Baada tu ya Kuisikia hii Nukuu ya Rais ya Radio One Leo, kuanzia sasa sina Lawama na Mtu nitamsubiria huyo wa Kumrithi 2030

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
"Kila Matokeo ya Mitihani yakitoka Wizara ya Elimu akina Mkenda huniletea Vitabu vikubwa pamoja na Flash hivyo nikiiweka tu katika Computer yangu Kwanza huanza Kuangalia Kwetu Mkoani Kusini Unguja kisha nikiona huwa nasema Mama yangu ni nini hiki? Yaani Mkoa anaotoka Rais ndiyo unaongoza kila mara kwa kufanya vibaya katika Mitihani nchi nzima? Sasa nimewaagiza tuanze kulifanyia Kazi ili Kuuinua huu Mkoa na Kuondoa Aibu hii" amesema Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan.

Chanzo: Nukuu ya Rais ya Redio One Leo.

Leo nimeyakumbuka maneno na Mafundisho ya Mhadhiri wangu Kipenzi wa Somo la Print Media, Critical and Logical Reasoning SAUT Mwanza 'Genius' Fr. Bishop. Dk. Bernadine F. Mfumbusa ( anayehudumu Kondoa kwa sasa ) tulipokuwa Darasani aliwahi kutuambia kuwa kabla ya kuanza Kumchambua Mtu Kimantiki ili tusisumbuke nae au asitupotezee sana muda tuanze Kuifuatilia Historia yake ya Kimaisha, Elimu na Uelewa ili tuweze kupata Hitimisho sahihi juu yake.

Hivyo nami GENTAMYCINE baada ya Leo kuisikia hii Nukuu Natangaza rasmi Kustaafu Kumjadili Mtu kwani nimegundua kuwa kumbe nilikuwa namuonea Mtu bure na tena huenda napaswa hata Kumuomba Radhi kwani kama tu Mkoa wake Umetukuka kwa kuwa Kinara wa Matokeo mabaya Tanzania nzima Mimi ni nani nimlaumu wakati nimeshajua Chanzo cha Tatizo ni nini?

Ngoja nami sasa nijiandae Kisaikolojia kuwa Mvumllivu kwa Tanzania ya 2021 hadi 2025 na ile ijayo ya 2025 hadi 2030.
 
Wembe ni ule ule USHINDI...

Chato na Geita wana shule nzuri toka kwa Museveni, walitoa wanafunzi bora, shule bora... kanda ya ziwa ilifana kuanzia kule serengeti kwenye zile shule pacha kahama kwenye kwema shools na ile nyingine mpaka huko kagera kwenye shule pacha za kaizirege na wababe wengine wabobezi wa elimu huko kagera pamoja na shule za katoliki za st. peter clvrs...

Unguja wana kuja sasa... pemba tume anza tuna tawi la chuo cha ustawi kama sijakosea... hivyo mambo mazuri yana kuja, tuna tawanya maendeleo ktk nyanja zote kielimu, sanaa, utamaduni, mazingira, uchumi nk...

Tuendelee kuunga juhudi maana asali bado ipo ya kutosha, na kila mtu atakula kwa urefu wa kamba kama lisu, mbowe, mdee na wengine...
 
Kuna methali nyingi za uongo... Mojawapo ni hii...

"Samaki mmoja akioza, ni wote"
 
Darasani kuna mwalimu mmoja anawafundisha wanafunzi wengi kwa wakati mmoja na kwa mfumo mmoja lakini kuna watakaofaulu na kufeli.
Hii haina maana kuwa kuna waliopendelewa zaidi ya wengine.
 
Mtu anaweza kufanikiwa zaidi bila kujali katoka kwenye changamoto gani, tabia za jamii ya mtu haziwezi kumzuia mtu kufanikiwa kama akiamua kupambana, kwahiyo hoja haina ulazima kwa kila mtu au watu
 
Hapo tujiandae kusikia ufaulu kupanda maeneo ya visiwani.

Ufaulu umepanda kwa asilimia nne nukta sita.

Kwa maigizo hawajambo hawa.
 
Shida ya maneno kama haya mwisho wake ni kuanza kuzipendelea shule za huko kama ilivyokuwa Chato. Mitihani ijayo tutaanza kuona vinara wanatoka Zanzibar na Pemba sasa, wabongo wanajua sana kucheza na saikolojia ya kiongozi ili mambo yaende
 
Kanda ya ziwa inajulikana yote hadi kagera wako vizuri,mpendelee au msipendelee.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…