Elections 2015 Baada ya Masheikh wa Bagamoyo, Wachungaji wamzamia Edward Lowassa kumuomba kugombea Urais

Elections 2015 Baada ya Masheikh wa Bagamoyo, Wachungaji wamzamia Edward Lowassa kumuomba kugombea Urais

BREAKING NEWS: UMOJA WA WATU WALIOATHIRIKA NA MAGONJWA YA AKILI (UWAWAMA) wamemchangia Mh. Edward Lowassa shillingi Laki nane na kumsihi kuchukua fomu ya kugombea uraisi wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Akizungumza walipokwenda kumtembelea nyumbani kwake mjini Dodoma wanachama hao wakiongozwa na Mwenyekiti wao Ndugu Taabani Maajabu walimueleza kuwa wamesukumwa kumuomba Mh. Lowassa kugombea kutokana na umahiri wake katika kusimamia uboreshwaji wa sekta ya afya wakati akiwa waziri Mkuu wa kwanza wa Awamu ya nne. Waathirika hao wamemuelezea waziri Mkuu huyo mstaafu aliyekuwa karibu na wagonjwa wengi nchini na hasa waathirika wa magonjwa ya akili kuwa mtu shupavu na mbisho aliyewapigania sana kuanzisha mifuko yao ya maendeleo alipokuwa waziri mkuu. Kwa kutambua uwezo wake waathirika hao wa magonjwa ya akili wamemuomba Mh. Lowassa asisite kuchukua fomu na wao watakuwa nyuma yake kuhakikisha wanampigania mpaka kufikia mwisho wa safari mpya ya matumaini.
 
Pwahahhahha.....Hatimae wachungaji wa pentekoste kutoka wilaya zote tanzania waenda nyumbani kwa Lowassa dodoma kumshawishi achukue fomu ya urais
Wamesema mungu kawaonyesha na wanamwamini ni kiongozi bora
Acha EL andelee na Sinema!

Wanamchunga nani? Wamesahau Richmond, ama kweli njaa ya self proclaimed bishops, wachungaji!
 
hakuna namna ya kuuzima huu moto.badala ya kutumia maji,gari za petrol zinapanga foleni!!mie yangu macho!!mwaka huu raha kweli kweli!!!!
 
Mh lowasa aliyekumbwa na kasheshe ya RICHMOND kawakusanya wachungaji wa pentekoste ili waweze kumfagilia mjini dodoma. maswalivyangu ni je....
1. mungu amewatokea wote kwa wakati mmoja wakutane dodoma kumfagilis?
2. hamis mgeja toka shinyanga ameambiwa na nani kuwa wachungaji wameoteshwa na watakutana dom kumfagilia jamaa?
3. nani kawalipa nauri na pesa xa kujikimu dodoma?
4.je wachungaji toka bihalamulo,kasulu na iringa kweli waumini wanazo hizi taarifa
5. umati huu ni mkusanyiko, PRC wa dodoma ametoa kibali? kama hajatoa, je tiss na polisi mnafanya nini?. ni aibu kwa serkali ya ccm na mkuu wa polisi
 
View attachment 237107

View attachment 237108

Leo katika Hali isiyo ya kawaida wachungaji wavamia Eneo la Area D ambapo ni Makazi ya viongozi mbali mbali wakimsaka Edward Lowassa. viongozi hao wa dini walikuwa na shauku kubwa na nyuso za furaha wakiimba nyimbo za matumaini Mapya na Edward lowassa.

Aidha misururu hio imesababisaha Ndugu Samwel Sita kusubiri kwa Muda kupisha viongozi hao kwenda kuiona nuru ya MATUMAINI. pia ilimuwia vigumu ndugu Fredric Sumaye kuwahi appointments yake na Spika wa Bunge kupisha msafara takatifu kwenda Jirani yake Edward Lowassa.

Mambo yanazidi kupamba moto kuelekea nuru ya matumaini kwa Watanzania ambao mara zote wamuonapo Edward Lowassa hupata faraja.

Wachungaji hao wametabiri na kuahidi kunena kwa vitendo, na mpaka sasa bado wanaendelea kujieleza ni nini wanacho muahidi bwana Edward Lowassa kama balozi wamuaminiye katika safari ya MATUMAINI,

Nitaendelea kukujuza.

MAAMUZI NA MATUMAINI MAPYA NA EDWARD LOWASSA 2015.

Hivi John Okello wewe ni nani kwa EL?? Samahani ningependa kujua tu mkuu...wala sina nia mbaya kuuliza
 
Pwahahhahha.....Hatimae wachungaji wa pentekoste kutoka wilaya zote tanzania waenda nyumbani kwa Lowassa dodoma kumshawishi achukue fomu ya urais
Wamesema mungu kawaonyesha na wanamwamini ni kiongozi bora
Acha EL andelee na Sinema!

Waumini Wanatoa Sadaka Zao Kwa Shida Huku Wakijifunga Mkwiji Wao Wanazitumbua Tu Kwa Kujipendekeza. Kumbe Sikukosea Kuacha Kusali Huko Makanisani Na Kuamua Tu Kugeukia Kusali Kwa Miungu Yangu Ya Kizanaki / Kitutsi Na Kiyao Kwani Hainiombi Sadaka Na Inanibariki Kuliko Hata Huko Kwa Hao Wanafiki.
 
Bado natazama tu sijajua mantiki ya haya mambo. hali hii ilianza kidogokidogo na sasa inakomaa. Sasa vyombo vya uteuzi vya CCM vitaangalia hawa waandamaji au utaratibu wao.
Naamini mtu afaaye ameshachunguzwa na vyomo mbali mabali kama usalama wa taifa watu maarufu kama maraus wastaafu nk. kwa hivo hao watamshawishi huyo mtu huyo kuchukua fomu kama Nyrere alivomshawishi Mkapa.
kwangu mimi haya yanayotokea ni kama fujo tu. hayawatendei haki watarajiwa wengine. tena pale viongozi wa dini wanapofanya hivi ni hatari sana ni kama kushinikiza. wangeweza kupendekeza kwa namna nyingine kama kwenda kwa rais, kuandika barua labda kwa viongozi wa ccm na sio kukimbizana mabarabarani. Naanza kutia shaka credibilty ya viongozi wetu wa dini.
 
Mungu amlinde RAISI WETU, RAISI WA WANYONGE,EDWARD LOWASSA.
 
kweli tanzania tumekwisha,hivi vikanisa vidogo vina matatizo sana,hasa kwenye upande wa pesa wana njaa sana .nasikia EL kampa pesa MGEJA kawapata hao wachungaji njaa,nimefuatilia karibu wote ndio wale makanisa yapo nyumbani yeye na familia yake ndIo waumini,kweli kiongozi anayetoa rushwa ili aende ikulu nikumwogopa kama ebola. ccm kazi tunayo
 
Inakuaje watu kutoka pande zote za Tanzania kutoka makundi tofauti wakaenda kwa Lowasa Siku moja?
 
Nyumba ya Lowassa iko busy kawa ward ya akina mama wajawazito.
 
Kinanipelekea kukubali Lowassa achukue nchi, ni kutoa Kibano kwa wale wote waliokuwa wakishutumu.. Penye ugomvi, mengi yataibuka yatakayotusaidia.. Kuna watu watakimbia nchi hii..
Lowassa lazima atalipa kisasi tu, Kupitia vyombo vinavyohusika
 
Back
Top Bottom