Baada ya Kifo cha Rais Magufuli: Nani anafaa kuwa Makamu wa Rais Tanzania?
Naona Bashiru anapigiwa Sana Chapuo kwenye Mitandao Mingi.

Ila Kwa Maoni yangu Bashiru simuoni Kama ni Mtu sahihi kabisa Kuwa Makamu wa Rais

Kwa Hoja zangu kadhaa

1.Bashiru ni Mtu anayedhani hakuna mfumo zaidi ya socialism, kwenye kuamini mfumo (Economy)yaan Tuna Mixed , Capitalism na Socialism, Naona Kwa Sasa ni Vema tukawa na mtu wa Kuweza kuyaona Mazuri ya Capitalism na mazuri ya socialism akayachanganya,

Dr Bashiru Ni Mfuasi wa Siasa za Nyerere ambaye kafanya kazi kubwa kuliko wote waliowai kuongoza Tanzania, wenda ni Kwakuwa alikaa Sana madarakani, Ila Nyerere Mwenyewe alifika Muda akasema Hapa basi maana aina ya uchumi unavyobadilika uwezi Kuwa static lazima ubadilike, aliamua ku step down akawaacha Kina Mwinyi, Ila Bashiru maono yake anadhani sisi bado tupo ujamaa wa URUSI

2.Namba Mbili Bashiru ni mtu Mwenye Kubadili misimamo kwenye Mambo ya Msingi saa nyingine Kuyakana hata maandishi yake, Mfano Bashiru amewai itetea serikali Tatu, Lakin Muda huu kageuka, Alikuwa kama alivyo Pole pole au Kabudi, hawa wote ni Wale walioikubali Randama ya Katiba ya Warioba Lakin leo wana Msimamo tofaut , Mtu anayegeuka geuka si wa Kuamini Sana,

3.Bashiru Kiongozi wetu ana hulka ya Kanda yetu Ile ambayo inaona kila kitu wao wanaweza, ndo tuna akili kuzidi wengine, IMLA itatawala.

4.Bashiru hakuwai kufanya kazi ya Kumpa Credit yaan remarkable task ambayo ni reference , hata ile report ya Mali za CCM alitambalia nguvu za uthubutu wa Magufuli, na mbaya zaidi ile report ngoja nisi Disclose Sana Lakin Kuna mambo hayako sawa sana . Tuiache

5.Visasi

Nitaendelea baadae


Note that haya ni Maoni yangu kabisa, pamoja na Kwamba ana Madhaifu hayo anatuzidi sifa wengi tunaotajwa tajwa kwa Wakati huu,

Hata wengine tutawachambua

Ila Mama akitaka afanikiwe avae viatu vyake asiige kuvaa vya Magufuli,

Ila avae zaidi ya Viatu vya Magufuli. Avae Vyake ,

Tunataka Makamu atakaye weza Kusimama na Mama bila kuogopa au kummislead

Achague mtu asiye na Jina sanaa ila Mtendaji, Naona atoke Jeshini
Kitendo cha kumuwazia Bashiru tu kwenye hiyo nafasi tayari wewe mwenyewe si mtu sahihi
 
Umakamu wa Rais ni cheo kisicho na nguvu yeyote kikatiba.
Wampe hata babu tale tu inatosha au gwajima.
 
Mshenzi ni wewe ambaye unadiliki kuwatukana watu wa kasikazini bila kuwa na ushahidi.

Kwa taarifa yako kipindi hiki sasa ndiyo kimefika kwa watanzania woote kufaidi keki ya taifa letu.

Kipindi chenu kimekwisha kwa maana mmetupelekesha kadri mlivyotaka.
Tulieni sindano iwaingie vizuri .
Utampelekesha mkeo bwana mdogo 😁 af kuwa na adabu kidogo maana unaowaheshimu wananitambua.
 
Wana JF

Sote humu tunaangaika kupata mtu sahihi wa kusaidiana na Rais SSH, huku tukitaka kitoona mabaki ya CCM ya zamani iliyokuwa Na malengo ya kujirundikia Mali huku ikilindana kiutawala na kufanya wanyonge tuwe maskini wa kutupwa kabla ya Rais Hayati JPM kuipangua na kuirudisha kwa wananchi. Vyeo vya kulindana na kurithishana vinaweza kurudi ikiwa hatutamchagua mwanamapinduzi wa kweli.

Dr. Charles Kimei amefanya mapinduzi makubwa katika sekta ya kibiashara ya kibenki mpaka akacha urithi mkubwa wa kimaendeleo benk aliyoiongoza ikapata mafanikio. Yeye akiwa mshauri wa mwenendo wa kiuchumi aliwahi kusahihisha makosa fulani tunayopitia akataka kuletewa zengwe kabla ya kuambiwa kanusha ili alinde ugali wake kwani alikuwa anakalibia kustaafu.

Kwa udhubutu wake kusema ukweli na makosa anayoyaona kiuchumi, na alighubikwa na serikali isiyotaka ukweli, sasa ni wakati wa CCM kumchagua akatuletee maendeleo kwani hana makundi. Sisi tunachotaka ni maendeleo dhabiti ya watu na vitu sio vitu tu huku wanyonge tukisaga Lami. Angalau tukimkosa Antoni Mataka naye anafaa, Mkoa wa Simiyu ulikuwa nyuma sana na ameunyoosha, ameonyesha diplomasia makini kwa kutatua migogoro ya wafanyakazi.
Huyu jamaa ilibidi awe PM au waziri wa fedha,
 
Back
Top Bottom