Baada ya kumjali na kupigania mafanikio yake, leo nimegeuka kuwa mshamba

Baada ya kumjali na kupigania mafanikio yake, leo nimegeuka kuwa mshamba

Pole Sana Mkuu!!!,Hawa viumbe Ndivyo walivyo huwa hawakumbuki mema waliyotendewa.
 
Bro nahisi ushauri huuu hapa umeupata..... Thanks bro carlos ushauri amaizing sana
Sometimes letting go is the best way to go!!



Kwa kuzingatia sasa Ana mshahara wake , nakushauri kama ifuatavyo

[emoji117]Embu wewe mwenyewe Jiondoe kwake.

[emoji117]Kata Nyuzi ya Mawasiliano iliyokuwepo.
Ndiooo ,usimtafute kwa meseji, kwa simu wala kwann,
[emoji117]Achana na hasra, chuki nakuwaza ulichowekeza, amini nakuambia kadri ambavyo unayawaza haya ndivo unazidi kuumia.

[emoji117]Kuwa Chanya...yaan jipende, kuanzia mavazi, mwonekano, maisha ,kazi ,kua mwenye furaha

[emoji117]HAKIKISHA UNAMUONYESHA KUA UNAFURAHA BILA KUMTAFUTA, ..WATU WABAYA WANAKAWAIDA YA KUTAKA KUONA UBAYA ALOKUFANYIA UNAKUONDOLEA FURAHA. NAHAPA UKIWAJULIA, NIWAO WENYEWE WATAUMIA ( ZINGATIA SANA HILI) .

Hakikisha Sanaaa Hauwi mtu wa mitandaoni sanaaaa , ila kua mtu wa mtandaon kwa 'Nadra yenye Uhakika".. Hapa lengo ni kumrudisha kama bado unamhitaj, nahapohapo lengo nikuendelea na Maisha yako wewe kama wewe.


Kwahiyo,
[emoji117]ACHA KUPOST POSTS ZINAKUONYESHA UNA HUDHUNI ,ACHA KABISAAAA.
kama ni jumbe ,tafuta zile jumbe zinazokuonyesha una furaha mfano"Life is full of surprises "..... Love and happiness ".
Yaaan ukipost leo, unatulia kama siku nne au wiki unapost tena , kama ni picha Weka zinazokuonyesha umecheka ,umetabasamu, uko na jamaa zako wakike au wakiume mkifurahi.

[emoji117]Hakikisha Asijue ratiba za Maisha yako kupitia mtandao..yaan hapa asijue upo wapi siku hizi, unafanya nn, upo na nani n.k


[emoji117]USITUMIE WATU KUMBEMBELEZA.


[emoji117]USIJE KUMBEMBELEZA, AU KUMUOMBA MSAMAHA, KUJARIBU KUHOJI KUNAN, KWANN KABADILIKA N.K ACHAAAAAAAAAAAAAA.


[emoji117][emoji117][emoji117]HIZI MBUZI ZISIZOJIELEWA ,HUJA KWENYE MAISHA KUFUNDISHA ..NAHIVO JIONE WEWE NI BORA, WA THAMAN, HB, MWENYE MAISHA. HUWEZ AMIN, ASIPOJIRUDI, ATAKUJA BOOOOONGE LA DEMU KISUUUUUUUU KIKALIIII PISI YENYE KUUMBWA NA KUUMBIKA, ACHANA NAHILO GARI LA MKAA.
 
Kama uliweza kumpigamia na kapata Kaz, baadaye kiburi na makucha ya nyodo, mi nakushaur pigaNia hafukuzwe kazi, Kama umempandisha kumshusha rahisi kweli, ungekuwa umemsomesha ingekuwa na ugumu, kumfukuzisha mtu Kaz kitu simple kweli, unacheza michezo hapo kazini kwake.
 
Pole sana kwa changamoto hakuna haja ya kuwa na mawazo kuna maisha baada ya kuachwa, songa mbele endelea na mambo yako achana naye kabisa huyo hakufai ipo siku atakutafuta.
 
Kamwe usije ukampenda mwanamke akiwa kwenye shida ila kama nikumsaidia msaidie tu. Furaha au huzuni huwa vinatafuta pakupumzikia kwa muda.
Pole bro endelea na maisha yako yana umuhimu mno kuliko huyo uliekutana nae ukubwani.
Uko sahihi mkuu
 
Kwa waliopitia hii hali mtakuwa mnajua kuwa maneno ya ushauri kama hayana msaada vile! Hata Rais akushauri au malaika akutokee akushauri bado tu maumivu yatakuwepo! Wengine watakuambia achana nae usimtafute au usiombe mtu akumbembelezee ilihali ndio kitu unachofanya!
Sasa ni hivi TIME HEALS kwa sasa huna la kufanya zaidi ya kukaa dawa ikuingie haswa, ujifunze jinsi binadamu tulivyo! Alafu as time goes unaizoea hali, labda after two years utakuwa umemsahau permanently!
Usiache kuongea na watu pale utapoona hali mbaya zaidi, pia ongea na watu wakupe exprience zao na jinsi wamesurvive sahivi wako poa. Kwa sasa dawa lazima ikuingie
 
Sometimes letting go is the best way to go!!



Kwa kuzingatia sasa Ana mshahara wake , nakushauri kama ifuatavyo

[emoji117]Embu wewe mwenyewe Jiondoe kwake.

[emoji117]Kata Nyuzi ya Mawasiliano iliyokuwepo.
Ndiooo ,usimtafute kwa meseji, kwa simu wala kwann,
[emoji117]Achana na hasra, chuki nakuwaza ulichowekeza, amini nakuambia kadri ambavyo unayawaza haya ndivo unazidi kuumia.

[emoji117]Kuwa Chanya...yaan jipende, kuanzia mavazi, mwonekano, maisha ,kazi ,kua mwenye furaha

[emoji117]HAKIKISHA UNAMUONYESHA KUA UNAFURAHA BILA KUMTAFUTA, ..WATU WABAYA WANAKAWAIDA YA KUTAKA KUONA UBAYA ALOKUFANYIA UNAKUONDOLEA FURAHA. NAHAPA UKIWAJULIA, NIWAO WENYEWE WATAUMIA ( ZINGATIA SANA HILI) .

Hakikisha Sanaaa Hauwi mtu wa mitandaoni sanaaaa , ila kua mtu wa mtandaon kwa 'Nadra yenye Uhakika".. Hapa lengo ni kumrudisha kama bado unamhitaj, nahapohapo lengo nikuendelea na Maisha yako wewe kama wewe.


Kwahiyo,
[emoji117]ACHA KUPOST POSTS ZINAKUONYESHA UNA HUDHUNI ,ACHA KABISAAAA.
kama ni jumbe ,tafuta zile jumbe zinazokuonyesha una furaha mfano"Life is full of surprises "..... Love and happiness ".
Yaaan ukipost leo, unatulia kama siku nne au wiki unapost tena , kama ni picha Weka zinazokuonyesha umecheka ,umetabasamu, uko na jamaa zako wakike au wakiume mkifurahi.

[emoji117]Hakikisha Asijue ratiba za Maisha yako kupitia mtandao..yaan hapa asijue upo wapi siku hizi, unafanya nn, upo na nani n.k


[emoji117]USITUMIE WATU KUMBEMBELEZA.


[emoji117]USIJE KUMBEMBELEZA, AU KUMUOMBA MSAMAHA, KUJARIBU KUHOJI KUNAN, KWANN KABADILIKA N.K ACHAAAAAAAAAAAAAA.


[emoji117][emoji117][emoji117]HIZI MBUZI ZISIZOJIELEWA ,HUJA KWENYE MAISHA KUFUNDISHA ..NAHIVO JIONE WEWE NI BORA, WA THAMAN, HB, MWENYE MAISHA. HUWEZ AMIN, ASIPOJIRUDI, ATAKUJA BOOOOONGE LA DEMU KISUUUUUUUU KIKALIIII PISI YENYE KUUMBWA NA KUUMBIKA, ACHANA NAHILO GARI LA MKAA.
Mkuu ña mimi namuongeza 1
ashukuru kuna kitu Mungu kuna kitu amemuepusha.
 
Hapo mm ndio huwa nakuwaga tofauti kidogo na wengine. Kama ni wake, basi hataondoka. Kitendo cha kuondoka tu, huyo sio wake. Yani aende huko apelekewe moto weee, mambo yakiwa magumu ndio arudi tena kwa jamaa???
Sina hakika sana lakini ninachojua watu wengi wanapitia changamoto mbalimbali wanapokuwa pamoja. Wengine wanaishia hata kuachana, wanaishi miaka kisha wanarudiana. Wengine hasa wanaume uwa wanaweza kumuacha mtu wake kwa tamaa ya mwili tu akidhani ni upendo. Ila akimaliza haja iliyompeleka akili inarudi. Maisha yanaendelea.
So mambo ni mengi na watu wamebeba stori tofauti za maisha hasa za kimahusiano. Huyo mwanamke anaweza kurudi na muhusika akajilaumu sana kupoteza muda kwa kuhuzunika kuondoka kwake. Yote yanawezekana.
 
Atakuwa ni mpenzi wako wa kwanza huyo.

Ukipata mwingine akakupiga tukio kama hilo tena ndo utakuwa umefuzu.

Utakuwa sawa muda si mrefu, ila ukiendelea na ujinga wako wa kukaa ndani utachelewa kuwa sawa.
Kabisaaa
 
Bado una kaujana,under 25 hapo. Hayo mambo ya kawaida. Wapo wenzio walisomesha kuanzia form 1 mpaka chuo,bado demu anageuka. Unapoteza muda tu kujifungia ndani. Ni rahisi sana jifikirie tu mademu kibao,utawapata tu mbele huko. MUHIMU kwako kwa sasa ni kupambana sana kupata life la maana. Maana utambue tu amekukimbia sababu huna life la uhakika. So hiyo ikupe hasira kupambana kupata life ndefu. Huyo msahau haraka,tena wewe una bahati hujapteza aset zako nyingi na muda kwa huyo demu. Na bahati nyingine amekuonyesha makucha kabla hamjafika mbali kuwa mke. Msahau,endelea mbele. Na ipo siku tena atakutafuta nae akitendwa huko. Narudia tena wewe una bahati sana. Jione una bahati sana.
 
Nilimkuta akiwa ana stress za maisha baada ya kumaliza masomo yake katika chuo fulani. Nilimshika mkono, nikamfuta machozi kisha nikampenda na nikamfundisha kunipenda, nikaishi nae kwa zaidi ya miez kumi. sikuhitaji kumuona akiwa katika msongo wa mawazo bali nilitafiti nikagundua shauku yake ilikuwa ni kupata kazi au biashara ainue familia yake na ajenge mustakabali wa maisha yake.

Niliamini katika falsafa ya ushirikiano katika kujenga mustakabali wetu kwani kila mara alionyesha kuwa mimi ni chagua sahihi kwa kauli na matendo. Nilipambana kwa hali na Mali kwa kipato changu cha kawaida na hii exposure ndogo mpaka nikafanikiwa akapata kazi kwenye shirika moja la miradi ya afya hapa nchini akaenda kufanya kazi nje ya mkoa niliopo mimi.

Wiki mbili baada tu ya kuajiriwa alibadilika sana alibadilika sana, ninaweza kumpigia simu nakuta yuko busy kuanzia saa tano mpaka saa saba usiku na anaona simu yangu inaingia hapokei na akimaliza kuongea hanitafuti hata nikimuulza hatak kusema anaongea na nani, akaenda mbali zaid ukimtumia sms anakujib kwa mkato na ikafikia hatua hataki kunitafuta na nikimtafuta hapokei simu.

Nimewahi kwenda huko anakofanyia kazi nimekaa siku tatu yaani muda wote hajiamini na hawez kutoka nje akaongozana na mm. Dharau na kiburi ndio umekuwa mtindo wa maisha yake. Naishia kuitwa mshamba kwa kumfatilia eti nijiamini. Kifupi nimejitoa kwa mengi nikijua huyu atakuwa mke wangu halaf amekuja kunibadilikia ghafla, inauma sana na Niko katika wakati mgumu sana ukizingatia niko naandika tasnifu yangu niweze kumaliza shahada yangu ya uzamili lakini nashindwa hata kusimamia biashara zangu zinanishinda.

Nabaki muda wote ndani nimejifungia tu roho inaniuma sana kila nikiwaza mawazo yangu yananipeleka mbali zaidi ya jinsi ambavyo siwez kuelezea, nimepitia changamoto nyingi katika maisha yangu lakin hili naona linanizidi.. ndugu zangu naona kabisa jahazi linazama.

Mwenye ushauri mzuri utakaonisaidia na kunitoa ktk hii hali naomba aje PM au hapa hadharani anishauri. Jf naona ndio second home yangu naamini ndugu zangu wenye busara zaidi mtanisaidia.
Sina Zaid ya kukuambia Mungu kakuonuesha mapema kwa sababu Nia yako ilikua Safi lakini huyo sio mtu kwako achana nae Mungu atakulipia na ipo siku utaleta mrejesho hapa
 
Back
Top Bottom