Baada ya Mbowe kugeuka na kuwa kama kina Shibuda, John Cheyo na Mrema ni upi mustakbali wa siasa za upinzani Tanzania?

Baada ya Mbowe kugeuka na kuwa kama kina Shibuda, John Cheyo na Mrema ni upi mustakbali wa siasa za upinzani Tanzania?

Usituchoshe na swaga zako za kumwandama mwenyekiti bora kabisa. Kama umemchoka au umewachoka Chadema ishilia mbali. Kila siku kumshambulia Mbowe tu basi. Wewe umesacrifice nini kwa chama badala ya tararira zako za kila siku.
Utatulia tu.
 
Akili zangu ziko vizuri, ila misimamo yangu haiendani na matamanio yako.
Mimi sio mpenzi wa vyama vyenu, mtazamo wangu Mara nyingi umejikita kwenye maslahi ya wananchi na washangaa nyinyi mnaojitoa ufahamu kisa una mapenzi na chama fulani so hata kikosea hakipaswi kusema kutokana na hizo fikra mnajikuta mpo chama kimoja tofauti ya mitazamo yenu mmoja anamuona mwenzio ni msaliti hama ni mshabiki wa chama kingine.Kama aina hii ya siasa ngumu vyama vyenu kuendelea
 
Mimi sio mpenzi wa vyama vyenu, mtazamo wangu Mara nyingi umejikita kwenye maslahi ya wananchi na washangaa nyinyi mnaojitoa ufahamu kisa una mapenzi na chama fulani so hata kikosea hakipaswi kusema kutokana na hizo fikra mnajikuta mpo chama kimoja tofauti ya mitazamo yenu mmoja anamuona mwenzio ni msaliti hama ni mshabiki wa chama kingine.Kama aina hii ya siasa ngumu vyama vyenu kuendelea

Mkuu ni maslahi yapi ya wananchi umesimamia boss? Ungekuja na jina lako halisi ili tuone ulichowasaidia wananchi. Sasa uko na fake I'd kisha unasema unasimamia maslahi ya wananchi.
 
Kwa hali inavyoendelea nchini ni dhahiri hakuna tena upinzani. Bali kuna uungwaji mkono juhudi wa Wapinzani kwa CCM kila mmoja kwa staili yake. ACT Wazalendo wanakula pamoja na CCM kule Zanzibar na CHADEMA nao wanatafuta robo mkate wao huku Tanganyika.

Kabla CHadema hawajaanza kupetiwapetiwa, Kutomaswatomaswa na kulambishwa asali na CCM hii ya leo ya Kinana na Samia, walikuwa wakitokwa povu sana kuhusu ACT Wazalendo kuingia katika serikali ya umoja wa Kitaifa huko Zanzibar. ACT walikuwa wakijitetea kuwa eti ni takwa la kikatiba kuingia humo huku CHADEMA wakiwaita ACT Wasaliti kwa hoja ya kuwa wamewasaliti Wazanzibar kwa kushiriki kula matunda ya uchaguzi haramu.

Leo tunaona CHADEMA nao wamekinga mkono kula ruzuku ambayo hapo mwanzo walisema ni haramu kwa kuwa imetokana na uchaguzi haramu. Kiufupi wamelamba matapishi yao!.

Ukiachilia mbali hilo, CHADEMA walikuwa wakijulikana sana kuwatukana akina hayati Lyatonga Mrema , John Cheyo na Shibuda kuwa eti ni makada wa CCM kutokana na kuwa na siasa za mrengo wa kukubaliana na CCM katika mambo mengi. Leo tunamuona Mwenyekiti Mbowe naye akigeuka kuwa Cheyo na Shibuda aliyechangamka zaidi.

Mbowe leo kaibeba rasmi mikoba ya John Cheyo na ameanza kutumia arguments zilezile za John Cheyo kuwa anataka siasa za "maridhiano", ambazo kimsingi siasa za hivyo ni za kutomasanatomasana, kubembelezanabembelezana ilimradi tu kila mtu aachiwe sphere yake ya influence ili aweze kula kwa urefu wa kamba yake.

Tujiulize, Hizi sifa ambazo Mbowe anazitoa kwa Samia zina tofauti gani kwa mfano na Sifa za Cheyo au Shibuda walizokuwa wakizimwaga kwa Magufuli?

Hii inaonyesha kuwa pengine ukiwa mpinzani na ukaanza kuzeeka, unaanza kuwa na tabia za OLD MAN CCM SYNDROME. Yaani unaanza kuwa na tabia zile za kiCCM CCM. Unaanza kujisogeza kwa CCM, unaanza kuongea kama wanaCCM, na unaanza kubehave kama wanaCCM

Huu ni muda muafaka kwa wanaCHADEMA kumtafakari Mwenyekiti Mbowe kuona kuwa , Je ni kweli siasa hizi za kulala kitanda kimoja na CCM anazoanza kuzifanya zinatokana na utafiti wa kina na upeo wa kisiasa au zinatokana na

1. Mosi, Je ana makubaliano ya siri na CCM ikiwa kama sababu ya kuachiwa kwake Jela na kwa hivyo anafuata script aliyotengenezewa AU

2. Je ana masilahi bianfsi ikiwemo ya kibiashara au kurudishiwa mali zake alizoporwa na serikali ya CCM kipindi cha Mwendazake?

3. Au je ni uzee na uchovu(wa Kisiasa) kwa hiyo ndo ameamua kwenda na falsafa maarufu ya "Kama huwezi kuwashinda, basi ungana nao?".

Katika nchi yoyote ukiona UPINZANI unafanya ROMANCE na Chama Tawala, Jua kuwa hakuna upinzani hapo bali kuna genge la wapiga dili wa kisiasa
Mkuu uwe unaandika hoja yenye maantiki. Hao ambao unawafananisha na Mbowe wamepata kuwekwa jela, kuharibiwa mali zao ama hata kufungiwa fedha? Mbowe ameyapitia. Wakati hayo yote yanatendeka wewe na wezako wa aina yako mlikwenda walau kumpa pole? Mwache Mbowe na mama, Rais wetu mpendwa waturejeshee heshima ya Taifa letu, lirudi katika uhalisia wake kama zamani.
Ilifikia hatua hataki mwana ccm aende kumuanglia mwanachadema kama anaumwa
Siasa sio uadui ila kwa magufuli siasa ni uadui
Mkuu yaani mke wangu ni CHADEMA na anaumwa imempanda ile mbaya na mimi Mjumbe CCM Kata nisiende kumwana mke wangu? Kweli hali ile ilikuwa ngumu kumeza.
 
Wapinzani sisi hatuelewi huo msimamo wa viongozi wa CDM kwa muongozo wa Mbowe. Wao viongozi waendelee na siasa za kujikomba, lakini sisi hatuna muda huo. Kama Mbowe aliweza kumpokea Lowassa na watu wakamvumilia, basi safari hii atajua hana ushawishi huo aliodhani anao. Ni muda mrefu Mbowe alishaonyesha kupoteza mwelekeo.
Umeanza kuwa na akili
 
Mkuu uwe unaandika hoja yenye maantiki. Hao ambao unawafananisha na Mbowe wamepata kuwekwa jela, kuharibiwa mali zao ama hata kufungiwa fedha? Mbowe ameyapitia. Wakati hayo yote yanatendeka wewe na wezako wa aina yako mlikwenda walau kumpa pole? Mwache Mbowe na mama, Rais wetu mpendwa waturejeshee heshima ya Taifa letu, lirudi katika uhalisia wake kama zamani.

Mkuu yaani mke wangu ni CHADEMA na anaumwa imempanda ile mbaya na mimi Mjumbe CCM Kata nisiende kumwana mke wangu? Kweli hali ile ilikuwa ngumu kumeza.
Jela siyo hoja. Watu wema na hata majambazi hukaa jela
Ishu hapa ni kuanza kufanya siasa zilezile za akina Shibuda
 
Watanzania wengi wana PhD lakini hawajui hicho kingereza, kama nasema uongo mwambie Profesa Ndalichako aongee sentensi kumi za kiingereza fluently bila hesitations.
Mkuu unamwingizaje huyo mama humu? Haipendezi! Humu tunatakiwa kutoa hoja kulingama na hoja iliyotolewa.
 
Tuacheni kejeli instead tuwapongeze Samia na Mbowe kwa kuweka masilahi ya nchi yetu mbele kuliko kitu kingine chochote.

Hii nchi angeendelea kuwa hai yule HAYAWANI wa Chato ingekuwa nchi ya hovyo kuliko Yemen na Somalia
Muache aendee kuoza huko aliko
Sahihi ni maslahi ya wanasiasa, maslahi ya nchi ni hapana.

Sent from my TA-1033 using JamiiForums mobile app
 
Watanzania bado hawajataka mabadiliko, ndio maana matumaini yako kwa wana-siasa, tunaishia kuwalalamikia wakati wao wako kwa maslahi yao pia.

Sent from my TA-1033 using JamiiForums mobile app
 
Jela siyo hoja. Watu wema na hata majambazi hukaa jela
Ishu hapa ni kuanza kufanya siasa zilezile za akina Shibuda
Mkuu hapo ndipo unapo changanya mambo jambazi kuwekwa jela ni sahihi maana ni jambazi na imethibitishwa na mamlaka husika kwamba ni Jamani na aende jela. Sasa Mbowe ni jambazi ki-vipi mpaka umfananishe na hoja yako.
 
Mkuu hapo ndipo unapo changanya mambo jambazi kuwekwa jela ni sahihi maana ni jambazi na imethibitishwa na mamlaka husika kwamba ni Jamani na aende jela. Sasa Mbowe ni jambazi ki-vipi mpaka umfananishe na hoja yako.
Nimesema kuwa watu wema na majambazi wote hujikuta jela sometimes kutokana na mazingira fulanfulani hivi lakini jela isiwe sababu ya kuwafanya watu wema wapoteze misimamo yao mizuri kwa hofu ya kwenda jela tena kama wema wao ndo ulipelekea wakabambikiziwa kesi
 
Mkuu u
Jela siyo hoja. Watu wema na hata majambazi hukaa jela
Ishu hapa ni kuanza kufanya siasa zilezile za akina Shibuda
Mkuu usimfananishe Mbowe na hao wengine, itaonekana aidha hauzijui siasa za hapa nchini ama wakati vyama vingi vinaanzishwa ulikuwa mdogo. Mbowe hajawahi kuhama chama chake. Kama angetaka angeweza
 
Kuteseka ni sehemu ya struggle. Kama hutaki kuteseka kaa pembeni ili walio tayari hata kufa ili kuleta mabadilikio ya kweli washike usukani. Kuliko kusaliti stuggle na kuanza kujikombakomba kwa CCM bora ukae pembeni ulee wajukuu au ule bata kadri unavyoweza
Mkuu wakati ule Mbowe amekaa pembeni (jela) kinyume na taratibu mbona wewe haukujitokeza kuongoza harakati.
 
Nimesema kuwa watu wema na majambazi wote hujikuta jela sometimes kutokana na mazingira fulanfulani hivi lakini jela isiwe sababu ya kuwafanya watu wema wapoteze misimamo yao mizuri kwa hofu ya kwenda jela tena kama wema wao ndo ulipelekea wakabambikiziwa kesi
Mkuu mbona unatoa Hoja kama nchi yetu inatawaliwa ki-dictate? Hii ni nchi ya vyama vingi, hivyo lazima vyama vikae pamoja na kuzungumza masuala ya Nchi kwa mustakabali wa maendeleo ya Nchi. Miaka 6 iliyopita haikuwa hivyo ndio maana wale wenye roho nyepesi walihongwa
fedha ama vyeo, na kama yeye angekuwa na roho yepesi angetumbukia huko.
 
Tumeshawekeza nguvu nyingi sana kupitia CHADEMA kiasi kwamba ikianza kuwa CCM B tunakuwa tumepoteza miaka mingi sana ya nguvu tuliyoitumia kwenye chama hicho ambacho tumekisaidia kufika hapa kilipo kwa machozi, jasho na damu
Mkuu waliopoteza nguvu nyingi wanajulikana, aidha wewe umepotezea humu JF tena nyuma ya keyboard. Wezio walikuwa front, walioteleza wanajulikana na waliojeruhiwa wanajulikana.
 
Sasa ndo wavae viatu vya Cheyo na Shibuda kwa kasi namna hii?.

Maana hata kina Cheyo argument yao ya kujikomba kwa CCM ni hiyohiyo mnayoita siasa za "kisataarbu"
Sasa si ulete wazo mbadala ?!. Unabeza huku huna lolote la tofauti !!.

Kama ulimsikiliza Samia vizuri. Alisema "kuna nchi huko zimepigana vita vya silaha misituni , bado suluhu haikupatikana. Suluhu ilikuja kupatikana ktk mazungumzo mezani"

Sasa wewe kama hutaki mazungumzo lete njia mbadala. Tuione hasa kwa nature ya waTz
 
Chawa mnamaumivu makali kama vile mmepitshiwa pasi ya umeme. Mnajisikia vibaya pale mama asivyopenda visasi kama mtangulizi siyo !!

Poleni chawa
Mkuu yaani wameumia sana jana, bado mtaumia sana. Jirekebisheni zama zinabadirika kwa kasi sana.
 
Ajabu hata hao wanachama wao wa chadema hakuna walichofanya wakati akina Mbowe wanapitia mateso.
Mkuu wewe ndio hukujua walichokuwa wanafanya kwa sababu furaha yako kubwa sana. Wenzio walikuwa wamezama katika MAOMBI mazito ambayo yamekufichua wewe kutoka huko kwenye mema ya Nchi, ni kama vile kiroboto kwenye ngozi ya ng"ombe,
 
Back
Top Bottom