Bams
JF-Expert Member
- Oct 19, 2010
- 19,362
- 48,879
Huko Kata ya Ruhuhu, wilayani Ludewa, mkoani Njombe, karatasi za kupigia kura hazikuwa na majina ya wagombea kupitia CHADEMA.
Wananchi waliweza kuzuia uchaguzi usifanyike. Mtendaji kata bwana Yusufu Lukuwi (mtoto wa Kidulile), alipoona wananchi wamechachamaa, alitoa taarifa Wilayani, na msimamizi wa uchaguzi akatuma gari, wakaondoka naye, haijulikani wameenda naye wapi.
Wakati wananchi wakidhibiti kuhakikisha hakuna box la kura linaingizwa kituoni, zilipatikana taarifa kuwa kuna maboksi yenye kura za wagombea wa CCM, yamefichwa nyumbani kwa mwalimu wa shule ya msingi Ngelenge, bwana Kayombo. Wananchi wakaamua kwenda kuyachukua maboksi hayo, lakini walipofika nyumbani kwa mwalimu huyo, tayari alikuwa ametoroka, na mpaka muda wa saa 1 usiku, alikuwa hajapatikana.
Wananchi wa Ruhuhu wamejiapiza kuwa mtendaji na huyo mwalimu, kamwe wasionekane kijijini pao.
Mpaka muda wa kupiga kura unaisha, hakuna aliyepiga kura.
Kwa uchaguzi huu, hakika Mchengerwa amevunja rekodi. Na hawa viongozi wa kupatikana kwa kupora haki za wananchi, watakuwa na wakati mgumu sana katika uongozi wao. CCM wasidhani wamewasaidia jwa huu uharamia, bali wamewapa majuto, na sia ajabu, wengi wataachia njiani.
UPDATE:
Maeneo ambayo CHADEMA waluweka wagombea, majina yao yakaenguliwa, kisha rufaa zao zikashinda, majina yakawekwa kwenye karatasi za kupigia kura, na uchaguzi kukamilika, matokeo ya mwanzo kutangazwa ni kijiji cha Lupingu: CHADEMA imeshinda:
Kijiji Cha LUPINGU imeshinda CHADEMA, kitongoji cha LUPINGU imeshinda CHADEMA kitongoji cha LUKUYUSI bado Matokeo yana ukakasi, kuna vurugu kubwa sanaaaa huko.
Kijiji Cha LUPINGU ina vitongoji 3 mpaka sasa tumeshinda kijiji na kitongoji 1. Kitongoji cha ISANGA wameshinda CCM.
Taarifa Imetolewa na mwenyekiti wa BAVICHA Mkoa wa Njombe, na Lupingu ndiko kijiji anachotokea huyu mwenyekiti.
Wananchi waliweza kuzuia uchaguzi usifanyike. Mtendaji kata bwana Yusufu Lukuwi (mtoto wa Kidulile), alipoona wananchi wamechachamaa, alitoa taarifa Wilayani, na msimamizi wa uchaguzi akatuma gari, wakaondoka naye, haijulikani wameenda naye wapi.
Wakati wananchi wakidhibiti kuhakikisha hakuna box la kura linaingizwa kituoni, zilipatikana taarifa kuwa kuna maboksi yenye kura za wagombea wa CCM, yamefichwa nyumbani kwa mwalimu wa shule ya msingi Ngelenge, bwana Kayombo. Wananchi wakaamua kwenda kuyachukua maboksi hayo, lakini walipofika nyumbani kwa mwalimu huyo, tayari alikuwa ametoroka, na mpaka muda wa saa 1 usiku, alikuwa hajapatikana.
Wananchi wa Ruhuhu wamejiapiza kuwa mtendaji na huyo mwalimu, kamwe wasionekane kijijini pao.
Mpaka muda wa kupiga kura unaisha, hakuna aliyepiga kura.
Kwa uchaguzi huu, hakika Mchengerwa amevunja rekodi. Na hawa viongozi wa kupatikana kwa kupora haki za wananchi, watakuwa na wakati mgumu sana katika uongozi wao. CCM wasidhani wamewasaidia jwa huu uharamia, bali wamewapa majuto, na sia ajabu, wengi wataachia njiani.
UPDATE:
Maeneo ambayo CHADEMA waluweka wagombea, majina yao yakaenguliwa, kisha rufaa zao zikashinda, majina yakawekwa kwenye karatasi za kupigia kura, na uchaguzi kukamilika, matokeo ya mwanzo kutangazwa ni kijiji cha Lupingu: CHADEMA imeshinda:
Kijiji Cha LUPINGU imeshinda CHADEMA, kitongoji cha LUPINGU imeshinda CHADEMA kitongoji cha LUKUYUSI bado Matokeo yana ukakasi, kuna vurugu kubwa sanaaaa huko.
Kijiji Cha LUPINGU ina vitongoji 3 mpaka sasa tumeshinda kijiji na kitongoji 1. Kitongoji cha ISANGA wameshinda CCM.
Taarifa Imetolewa na mwenyekiti wa BAVICHA Mkoa wa Njombe, na Lupingu ndiko kijiji anachotokea huyu mwenyekiti.