Baada ya kuacha kumlea mwanangu kimayai, nimeona akiimarika

Baada ya kuacha kumlea mwanangu kimayai, nimeona akiimarika

Mambo mengine yanashangaza. Nikiwa nasoma chekechea mzazi alikuwa anakupeleka shule wiki ya kwanza tu, ukishika njia shule unaenda mwenyewe. Na hapo unavuka barabara ama na kimto

Lakini Hawa kina Junior hata Kama shule ipo nyuma ya nyumba mzazi unampeleka na kumrudisha, Mtoto hajifunzi kujitegemea kabisa.
 
Haya maisha haya unaweza ukalea mtoto hivyo baadaye linakuja kuwa tofauti.

Lea mtoto vizuri wala asipitie shida ambazo umepita kwasasa mazingira ni tofauti na tuliyokulia wengi.

Mazingira ya sasa ni mazingira ya kisasa tofauti na awamu za ujima.

Kikubwa ni kumpa stadi za maisha na sio kumpa mikazi migumu mpaka mtoto akuchukue kisa unataka kumpitisha njia uliopita.

Tutajikuta tunatengeneza kizazi cha watu wenye roho mbaya kama Magufuli , na baadaye ndio wanakuja kuwa Marais wanaanza kuwapitisha wananchi kwenye magumu kisa wao walipitia magumu.
Nadhani haujamuelewa
Hata kufua nguo zake baadhi ni kazi ngumu..
Mwisho wa siku watoto hasa wa kiume ni lazima umtengeneze kiume
 
Haya maisha haya unaweza ukalea mtoto hivyo baadaye linakuja kuwa tofauti.

Lea mtoto vizuri wala asipitie shida ambazo umepita kwasasa mazingira ni tofauti na tuliyokulia wengi.

Mazingira ya sasa ni mazingira ya kisasa tofauti na awamu za ujima.

Kikubwa ni kumpa stadi za maisha na sio kumpa mikazi migumu mpaka mtoto akuchukue kisa unataka kumpitisha njia uliopita.
Mkuu ni wapi nimeandika mtoto analelewa ili akiwa mkubwa lazima awe unavyotaka??

Nadhani hata mtoto huna au elimu ya malezi huna kabisa.

Malezi ni elimu pana sana, kasome vitabu vya malezi au nyuzi za humu ndani.

Ila huyi wangu ngoja nikomae nae, kuna baadhi ya vitu tayari anavijua ambavyo wenzake shuleni hawajui kabisa kama nlivyovitaja,

Unajua hata kuandika barua ya posa mkuu ?? 😁😁
 
Bado sijutii uamuzi nliofanya,

Hapo awali mtoto nlikuwa namlea kimayai huku nikijioa moyo sitaki apitie shida nlizopitia kumbe nlikuwa navuka mipaka kabisa ambayo haikuwa vema kwa mtoto,

Nikabadili malezi na kweli dhana yangu ya kutotaka mtoto asipate ahida nlizopitia nliendelea nayo ila iliishia tu kuhakikisha mtoto anapata chakula, anavaa, anapata elimu, n.k na sio kuvuka mipaka.

Schoolbus nliacha kulipia maana shule ipo karibu tu kutembea ni dakika 25, kuna wenzake wanaosoma shule za kata hutembea masaa sasa mimi nikaona kwani huyu ni kilema hadi asitembee??

anajifulia,,, Zamani lilikuwa jukum la haus gel ila nikaona huu upuuzi tu, kwani mikono yake imevunjika?? mama yake alisema namtesa ila nikamkumbusha adha atayopata mtoto endapo asipokua na msaada.


anapalilia bustani ndogo .

, anafyeka nyasi (sio ombi)...Saizi silipi mtubaje kufyeka,

kutandika kitanda,...Ashazoea kabisa,

kufagia uwanja ... Hapa saus gel nae kapunguza mzigo

Zamani mchana mama yake alipendelea kumwekea ratiba apikiwe wali au chips, nikaona hayo ndio ni mapenzi ya mama hasa ukiangalia uwezo wa kumudu hivi vitu upo lakini kama baba niliingilia kati hii ishu, Saizi mchana ni ugali kwa kwenda mbele nimempiga marufuku house girl kumpikia wali au chips, Saizi ni ugali tu na hii ni kwa faida ya mtoto.

Kucheza nje na wenzake,..ni haki yake, tatizo wazazibwenye uwezo huwa tunawaona watotot wetu ni kama malaika wasicheze nje na wenzao, Nlikuwa namfungia ndani nikamnunulia Playstation kuchezea game na kuangalia katuni ila kiukweli maisha halisi sio katuni bali ni watu, japo kwa tahadhari.

Shule kwangu nataka mtoto awe na uwezo kawaida tu, kipimo changu huwa ni wastani, yeye hushika nafasi ya tano kati ya wanafunzi 30 na mimi wala sina shida kabisa, sina mambo ya kuhakikisha anashika nafasi gani, ilimradi ana wastani unaoridhisha wala sina shida, ila huo wastani asipoufikia hata awe wa kwanza hapo nina shida.

Huu ni mwaka wa pili nadhani tangu nibadili style ya malezi na sijaona anakosa chochote zaidi ya kupata vingi zaidi.

Ushauri wangu kwa wazazi wenzangu ni kwamba wazazi wenye uwezo msitumie visingizio vya sitaki mwanangu aishi shida nlizopitia huku mkivuka mpaka huo na kutengeneza mtoto ambae ni mayai mayai.

hata maua ukiyamwagilia sana maji mizizi yake huwa mifupi maana maji yapo tele ila mvua kali au upepo mkali ukipita maua yanatoka kwasababu mizizi haijaenda chini kutafuta maji kama maua yanayomwagiwa wastani tu yenye mizizi mirefu inayotafuta maji yaliyo chini hata mvua kali au upepo mkali ukipita mizizi inashikilia ua halitoki.

nitakuja kusoma uzi huuu
 
Mambo mengine yanashangaza. Nikiwa nasoma chekechea mzazi alikuwa anakupeleka shule wiki ya kwanza tu, ukishika njia shule unaenda mwenyewe. Na hapo unavuka barabara ama na kimto

Lakini Hawa kina Junior hata Kama shule ipo nyuma ya nyumba mzazi unamfata na kumrudisha, Mtoto hajifunzi kujitegemea kabisa.
Hali ya kiusalama ya zamani sio sawa na sasa,hiyo ni moja ya sababu kuu.
 
Malezi ya mtoto ni issue ya kubalance tu,

Usimpe sana raha wala asipate tabu sana,kikubwa awe na uwezo wa kuishi kwenye hali zote mbili,

Kama tunavyojua kua life is very short,ni lazima mtoto umuandae kuishi maisha hata kama Mungu atakuchukua,

Usimpe mtoto kila akitakacho wala usimnyime kila akitakacho
 
Back
Top Bottom