Baada ya tamko la TEC, tunasubiri tamko la BAKWATA

Baada ya tamko la TEC, tunasubiri tamko la BAKWATA

Acha masihara mkuu

BAKWATA inayoshindwa kusimamia waislamu itawezaje kusimamia mambo ya nchi


BAKWATA ni CCM B


Nawashangaa waislamu wanaowasikiliza BAKWATA.
 

Attachments

  • IMG-20230822-WA0011.jpg
    IMG-20230822-WA0011.jpg
    59.6 KB · Views: 1
FF, Zawadini na wale wengine Kuna wito wenu huku
Asante sana. Sikujua aulizwe kikongwe kwenye nini. Nikishapata naweza kusema kitu, ila niseme hili la kumaliza Form 4:

Mimi na huyo mwezangu FF, kama alivyoitwa, huenda ni kweli tumemaliza For 4, ila sina hakika huyu aliyetoa kauli/andiko hili, kama yeye hata hiyo F4 kafika.

Niwajuze tu wale wanaodanganywa kwamba sisi elimu yetu ni madrasa waendelee kudanganywa. Sisi tunaosoma madrasa ni kweli tunasoma madrasa lakini baadae tunabanana humu humu kwenye elimu dunia, tena tunabanana kikwelikweli.

Ukitaka kuthibitisha muulize mwenzenu Pascal Mayalla, huenda atakupa ushuhuda kama atakuwa mkweli.

Mkuu, baadhi yetu humu JF, huwa tunadhani wengine ni vichwa vitupu lkn ukipata taarifa tu unajishtukia. Mfano mzuri ni wewe brazaj kuhusu Zawadini na uandamizi humu JF.

Mimi huwa nasema tujitahidi kufikiria kabla kuandika.

Nasubiri kujua aulizwe kikogwe kwenye nini? Nasubiri kwasababu nataka nijadili pia kuhusu hili ikimpendeza aliyeandika.
 
Ajabu na kweli. Huu Mbona wala si u Simba wala u Yanga; u Arsenal wala u Man U?

View attachment 2724885

Waraka wa TEC ulikuwa kwa wa waumini dhidi ya mpango wa serikali kuhusiana na mkataba wa bandari.

Waraka wa TEC ulikuwa kwa manufaa ya watanzania wote yaani wakristi, waislam na hata wasio waumini.

Sasa wa hawa ndugu utakuwa ni wa nani dhidi ya nani? Kwamba utakuwa wa maslahi kwa nani?

Hata hivyo, kwa kuanzia hadi mtu unajiuliza

"Hivi waraka huo ambao nao wangependa kuwasomea waumini wao, wenyewe wanao?"
Hawa jamaa wanapenda sana ligi. Ndio maana utawakuta vijiweni wakibidshana kuwa Yesu sio Mungu.

Anyway, kwa kuwa TEC walipinga uuzaji wa bandari nao kama wana ubavu basi waje waupinge tuone kama wana hizo guts.
 
Wengine bora liende hawana msimamo wala kuhoji

Ova
 
Tatizo ni kwamba TEC wameujadili mkataba ila wengine wanawashambulia TEC na sio hoja.
 
Asante sana. Sikujua aulizwe kikongwe kwenye nini. Nikishapata naweza kusema kitu, ila niseme hili la kumaliza Form 4:

Mimi na huyo mwezangu FF, kama alivyoitwa, huenda ni kweli tumemaliza For 4, ila sina hakika huyu aliyetoa kauli/andiko hili, kama yeye hata hiyo F4 kafika.

Niwajuze tu wale wanaodanganywa kwamba sisi elimu yetu ni madrasa waendelee kudanganywa. Sisi tunaosoma madrasa ni kweli tunasoma madrasa lakini baadae tunabanana humu humu kwenye elimu dunia, tena tunabanana kikwelikweli.

Ukitaka kuthibitisha muulize mwenzenu Pascal Mayalla, huenda atakupa ushuhuda kama atakuwa mkweli.

Mkuu, baadhi yetu humu JF, huwa tunadhani wengine ni vichwa vitupu lkn ukipata taarifa tu unajishtukia. Mfano mzuri ni wewe brazaj kuhusu Zawadini na uandamizi humu JF.

Mimi huwa nasema tujitahidi kufikiria kabla kuandika.

Nasubiri kujua aulizwe kikogwe kwenye nini? Nasubiri kwasababu nataka nijadili pia kuhusu hili ikimpendeza aliyeandika.

Uzi wangu uliunganishwa hapa. Comment ya kwanza ya brazaj kwenye uzi huu ilikuwa Uzi kamili ambako nilikuita pia katika comment ya hapa kujumuika ikikupendeza.

Niseme wazi hakuna nilipojikita au kukomaa kuhusiana na elimu kulingana na ulivyoandika.

Kuhusiana na kikongwe ni wazi huo ni utambulisho usio rasmi wa huyo huyo FF kama unavyosomeka pale au kama zilivyo tambulisho zingine pendwa za awaye yote.

Huyo kikongwe amewahi kujinasibu na picha hii, kuwa tena yeye ni jimama haswa!

1689438761802.png


Wafanya mchezo hapo ndugu yangu?

Rejea Uzi huu kuzifahamu cheche zake Hadi kufuzu kuitwa kikongwe:

Watanzania wakamatwa Kenya wakiwa njiani kwenda kujiunga na Al Shabaab

Kikongwe ni legend huyo si kina Paskali. Kwa huyo hao mbona ni mabwana wadogo?

Chezea kikongwe wewe?
 
Uzi wangu uliunganishwa hapa. Comment ya kwanza ya brazaj kwenye uzi huu ilikuwa Uzi kamili ambako nilikuita pia katika comment ya hapa kujumuika ikikupendeza.

Niseme wazi hakuna nilipojikita au kukomaa kuhusiana na elimu kulingana na ulivyoandika.

Kuhusiana na kikongwe ni wazi huo ni utambulisho usio rasmi wa huyo huyo FF kama unavyosomeka pale au kama zilivyo tambulisho zingine pendwa za awaye yote.

Huyo kikongwe amewahi kujinasibu na picha hii, kuwa tena yeye ni jimama haswa!

View attachment 2725172

Wafanya mchezo hapo ndugu yangu?

Rejea Uzi huu kuzifahamu cheche zake Hadi kufuzu kuitwa kikongwe:

Watanzania wakamatwa Kenya wakiwa njiani kwenda kujiunga na Al Shabaab

Kikongwe ni legend huyo si kina Paskali. Kwa huyo hao mbona ni mabwana wadogo?

Chezea kikongwe wewe?
Sasa sijui njadiliane na nani, ila angalau nimelisemea hili la elimu na huenda watu watafahamu sasa.
 
Baada ya TEC kuukataa mkataba wa DPW hadharani bila kumumunya maneno, sasa tunasubiri tamko la BAKWATA nao tusikie watasema nini. Ni matumaini yangu kwamba BAKWATA watafuata nyanyo za TEC kwa kuukataa mkataba wa DPW bila kupepesa macho.

Aidha, inawezekana BAKWATA wakaukubali mkataba na endapo watafanya hivyo basi watakuwa na sababu za msingi. Au wanaweza kuukubali na kutoa maoni kuhusu kuboreshwa vipengele vyenye utata, hasa vile vinavyohusu muda wa mkataba na vinavyobagaza mamlaka ya nchi (sovereignty).

Kimsingi ni vigumu kubashiri nini BAKWATA watasema lakini kwa kuwa bado hawajatoa tamko hadharani, ngoja tusubiri tuone watakuja na tamko zito au jepesi kiasi gani. Waswahili wanasema 'usiusemee moyo' au 'usiandikie mate wakati wino upo'. Kwa maana hiyo, hebu tuvute subira kidogo tusubiri kusikia BAKWATA watakuja na tamko la aina gani. Wakati ukifika wataanika kila kitu hadharani. Subra yavuta kheri.
Wao hawana shida na mkataba wana tatizo na TEC
 
Sasa sijui njadiliane na nani, ila angalau nimelisemea hili la elimu na huenda watu watafahamu sasa.

Mkuu la elimu si geni na wala si lako. Hilo linajulikana kwa wengi kama si wote.

Bila shaka ndiyo maana umetambua hayupo mwenye kujadiliana nawe kwenye hilo. Beberu akiyaita ya namma hiyo - trivial!

Yaani mithili ya 10 + 0 tu.

Habari ndiyo hiyo ndugu.
 
Mkuu ni mapema sana kuwahukumu. Kwanini tusivute subira tusikie kutoka kwao wenyewe badala ya kubashiri mambo?
Tayari walishatoa mwelekeo kama umesikia kamati ya ulinzi na amani ya mwanza, shekhe tayari ametoa msimamo unaonyesha kuwa sehemu zote zikae zikubaliane ili kukomesha haya marumbano yanayoendelea mitandaoni, Ila Mama Karikoroga.
 
Mkuu la elimu si geni na wala si lako. Hilo linajulikana kwa wengi kama si wote.

Bila shaka ndiyo maana umetambua hayupo mwenye kujadiliana nawe kwenye hilo. Beberu akiyaita ya namma hiyo - trivial!
Nilikuwa najadil comment namba 97 ya Huyaa ambayo wewe ulinitag mimi Zawadini na FF. Fanya rejea. Sasa ukisema sio geni kwamba FF ndo ambaye angalau kamaliza F4 au kwamba akina FF ndo hatujasoma?

Nilikuwa najibu kwa muktadha huo kwamba kama mahala watu huwa wanaambiwa wavaa kobadhi, kama munavyoita, hawajasoma na wanaenda darsa tu imekula kwao, kwani hao wanaodiwa hivyo, ni kweli wanaenda madrasa lkn wakirudi madrasa wanabanana na wanaoenda shule, tena wanabanana kisawasawa na nikasema wakawaulize wanaotujua.

Sasa ukisema hayuko mwenye kujadiliana nami, huyu Huyaa alikuwa anajadiliana na nani kwenye hili? Au alikuwa anaogea uupuuzi tu apuuzwe? Na kama apuuzwe nani atampuuza wakati watu wameshaaminishwa nao wakaamini bila kufanya angalau tafakuri?

Kuna matamshi mtu huyasema akiamini yeye ni mwerevu ila katika Uhalsia ni mjinga (hajui). Mtu kama huyu anapaswa afunzwe ili ajue, kwani sio kila aliyesoma ni mtambuzi. Wengine ni wajinga pamoja na kusoma kwao.
 
Nilikuwa najadil comment namba 97 ya Huyaa ambayo wewe ulinitag mimi Zawadini na FF. Fanya rejea. Sasa ukisema sio geni kwamba FF ndo ambaye angalau kamaliza F4 au kwamba akina FF ndo hatujasoma?

Nilikuwa najibu kwa muktadha huo kwamba kama mahala watu huwa wanaambiwa wavaa kobadhi, kama munavyoita, hawajasoma na wanaenda darsa tu imekula kwao, kwani hao wanaodiwa hivyo, ni kweli wanaenda madrasa lkn wakirudi madrasa wanabanana na wanaoenda shule, tena wanabanana kisawasawa na nikasema wakawaulize wanaotujua.

Sasa ukisema hayuko mwenye kujadiliana nami, huyu Huyaa alikuwa anajadiliana na nani kwenye hili? Au alikuwa anaogea uupuuzi tu apuuzwe? Na kama apuuzwe nani atampuuza wakati watu wameshaaminishwa nao wakaamini bila kufanya angalau tafakuri?

Kuna matamshi mtu huyasema akiamini yeye ni mwerevu ila katika Uhalsia ni mjinga (hajui). Mtu kama huyu anapaswa afunzwe ili ajue, kwani sio kila aliyesoma ni mtambuzi. Wengine ni wajinga pamoja na kusoma kwao.

Ninakazia nilikuita kujadili hoja yangu iliyokuwa uzi kamili kupitia hiyo comment aliyoitwa FF.

Si mara ya kwanza kukuitisha kwenye hoja zenye maslahi mapana kwetu sote. Si kwenye u dini, kashfa, kejeli, ubaguzi wala vya namna hiyo. Ninaamini hilo walijua vyema.

Nikiamini kama vitani kuliko na friendly fire nadra makombora kukosea shabaha na kuwaangukia ndugu, vivyo hovyo humu ndugu wavukao mipaka huwaasa hadharani na faraghani.

Mbona masheikh na waislam hawa ni ndugu wa wote?



Tuseme masheikh kama hawa hawakuvutii wewe? Ila aina hIzi za watu wasiokuwa na msingi wowote?



Mbona wengine baina yetu ni waislam pia?

Haipo vita ya kibaguzi kwenye mkataba wa Bandari. Hapa pana suala la kisheria siyo kidini.

Tusiondolewe kwenye reli kirahisi namna hii.

Sisi sote ni ndugu.
 
Back
Top Bottom