Baada ya kampuni ya michezo ya kubahatisha ya Betika kunipatia pesa zangu nilizokuwa nikilalamikia kutopewa, sasa kwa hiari yangu ninafuta malalamiko

Baada ya kampuni ya michezo ya kubahatisha ya Betika kunipatia pesa zangu nilizokuwa nikilalamikia kutopewa, sasa kwa hiari yangu ninafuta malalamiko

Wakusoma 12

JF-Expert Member
Joined
Jul 3, 2017
Posts
4,035
Reaction score
11,462
Wakuu heshima kwenu, ni dhahiri sasa kampuni ya michezo ya kubahatisha betika ilikuwa na tatizo LA kiufundi na wala si matapeli kama nilivyokuwa nikiwafikiria. Hii ni baada ya kufanikiwa kutoa kiasi kikubwa cha pesa nilichoshinda baada ya kutabiri kwa ufasaha matokeo ya michezo ya Mpira wa miguu.

Hivyo niliwahi kuleta malalamiko hapa ya kuwalaumu baada ya pesa yangu kukwama kwa muda wa takiribani wiki mbili kwa sababu za kiungwana naona ni haki kufutilia mbali malalamiko yangu juu yao na yote niloyasema juu yao nimeyafuta hii ni baada ya kurekebisha kasoro kadha wa kadha.
 
Back
Top Bottom