Habari zenu wakuu, Jf ni sehem nayoiheshimu na imejaa watu wazima wenye hekima na wanaojitambua natumaini mtanipa ushauri mzuri na wenye hekima.
Nipo kwenye mahusiano na binti 24 years old, Tumekuwa na mahusiano kwa mda wa miaka miwili na mda wote nilikuwa nikijitahidi sana kumlinda na mimba sababu yupo kwao mipango yetu ilikuwa ni kuzalia kwenye ndoa hivyo mda wote tuliokuwa tunakutana nilizingatia sana kinga ili kumlinda na mimba.
Sasa shida imekuja tokea miezi miwili iliyopita alikuwa kabadilika sana yani hata kukutana na mimi ni hadi aamue kwa kujiskia yeye tofauti na zamani, akija kwangu simu ataiacha kwao sababu hatuishi mbali na simu nilimnunulia mimi, hadi nikajiuliza simu imeficha nini lakini niliendelea kuwa mvumilivu.
Mara ya mwisho nikakutana nae kimwili siku moja baada ya kumaliza period na siku ya 27 ya mzunguko wa hedhi ndio ikawa mara ya mwisho kusex nae na mara zote nilitumia condom kwa usahihi na wala haikupasuka wala kupata damage yoyote,na hata mda wa kusex alikuwa yupo yupo tu yani najihisi nipo peke yangu kitandani.
Sasa baada ya kupita siku karibia 36 bila kuona siku zake, ikabidi nimuulize vipi kuna tatizo, akawa kakaa kimya tu anasema hajielewi labda ni mabadiliko tu, kwa vile nilishaona ile sio hali ya kawaida na haijawahi kutokea ikanibidi niende pharmacy nikanunua Baby check, kwa ajili ya kupima mkojo wake ili nijue kama ana ujauzito
Jioni nikampa nikamuekekeza acheki mkojo wa asubuhi akiamka, ilpofika asubuhi akachek na matokeo yakawa ni haya [emoji116], akanitumia hiyo picha whatsap
View attachment 1500024
Alama mbili zikatiki kuwa ni mjamzito, ikanibidi nionane nae jioni ile tujadiliane na maswali nliyokuwa nayo kichwani inawezekana vipi mtu usex kwa kutumia condom kwa usahihi na tena kwenye siku ambazo sio za kushika mimba na mtu apate mimba?
Nilivyoonana nae ikanibidi nimbane kisawa sawa kwa tecknic nazozijua mimi ili aseme ukweli kama aliteleza, baada ya kumbana huku akilia kuwa mimba ni yangu nikamwambia pia kama bado utaniaminisha mimba ni yangu mimi sina tatizo mtoto akizaliwa tutaenda kucheki DNA, kuthibitisha kuwa ni wangu ili nilee damu yangu, Akasema hataki kuzaa hivyo tuitoe, mimi nikasimamia msimamo wangu kuwa damu yetu haipotei kama mimba ni yangu ajiamini kwanini aogope hadi atake kuitoa na uwezo wa kulea upo.
Ikabidi aongee ukweli kuwa alinisaliti na mtu mwenyewe aliyechepuka nae haijui hata background yake hata kazi anazofanya hazijui, niliishiwa nguvu pale nilipo mwambia alete simu yake ampigie huyo jamaa kuwa ana mimba yake
Baada ya kumpigia jamaa akakubali na kusema hana tatizo , nilibaki na mshangao na machozi yalinitoka, na kama isingekuwa kutumia condom basi ile mimba ilikuwa niikubali kwa mikono miwili na ukiangalia kwetu kutoa mimba ni haram na kosa kubwa wakati uwezo wa kulea upo
Pale ndipo nilipoamini kuwa wanawake ni watu wakuishi nao kwa akili sana, kukuletea mtoto asie wako hawaoni kazi, naamini kuna watu wengi mnalea watoto ambao sio wenu, mimi nimeponyea kwenye tundu la sindano
nichukue fursa hii kuwashauri vijana ambao hamko kwenye ndoa acheni kuruka na wanawake kavu kavu, hasa hawa mabinti under 28, hawafai hata kidogo ni wachache sana wametulia ila wengi ni mafia, kukuleta mimba isiyo yako huwa hawaoni tabu
Ni heri mtumie condom tu ili kuepukana na huu mchezo tunaochezewa wanaume, ifike mahali tuseme basi kulea watoto ambao sio wetu tumechoka
Vile vile tokea hili tukio litokee nipo katika wakati mgumu sana, mawazo hayaniishi sababu kutendewa unyama kama huu na mtu niliyempenda inaumiza sana, na huyu mwanamke kila kukicha ananiomba msamaha akilia, hivi nawezaje kusamehe usaliti kama huu? ndio maana kwenye heding nikaomba ushauri wenu namna ya kuanza maisha mapya yenye amani nimechanganyikiwa kwa kweli