Baada ya kustaafu katelekezwa na mke na watoto wake. Anaugua ugonjwa wa akili kwa sasa

Baada ya kustaafu katelekezwa na mke na watoto wake. Anaugua ugonjwa wa akili kwa sasa

All women are devils only your mother might be good to you, But she is still a devil to your father.

Mzee mmoja aliniambia kijana hata "Mama" awe mbaya na muovu kiasi gani na Baba awe mzuri kiasi gani, Siku zote watoto watakuwa upande wa Mama kumtetea maovu yake.

As a Man, lazima uwe na "back up plan" ya ku survive individually wakati wowote ule.
Hatari sana
 
Hila hela za kustafu sijui zina shida gani unakuta mtu anajielewa ana akili timamu kabla hajapata zile hila wakishastaf ile hela ikiingia kwenye account anaona kuna million 100 hapo akili inabadilika hela ikiisha akili zinarudi na hata sisi tunaoandika hapa tunawaponda wazee wetu lakini mwisho wa siku na sisi ni hvyo hvyo
Maskini akipata matako hulia mbwata....

Apa wahenga walimaanisha akili sio matako....wakao akili za masikini ni kama matako tu,hazina akili kama chawa wa ccm.

Na 90% ya wafanyakazi wa serikali akili zao kama matako....
 
Yule mzee na familia yake nimeishi nao jirani sana mzee alikua mtu poa na watoto wake walisoma shule nzuri sana ila ndo hivyo wamemtelekeza. Kuna wakati alikua anahudumiwa na binti yake kama kumpikia na kumchotea maji mke wake alisepa sijui alienda kudanga wapi.
Najiuliza hayo mapato ambayo yanatokana na nyumba zake yanakwenda wapi?
Kama wamemtelekeza kwa nini asingeuza baadhi ya nyumba akapata pesa za kujikimu?!
 
Kuna mengi ya kujifunza kuhusu kustaafu
Kweli kabisa.
Inakuwa mbaya zaidi **** huna kipato, hata Kama so kikubwa Sana lakini Cha kuaminika.
Kwa mfano kuwekeza kwenye Treasury bonds; unaendelea kupata kipato cha uhakika.
 
Kuna jamaa yangu alikua benchi,hata hela ya kula hana,anadaiwa kodi,.jamaa anahangaika kukopa ili asogeze siku hadi apate mishe, mke wake anamchora tu na kumpa moyo,jamaa akakuta kabatini mwanamke kaficha laki tisa,.900000/= nyekundu tupu..jamaa kapita nazo kimya kimya,.
Huyu ndo mim mtupu
 
Huyo mtoa stori ni muongo!Mzee kama ana nyumba mikoa mbali mbali si anakula Kodi tu na kuvuta dogodogo Moja maisha ya upweke unayatoa wapi Tena na mtonyo unao.
Mkuu kama una kitega uchumi cha nyumba za kupangisha unaweza kuelewa nini maana ya kuwa na nyumba za kupangisha na ukafa njaa.
mimi ndo maana naona ni heri uweke fedha yako kwenye bond kuliko kuendelea kujenga majengo ya kupangisha.
Sikatai kuna watu wamefanikiwa kujenga kwenye maeneo maalum ambayo yanashindaniwa kupangishwa,lakini maeneo mengine ukipata mpangaji unamshukuru Mungu.

Pia kuna ndugu wakishajua nyumba ni yako,wanapanga ndio
lkn akiwa na changamoto sahau kodi n.k
hivyo unaweza kufa njaa na nyumba unazo.
 
Dahh wanawake tuna roho mbaya sana muda mwingine aise!!

Sasa na hao watoto pamoja na utu uzima wao wameshindwa hata kung'amua jema na baya?!

Ila malipo ni hapa hapa duniani
 
Kunawanawake wabinafs sana aisee na kunawatoto akili hawana kabisa
 
All women are devils only your mother might be good to you, But she is still a devil to your father.

Mzee mmoja aliniambia kijana hata "Mama" awe mbaya na muovu kiasi gani na Baba awe mzuri kiasi gani, Siku zote watoto watakuwa upande wa Mama kumtetea maovu yake.

As a Man, lazima uwe na "back up plan" ya ku survive individually wakati wowote ule.
Sahihi
 
Kuna mambo hayapo wazi kwenye hii story.
Ni lazima mzee kuna kitu alizingua,. Tuseme hajazingua kitu mtu una pesa na mali urukwe na akili kisa mke? Si umtimue watoto wake wamfate huko?

NIni hasa kinampa stress?

Hakuna mtoto ambae alikupenda tangu utoto wake aje kukubadilikia ukubwani bila sababu.

Kuna mambo ya ndani kabisa ambayo hayapo wazi hapa.
Inaelekea migogoro na mkewe ndani ilianza kabla ya kustaafu. Na mwanamke akavumilia Kwa sababu alikuwa na lengo au aliwekeza huko kwao. Kwa kawaida kama alivyosema mdau hapo juu kuwa siku zote watoto huchagua upande wa mama hata akiwa muovu kiasi gani ndivyo ilivyotokea.
 
Jamani mimi niwape ushuhuda kidogo,si kwamba naunga mkono watu wasioe,hapana
bali ukioa usijisahau.Kama unafanya kazi,jitahidi weka akiba na kuiheshimu pensheni,
Nimejifunza kwangu mimi mwenyewe,hivyo sishangai kwa yaliyompata huyo mzee.

Mimi kufuatana na shughuli zangu kuwa mbali,nilikuwa nikipata kipato
namkabidhi mke wangu pesa ya matumizi ili kutunza familia,hata karo za watoto naendelea na mishe ya kusaka pesa. Nilifikia hatua ya kuacha na kadi ya benki ili kuondoa usumbufu,
Akilini nikijua mambo yote yako poa.Kumbe haikuwa hivyo
Nadhani kuna shetani alipitia. Karo zikawa halipwi ila muda ukifika anakopa anawapa watoto wanaenda shule.
Tena mikopo ya liba hivyo inaendelea kuzaa deni linaongezeka mimi sina habari.

Baada ya madeni kuwa makubwa,mtu mmoja rafiki yangu ambaye alisikia habari hizo
akanifuata,na kunishauri kuwa pamoja na mishe zangu za kusafiri nijitahidi kumsaidia
mke wangu kulipa ada za watoto anapata sana shida kutafuta pesa.
Niliposikia hivyo nilistuka nadhani naye alijua.lkn nikamwambia sawa nitajitahidi,maana niliona nikionyesha kukerwa
naye atashangaa sana kwa jinsi alivyotujua tunavyoishi na mke wangu.

Nilipoenda kumwuliza akakana,akasema humna kitu kama hicho.hivyo nikaanza utafiti binafsi
Niliyoyakuta ilikuwa story ndefu.Namshukuru Mungu tulifanikiwa kuyamaliza,na nilifanikiwa kulipa hayo madeni,
kuanzia hapo nikaanza kulipa karo kwa mkono wangu mwenyewe
na kufuata ushauri wa mchungaji mgogo kwamba unapotoa matumizi,hakikisha unatoa sebureni siyo chumbani
ili watoto waone jitihada zako za uwajibikaji.

Baada ya kubadilisha mfumo wa maisha tunaendelea vizuri na maisha.
Hivyo vijana msiogope kuoa,kama unamcha Mungu hakuna ubaya utakaofanyika chini ya kapeti usijue.

Tunaolaumu kwamba wanaume hawawajibiki japo sikatai lakini tujitafakari.Hata kama hawawajibiki ni kwa nini tunasubiri wazeeke ndo tuwanyanyase? kwanini msiwakimbie mapema mkaolewe au mkaanzishe maisha nje ya hao wanaowanyanuyasa?

Mi nadhani vijana chukueni ushauri huu,wazazi wako ni wazazi wako.Asiwepo hata mmoja wa kukuambia ubaya wa mwenzake maana walipokutana hukuwepo na wewe
usijifanye bingwa wa kulipa kisasi itakughalimu.Baba asingempa mimba mama yako,usingezaliwa.
Na baba bila mama mimba yako isingetungwa na usingekuja duniani.
Hata kama hukutunzwa. Watunze wazazi wako kwa kadri ya uwezo ulio nao
maana wamekuleta duniani.
Na Mungu atakubariki.
Mimi niko tofauti kidogo pesa ya ada nampa yeye anaenda kulipa risiti huwa nadai dec,pia matumizi ya nyumbani ni kila j2 tunafanya nae shoping ya wiki nzima....kwahiyo hapo hana namna ya kuniletea usanii
 
No woman no cry.🎶🎶🎶🎶🎶🤣🤣🤣🤣💺
 
Wanaume hapa mna cha kujifunza

1. Sio kila mwanamke anafaa kuwa mke

2. Usioe Kwa mihemko

3. Mwanamke anasamehe ila hasahau, ukimfanyia ubaya Leo hasa ule wa kujirudia na akakutoa moyoni usitegemee km atakuja kugeuka nyuma na kukupenda kama awali. Upendo ukiisha umeisha Mazima tunaishi Kwa mazoea

Wanawake pia, tuna nafasi kubwa ya kuweka bond Kati ya Baba na mtoto.

Tunapokosea
Tunaweka tabaka Kati ya Baba na watoto. Mfano baba anatoa hela za mahitaji, chakula na Ada anampa mke Kwa ajili ya watoto. Mama na chuki zako unafanya km pesa umetoa mfukoni mwako n kwamba wewe ndiye unayehangaika kuhudumia familia

Hii inaweka mpasuko Kati ya Baba na watoto, usitegemee kama watoto watakuja kumjali baba yao ambaye waliona hakuwahi kuwajali na kuwapigania kama Baba zaidi watakaye mjali ni mama

NB. Ugomvi Kati ya wanandoa usiwahusishe watoto ili mmoja aonekane mzuri kuliko mwenzie. Pambaneni wenyewe
 
Yule mzee na familia yake nimeishi nao jirani sana mzee alikua mtu poa na watoto wake walisoma shule nzuri sana ila ndo hivyo wamemtelekeza. Kuna wakati alikua anahudumiwa na binti yake kama kumpikia na kumchotea maji mke wake alisepa sijui alienda kudanga wapi.
Kuna story kama hii pia Kisongo-Arusha....ila mke wa mzee ni Mmeru balaaa sana mzee ameamua kunywa banana tu sasa kupunguza mawazo
 
Nashindwa sometimes kuelewa nini faida na umuhimu wa ndoa kama mambo yenyewe huwaga hivi.

Kuna mzee mmoja alikua jirani yangu, alikua mhandisi wa shirika moja kubwa hapa nchini

Mzee huyu kutoka kule migombani alioa mke wa migombani pia. Maisha yalikua mazuri wakati mzee bado anafanya kazi.

Alijenga nyumba mikoa mbalimbali na alijitahidi kuwasomesha watoto wake shule nzuri hizi za saint saint.

Watoto wake wote wana shughuli zao nzuri tu.

Baada ya kustaafu hapo ndo akaanza kuona rangi halisi ya mke wake. Kwanza alimtumia wakora wamfanye kitu mbaya ili mke arithi mali mapema bahati nzuri ndugu wa mume wakashtukia mapema mission ikabuma.

Tangu wakati huo mke akaanza kumtenga mume wake na kibaya zaidi hadi watoto wake aliowasomesha wakamtenga baba yao na kumsahau kabisa(sijui mama yao aliwaambia nini)

Dingi akaanza kunyimwa chakula, dingi akakimbiwa chumba na mke wake(alikua anatuambia vijana na kutuhasa juu ya makabila ya kuoa)

Baada ya muda mzee kaanza kurukwa na akili kwa maisha aliyokua anaishi.

Kwa sasa mzee karudi kwao lakini akili yake haiko sawa kaacha mali zote anaishi kijijini kwao. Watoto wake wamemtupa hawana time na baba yao

Je nini hasa wamama wanawaambia watoto wao kiasi cha watoto kuanza kumchukia baba yao na kumtenga ili hali aliwasomesha na kuwalea vizuri na juhudi zake waliziona.?

Hili ni janga kwenye familia nyingi baba akistaafu anaishi maisha magumu ya kunyanyasika juhudi zake zote alizofanya kujenga familia bora zinakua kazi bure anaishia kutengwa na kupata msongo wa mawazo na mwisho kufa.

KATAA NDOA NI UUAJI NA UTAPELI
Nyumba alimilikisha watoto ambao ndo hao wamemtelekeza kwa hiyo kwa sasa hana uwezo wa kufuatilia tena amekua na tatizo la ugonjwa wa akili na hili limetokea miezi michache baada ya kustaafu ndo mke nae akaanza hapo hapo ukatili dhidi ya mume wake kwa kushirikiana na hao watoto wake. Na pia mzee alikuwa na watoto wengi
Hawa watakua wamachame tu wanawake wa kimachame ni wa kuogopwa kuna mama mmoja alikua na mumewe na wote walikua watumishi kanisani mama akazaa na padri kiburi kikaanza hapo kuna sku mumewe akampiga sababu alichelewa kurudi mama akamwambia mumewe hutanipiga tena baada ya hapo mzee alianza kudhoofu mpk akafa

Sent from my PRA-LA1 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom