Baada ya kumsikiliza mama wa Feitoto, ni dhahiri Fei na familia nzima wamerubuniwa

Anapambania maslai sawa ila afuate taratibu sio kupita njia za matapel
 

Tumia akili kufikiri sio unatumia tumbo
Wakati feisal anasaini huo mkataba alikuwa hana thamani ya hela iyo,

Wenzetu ulaya mchezaji akisaini mkataba kuna vipengele vya kuongezeka bonus na rewards pale ambapo kiwango chake kinazidi kupanda sometym hata timu aliyotoka (iliyomuuza) inaahidiwa lbd ikiwa timu itashinda Uefa Champion league tutawaongezea kiasi kadhaa..

Next time fikiria Yanga wangekuwa ndio wanavunja mkataba wa feisal kwa 7bu performance yake imeshuka…. Mngesemaje tena kaonewa kamwaga jasho lko na mashuti yake ya mbali leo wamemuacha
 
Ndio alishwe ugali sukari
 
Sasa wewe unaongea nini na mimi nimesema nini? Mimi nimeongelea kiwango cha chini cha mishahara kutokana na ukubwa wa timu hizi mbili. Na pia nimegusia kuthaminisha kipaji chake ndani na nje ya uwanja? Katika post yangu hapo wapi nimeongelea mambo ya kuvunja mikataba?

Hata katika ligi nzima kiwango cha chini cha mishahara inabidi kiongezwe.
 
FEISAL si alitaka kuvunja mkataba kwa kuwalipa YANGA, fedha ya kuvunja mkataba zaidi ya shilingi million 100?
Kwanini, Yanga walikataa kama hawana manufaa naye?
KIFUPI: Yanga wamwachie FEISAL akatafute maisha sehemu nyingine, siyo sahihi kupotezea madai yake eti Kwasababu MAJIMAJI ilikosa million 1, kwani FEISAL ni mchezaji wa MAJIMAJI, hata umlinganishe na uwezo wa timu hiyo?
FEISAL anaangalia uwezo wa kifedha wa Yanga na mchango wake ktk. Timu ya Yanga, ukilinganisha na malipo ya Wachezaji wengine ndani ya timu husika.
 
Mimi nitakua Simba hadi kufa...kuhusu hili shauri la Feitoto ni vile kila mtu kwa mtazamo wake ataichukulia..halafu mbumbu sio timu au Club...mbumbu ni individual hata Yanga huko kuna mambumbu kibaooo...
Feitoto hapa kisheria anajipotezea muda
 
Haya amesharuhusiwa kuondoka. Afuate utaratibu, aondoke. Maana Yanga ni kubwa kuliko yeye.
 
Angalia mzizi wa hoja yangu acha kuanza kuponda kabla hujasoma..nachosema angefuata utaratibu wa kuomba kuongezewa mkatba ujao au kuomba kurekebishiwa huo wa sasa...mimi nachoona anapoteza muda mrf na hizi kesi..
 
Poor reasoning

Mwambie Azizi Ki kuanzia leo awe ana chukua 4M kwasababu kuna timu ya majimaji ilikosa pesa ya nauli
Hili jukwaa limesheheni wachangiaji ambayo akili ni kijikoCha chai na I.Q ambayo kwa nchi ambazo ziko serious na ustawi wa baadaye wa Taifa wangepigwa ban ya kuzaa ili wasiendelee kujaza nchi mataahira. Si unyamaze tu kuliko kuonyesha uchi wako wa akili?
 
Basi wakomae mikataba ijayo iwe ya kuwa feva wao...kwa sasa tayari wameshasaini..
 
Nimewakaushia sio kama siwaoni ila sometimes upuuuzi unapozidi unakosa uvumilivu

Huyo mdau niliyemjibu, aliandika kuwa 4M ni pesa nyingi akajenga hoja kuwa Fei hapaswi kulaumu kwasababu kuna timu huko imekosa 1M ya nauli

Hiyo ni Argument from ignorantium, timu kukosa 1M sio kigezo cha mtu mwingine kushindwa ku demand pesa zaidi ya ile anayolipwa

Na ndio maana nimemuambia kama anaona hiyo ni reason, basi kamfate AziI Ki muambie kuanzia leo utalipwa 4M kwakua tumeona kuna timu imekosa 1M ya nauli, hivyo 4M ni pesa ngingi sana

Wote mliojibu hiyo post yangu, mmeijibu kimhemko na ndio maana wengi wenu nimewapuuza
 
Mie ninachojiuliza ni nani alimdanganya Fei?,kijana wa watu mpaka anajikuta nje ya kipaji chake kwa zaidi ya miezi kadhaa?,mikataba haifanyi kazi kwa huruma mkataba ni written documents yenye maelezo ya Kila kipengele na tafasiri yake,Mama(familia yote) imedanganywa kuwa huruma inaweza kuvunja mkataba..hope Yanga haina shida na Fei ila Yanga inalinda heshima ya Taasisi pamoja na kuheshimisha mpira wa miguu na kanuni zake zote zilizotungwa na FIFA.
 
Wakati anasaini kiwango chake kilikuwaje? Na je kiwango kingeshuka mshahara ungepunguzwa?
 
unapozidi

Mdau nakuunga mkono Hawa wanaoilaumuYanga ndiyo mataahira. Niwape mfano rahisi unaoendana na akili zao finyu. Hivi ukioa mwanamke wa kawaida kabisa na ukapangiwa mahari na ukalipa vzuri. Mwenye mke ukamtunza vizuri na akapata Ile sura iliyofubaishwa kwa kukosa huduma huko kwao.Je ni halali kwa Wazazi kurudi kudai mahari nyingine kwa kigezo Cha kwamba hii pisi haikustahili mahari ya mwanzo.Ishu ya mkataba haina siasa
 
Wakati anasaini kiwango chake kilikuwaje? Na je kiwango kingeshuka mshahara ungepunguzwa?
Value ya mchezaji ina vigezo vyake mzee unafikiri kwanini kina Kambole hawapo, na Feisal mnazidi kumng'ang'ania?

Unafikiri kiwango kingeshuka mngebaki naye hapo Jangwani?

Ni kwasababu huyo ni valuable asset na ndio maana mpaka sasa yupo, na walioshuka wote mmewatimua hata hiyo nafasi ya kuomba kupunguziwa mshahara wameikosa
 
Feisal amerubuniwa na waswahili wa Simba kwenye vijiwe vya kahawa.Feisal amengarishwa na Nabi.Angesubiri mpaka mwaka huu ufike Dec. ndiyo aanze kudengua kusaini mkataba mpya Kama akina Azizi K.Alidhani angeifanya Yanga ipanick kucheza michezo yakimataifa bila yeye.Kumbe maskini wa Mungu angeweza Kupata timu ambayo ingempa mkataba mnono. Sasa hivi anakula uono na zile vocha za washabiki zimekata Nitashangaa Kama Yannga anamlipa 4M
 
Sasa turudi kwenye hoja. Fei ana haki ya kudai maslahi zaidi. Lkn anapaswa kufuata taratibu sahihi. Hoja za kishabiki za mitaani hazitamsaidia
 
Nakuelewa kidogo ,Ila ukakasi upo hapa tu ,why vilabu vina power ya kuvunja mkataba wa mchezaji muda wowote wakiona hawajaridhishwa na kiwango chake?
Hiyo Sheria sijui kanuni mbona km imeegemea upande mmoja?
Mifano ipo mingi tu ya vilabu kumvunjia mkataba mchezaji hata Kama yeye hakutaka kuondoka kwa muda huo Ila vilabu vinakua na power Sana had wachezaji wanajikuta wanaondoka bila kupenda.
Naomba elimu juu ya hili.
 
Ni mzawa gani amewah thaminiwa kwenye hivi vilabu ?
Why vilabu vina power ya kumvunjia mchezaji mkataba hasa club isiporidhishwa na kiwango Cha mchezaji Ila mchezaji kuvunja mkataba inakua ngumu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…