Baada ya Hayati Magufuli kuombewa Chato, Mwanza nao wanaandaa maombi, binafsi naona haya yanayofanyika baada ya Chato yako kimkakati

Kwa hiyo "Walokole" wote tayari wapo mbinguni?

Haya ni maajabu!
 
Hili gazeti lako halina point
 
Aombewe kwa lipi??wanafiki tuh hawana lolote na udini wao,if they real love him like the way they pretend it to be waende kwa Gwajima wakaongee nae AMFUFUE ILI ARUDI NA KAZI IENDELEE..
Mbona una hasira sana na kwa Taarifa Yako ataombewa katika Parokia zote Tanzania Hadi Zanzibar
 
Mimi naamini wewe chiembe ndiye mwenye agenda hii maana umeileta taarifa hiyo humu kuipigia promo.
 
MRUMI anazingatia MAOKOTO,lazima watu wapeleke tozo na kodi kwa MRUMI siku hiyo.
Habari za maombi ya kupunguziwa adhabu hizo ni nadharia tu wala hazina uhalisia hata kidogo.
 
Walio hai wanajua watakufa, lakini wafu hawajui neno lolote, waache wamepata jambo lakuwapotezea muda😚😚😚
 
Hivi ni kwa mujibu wa dhehebu lako mnavyoyafahamu na kuyafafanua maandiko matakatifu, Roho wa Mungu tunayeamini ndiye mwalimu mwenye kuongoza na "msemesha ndimi" za kanisa, anao utajiri makubwa wa karama, anampa huyu utambuzi na kumfumbia mwingine, yote ni kwa sifa na utukufu wa Mungu, kabla ya madhehebu yenu, kanisa katoliki lipo likifafanua maandiko kwa maongozi ya Roho wa Milele, kwa mamlaka yake kanisa linatumia vyanzo 3 vya ualimu wake, navyo ni 1. Biblia takatifu (holy scriptures) 2. Mapokeo hai (holy traditions) 3. Mamlaka funzi (magisterium). Mambo haya matatu yanatumika kwa pamoja kufafanua na kufundisha jambo moja pasipo kupingana, hivyo kila andiko ktk biblia linafundishwa kadiri ya mapokeo ya kale ya kanisa na mamlaka fundishi za kanisa linavyolipokea kupitia mababa watakatifu, makardinali na maaskofu wanavyoangaziwa na Roho wa Mungu. Kwa mfano, jambo la vitabu vya biblia takatifu, wakatoliki wanatumia biblia ya vitabu 72 tofauti na madhehebu mengine yanayotumia biblia ya vitabu 66, walioamua kupunguza vitabu 6 walikua na sababu zao na kanisa haliendeshwi kwa kusikiliza wapinzani wake wanasema nini, linamsikiliza Mungu, hivyo likaendelea na mambo yake, kwa upungufu huo wa vitabu kadhaa ktk biblia yenu, kuna taarifa nyingi mnazokosa na hivyo hatuwezi kuelewa kanisa linalofundisha kwa biblia yenye taarifa nyingi zaidi ya mlizokuwa nazo. Uhalali wa kanisa kutumia mapokeo yake upo hata ktk biblia mliyokua nayo ninyi, itoshe kusema kati ya mwaka 295BK biblia ilipoanza kutumia ktk kanisa wakati huo likiwa kanisa moja tu katoliki la mitume, Mwenyezi Mungu amefunua na kufundisha mambo mengi kwa njia zake ktk kanisa ambayo hayakuwa yameandikwa, kuna nyakati watakatifu walioko mbinguni wametokea ktk kanisa na kuleta jumbe za Mwenyezi Mungu akitaka jumbe hizo zitambulike kama "kweli za kiimani" na zishikwe na wafuasi wa "Mwanae mpenzi" pia kanisa ktk ukulu wa kiti cha Petro mtume, linapotimiza wajibu wake wa kufundisha Imani, maadili na ibada, linaelekeza historia ya wanadamu kadiri ya nyakati walizopo, mafundisho ya kanisa kipindi cha zama za utumwa na ukoloni ni tofauti na sasa kwenye zama za ubeberu, sayansi na teknolojia, haya yote ni kazi ya Roho mtakatifu, tajiri wa nyakati zote, kila siku anao ujumbe mpya kwa ajili yako ya leo na kesho pia atakua na lingine kwa ajili yako kama utamsikiliza na kumpa muda akufundishe, anafanya hivyo kwa kanisa, taifa na jamii inayompa nafasi alifundishe. Je, unampa Roho mtakatifu nafasi ktk maisha yako? Je, familia yako? Jamii? Kanisa lako? Kama kweli, basi lazima utakua unashuhudia surprise nyingi kutoka kwake, akikuelekeza jinsi ya kumjua, kumpenda na kumtumikia Mwenyezi Mungu ili mwisho mwishoni uweze kufika kwake mbinguni.
Nimefurahi kupata fursa hii kuandika kitu kuhusu Imani kuu hata hivyo yako mengi, karibu kanisa lenye misingi ya mitume, iliyotabiriwa kuwa misingi ya ulimwengu huu itapambana nayo lakini haitalishinda, mfano swali la kuombea marehemu, kwetu hata mtoto wangu wa miaka saba anayefuata mafundisho ya komunyo yakwanza analifahamu na kulieleza kinaga ubaga, wakati huko kwenu hata mchungaji mwenye PhD ya teolojia hajui chochote, hivyo ndivyo anavyoshangaza Roho mtakatifu ktk maweza yake.
Barikiwa.
 
Mbona una hasira sana na kwa Taarifa Yako ataombewa katika Parokia zote Tanzania Hadi Zanzibar
Sasa me nakushauri jambo la maana unakataa kama zuzu,mwiteni Askofu Gwajima amfufue hamtaki,Sasa hata mkikomaa kumuombea ndo Nini,atarudi huyo kwani?

Mtaomba hadi mjinyee,harudi Ng'oo?!?..
 
Hata aombewe wapi!! Kama hamta sema nanibali mpiga Lissu risasi na kuwapoteza kina Ben, basi hatakaa aione pepo. Atakuwa kuni maisha yake yote huko ahera
 
Hata aombewe wapi!! Kama hamta sema nanibali mpiga Lissu risasi na kuwapoteza kina Ben, basi hatakaa aione pepo. Atakuwa kuni maisha yake yote huko ahera
Itakuwa jamaa wanajua ndio maana wamegauza kanisa kuwa taasisi ya kufanyia laundering criminals (kutakatisha wahalifu)
 
ulitakiwa kuandika kwa kuweka aya, huo ndio uandishi wa wasomi. najua wewe ni msomi, na ninakuheshimu kwa hilo.

tukija kwenye hoja, Kama uliwahi kusoma Biblia hata mara moja tu, utakubaliana na mimi kwamba kanisa lako katoliki linapingana na wokovu aliouleta Yesu Kristo, na karama zote za Roho Mtakatifu. In fact, kanisa lako linamkataa Roho Mtakatifu, kwasababu hata ujazo wa Roho Mtakatifu ambao kanisa la kwanza (kitabu cha matendo) waliishi, ninyi mnakataa na hakuna yeyote kanisani mwenu hadi makao makuu vatican wanakoataka kuruhusu ushoga, ambao wanajazwa Roho Mtakatifu, hivyo usimsingizie Roho kwamba mnaye au kwamba anawaongoza.
Nitakufafanulia machache halafu ujiulize mwenyewe na ukasaidiane na wenzako wasomi kujibu.

1. Kanisa la kwanza, lile la mitume, hawajawahi kuomba kwa bikira maria, never, ila ninyi je?

2. Kanisa la kwanza walihubiri watu waokoke kwa kumwamini Yesu Kristo, na wajazwe Roho Mtakatifu, je, nini mnahubiri watu waokoke? mbona mnasema kunena kwa lugha ambako ndio kujazwa Roho haitakiwi? mbona hata karismatic wanaojaribu kupambania wokovu mnawafukuza na kuwatenga?

3. Kanisa la kwanza, hawajawahi kuomba kwa wafu, waliomba kwa Jina la Yesu Kristo, ninyi mnaomba kwa wafu, hata juzi mliomba kwa magufuli na mlimwombea.

4. Kanisa lq kwanza liliamini mtu anatakiwa kuokoka na kuacha dhambi, baada ya kifo ni hukumu na mtu anapokufa anaenda na matendo yake, ninyi mnaamini mtu akifa padre anaweza kumwombea msamaha kwa Mungu akasamehewa. hii ni ajabu kabisa. Kitabu cha Ufunuo anasema "Heri wafu wafao katika Bwana, maana matendo yao wataenda nayo", pia Waebrania inasema, kama mtu alivyoandikiwa kufa mara moja na baada ya kifo ni hukumu. ninyi mmebadilisha kwamba mtu akifa maiti inaweza kuombewa ikasamehewa, inasamehewa ikiwa imetubu lini sasa? enyi vipofu.

5. Kanisa la kwanza liliamini matendo ya miujiza. ni kweli siku hizi kuna manabii wa uongo wengi wanafanya miujiza feki. lakini hiyo haizuii au haimaanishi miujiza halisi haipo. Ninyi, hata ukiita askofu wenu hakuna mwenye uwezo kukemea hata pepo tu, hayupo. mioyoni mwenu kuna Mungu kweli? Yesu alisema pozeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo...Pia Yesu alisema, enendeni ulimwenguni mwote mkaihubiri injili, aaminiye na kubatizwa ataokoka, asiyeamini atahukumiwa, na ishara hizi zitaambatana na wote waaminio, kwajina langu watatoa pepo, watasema kwa lugha mpya...., ninyi hamtaki kusema kwa lugha ya Roho, na hamtoi hata pepo kilema tu hamuwezi.

6. Kanisa la kwanza, au nisema Yesu alisema tukaihubiri injili, aaminiye na kubatizwa ataokoka. hakuna mtume au yeyote kwenye kitabu cha matendo aliyebatiza watoto wadogo, kwasababu hawawezi kuamini, ila wale wenye akili wanaoamini kwanza, na kubatizwa hao ndio wanaookoka. ninyi mnabatiza watoto wadogo, ambao hawajaamini, na hata kuokoka kwenyewe ambako Yesu alisema "ataokoka" mnakupinga. ajabu sana.

kwa hayo machache, jitafakari kama kanisa lenu hili ndilo lile lile la mitume au la. Warumi 1:26 inapinga kabisa ushoga na ufiraji, ila mnakijua mnachokifanya vatican sasaivi. okokeni muikimbie hukumu ya Mungu iliyo mbele yenu. ajabu yake ni kwamba, ninyi wenyewe mnajua fika mioyoni mwenu kwamba hamna Mungu, mnaabudu tu dini na mapokeo ya dini yenu, ila mna uhakika kabisa mioyoni mwenu kwamba hakuna Roho wala chochote cha kimungu. na wengi wa waumin iwenu wapo hapo ili wazikwe na kuombewa msamaha wakifa wakiamini kwamba wakiwa maiti watasamehewa, na huo ndio uongo mkubwa sana shetani ameuweka na unapoteza wengi jehanum.
 
Kwa hiyo "Walokole" wote tayari wapo mbinguni?

Haya ni maajabu!
pambania roho yako, siwezi kusema wote wapo, ila walau wote waliowahi kuokoka walipata nafasi ya kumjua Mungu, wengine wamemuacha wakiwa humohumo, na wengine wameendelea na Mungu hadi mwisho. haya madhehebu unayoyaona, ni taratibu za wanadamu tu, kinachomata ni kama dhehebu hilo lina misingi ya Kibiblia inayoweza kumwongoza mtu amtafute Mungu na kumwona? hapo ndipo pa muhimu sana kuelewa.

sasa kwa mfano, Yesu Kristo alisema, nitawatumia msaidizi,Roho Mtakatifu kwasababu peke yenu hamuwezi lolote. kwenye Mathayo 28 alisema na ishara hizi zitaambatana na wale waaminio, kwa JIna langu watatoa pepo, watasema kwa lugha mpya (lugha ya Roho yaani kunena kwa lugha), sasa ukiona kuna kanisa halina misingi ya kumpata Roho mtakatifu na wanapinga udhihirisho wa kunena ambao hata Yesu aliusema, jua hilo kanisa haliwezi kumfundisha mtu akapata Roho kwasababu wanampinga Roho. hivyo halitamsaidia hata akisali hapo.

na lile linalofundisha na kuhamasisha Roho (mfano tu), hao watasaidia watu kulingana na misingi yao, wampate Roho, na ukiwa na Roho wa Mungu wewe ndio mwana wa Mungu. imeandikwa walakini awaye yote asipokuwa na huyo Roho, huyo sio wake. hivyo ninyi nyote msio kuwa na Roho, sio watu wa Mungu.

misingi ya dhehebu ni muhimu sana, kwasababu ndio misingi inayoweza kumsadia mtu kwneye harakati za kutafuta uso wa Mungu.

kitu kingine, Yesu alisema ombeni kwa Jina langu, dhehebu lignine linaomba kwa maria na wafu, unategemea nini hapo?

Biblia inasema baada ya kifo ni hukumu (hakuna msamaha ukiwa umekufa) dhehebu la katoliki linaombea maiti asamehewe, kitu ambacho hata kwenye Biblia hakipo, unategemea nini? na Ufunuo anasema heri wafu wafao katika BWana maana matendo yao yaambatana nao, yaani ukifa, umeondoka na matendo yako utaenda kuhukumiwa nayo. naamini kama Mungu angeamua kwamba mapadre wawaombee maiti wasamehewe dhambi (badala ya mtu mwenyewe kutubu kabla ya kufa) basi, makanisa yangejaa majeneza na mochwari zingejengwa makanisani ili maiti ziombewe zisiende motoni.kitu cha ajabu kabisa hiki. shitukeni, mbona jambo hili lipo wazi sana? hata mtu wa kawaida mbona inaonyesha kabisa mmepotea? kweli muombee maiti isamehewe kweli? kwahiyo mtu asitubu ili akifa ninyi mmtubie kwa Mungu, mbona ajabu hii?
 
Biblia haijaandika kila kitu. Usikremu.
kwahiyo vingine kama hivyo vya kuomba kwa bikira maria badala ya JIna la Yesu, na hiyo kuombea wafu wasamehewe dhambi, hata ikitoka kwa shetani fresh tu, kwasababu Biblia haikuandika kila kitu?
 
ndugu, hakuna dhehebu la matendo ya mitume,nilivyoandika hivi nilidhani pengine ungekuwa uliwahi kusoma icho kitabu cha matendo.naona wewe bado. kwa kifupi, baada ya Yesu kupaa, kanisa ndio lilianza siku ile ya pentecost baada ya Roho kushuka wakiwa gorofani, watu 120, ndani yake walikuwepo mitume 12 na wanafunzi wengine wa Yesu. hao ndio walianzisha kanisa, na hilo ndilo kanisa la mitume la kwanza. walihubiri wakafika hadi ANTIOKIA kule Uturuki watu wakawaita "hao ni wakristo" yaani watu wa Kristo, wanaoamin Yesu Kristo, na neno MKristo ndio likaanzia hapo. sasa mitume wale wa Yesu yale yaliyotendeka yameandikwa kitabu cha matendo yaliyo mengi, ndio maana nilirefer icho kitabu. na harakati zao zote za imani, hazifanani kabisa na kanisa lako katoliki. sina chuki na kanisa ila najaribu kuwafumbua macho, kwasababu hata nikiwa na chuki,nitawafanya nini? nanawa tu mikono, wale waliookoka wameshaona utofauti na wamemwona Mungu, wewe ni hiari yako kuendelea kuabudu dhehebu na mapokeo ya wanadamu badala ya kuokoka na kumwabudu Mungu.
 
Mamamaee unateseka ukiwa wapi goroko wewe
ungeliokoka usingenitukana hivyo kwa kutetea tu dhehebu linaloongozwa na mtu anayesapoti ushoga pale vatican. ndio maana tunasema muokoke. dhehebu haliokoi mtu, ila wokovu katika Yesu Kristo ambao mnaukataa.
 
Walokole wajuaji sana, wakatoliki kufanya mambo yao unawaita wapinga Kristo..

Wewe haya mamlaka ya kuhukumu wengine ulipewa na biblia ipi? tuwekee hilo andiko hapa.

Muachage ujinga.
sasa, kama Biblia haielekezi watu waombee wafu, wawatubie dhambi wafu, au waombe kwa maria bali wanatakiwa kuomba kwa kupitia JIna la Yesu tu, na kanisa lako linafanya hayo kinyume na Biblia, na liko mbioni kuhalalisha ushoga, unataka tuseme ni kanisa la Kristo au la mpinga kristo? be fair.
 
We nae na huo ulokole wako!! Usilazimishe watu kuokoka Kila mtu aamini anachoamini
Yesu alitaka muokoke, ama la mtaenda motoni. wewe unasema nisilazimishe? ni kweli silazimishi, ni hiari yako, ila kuambiwa utaambiwa tu upende usipende.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…