Baada ya Sudan kutangaza uhusiano na Israel, Wananchi wapinga

Baada ya Sudan kutangaza uhusiano na Israel, Wananchi wapinga

HAKUNA MUSLIM ATAKAE IPENDA AU KUIKUBALI ISRAEL MILELE.

UKIONA NCHI YA KIARABU IMEPATANA NA ISRAEL NI SABABU TU YA VIONGOZI VIBARAKA WA MABEBERU WAMELAZIMISHWA NA US NA HAWAWEZI KUPINGA WAKIHOFIA KUTOLEWA MADARAKANI NA MABEBERU AMBAO WANAWALINDA.

nimetumia capital letter,
 
Ni kweli na inajulikana.Lakini inashangaza mara nyingi wakristo nchi mbali mbali huwa wanawaunga mkono wayahudi wawakandamize wapalestina.Utadhani hawajui kuwa Palestina ina wakristo.
Wakristo vile vile wananyanyaswa sana katika nchi zenye waislamu wengi kama Pakistan, Indonesia, Iraq, Misri nk.
 
HAKUNA MUSLIM ATAKAE IPENDA AU KUIKUBALI ISRAEL MILELE.

UKIONA NCHI YA KIARABU IMEPATANA NA ISRAEL NI SABABU TU YA VIONGOZI VIBARAKA WA MABEBERU WAMELAZIMISHWA NA US NA HAWAWEZI KUPINGA WAKIHOFIA KUTOLEWA MADARAKANI NA MABEBERU AMBAO WANAWALINDA.

nimetumia capital letter,
Kwanini wasiipende?,suala la palestine sio la kidini,,dini ya kiyahudi haina ushindani na dini ya kiislamu kwa namba yeyote ile,na infact myahudi anaruhusiwa kuingia msikitini kuliko kuingia kanisani,
Wapalestine walibugi mwaka 1967 kwa kuyaacha makazi yao kukimbia vita ,wasingekimbia ile nchi ingekuwa na mchanganyiko wa watu na wala ishu ya palestine haingekuwa kubwa kiasi kile
 
Ni kweli na inajulikana.Lakini inashangaza mara nyingi wakristo nchi mbali mbali huwa wanawaunga mkono wayahudi wawakandamize wapalestina.Utadhani hawajui kuwa Palestina ina wakristo

Ni kweli na inajulikana.Lakini inashangaza mara nyingi wakristo nchi mbali mbali huwa wanawaunga mkono wayahudi wawakandamize wapalestina.Utadhani hawajui kuwa Palestina ina wakristo.
Nchi nyingi za EU huwatetea wapalestine,shida iko kwa US,lakini kuna hawa bornagain wao hudhani bila kuiunga mkono israel hawatapata freepass ya kuingia mbinguni,
 
Wakristo vile vile wananyanyaswa sana katika nchi zenye waislamu wengi kama Pakistan, Indonesia, Iraq, Misri nk.
Wewe unazungumzia kunyanyaswa na ushahidi huwezi kuupata wa kutosha.Lakini waislamu wanauliwa kwa maelfu ndani ya nchi zao kunakofanywa na mataifa ya kikristo na mayahudi wachache kwa kutumia silaha za kisasa zilizotayarishwa na nyengine zikifanyiwa majaribio kwao.
Katika waathirika wakubwa ni huko Pakistan,Afghanistan,Libya na kwengineko kwingi.
 
Nchi nyingi za EU huwatetea wapalestine,shida iko kwa US,lakini kuna hawa bornagain wao hudhani bila kuiunga mkono israel hawatapata freepass ya kuingia mbinguni,
Hao wanaoona bila kuiunga mkono Israel ni wengi na ndio wenye nguvu sana.Kila siku Israel inavunja majumba ya wapalestina na kuwajengea watu wao maeneo hayo hayo na kinachosikika ni maneno laini tu ya kuwalaumu lakini hakuna azimio la maana linalotolewa wala hatua za nguvu zinazochukuliwa na mataifa hayo.
 
Hao wasudan waachwe wasote kama wanacheza, nchi yao imekuwa kwenye vikwazo kwa muda mrefu lakini bado hawaoni.

Lini wapalestina wakawa na undugu na wanubi, hao waache uongo.
Hahahaaaaa Eti lini wapalestina wakawa na undugu na wanubi. 🤣🤣🤣
 
Kwanini wasiipende?,suala la palestine sio la kidini,,dini ya kiyahudi haina ushindani na dini ya kiislamu kwa namba yeyote ile,na infact myahudi anaruhusiwa kuingia msikitini kuliko kuingia kanisani,
Wapalestine walibugi mwaka 1967 kwa kuyaacha makazi yao kukimbia vita ,wasingekimbia ile nchi ingekuwa na mchanganyiko wa watu na wala ishu ya palestine haingekuwa kubwa kiasi kile
Bro Ata wasingekimbia isingebadili kitu.
MKOLONI WA PALESTINE UK ALIIACHA ILE NCHI CHINI YA JEWS SETTLERS. ALIANDAA MAZINGIRA YOTE KUHAKIKISHA AKITOKA YEYE WAYAHUDI WANASHIKA HATAMU PALE PALESTINE.
 
Bro Ata wasingekimbia isingebadili kitu.
MKOLONI WA PALESTINE UK ALIIACHA ILE NCHI CHINI YA JEWS SETTLERS. ALIANDAA MAZINGIRA YOTE KUHAKIKISHA AKITOKA YEYE WAYAHUDI WANASHIKA HATAMU PALE PALESTINE.
Sio kweli,muingereza aliigawa palestine pande mbili,,waisrael waliridhika kuwa na tel aviv kama mji mkuu,,kipindi hicho jerusalem ukiwa chini ya jordan,vile vita vya 1948,wayahudi hawakuwa hata na nia ya kuiteka jerusalem,,uingereza waliondoka na kuicha jerusalem chini ya jordan,mfalme wa jordan alijenga hadi ikulu pale,
Jerusalem ilitekwa 1967
 
Leo baada mafanikio ya kuimega Sudan ndio watu wanasema Sudan ni ya Wanubi lakini huko nyuma tuliambiwa Omar Albashiri ni mwarabu anaongoza serikali inayouwa waafrika.Ajabu kabisa.
Vyovyote iwavyo wasudan wengi wawe weusi au wekundu lakini ni waislamu.Na waislamu ni ndugu sana na wapalestina.Kama haitoshi hiyo hata wangekuwa ni dini tofauti basi matendo ya Israel kwa wapalestina kuwavunjia majumba yao haikubaliki kibinadamu.
Na vitendo vya wapalestine magaidi kuwachoma visu waisrael na kurusha maroketi israel huku waking'ang'ania ardhi za waisrael hakikubaliki
 
Ni kweli na inajulikana.Lakini inashangaza mara nyingi wakristo nchi mbali mbali huwa wanawaunga mkono wayahudi wawakandamize wapalestina.Utadhani hawajui kuwa Palestina ina wakristo.
Pia Israel kuna waislamu cha ajabu waislamu wanaichukia israel utafikiri walihimizwa chuki kwenye dini
 
Na vitendo vya wapalestine magaidi kuwachoma visu waisrael na kurusha maroketi israel huku waking'ang'ania ardhi za waisrael hakikubaliki
Hizo ni hasira za wapalestina wasiokuwa na silaha.Kama wangekuwa na makombora mazito kama yale wanayotumia Marekani maeneo ya waislamu basi wapalestina wangekuwa na haki kuyamimina hata ikulu ya Israel.Mtu anayekufukuza nyumbani kwako ukiweza kupambana naye usimuonee huruma.
Watu walioletwa mwaka 1948 hawawezi wakaitwa wenye ardhi wakati mababu waliofukuzwa enzi hasa na vijana wa leo wapo hai na si historia.
 
Yaani kurudisha mahusiano na Israel kulete vita vya wenyewe kwa wenyewe hii imekaaje?
 
Ni kweli na inajulikana.Lakini inashangaza mara nyingi wakristo nchi mbali mbali huwa wanawaunga mkono wayahudi wawakandamize wapalestina.Utadhani hawajui kuwa Palestina ina wakristo.
Hoja pale siyo ukristu kwani wayahudi ni dini inayojitegemea na tofauti na ukristu. Hoja ni mtu arudishiwe eneo lake
 
Sudan is not an Arabic nation let’s not confuse

Sio sisi tunaochanganyikiwa.Wazungu na mabeberu ndio wanaoanza kutuchanganya na sisi kwa ujinga wetu tunajichanganya tena
Wakati wa kampeni za kuigawa Sudan mapande maweili na kuzuia ushawishi wa Sudan kuingia kusini ya Afrika tuliambiwa Sudan kuna waarabu wanawatesa na kuwauwa waafrika.Hata vyombo vya habari vya Tanzania vilikariri sana na kwa nguvu habari hizi.Wakati yakifanyika hayo viongozi karibu wote wa Serikali ya Sudan ni waafrika rena weusi au machotara.
Viongozi wenyewe wa Sudan hawakuweza kujieleza vizuri na kuishinda propaganda hiyo na hatimae wakawapa nguvu mabeberu na wakaigawa nchi nzuri na tajiri.Baadae wakageukiwa wao wenyewe na kusambaratishwa kwa kupinduliwa Hassan Albashiri kwa maandamano.
Kama ilivyo kwa nchi zote duniani si rahisi kukuta watu wa kabila moja pekee lakini kwa Sudan ni zaidi na hii ilitoa fursa kubwa ya kupandikiziwa fitna.Lugha kubwa ya Sudan ni kiarabu na kinazungumzwa na watu wa rangi zote hata Wanubi wa Juba.Zipo nchi nyegine za Afrika wanazungumza kifaransa na ambayo ni lugha isiyo na asili na nchi hizo tofauti na kiarabu na haijawa shida kufanyiwa fitna na ndio huonekana wao ni wastaarabu zaidi kwa kuzungumza lugha hiyo.
 
Hii habari imekua si nzuri kwa wenzetu waarabu na wale wahafidhina wa humu jf sijui kwa nn? Israel kuwa na aman na nchi za kiarabu ni Jambo jema sana lakn waarabu waliowengi hawataki Aman kabisa na Israel , SS wakristo tunafundishwa kuwa na amani na watu wote wenzetu akina faiza f...wao ni tofauti.
.
Nimeishi Israel lakini sijwahi kuona dini inayoitwa "Christianity" Bali pote nilipotembelea kwa asilimia 90% nimekutana na dini inayoitwa "Judaism".
Sasa kidogo huwa nashangaa nikimuona mtu anawahusisha wa Israel na dini ya kikristo angali wao hata huyo yesu tunaemjua Sisi huku wao hawamjui.
 
Back
Top Bottom