Baada ya njia za giza kugonga mwamba kwenye kusaka utajiri, nimeamua kufanya hivi

Baada ya njia za giza kugonga mwamba kwenye kusaka utajiri, nimeamua kufanya hivi

dah nmesoma sana ngoja na mimi ntoe kisa kilichosababisha niape kuwa sitakwenda kwa mganga tena kwenye maisha yangu.

ilikuwa 2002,tunatoka dar tunakwenda mkoa wa kigoma kwa wanojua bara bara enzi hizo wanajua ni jinsi gani kulikuwa na majambazi hasa ndani ya mapori ya Tabora,bahati haikuwa yetu mida ya saa 5 usiku wakati tupo road tukakuta bara bara imewekwa bonge la gogo mzee akataka kujitahid aligeuze ghafla walitokea watu wamebeba bunduki ndo kwa mara yangu ya kwanza kuone mtu kashka bunduki huku kajizungushia mkanda wa risasi mwilini bro wangu ile kuwaona tu akakata moto tuliokuwa hatujazmia tulikuwa watatu 3 mimi mzee na bimkubwa.

Tulichezea sana vitasa mzee alidhalilika mno mwisho wa siku walichukua mpka viatu nakumbuka viatu vyangu vya kitoto vya kuwaka taa,then wakaondoka mpka na gari tulikaa pale mpka saa 11 ndo tukapata msaada tukaenda polisi but hawakuwa na msaada mzee akapiga simu kigoma ikatumwa nauli tukaenda moja kwa moja mpka kwa baba yake(means babu),sasa babu yeye kila alivyokuwa anahadithiwa alikuwa anacheka mno hasa akimuangalia bro na ujanja wake ote et kazimia,upande wa baba yeye alikuwa na hasira mno alichokuwa anataka yeye ni wale watu awashikishe adabu hata kufa wafe basi ilivyofika usiku tukaelekea sehemu fulani inaitwa ujiji kwa mzee fulani alikuwa anaitwa juma njemba.

Nadhani kwa watu wa kigoma wanaweza kuwa wanamjua,akaelezewa kila kitu akasema hicho ni kitu kidogo sana,huku na yeye anacheka kisha akasema kuwa pale kwake kuna mbuzi alimchinja sababu ya sherwhe ya mwanae hvyo itatubidi tumtafutie mbuzi mwengne amreplace ili iwe kama malipo yake baba akakubali,kilichofata akawaita wajukuu zake walete (ubumba) ni udongo fulani hivi wa mfinyanzi kisha akawa anatengeneza kimdoli kidogo cha udongo kama vile vya kitoto toto,baada ya kukitengeneza akaanza kukiandika maneno yake kisha akakisimamisha chini,then akaanza kuongea maneno yake aliongea sana baada kama ya saa 1 akasema mtu yoyote ndani ya hichi chumba haruhusiwi kukimbia wala kupiga kelele kwani kwa kufanya hivyo ndo itakuwa kifo chake.

Basi aliendele kusema maneno yake ghafla yule mdoli pole pole alianza kukua na kuwa mkubwa pole pole,baada kama ya dakika arobaini alikuwa ni mkubwa kama binadamu mwenye mwili mkubwa alikuwa anamkono na kifua kikubwa na mrefu,kwa mara ya pili bro tena akazimia kwa mara ya pili mim mkojo ulishantoka natetemeka kama nmepatwa na dege dege,mwisho yule mdoli akaambiwa shtaka letu kisha akaambiwa nenda hivi vitu vinatakiwa leo leo,theb yule mtu akafungua mlango akatoka mbio alikuwa ni mwanaume lakini yupo uchi na ni mweusi tii kama mkaa mpka macho hakuwa na ichi kiini cheupe ye alikuwa na kiini cha moja kwa moja cha weusi,alivyoondoka tukaanza kumpepea na kumwagia maji bro alivyoshtuka yule mzee akatuambia kazi imeshakwisha kesho mtayapata majibu yenu.

Ilivyofika asubuhi tukapigiwa simu nakumbuka enzi hizo kulikuwa kuna buzz siyo hii tigo na hata simu zilikuwa za mezani,tukaambiwa kuwa kuna gari imepatikana Tabora yenye namba kama tuliyoripoti pamoja na vitu vingine,tukaanza safari na treni mpka tabora kufika kule tukakuta vitu vyetu na vingne vingi tu ila mzee alisema vyote vilikuwa vyetu hela zilikuwa kama 1m lakini zilipatikana 7m polisi hawakuchukua hata cent na hata walivyopewa walikataa kata kata hakikupotea hata kifungo kisha baada ya kuchukua tukaambiwa kuwa hao majambazi waliotuibia walikutwa msituni wakiwa wameuwawa wakasema wanahisi ni wanyama wakali ndo waliwauwa maana walikuwa wanaalama za meno makali milini mwao na kucha.

lakini wakashndwa kuelewa kama ni wanyama ndo waliwashambulia ni wanyama aina gani na kwanini hawakuwapiga hata risasi moja hao wanyama na wakati walikuwa na silaha nzito?Baada ya maelezo mengi mzee akawasha gari mpka kigoma stend ya kwanza mpka kwa yule mganga tulinunua mbuzi na zawadi nyingne nying lakini mzee aligoma hakutaka chochote zaidi ya mbuzi tu,basi tukampka mbuzi wake, akasema imebaki kazi moja tu na kazi yenyewe ni kumrudisha yule kiumbe(mdoli mtu)ili asitudhuru na sisi maana ni wetu hapo mdipo ilipokuwa mtihani maana kuna msharti mengi tulikosea plus kujisahau sasa akawa anatuandama sisi atuue dah kila mmoja nyumbani anaalama ya yule kiumbe yangu ni kungatwa skio na kula kipande nikipata mda ntawamalizia kisa changu but mpka leo mimi kwenda kwa waganga ni big no,but thanks god tulitoka salama

picha ya nilipongatwa kwenye skio ambyo ni alama ambayo sitaweza isahau mpka kifo

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
Hahaha andika uzi mkuu

Sent from my TECNO WX3 using JamiiForums mobile app
 
Kaka ulipitia magumu sana, pole kwa hayo umenikumbusha na mm niliwahi kupanda mliman nadhan wakaz wa Mwanza wanaelewa jiji lilivyo. Aise sasa nmemalza kukwich na mke wa mtu ilikuwa kama saa 6 ucku nikaamua kurud aiseee nilikuta na fisi wa kufa kufa yan niljikuta nipo gheto lkn kesho yake sasa nilikuwa nakanda tu vidonda

Sent using Jamii Forums mobile app
Hiki kisa ujege ukisimulie muraa
 
"Mwanangu Endelea kupambana"

Hii line ni fupi sana lakini ina maana nyingi ndani yake,inaumiza,inasikitisha na inaliza pia. Leo nilikua napitia uzi wako flani jooohs kati kati ndio nikakuta link ya huu uzi wako,nikau click naangalia ni wa lini naona eti ni uzi wa APRIL nimeshangaa sana.

imekuaje sijaona uzi kama huu uliochangiwa mpk kufika page ya 64,yani ni sawa na member wa JF aseme haujui uzi wa mshanar ule wa snap it,show it au uzi wa kula tunda kimasihara hizo ni nyuzi ambazo huwezi kuwa member wa JF usizijue.

mimi leo ndio naona huu uzi nimesoma page kwa page nimejifunza mengi sana,unajua duniani bado kuna mapya mengi hatujayasikia namimi leo kuna mapya nilikua sijawahi yasikia ila nmeyasoma toka kwa muhusika kbsa,Asante kwa somo hili.

Jooohs "Mwanangu Endelea kupambana" usisahau kauli hii ya huyu rafiki yako ikawe chachu ya wewe kuinuka hata utakapoona umedondoka kabisa usichoke kupambana,kila mtu ana verse/line ambayo hatokaa aisahau ktk maisha yake iliyotoka kwa mtu anaemjua/mpenda/rafiki/mzazi/ndugu,nk

Mimi nakumbuka baada ya kuchokwa na ndugu/marafiki kwasababu ya tabia yangu ya kuomba hela wanisaidie,kuna kaka mmoja (si ndugu yangu) ni mkubwa kwangu nilimzoea kiasi huwa nilikua nikiomba hela kwa ndugu wote wakininyima yeye huwa ndio mtu wa mwisho mimi kumuomba,na alikua akinipa kweli.

siku 1 Baada ya kuchoka ile omba omba hela kwa ndugu nikaamua kwenda tafuta maisha,nikiwa njiani nikasema acha niombe ndugu na jamaa hela mara ya mwisho maana najua ndio sitokuja waomba tena na tena,kama ilivyo kawaida wote walinichomolea,Nikawa na mtu wa mwisho ambaae n yule kaka alikua akiitwa Thomas (tom) nikampgia simu Tom nikamwambia naomba nisaidie hela kidogo nimeamua kwenda tafuta maisha nimefika hapa sina pakulala wala sijala hadi saivi.

Akanipgia simu akaongea sana na ktk ongea yake alinieleza kwa kifupi historia ya maisha yake mpk pale alipo namwsho akaniambia line ambayo sitokaa niisahau hadi leo hiii

"Mdogo wangu Huko ulipo upo katika mkoa wa watu,hamna anaekujua ACHA AIBU fanya kazi yeyote ile inayokuja mbele yako ila tu Usiibe cha mtu/usiwe mwizi"

leo
sina hela kwenye simu nina 10,000 tu ila nitakutumia mdogo wangu uanzie maisha,TOM alinitumia sh.9000 kwenye simu baada ya pale akaniambia Ukabarikiwe mdogo wangu. akaniaga.

ile kauli yake imekua kama muhuri ktk maisha yangu,sijawahi isahau kila ninapoikumbuka Nimefanya kazi za ajabu sana mimi ktk haya maisha na yote ni kwasababu ya ile kauli ya TOM haikuwahi futika na haitofutika.

Jooohs kauli ya rafiki ako imebeba ujumbe mwingi ndani yake,si rahisi kuielewa lakini kama si zile kelele pale kwenye nyavu wakati umeenda msalimia mngepata kuongea angekwambia mengi sana sana lkn aliamua kufupisha yote na akayaweka yote aliyotaka kukwambia ile siku ktk line 1 tu.

"Mwanangu Endelea Kupambana"


Usimuangushe narudia tena

Usimuangushe Augustino..
 
Wakati mwingine unafika kipindi kigumu mpaka unaona mbele kote ni Giza tu, mpaka Leo nikimwona mtu anatembelea gari Kali nyumba na biashara iliyonona huwa namwogopa kabla ya kumheshimu, kwenye maisha kama huna roho ngumu hutoboi. Pole kiongozi wewe ni zaidi ya kamanda
 
Back
Top Bottom