Aziz Ali wa Gerezani na Mtoni Dar es Salaam

Aziz Ali wa Gerezani na Mtoni Dar es Salaam

Wanamajlis,
Katika mambo yanayonishangaza katika historia ya TANU kama nilivyoiandika ni jinsi inavyopandisha ghadhabu kwa baadhi ya watu.

Nimeeleza hapo juu chanzo cha khitilafu katika kuandika historia ya TANU.
Kiasi nahisi imewatisha baadhi yetu.
 
Duduwasha,
Sioni tena lile bandiko lako la matusi.
Ikiwa umelifuta basi umefanya jambo jema.

Ahsante sana.
 
Umedandi ukuni usioujua sasa unakuunguza hujui hata nini kinazungumziwa nadhani hata Mada pia hujui inahusu nini! Ukishikwa na uharo nenda washroom maana umeleta kichefuchefu... Me sijawahi jiuma nasimia hoja moja kwanza... Watu Wa aina yako huwa wanafail sana maisha
Hii ni open forum kila member anachangia,hakuna anayedandia hapa,kifupi huna la maana lolote unalochangia hapa zaidi ya kupost maneno machafu ambayo ndio maisha yako, siku nyingine unapokua hujui jambo ni bora ukapita kimya tu kuliko ulivyojiaibisha kwenye hii mada kwa kujionyesha wazi kabisa kua Kichwani u mweupe na huna ujualo!
 
Duduwasha,
Nakuwekea hapo chini niliyoandika katika kitabu cha Abdul Sykes ili uone
chanzo cha matatizo ya historia ya TANU:

''Kwa mara ya kwanza historia ya TANU ilitaka kuandikwa na Abdulwahid
mwenyewe.

Baada ya kupatikana kwa uhuru mwaka 1961 na TANU ilipokuwa sasa
inataka kujiimarisha kama chama cha umma, inasemekana Nyerere wakati
ule Waziri Mkuu alimuomba Abdulwahid aandike historia ya harakati ya
Waafrika wa Tanganyika dhidi ya ukoloni wa Waingereza.

Hii kwa hakika ndiyo historia ya TANU.

Dr Wilbert Kleruu ambae ndiyo kwanza alikuwa ametoka masomoni Amerika
alichaguliwa na TANU asaidiane na Abdulwahid katika utafiti na uandishi wa
historia ile.

Abdulwahid alirudi kwenye ofisi za TANU makao makuu; kwenye ofisi yake
ya zamani aliyokuwa akiitumia kama rais wa TAA.

Nyaraka zake binafsi, za baba yake nyingine kuanzia mwaka wa 1929 wakati
wa enzi za African Association zililetwa pale kwa utafiti kama ushahidi wa yale
yaliyopitika zama hizo.

Maelezo ya Abdulwahid katika kuanzishwa kwa African Association bila ya
kutegemea inasemekana hayakumpendeza Nyerere, kwa kuwa mwanzo wa
harakati dhidi ya ukoloni jinala baba yake Abdulwahid, Mzee Kleist Sykes,
lilikuwa likitawala.

Halikadhalika ilipofika kueleza namna TAA ilivyokujabadilishwa kuwa TANU
watotowake wote watatu - Abdulwahid, Ally na Abbas wakiongozwa na
kaka yao mkubwaAbdulwahid wakawa wanatawala harakati zile.

Historia hii inasemekana haikumpendeza Nyerere na baadhi ya viongozi
wa TANU.

Haukupita muda Abdulwahid akatambua kuwa viongozi wapya walioshika
nafasikatika TANU kwa kweli hawakuwa na nia hasa ya kutafiti na kuandika
historia yaTanganyika bali nia na azma yao ilikuwa na kumjenga Nyerere
na kumkuza kwa sifa ambazo hazikumstahili.

Abdulwahid alipong’amua hili haraka akajitoa katika kazi ile.

Hata hivyo Dr. Kleruu aliendelea na utafiti na akaandika historia ya TANU.

Historia hii inasemekana ilifuta mchango wa akina Sykes na wazalendo
wengine katika kuunda African Association na baadae kuasisi TANU.

Hata hivyo baada ya kazi hii kukamilika haikuchapishwa na ikabaki katika
maktabaya TANU, Mtaa wa Lumumba, Dar es Salaam.

Lakini baadae kazi ile ilitoweka na ikachapishwa baada ya ‘’mwandishi,’’
kufanya mabadiko kadhaa katika mswada ule ili usitambulike chanzo chake.

Hata hivyo TANU iligundua kuwa ile ilikuwa historia yao iliyoandikwa na Dr.
Kleruu
na wakafanya bidii kuzuia isichapishwe.

Kimya kimya TANU ikafanya juhudi ya kuzuia kitabu hicho kisitoke toleo la
pili.

Lakini hili halikuwezekana na kitabu hicho kimechapishwa sasa mara kadhaa.

Uandishi wa kitabu kile haukutofautiana sana na kitabu cha TANU kilichotoka
mwaka 1981 kilichoandikwa na Chuo cha TANU cha Kivukoni.''

Duduwasha,
Nakuomba ruksa nisimame hapa kisha In Shaa Allah tutaendelea na mkasa
huu wa kuandika historia ya TANU.

Sasa ukisema kuwa kulikuwa na wazee wakati ikiandikwa historia ya TANU
na wakaikubali historia iliyoandikwa ni muhimu pia ukajua hao waz ni wazee
gani.

Nakueleza haya kwa kuwa hao wazee ninaowajua mie waliokuwa katika
Baraza la TANU walipigwa marufuku kufika Ofisi ya TANU na Baraza la
Wazee wa TANU likavunjwa kwa kushutumiwa kuchanganya dini na siasa.

Haya yalitokea mwaka wa 1963.

Wakati huo mwenyekiti wa Baraza hilo alikuwa Mzee Idd Tulio aliyechukua
uongozi mwaka wa 1958 baada ya Sheikh Suleiman Takadir aliyekuwa
mwenyekiti wa Baraza la Wazee kufukuzwa chama baada ya ugpmvi na
Mwalimu Nyerere kuhusu Kura Tatu.

Huu ni muhtasari tu.
Yako mengi.
Mkuu wangu Mohamed, unavyoandika, you sound like Nyerere hakutaka mchango wa hawa aliowakuta wakiongoza TAA kabla yake utambulike. Ukiisikiliza hotuba ya Nyerere kwa wale aliowaita wazee wa Dar es salaam wakati anaaga baada ya kuchaguliwa Mwinyi, inafuta kabisa mengi unayoyaandika.

Kuna kitu hujakiweka wazi.
 
Mohamed Said, historia zako nzuri sana tatizo haziko balanced zimeegemea sana kuonyesha ni waislam tu waliopigania uhuru wa Tanganyika kitu ambacho ni uongo! Angalizo: mimi ni muislamu..jitahidi kua fair kidogo ili hizi historia ziwe zimebalance na sio kuvutia upande mmoja tu. Thanks.
..Mi nadhani hapa amemzungumzia zaidi Aziz Ally...na sykes. Kupogania uhuru ni sehemu mambo waliyofanya...hakuna udini hapo
 
Hahaaaa ahsante ingawa hujajibu swali langu!

Majina yote yana asili ya Uingereza, nashangaa anaposema aliletwa na Wajerumani kupigana na Wareno - binafsi sijawahi kusikia kwamba wajerumani waliwahi kupigana na Wareno, ninacho fahamu ni kuhusu wanajeshi kutoka Africa kusini chini ya General Jan Smuts walisaidiana na wanajeshi wa Uingereza nafikiri na Wabelijiji kumung'oa Mjerumani kutoka kuloni lake la Tanganyika.
 
Unataka nikupe story wakati history za Uhuru Wa aina zote upo shuleni mkuu rudi shule tena kama ulipitwa.. Huyu Mo yeye anachotaka zaidi ni kipotosha na kuchomeka uislam zaidi uonekane ndio uliyafuta Uhuru wa Tanganyika... Kuna yaliyo sawa kutoka shule ila wengine wasiohusika kisa tu walikiwepo na ni Muslim basi anataka waingizwe kwenye history.. Kuna sie mababu zetu walikuwa ni Machifu na wapipambana na kupigania himaya zao na historia tushafuatilia kidogo lakini hatuwezi wekwa kivile kwani Uhuru ulipatikana kiakiri zaidi ya nguvu tofauti na plan za mababu zetu...Akili za Nyerere ndizo zilileta Uhuru na sio hiyo miuza kahawa na pesa zilitumika kugharamia ni za John Rupia. Pia. Kina kambona n.k sio hao makachara mifukoni vumbi tupu
..Una kashfa sana mzee...punguza chuki ya dhahiri.Hata ww nadhani hujaelewa huyu mzee mo anazungumzia nini...mimi kwa uelewa wangu kazungumzia umaarufu,kazi,sehemu(daresalaam).na shida kwako ni dini hakuna kingine mkuu si ndiyo??kwa hiyo ulitaka aziz ally awe mkatoliki kama wewe na mimi ndio uwe positive na hii historia...Aziz hakuwa mwanasiasa alikuwa mfanyabiashara (contractor) na ndivyo alivyoandika mwandishi kwa hiyo yeye kusaidia sehemu ya uhuru kwa harakati za daresalaam haikuwa issue kubwa mpaka awekwe kwenye historia...ukisema hivyo kwamba wapigania uhuru wapo wameandikwa kwenye vitabu unatoka nje ya historia hii.unachofanya ni kumshambulia makusudi mzee mo.said na hupendi kusikia waislamu wamefanya kitu kizuri...ndivyo nilivyokuelewa samahani japo ndiyo ukweli...By the way mimi ni mkatoliki naitwa Franklin.....
 
lete na historia ya vituo hivi,kwa matias,kwa mfipa,kwa ali maua,kwa mtogole.
 
Aziz ali mtu,mdigo mtu wa Moa kwa wadigo ndo wa kwanza kumilik gari Africa
 
..Mi nadhani hapa amemzungumzia zaidi Aziz Ally...na sykes. Kupogania uhuru ni sehemu mambo waliyofanya...hakuna udini hapo

Well said mkuu, Moh anazungumza aliyo yaona na kusikia - mambo mengi/harakati zilianzia hapa Dar kila mtu analijua hilo sasa kama Watanganyika majasiri wakati huo majority walikuwa ni Waislaam, je, mnataka hilo lisisemwe - mbona baadae walikuja wakristo na wapagani mfano: Paul Rupia, Dk.Mtahangarwa, Dk.Kyaruzi nk.

Haya mambo ya kumkandia Moh. eti yuko biased binafsi nashindwa kuelewa hoja za namna hiyo - tatizo kubwa hapa watu wengi utamani Nyerere ndiye ahusishwe kwa kila kitu - wakati yeye alikaribishwa tu na kukriminiwa na Waislaam, waislaam hao hao ndiyo walipedekeza Nyerere aingoze Chama kutokana na Usomi wake, lakini hilo halina maana kwamba wapigania uhuru wengi wa wakati huo walikuwa wasomi sana au nini sijui, waislaam wengeweza kudai uhuru wa Tanganyika bila ya kumshirikisha Nyerere. Haya mambo ya kuchukulia mtu mmoja kama Alpha na Omega hayafahi hata kidogo, kuna,watu wengi tu wakichangia sana katika harakati za kudai uhuru lakini awatajwi kwenye vitabu vya historia ya Taifa letu na ukichunguza sana utakuta ni wale waliopishana kiswahili na Nyerere! Sikatai Nyerere alijitahidi sana pamoja na wenzake kutufikisha tulipo kitu kilicho kuwa kinanishangaza katika mojawapo ya hulka yake ni kuendekeza vinyongo - sikumbuki kama aliwahi kuhudhulia mazishi ya wanaharakati wenzake mfano: Prof. Abdallahaman Babu, Zuberi Mtemvu, Kasela Bantu, Oscar Kambona, Bibi Titi na wengine wengi tu - kitu hiki kilinishangaza sana.
 
Mkuu wangu Mohamed, unavyoandika, you sound like Nyerere hakutaka mchango wa hawa aliowakuta wakiongoza TAA kabla yake utambulike. Ukiisikiliza hotuba ya Nyerere kwa wale aliowaita wazee wa Dar es salaam wakati anaaga baada ya kuchaguliwa Mwinyi, inafuta kabisa mengi unayoyaandika.

Kuna kitu hujakiweka wazi.
Gagnija,
Kitu gani sitaki weka wazi?
Niulize na ikiwa ninalo jibu nitaliweka hapa jamvini.
 
..Mi nadhani hapa amemzungumzia zaidi Aziz Ally...na sykes. Kupogania uhuru ni sehemu mambo waliyofanya...hakuna udini hapo
Tonic Jr,
Mimi naandika yale niyajuayo.
Ikiwa wewe unaona ipo kasoro basi rekebisha.

Hapa ni mahali sote tunasomeshana.
 
Majina yote yana asili ya Uingereza, nashangaa anaposema aliletwa na Wajerumani kupigana na Wareno - binafsi sijawahi kusikia kwamba wajerumani waliwahi kupigana na Wareno, ninacho fahamu ni kuhusu wanajeshi kutoka Africa kusini chini ya General Jan Smuts walisaidiana na wanajeshi wa Uingereza nafikiri na Wabelijiji kumung'oa Mjerumani kutoka kuloni lake la Tanganyika.
Bukyanagandi,
Nilichosema ni Wazulu walipigana na Wareno Mozambique.

Rudia kusoma upya tafadhali.
 
Well said mkuu, Moh anazungumza aliyo yaona na kusikia - mambo mengi/harakati zilianzia hapa Dar kila mtu analijua hilo sasa kama Watanganyika majasiri wakati huo majority walikuwa ni Waislaam, je, mnataka hilo lisisemwe - mbona baadae walikuja wakristo na wapagani mfano: Paul Rupia, Dk.Mtahangarwa, Dk.Kyaruzi nk.

Haya mambo ya kumkandia Moh. eti yuko biased binafsi nashindwa kuelewa hoja za namna hiyo - tatizo kubwa hapa watu wengi utamani Nyerere ndiye ahusishwe kwa kila kitu - wakati yeye alikaribishwa tu na kukriminiwa na Waislaam, waislaam hao hao ndiyo walipedekeza Nyerere aingoze Chama kutokana na Usomi wake, lakini hilo halina maana kwamba wapigania uhuru wengi wa wakati huo walikuwa wasomi sana au nini sijui, waislaam wengeweza kudai uhuru wa Tanganyika bila ya kumshirikisha Nyerere. Haya mambo ya kuchukulia mtu mmoja kama Alpha na Omega hayafahi hata kidogo, kuna,watu wengi tu wakichangia sana katika harakati za kudai uhuru lakini awatajwi kwenye vitabu vya historia ya Taifa letu na ukichunguza sana utakuta ni wale waliopishana kiswahili na Nyerere! Sikatai Nyerere alijitahidi sana pamoja na wenzake kutufikisha tulipo kitu kilicho kuwa kinanishangaza katika mojawapo ya hulka yake ni kuendekeza vinyongo - sikumbuki kama aliwahi kuhudhulia mazishi ya wanaharakati wenzake mfano: Prof. Abdallahaman Babu, Zuberi Mtemvu, Kasela Bantu, Oscar Kambona, Bibi Titi na wengine wengi tu - kitu hiki kilinishangaza sana.
..Watanzania siyo watu tunaopenda kutafuta ,kupokea ,kukubali na kurudisha kitu kama kilivyo..lazima kisemwe kipitishwe ktk dini,kiletwe kwenye kanda na makabila yake na ndipo upatikane ubaya wa kusemana lakini siyo kufumbua au kuelimishana...hii historia ya huyu mzee ni sahihi...uislam ilikuwa ni lazima uwe na nguvu maeneo(daresalaam) ambayo ameyazungumzia mzee Mo na ndiyo makazi ya kina Aziz..watu wanataka wasikie historia wanavyopenda wao ziwe kwa sababu wanaamini wao ni bora kuliko wengine au wao wanastahili yote hayo..wanasahau kwama siku zote ukitaka kwenda mbali lazima uambatane na mwenzako lakini ukitaka kwenda haraka nenda peke yako...Uhuru haikuwa safari fupi wala ya haraka Uamue uende peke yako.....ni safari ya muungano wa watu na mawazo yao na uwezo wao maana safari haikuwa fupi
 
Tonic Jr,
Mimi naandika yale niyajuayo.
Ikiwa wewe unaona ipo kasoro basi rekebisha.

Hapa ni mahali sote tunasomeshana.
..Mzee hiyo quote yangu napingana na wanaosema umeongelea udini.isome vizuri
 
Hawaweki historia hii kwenye vitabu, sababu ya kuhofia udini mtajua asili ya nchi yenu, imetokana na dini gani ndo maana wakawaachia nyerere, nyerere ni MTU mdogo sana kwenye Uhuru wa Tanzania, yaani tukiwafufua wazee Leo watalia kuona nyerere mnamuita baba wa taifa, ni hayo tu
 
Mkuu wangu Mohamed, unavyoandika, you sound like Nyerere hakutaka mchango wa hawa aliowakuta wakiongoza TAA kabla yake utambulike. Ukiisikiliza hotuba ya Nyerere kwa wale aliowaita wazee wa Dar es salaam wakati anaaga baada ya kuchaguliwa Mwinyi, inafuta kabisa mengi unayoyaandika.

Kuna kitu hujakiweka wazi.
Gagnija,
Ile hotuba ya Mwalimu Nyerere anaaga na kuwataja wazee wa Dar es Salaam
kila ninapoisikia hunijaza simanzi nyingi sana.

Nasikitika kwa kuwa wale wazee wote wana majina yao na kila mmoja wao
alikuwa na mchango wake katika kupigania uhuru.

Iweje hakuweza kuwataja kwa majina yao angalau wawili watatu hivi?

_F7Oz52i1_JqWSbrtBuf8AWfGPo-JKIpScb0EwoJzrPeXXBJZWVjS6TAJsZtF8zwBpgdDehwmocpxP-M8IT8fgBXlW82agpWvNuKOCq7fmcbnicSqPgaIQU_80A2JEbmYv_3CyZBaYZuYXMB6uxo4sVONHdbKOx8LIw9XdUCGUB2DtRZ_OuIebwGGbffixm4BLGsfNHdTm794nCmOz03kQTt91us-xMfLlaRKdXg3hFlY_4gA5Bs_JANtsF24Vo-vEfu6CgZIiC8oy1k03lpUD2t--7AwKyDoXhrJt1lUm2x4bZxUxdSiniNCI6h3HRwaB2AMQzckHzEb04-um2NOWQxIUZr6z0hRn9kQjuG_-r3hUMFmEpMKf23YnyH8Fur0cxXrHAhYaI-u4Rtla9Tbm2DfW072MnKO4JEA75DolrPiU2rsqZZOWWukn52hHjWPxFustTCiPra7aNNx2kBt6i3s_tcBVoThvJ35URfPJPEx8x23rv_jQzTD2mWP28zTQj2YRd_w8rOPk3X0OwguJenNws4I1w5KhXTWSOlwdFOFcDe3x6s8nqlbB1mhFjkhFH_DfnGrq9eI6FLA-RNPWR3ed7x7zZ7oudoAchVA5UljU-lcC-Pdw=w519-h692-no
 
Back
Top Bottom