufanya kazi ubalozini DC ili kumpa fursa ya kujiendeleza kielimu. Wasira hakuwa na sifa ya kujiunga na vyuo vya hapa nchini japo alikuwa na kiu ya kujiendeleza kielimu, lakini kwa mfumo wa elimu US, aliweza kusoma na kurudi na Masters Degree. Hapo inahusiana vipi na Nyerere kusomeshwa na wazungu!

Mzindakaya akiwa RC Morogoro aligombana na uongozi wa Mzumbe baada ya kukataliwa kusoma chuoni pale kwa kuwa hakuwa na sifa, bila shaka naye angapata fursa kama ya kina Wasira angetimiza ndoto yake. Pengine utakuwa umenipata nilimaanisha nini.
 
Mkuu ungejua ajenda zake ungeelewa... Huyo ni mmoja Wa watu anaotaka kuwaweka katika history ya Uhuru yaani anaanzia kwenye kizazi cha kwanza hadi cha mwisho.
Duduwasha,
Huna haja ya kunitilia maneno kinywani kwangu.

Hilo la kuwa mimi nina agenda hakika agenda ninayo nayo ilikuwa
ni kusahihisha historia ya TANU.

Hayo mengine usemayo mimi si yangu.

Ila nitakufahamisha kuwa Aziz Ali hakuwa mwanasiasa ingawa
alikuwa rafiki kipenzi na Kleist Sykes na alikuwa hapungui kwake.

Historia hii niliyoandika mimi binafsi imeninyanyua sana kabisa.
Kitabu kimependwa sana kinakwenda sasa toleo la nne.

Si hivyo tu kutokana na kitabu hicho nimealikwa vyuo kadhaa Afrika,
Ulaya na Marekani kuzungumza.

Halikadhalika kitabu kufanyiwa pitio na mabingwa wa African History.
Juu ya haya kitabu hiki kimevuruga akili wengi sana.

Prof. Haroub Othman alikuwa mwalimu wangu lakini akili ilimruka
aliposoma historia ya Abdul Sykes na kuasisiwa kwa TANU kiasi
alitaka kusikia kauli ya Mwalimu Nyerere mwenyewe achilia mbali kuwa
alinihoji na kisha kwenda kwa Ahmed Rashad Ali kupata ukweli zaidi.

Mohamed Said: Ahmed Rashad Ali Bingwa wa Propaganda za Ukombozi wa Afrika Sehemu ya Tatu

Kwa hiyo utaiona kuwa wewe si mtu wa kwanza kuchomwa na historia hii
na hautakuwa wa mwisho.

Kila siku hapa JF akinisoma mtu kwa mara ya kwanza lazima atapigwa na
mshangao na mnakasha utaanza upya.

Nimeweka rekodi hapa JF ya kufanya mjadala kwa takriban miezi sita.
Unaweza kuingia hapa ujionee mwenyewe vipi mjadala ulivyokuwa moto:
Historia ya Uhuru isimuliwavyo na Mohammed Said yakosolewa

Wote hao wamelikimbia jamvi wameniacha sasa niko pweke natoa darsa
kwa mtu mmoja mmoja kama wewe.

Duduwasha,
Ungependa kusikia nini likitokea baada ya Abdul Sykes na nduguye Ally
kufutwa katika historia ya TANU?
 
Elimu aliyotoa Nyerere haikuwa na msisimko wowote wa kiakili, Kweli?! Mohamed Said ni product ya elimu hiyohiyo, itakuwa matusi kwake kufikiri alitoka pale Mlimani bila uhuru wa mawazo. Sikuwahi kufikiri kuwa haya yangeandikwa na mtu kama wewe.

Fadhila niliyojaribu kueleza kwa baba yake Faiza ni sawa na ile aliyopewa Wasira miaka ya mwanzo ya 80 kwenda kufanya kazi ubalozini DC ili kumpa fursa ya kujiendeleza kielimu. Wasira hakuwa na sifa ya kujiunga na vyuo vya hapa nchini japo alikuwa na kiu ya kujiendeleza kielimu, lakini kwa mfumo wa elimu US, aliweza kusoma na kurudi na Masters Degree. Hapo inahusiana vipi na Nyerere kusomeshwa na wazungu!

Mzindakaya akiwa RC Morogoro aligombana na uongozi wa Mzumbe baada ya kukataliwa kusoma chuoni pale kwa kuwa hakuwa na sifa, bila shaka naye angapata fursa kama ya kina Wasira angetimiza ndoto yake. Pengine utakuwa umenipata nilimaanisha nini.
Nyerere hakutoa elimu. Serikali ya Tanzania ilitoa elimu. Nyerere alikuwa mfanyakazi na alichofanya ilikuwa ni job description yake kama rais.

Nyerere alikwenda kusoma wakati wa mkoloni. Kwa mfano uliotoa, basi tuseme Nyerere kasoma kwa fadhila za Gavana.

Kilichompeleka Wassira au babake Faiza ubalozi ni job description na wasifu wa kazi. Hiyo sio fadhila.

Anyway sitaki kutibua mjadala uliokuwepo. Hila kwa kifupi Nyerere hakujenga mfumo mzuri wa elimu. Unaweza kukubali au kukataa.
 
Nyerere hakutoa elimu. Serikali ya Tanzania ilitoa elimu. Nyerere alikuwa mfanyakazi na alichofanya ilikuwa ni job description yake kama rais.

Nyerere alikwenda kusoma wakati wa mkoloni. Kwa mfano uliotoa, basi tuseme Nyerere kasoma kwa fadhila za Gavana.

Kilichompeleka Wassira au babake Faiza ubalozi ni job description na wasifu wa kazi. Hiyo sio fadhila.

Anyway sitaki kutibua mjadala uliokuwepo. Hila kwa kifupi Nyerere hakujenga mfumo mzuri wa elimu. Unaweza kukubali au kukataa.
Zakumi,
Naona ukumbi umekuwa kimya.

Ndivyo tunavyoanza kwanza kwa vishindo na mie kushambuliwa na kuitwa
muongo, mdini na kila aina ya tuhuma na wakati mwingine matusi.

Duduwasha alidhani kuwa mimi natania katika historia hii sina ninalolijua.

Nimemuekea mengi ya ushahidi wa nyaraka, picha na historia yangu binafsi
nikilelewa katika mitaa ya Gerezani.

Duduwasha amekuwa kimya na namuuliza je angependa tuendelee na mjadala?
Hadi sasa hajanijibu yuko kimya.

Kimya kimetawala jamvi letu.
Wastawishaji baraza wote wameondoka wameniacha peke yangu jamvini.

Wanamajlis,
Nanyi hamna la kusema?
Tuufunge mjadala?
 
nashukuru sana mzee mohammad said ...nipo nyuma yako kuweza kusoma kazii zako hizi vizuri ...leo naomba niulizee kuhusu mapinduzii ya kumpindua nyerere .maana nilisoma pinduzi moja ambalo aliliandaa BIBI TITI MOHAMMAD so lakini yapo mapinduzi yaliyofail kama sita hivii ..lakini sijapata kuyafahamu sawa sawa .a hata waliofanya plani hizo hawapo katika vitabu vyako mfano COMMANDO TAMIMU ...nk vip hayaaa mapinduzii ..
 
Mkuu Mzee Mohamed Said, nakushuru sana kwa link hizi, na Darsa zako ambazo ni nadra kujulikana na Historians wengi kuhusu Tanganyika na wazee wetu mbalimbali waliotangulia ambao wameshiriki mapambano ya ukomboz kuifanya Tanganyika Huru na hatimae baadae Tanzania hii. Kiukweli Eneo la kuanzia shule ya Uhuru ilipo leo hadi Kariakoo yote, Upanga na Kisutu tunayoyaona leo yalikua na mitaa na nyumba ambazo kama tungeweza tungeyaacha kwa ajili ya Kumbukumbu, lakini ndo hivyo, mengi yameshavunjwa.
 
Mkuu Mzee Mohamed Said, nakushuru sana kwa link hizi, na Darsa zako ambazo ni nadra kujulikana na Historians wengi kuhusu Tanganyika na wazee wetu mbalimbali waliotangulia ambao wameshiriki mapambano ya ukomboz kuifanya Tanganyika Huru na hatimae baadae Tanzania hii. Kiukweli Eneo la kuanzia shule ya Uhuru ilipo leo hadi Kariakoo yote, Upanga na Kisutu tunayoyaona leo yalikua na mitaa na nyumba ambazo kama tungeweza tungeyaacha kwa ajili ya Kumbukumbu, lakini ndo hivyo, mengi yameshavunjwa.
Lipyoto,
Ahsante ndugu yangu.
 
nashukuru sana mzee mohammad said ...nipo nyuma yako kuweza kusoma kazii zako hizi vizuri ...leo naomba niulizee kuhusu mapinduzii ya kumpindua nyerere .maana nilisoma pinduzi moja ambalo aliliandaa BIBI TITI MOHAMMAD so lakini yapo mapinduzi yaliyofail kama sita hivii ..lakini sijapata kuyafahamu sawa sawa .a hata waliofanya plani hizo hawapo katika vitabu vyako mfano COMMANDO TAMIMU ...nk vip hayaaa mapinduzii ..
Al Sady...
Sina historia ya Bibi Titi katika ile kesi ya uhaini zaidi ya hayo ambayo
sote tumeyasoma.

Halikadhalika na ile kesi ya akina Tamimu na wenzake.
 
Al Sady...
Sina historia ya Bibi Titi katika ile kesi ya uhaini zaidi ya hayo ambayo
sote tumeyasoma.

Halikadhalika na ile kesi ya akina Tamimu na wenzake.
Wanamajlis,
Hebu jibuni swali langu kwanza.

Duduwasha nimemuuliza kama angependa nieleze nini kilitokea baada
ya Abdul Sykes kufutwa katika historia ya TANU.

Duduwasha yuko kimya.
Nyie mnasemaje?
 
shekh wangu mohamed Said mi hua nakufuatilia kimya kimya saana kwa zaidi ya miaka mi5 hapa jf, wewe ni mtu jasiri na msema ukweli na uhakika utaishi miaka mimgi sana saana katika fikra na akili zetu wengi baada ya kifo cha mwili wako mimi kwa heshima na taadhima nakuomba uendelee kutupa darsa hilo.
 
mzee wa porojo at work
Mtanganyika...
Mie sikujaaliwa na Mungu kuwa mtu wa ''porojo.''

Sijapata kuandika ''abstact,'' kwenye mkutano wowote ule wanapoalika
watu kuandika, ''paper,'' nikaacha kuitwa.

Ningependa kama ningekuwa na kipaji hiki cha porojo na uchekeshaji
lakini Allah hakunijaalia.

Inawezekana ni ujinga wako tu, au kibri, au kukosa adabu au hasad
na mfano wa hayo ndiko kunakokupelea kujaribu kuvunja heshima za
watu.

Aliyekutangulia nimemuandikia maneno hayo hapo chini ikiwa yalikupita
hebu yasome:

Duduwasha,
Ingelikuwa mimi naandika uongo nisingechukua muda ningekuwa nimeshafutwa
katika duru hizi za utafiti na uandishi wa historia ya Tanganyika.

Nakuwekea barabara niliyotembea:
  1. PUBLICATIONS/RESEARCH PAPERS/ARTICLES
  2. The Life and Times of Abdulwahid Sykes 1924 –1968 The Untold Story of the Muslim Struggle against British Colonialism in Tanganyika, Minerva Press London, 1998 translated into Kiswahili as Maisha na Nyakati za Abdulwahid Sykes 1924-1968 Historia Iliyofichwa Kuhusu Harakati za Waislam Dhidi ya Ukoloni wa Waingereza, Phoenix Publishers, Nairobi, 2002.
  3. The Torch on Kilimanjaro, Oxford University Press, Nairobi, 2006
  4. Contributing author for an African anthology: The Mermaid of Msambweni and Other Stories, Oxford University Press 2007, Nairobi.
  5. Contributing author Dictionary of African Biography (DAB), Oxford University Press 2011, New York.
  6. Uchaguzi wa Busara, Abantu Publications 2008, Dar es Salaam.
  7. In Praise of Ancestors (1987) Africa Events (London).
  8. Abdulwahid Sykes: Founder of Political Movement (1988) Africa Events (London).
  9. Islam and Politics in Tanzania (1989) Al Haq International (Karachi)
  10. The Plight of Tanzanian Muslim (1993) Change (Dar es Salaam).
  11. Tanzania - The "Secular" Unsecular State (1995) Change (Dar es Salaam).
  12. The Question of Muslim Stagnation in Education in Tanzania - A Muslim Riddle (Paper presented at the Conference of the Global World of the Swahili Intercultural Dialogue on the Indian Ocean Zanzibar, February 20 - 23, 2003).
  13. Islamic Education and Intellectualism in Eastern Africa ‘Themes from the Pulpit in Tanganyika (Tanzania Mainland) 1800 – 2000’ (Paper presented at International Symposium on Islamic Civilisation in Eastern Africa Kampala, Uganda organised by the Islamic Conference Research Centre for Islamic History, Art and Culture (IRCICA), Istanbul and the Islamic University in Uganda, Mbale December 15th – 17th 2003).
  14. Sheikh Hassan bin Ameir - The Moving Spirit of Muslim Emancipation in Tanganyika (1950 – 1968) (Paper presented at Youth Camp Organised by Zanzibar University, World Assembly of Muslim Youth (WAMY) and Tanzania Muslim Students Association (TAMSA) 27th February – 4th March 2004).
  15. Islamic Movement and the Christian Lobby in Tanzania - the Experience of the late Prof. Kighoma Ali Malima (1938 – 1995) (Paper Presented to Tanzania Muslim Students Association (TAMSA) Sokoine University of Agriculture (SUA) Morogoro 11th April 2004).
  16. Terrorism in East Africa the Tanzanian Experience (Paper Presented at the Conference on Islam, Terrorism and African Development University of Ibadan, Nigeria 8th - 10th February 2006).
  17. Al Marhum Sheikh Kassim bin Juma bin Khamis (1940 – 1994) and the Pork Riots of 1993. (Paper Presented at the Regional Conference on Islam in Eastern Africa: Islam Encounter with the Challenges of the 21st Century 1st - 3rd August 2006, Kenyatta University, Nairobi.
  18. Muslim Bible Scholars of Tanzania – The Legacy of Sheikh Ahmed Deedat (1918 – 2005) Paper Presented at the International Symposium on Islamic Civilisation in Southern Africa Organised by The Organisation of Islamic Conference Research Centre for Islamic History, Art and Culture (IRCICA) The National AWQAF Foundation of South Africa AWQAF SA 1 – 3 September 2006 University of Johannesburg.
  19. Tanzania: A Nation Without Heroes Seminar Organised by IFRA French Institute for Research in Africa and BIEA British Institute in East Africa 23rd and 24th September 2013 at IFRA Nairobi.
  20. Awards: Several Awards.
  21. Visiting Scholar: (2011)
  22. University of Iowa, Iowa City, USA
  23. Northwestern University, Chicago, Illinois, USA
  24. Zentrum Moderner Orient (ZMO), Berlin, Germany.
Duduwasha,
Unadhani hao hapo juu ni watu wa kufanyiwa mzaha?
Ungependa nikuhitimishie nini kilitokea baada ya historia ya kweli kukataliwa?

Mtanganyika...
Bado una fikra kuwa mimi ni mpiga filimbi wa Hamelin?
Unadhani mimi niko hapa JF kufanya mchezo?

Unataka mjadala na tujadili katika njia za kistaarabu.
La ikiwa historia hii inakuumiza hakuna anaekulazimisha kusoma.

Usije hapa kwa nia ya kutukana.
Huo si uungwana.

Kama ulivyoniiita mzee kwa hakika umri umekwenda basi nipe
heshima yangu ya uzee.
 
mzee mohammad usifee moyo hao vijana waachee wapigee kelele hao ndioo wanaoendelea kufichwaa hadii leo hawatakii kubadilikaa na kuwa wadomi pia huendaa level zao za kielimu ni ndogo unapowatajia hizo harakati xako ulizopita huko vyuoni dunia kote Hawajui thamani yake na hawajui maana yake ....HAO SIO WASOME WENYE UPEO TUWAACHEE TU
 
  1. PUBLICATIONS/RESEARCH PAPERS/ARTICLES
  2. Al Marhum Sheikh Kassim bin Juma bin Khamis (1940 – 1994) and the Pork Riots of 1993. (Paper Presented at the Regional Conference on Islam in Eastern Africa: Islam Encounter with the Challenges of the 21st Century 1st - 3rd August 2006, Kenyatta University, Nairobi.
Unataka mjadala na tujadili katika njia za kistaarabu.
La ikiwa historia hii inakuumiza hakuna anaekulazimisha kusoma.

Usije hapa kwa nia ya kutukana.
Huo si uungwana.

Kama ulivyoniiita mzee kwa hakika umri umekwenda basi nipe
heshima yangu ya uzee.
Naomba nikurejeshe nyuma kidogo. Sikujua kama Sheikh Kassim alikufa akiwa na umri mdogo hivyo (54). Kwa faida ya wanajamvi, na pia kuitendea haki historia, waweza kutujuza nini chanzo cha kifo chake?!
 
Back
Top Bottom