Baada ya Mbowe kugeuka na kuwa kama kina Shibuda, John Cheyo na Mrema ni upi mustakbali wa siasa za upinzani Tanzania?

Baada ya Mbowe kugeuka na kuwa kama kina Shibuda, John Cheyo na Mrema ni upi mustakbali wa siasa za upinzani Tanzania?

Wapinzani sisi hatuelewi huo msimamo wa viongozi wa CDM kwa muongozo wa Mbowe. Wao viongozi waendelee na siasa za kujikomba, lakini sisi hatuna muda huo. Kama Mbowe aliweza kumpokea Lowassa na watu wakamvumilia, basi safari hii atajua hana ushawishi huo aliodhani anao. Ni muda mrefu Mbowe alishaonyesha kupoteza mwelekeo.
Naona Tindo akili zako zinaanza kurudi sikutegemea kama utaandika hiki nikadhani labda account yako imekuwa hacked
 
Kama huwezi kuyaona maendeleo kwa kuwa wewe ni KIPOFU, hatuna msaada na wewe
Kwa hii miaka 60 unajisifu kwa maendeleo gani yenye kuendana na huo umri? Kama sasa wewe unaona kuna maendeleo najiuliza tafsiri ya kutokuwa na maendeleo kwa upande wako ni ipi?
 
Kwa hali inavyoendelea nchini ni dhahiri hakuna tena upinzani. Bali kuna uungwaji mkono juhudi wa Wapinzani kwa CCM kila mmoja kwa staili yake. ACT Wazalendo wanakula pamoja na CCM kule Zanzibar na CHADEMA nao wanatafuta robo mkate wao huku Tanganyika.

Kabla CHadema hawajaanza kupetiwapetiwa, Kutomaswatomaswa na kulambishwa asali na CCM hii ya leo ya Kinana na Samia, walikuwa wakitokwa povu sana kuhusu ACT Wazalendo kuingia katika serikali ya umoja wa Kitaifa huko Zanzibar. ACT walikuwa wakijitetea kuwa eti ni takwa la kikatiba kuingia humo huku CHADEMA wakiwaita ACT Wasaliti kwa hoja ya kuwa wamewasaliti Wazanzibar kwa kushiriki kula matunda ya uchaguzi haramu.

Leo tunaona CHADEMA nao wamekinga mkono kula ruzuku ambayo hapo mwanzo walisema ni haramu kwa kuwa imetokana na uchaguzi haramu. Kiufupi wamelamba matapishi yao!.

Ukiachilia mbali hilo, CHADEMA walikuwa wakijulikana sana kuwatukana akina hayati Lyatonga Mrema , John Cheyo na Shibuda kuwa eti ni makada wa CCM kutokana na kuwa na siasa za mrengo wa kukubaliana na CCM katika mambo mengi. Leo tunamuona Mwenyekiti Mbowe naye akigeuka kuwa Cheyo na Shibuda aliyechangamka zaidi.

Mbowe leo kaibeba rasmi mikoba ya John Cheyo na ameanza kutumia arguments zilezile za John Cheyo kuwa anataka siasa za "maridhiano", ambazo kimsingi siasa za hivyo ni za kutomasanatomasana, kubembelezanabembelezana ilimradi tu kila mtu aachiwe sphere yake ya influence ili aweze kula kwa urefu wa kamba yake.

Tujiulize, Hizi sifa ambazo Mbowe anazitoa kwa Samia zina tofauti gani kwa mfano na Sifa za Cheyo au Shibuda walizokuwa wakizimwaga kwa Magufuli?

Hii inaonyesha kuwa pengine ukiwa mpinzani na ukaanza kuzeeka, unaanza kuwa na tabia za OLD MAN CCM SYNDROME. Yaani unaanza kuwa na tabia zile za kiCCM CCM. Unaanza kujisogeza kwa CCM, unaanza kuongea kama wanaCCM, na unaanza kubehave kama wanaCCM

Huu ni muda muafaka kwa wanaCHADEMA kumtafakari Mwenyekiti Mbowe kuona kuwa , Je ni kweli siasa hizi za kulala kitanda kimoja na CCM anazoanza kuzifanya zinatokana na utafiti wa kina na upeo wa kisiasa au zinatokana na

1. Mosi, Je ana makubaliano ya siri na CCM ikiwa kama sababu ya kuachiwa kwake Jela na kwa hivyo anafuata script aliyotengenezewa AU

2. Je ana masilahi bianfsi ikiwemo ya kibiashara au kurudishiwa mali zake alizoporwa na serikali ya CCM kipindi cha Mwendazake?

3. Au je ni uzee na uchovu(wa Kisiasa) kwa hiyo ndo ameamua kwenda na falsafa maarufu ya "Kama huwezi kuwashinda, basi ungana nao?".

Katika nchi yoyote ukiona UPINZANI unafanya ROMANCE na Chama Tawala, Jua kuwa hakuna upinzani hapo bali kuna genge la wapiga dili wa kisiasa
Ina maana kuwa kweli huoni tofauti kati ya agenda ya kina Shibuda na hii ya Mbowe....!!?
 
Swali la msingi sana.Aeleze alivyotaka CDM ingefanya siasa za aina ipi?Je,wapigane ngumi?Waue watu?Wafanye ugaidi?Wapindue serikali?Watukane asubuhi ya leo hadi keshoye kwa mtiririko?Au ana chama chake mbadala akilete kifanye atakacho?
Mrema na lipumba walipofanya hivyo mbona mliwatukana?
 
Mfano south afrika wakati mandela kafungwa watu walikua wanaandamana
Ila Tanzania wakati mbowe na chadema wanashughulikiwa wote tulikua kimya alafu leo hii ndo tunajikuta tunauchungu wa mapambano kwanin ulikuwa huwatetei wakati wanateseka tuacheni unafki

Wewe umekaa nyuma ya keyboard alafu unataka wanaume wakupiganie maisha hayako na wahatarishe maisha yao na familia zao hivyo usipende sana mterereko we ni wa kiume
Chadema hawajawahi kuandamana kwa maslahi ya wananchi ndio hakupata sapoti kubwa ya watu Chadema inaandamana kwa mlengo wa maslahi ya chama chao ngoja nikuulize umekuona Chadema imeandamana kwasababu ya vitu kupanda bei? Missile of the Nation Hili swali kwanini Chadema hawapendagi kulijibu
 
Mimi naunga mkono chadema Kwa walichofanya, wametumia akili kubwa, coz uwez kubishana na serikali never

Chadema walikaa bila mikutano, walikaa bila mikutano ya ndani, walikuwa wanakamatwa kila siku, wanafungwa, na nyie mnao piga kelele sasa mlikuwa mnatengeneza watoto Tu nyumbani kwenu

Sasa now wameamua kusikilizana na serikali ili Tu warudi kwenye platforms upya, nyie mnaanza kelele sijui hata mnataka nn

Kudeal na serikali za kiafrika ni ngumu Sana, kushindana na serikali ni ngumu sana, serikali inaweza kufanya Jambo lolote

Mfano ishu ya wakina mdee, si unaona mpaka Leo ni wabunge? Na wote tunajua hawakutakiwa kuwa wabunge?

Hiyo ndio nguvu ya serikali,

Mbowe ameamua kuanza upya, chama kipate Ruzuku yake, Chama kishiriki Uchaguzi, Chama kipate wabunge hapo sasa ndio kitakuwa chama pinzani

Uwez kuwa chama pinzani na upinzani wako unafanya kwenye keyboard tu
Mrema na lipumba walipokuwa wakifanya hayo mbona mliwatukana?
 
Kwa hali inavyoendelea nchini ni dhahiri hakuna tena upinzani. Bali kuna uungwaji mkono juhudi wa Wapinzani kwa CCM kila mmoja kwa staili yake. ACT Wazalendo wanakula pamoja na CCM kule Zanzibar na CHADEMA nao wanatafuta robo mkate wao huku Tanganyika.

Kabla CHadema hawajaanza kupetiwapetiwa, Kutomaswatomaswa na kulambishwa asali na CCM hii ya leo ya Kinana na Samia, walikuwa wakitokwa povu sana kuhusu ACT Wazalendo kuingia katika serikali ya umoja wa Kitaifa huko Zanzibar. ACT walikuwa wakijitetea kuwa eti ni takwa la kikatiba kuingia humo huku CHADEMA wakiwaita ACT Wasaliti kwa hoja ya kuwa wamewasaliti Wazanzibar kwa kushiriki kula matunda ya uchaguzi haramu.

Leo tunaona CHADEMA nao wamekinga mkono kula ruzuku ambayo hapo mwanzo walisema ni haramu kwa kuwa imetokana na uchaguzi haramu. Kiufupi wamelamba matapishi yao!.

Ukiachilia mbali hilo, CHADEMA walikuwa wakijulikana sana kuwatukana akina hayati Lyatonga Mrema , John Cheyo na Shibuda kuwa eti ni makada wa CCM kutokana na kuwa na siasa za mrengo wa kukubaliana na CCM katika mambo mengi. Leo tunamuona Mwenyekiti Mbowe naye akigeuka kuwa Cheyo na Shibuda aliyechangamka zaidi.

Mbowe leo kaibeba rasmi mikoba ya John Cheyo na ameanza kutumia arguments zilezile za John Cheyo kuwa anataka siasa za "maridhiano", ambazo kimsingi siasa za hivyo ni za kutomasanatomasana, kubembelezanabembelezana ilimradi tu kila mtu aachiwe sphere yake ya influence ili aweze kula kwa urefu wa kamba yake.

Tujiulize, Hizi sifa ambazo Mbowe anazitoa kwa Samia zina tofauti gani kwa mfano na Sifa za Cheyo au Shibuda walizokuwa wakizimwaga kwa Magufuli?

Hii inaonyesha kuwa pengine ukiwa mpinzani na ukaanza kuzeeka, unaanza kuwa na tabia za OLD MAN CCM SYNDROME. Yaani unaanza kuwa na tabia zile za kiCCM CCM. Unaanza kujisogeza kwa CCM, unaanza kuongea kama wanaCCM, na unaanza kubehave kama wanaCCM

Huu ni muda muafaka kwa wanaCHADEMA kumtafakari Mwenyekiti Mbowe kuona kuwa , Je ni kweli siasa hizi za kulala kitanda kimoja na CCM anazoanza kuzifanya zinatokana na utafiti wa kina na upeo wa kisiasa au zinatokana na

1. Mosi, Je ana makubaliano ya siri na CCM ikiwa kama sababu ya kuachiwa kwake Jela na kwa hivyo anafuata script aliyotengenezewa AU

2. Je ana masilahi bianfsi ikiwemo ya kibiashara au kurudishiwa mali zake alizoporwa na serikali ya CCM kipindi cha Mwendazake?

3. Au je ni uzee na uchovu(wa Kisiasa) kwa hiyo ndo ameamua kwenda na falsafa maarufu ya "Kama huwezi kuwashinda, basi ungana nao?".

Katika nchi yoyote ukiona UPINZANI unafanya ROMANCE na Chama Tawala, Jua kuwa hakuna upinzani hapo bali kuna genge la wapiga dili wa kisiasa
Upinzani siyo kupinga kila kitu hata kiwe cha maana na kutukana.
 
Sio rahisi hivyo!!Nyie wafuasi wa MEKO tunajua hiki kinachoendelea kinawauma sana!!mlitaka ziendelee zile siasa za kishenzi tu!!kwani mlikuwa mnafaidika nazo!!wewe una uchungu na CDM kuliko mbowe??
Huyo unayemponda ni Chadema mwenzako Tena ana kadi kabisa ya hicho chama hii ndio shida yakufikiri kila anayeponda maridhiano ni shabiki wa Magu
 
Chadema hawajawahi kuandamana kwa maslahi ya wananchi ndio hakupata sapoti kubwa ya watu Chadema inaandamana kwa mlengo wa maslahi ya chama chao ngoja nikuulize umekuona Chadema imeandamana kwasababu ya vitu kupanda bei? Missile of the Nation Hili swali kwanini Chadema hawapendagi kulijibu
NI lini chadema wamerusiwa kuandamana hapa Tanzania
 
Mkuu unajitoa ufahamu ukumbuki kampeni ya UKUTA?
Ilifanikiwa kwani???? mbona haikufanikiwa
Niambie ni lini chadema wamerusiwa kuandamana nchi hii ya Tanzania, majaribio yote ya maandamano yalikuwa yanazuiwa na polisi

Ni uongo wa wazi kusema chadema walishawah kuandamana
 
Back
Top Bottom