Baada ya Lissu kufukuzwa uanachama wa chadema mwaka 2025,ungependa aelekee katika chama gani

Wakufukuzwa chadema ni king'ang'anizi Mbowe...hataki kuachia kiti kwa yeyote hata baada ya miaka 21 madarakani!!.
 
Chiembe said:
Chama kipi kinamfaa baada ya kufukuzwa uanachama wa chadema mwaka 2025? Mimi namshauri aende UDP Upendo
Bado dozi anayotoa Lissu haijafika hata robo, viembe tayari vinarukaruka! Hakuna wa kumfukuza Lissu. Endeleeni tu kujipanga kwenye msitari dawa iingie na ikifika tarehe 23/1/23, tutaongea lugha moja!
 
Chama kipi kinamfaa baada ya kufukuzwa uanachama wa chadema mwaka 2025? Mimi namshauri aende UDP Upendo.
Hata mimi naona kuna uwezekano mkubwa wa yeye kufukuzwa na itakua hivi:

Sasa hivi Mbowe atakua yupo bz na wale haswa wanaohusika kupiga kura, lakini TAL yeye anautumia muda huo kuongea sana kwenye social media,,,hii inaweza kumsababishia kushindwa kwenye box la kura.

Akishashindwa kwenye box la kura hata kubali matokeo na ataongea sana kwenye social media kwa jazba na hiyo itasababisha kuitwa kwenye kamati za chama na atakaidi. hali hii itasababisha kufukuzwa kwenye chama.
 
Sahihi kabisa
 
Kwan kauli ya kuhama chama lissu,ni nani kaitoa?.
 
Chama kipi kinamfaa baada ya kufukuzwa uanachama wa chadema mwaka 2025? Mimi namshauri aende UDP Upendo.
CCM itamfaa zaidi. Alete hizi changamoto anazozitoa huko chadema.

Chama kimepoa sana siku hizi. Binafasi namuombea aende Sisiemu. πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Chama kipi kinamfaa baada ya kufukuzwa uanachama wa chadema mwaka 2025? Mimi namshauri aende UDP Upendo.
Baada ya huu uchaguzi. Kosa kubwa linaenda kukimalizia hiki chama ni kumfukuza au kumfutia uanachama.
Ni kukipukutisha chama.
Wote wawili kaeni mkikilinda chama hiki kama ahadi zenu.
Rudini Meza moja myamalize..

Mkiweza pia muwashirikishe viongozi wenu wa kiroho watawasaiidia..
 
Hatutaki hata kumuona CCM .Nyau kabisa.Huko Ubeligiji hakuna vyama akajiunge ? Kwanza hana adabu kabisa.Anamuita rais wetu eti 'Samia na mwanae Abdul' bila hata kusema neno 'Rais". Rais ambaye alimuonyesha upendo hata wakati akiwa kitandani anaugulia risasi .Ama kweli,shukrani ya Punda ni mateke. Hata kama hana adabu kabisa basi aheshimu basi hata umri wake kwani hata huko kwao Singida kuna wakubwa.
 
Chama kipi kinamfaa baada ya kufukuzwa uanachama wa chadema mwaka 2025? Mimi namshauri aende UDP Upendo.
Huyu atakuja na kupokelewa CCM, lakini ni baada ya kakaake Wakili Msomi Mughway Lissu kumuombea msamaha sana!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…