Baada ya ukweli wa Erick Kabendera kubainika, wote walionituhumu kuhusika nimewasamehe kwani Mungu amewasamehe. Msirudie tena!

Baada ya ukweli wa Erick Kabendera kubainika, wote walionituhumu kuhusika nimewasamehe kwani Mungu amewasamehe. Msirudie tena!

kabendera kukiri na kuamua kuilipa serikali si ushahidi kwamba kweli alitenda makosa hayo! tumia akili kidogo paskali!

kwa bandiko lako hili unazidi kuitangazia dunia kwamba Erick alikua mhujumu uchumi na anamiliki genge la kivita.

badala ya kumsafisha mwandishi mwenzako et ww unajisafisha na kumkandia mwenzako,kwamba serikali makosa waliyomkamata nayo hayana uhusiano na uandishi wake wa habari.

sijui unakwama wap brother! mbona uko miongoni mwa wanaotumia ubongo wao? kwanini kuna wakati unaweka akili pembeni?

plz inapobidi kaa kimya usichokonoe vidonda vya watu
 
Wanabodi,

Kwa vile sisi binadamu tuna uwezo tofauti, na sio watu wengi wanajitambua uwezo wao katika kitu kinachitwa "self realization", ikitokea unajitambua, na unapokasirika kwa kutotendewa haki, kwa kutwishwa misalaba ambayo sio yako, na ukiumia na kulaani watesi wako, na unajua nini kitawatokea pale Mungu anapoamua kukutua msalaba huo, then sauti ya Mungu inakuingia, na hapo hapo unakumbuka na kuwasamehe watesi wako, kabla karma haijaanza kuwafanyia kazi.

Baada ya mwandishi wa habari za uchunguzi, Erick Kabendera kukamatwa na polisi na kushikiliwa mahabusu kwa miezi 7, msalaba wa kukamatwa nilibebeshwa mimi. Eti ni mimi Pascal Mayalla ndiye niliyesababisha kukamatwa kwa Erick Kabendera, kwasababu ya zile makala zangu za uzalendo humu JF.
Hizi ni Baadhi ya Makala Zangu Kuhusu Uzalendo, wale wenye muda, pitieni halafu mnieleze wapi nimemponza mtu yoyote?


Japo nilijifanya mgumu na sijali, kwasababu kiukweli kabisa, makala zile wakati zinaandikwa hazikuwa na lengo la kumchomea mtu yoyote, popote, na wala sikuwahi kuwafahamu waandishi wa makala hizo. Na mpaka sasa ninapoandika leo, bado siwafahamu waandishi wowote wa makala hizo, lakini kwa upande mwingine, kwa vile kuna mwandishi wa habari, Erick Kabendera, amekamatwa katika mazingira ya kutatatisha. Baada ya askari waliotumwa kumkamata kukataa kujitambulisha, hivyo kudhaniwa ni wasiojulikana na Erick akawagomea kuwafungulia, ndipo wakamfanyia utekaji kwanza; kwa kutekwa na kufichwa kusikojulikana kwa muda siku mbili za mwanzo, huku serikali wakitupiana mpira, mara ni polisi, mara ni immigration, na kosa lake mara ni uraia ila full kujiuma uma!.

Ila baada ya kufikishwa mahakamani ndipo kukaibuka uhujumu, utakatishaji fedha na magenge ya uhalifu. No one was sure axactly what is it, hivyo any reasonable man lazima ujiulize, "what if ni kweli mwandishi ni yeye?", "what if ni kweli zile makala zangu ndizo zimeiamsha serikali na kuichochea kumtafuta anayeandika?", "what if ni kweli mwanzo alitumiwa wasiojulikana ili wampoteze kama Azory Gwanda na Ben Saanane lakini baada ya Erick kuunguza picha, ndipo ikashindikana, na kuamua kumtafutia mashitaka yoyote ya kumbambikia just to silence him? Then japo nilikuwa najikaza kisabuni, lakini automatically nilianza kujihisi, na kila siku Erick alipokuwa akifikishwa mahakamani naumia, "what if sababu ni mimi?".

Kila uzi wowote kumhusu Erick Kabendera ukipandishwa humu JF lazima humo ndani ya uzi, lazima nilikuwa natajwa as a "snitch". Kila mateso aliyokuwa anakutana nayo Erick Kabendera, na mimi yalikuwa yananiumiza psychologically. Kwanza nikawa sichangii uzi wowote kuhusu jambo lolote kwa Erick Kabendera.

Mimi ni story teller, kwa wapenda nyuzi fupi, ishieni hapa, na kwenda kule kwenye hitimisho, wapenda mastory ya JF, tuendelee hapa

Sisi Wakristu wa kweli, tunaofuata mafundisho ya Mungu wa Kweli, na kufuata mafunzo ya Bwana wetu Yesu Kristo wa Kweli, tumefundishwa kusamehe hata saba mara sabini, hivyo mimi kwa upande wangu, niliisha kusamehe toka siku ile ya kwanza ulipopandisha bandiko hili kwa kulipuuza, kwasababu ulikuwa hujui utendalo. Pia nimewasamehe wale wote walionituhumu ni mimi kwa kuamini kuwa kweli ni mimi.

Hitimisho:
Hivyo kwa uzi huu, baada ya ukweli wa mashitaka ya Erick Kabendera kubainika, mimi nimewasamehe "Wale Wote walionituhumu mimi kuhusika na kukamatwa kwa Erick Kabendera, na kufuatia msamaha huo, pia "Mungu nae, amewasamehe" Hakuna tena adhabu ya karma kwenye kunisingizia mimi issue ya Kabendera, ila tafadhalini sana, msirudie tena kumtuhumu mtu mwingine yoyote kwa tuhuma ambazo hamna hakina nazo! Kauli huwa zinaumba, sisi wengine tunajijua kauli zetu na madhara yake, hivyo mkituudhi tusiposamehe.


Hivyo kwa upande wangu, uwe na amani kabisa, na wote mlionituhumu humu na kungine kote, muwe na amani, nimekusamahe na kuwasamehe wengine wote kwa roho safi na roho nyeupe, lakini ili karma isikushughulikie na wewe kwa upande wako, baada ya kuujua ukweli huu, do the right thing, hata kimoyo moyo tu, inatosha Mungu anasikia kila kitu hata usipozungumza, ile kuwaza tuu, is enough!

Ubarikiwe sana.

Paskali.
Pole Pascal, though nilikupa pole tangu siku ya kwanza. Tumekuwa wepesi sana kutuhumu.
 
Pole sana mayalla binafsi mpaka leo sioni kosa lako hata kama zile Makala zilikuwa za Kabendera japo haijathibitika kama zile ni makala zake.

Ulichofanya ni ku share zile makala kama makala zingine zozote zile hapa JF..

Wengi humu Jf walikuwa wanakupinga pale ulipokuwa unazipinga zile makala kuwa ni za uongo na zinamkosea heshima Rais. Watu walikuwa wanasema kilichoandikwa kwenye zile makala ndio hali halisi.

Lakini ilipokuja kuhisiwa kuwa mwandishi ni kabendera wale wale walikugeuka kuwa umemchomekea Kabendera.

Watanzania tumejaa unafiki ni vigeugeu na hatuna msimamo..

Ndio maana leo mtu huyohuyo akiwa chama tawala ataitwa kila majina mabaya ya ufisadi lakini siku akihamia upinzini ataitwa shujaa...

Leo tunashuhudia wanasiasa wakihamia chama tawala kwa kasi, huku wakitaja maendeleo chini ya Maguli. Lakini kiuhalisia wanawaza nafasi zao matumbo yao na famili a zao.

Kifupi usimwamini Mtanzania mara nyingi yeye anafuata upepo unakovumia..

Wakati mwingine naunga mkono Magufuli bora atuburuze tu mapaka tupate akili,maana hatujui tunataka nini.
 
Mkuu P umeeleweka... Nadhani hata nawe ulitegemea upinzani dhidi ya hili bandiko kutoka kwa watu waliokutuhumu...Ila binafsi nimekuelewa....Uwongo hauwezi simama mbele ya ukweli daima.
 
Ni sakata la Ndugu Erick Kabendera,

Kila mtu ana lake...Wengine watatunga ili kufurahisha nafsi zao na watu wao. Tafadhali ukipata habari yoyote kuhusu hii ishu ni vema ukaihakiki kabla ya kuiweka humu... Na wewe uliyeikuta humu ihakiki pia kabla ya kuisambaza kwa wengine.

Nimeandika sababu nimeshazishuhudia habar kadhaa za hivyo mpaka sasa na pia ni kutokana na kasumba ya baadhi ya wanajf hasa kwa matukio yanayotrend nchini.

Ni hayo tu.
 
Well said mkuu Slowly.

Pascal, pole sana kwa haya yote. Jamii yetu inapaswa ijifunze kuepuka kukumbatia speculations na notions zinazotokana na 'hearsay'. Tunachokifanya hapa ni kutengeneza "msiba juu ya msiba". Watanzania we are good at that! Let's learn to deal with facts instead of hearsays. Speculations huwa zinaua! Depressions, mental illnesses na suicidal dispositions mara nyingi husababishwa na vitu kama hivi, na ndiyo maana maradhi kama haya katika nchi zetu yako rampant.

Suala la EK linatia huruma. Sina hakika kama Eric ameonewa au la kutokana na jinsi kesi yake ilivyokuwa politicised, hivyo sitaliongelea sana suala lake hapa mpaka pale mambo yote yatakapowekwa wazi. Hata hivyo, ukweli kwamba Eric ameteseka, haukwepeki. Lakini pia jamii haikupaswa kumhukumu Pascal Mayalla bila ithibati thabiti - au kile tunachokiita "prima facie" - huku ikimmininia shutuma kenyekenye, badala ya kuzielekeza shutuma hizo kule zinakotakiwa: kwa watesi wa Eric. Huku ni kuhamisha magoli. Why are we avoiding the real antagonist of the protagonist in this infamous theatrical play?!

Hili jambo linadhikisha sana. Kinachotokea hapa hakina tofauti na kilichotokea Shinyanga na Mwanza mwaka 1976, wazee wetu kina Mabula Mazegenuka, kina Ng'wana Ng'hoboko, na wengine wengi, wakiwemo waganga wa jadi, wafanyabiashara na wakulima, waliposhutumiwa kuua vikongwe "wachawi" na hivyo - bila hata "prima facie" - nao wakauawa, na kwa jinsi hiyo, jamii ikajikuta ikitengeneza "msiba juu ya msiba", katika tukio lililosababisha kuundwa kwa katiba mpya ya 1977, na kujiuzulu kwa Waziri wa Mambo ya Ndani, ndugu Ali Hassan Mwinyi. Yote haya kwa sababu ya kitu kimoja: speculations.

Speculations, hearsays, na vitu kama hivyo, huwa si vitu vizuri muda wote, na aghalabu huwa havijengi. Tujifunze! We are better than this.
Shukurani ndugu kwa somo hili. Hapo juu kwa kina Mazegenuka nimekuelewa sana. Duh! Ama kweli nchi hii imetoka mbali.
 
Fake kivipi sasa?

Hajaachiliwa toka jela?

Hajalipa ama kutakiwa kulipa Tshs. 273M ili kununua Uhuru wake?

Mama yake hajafa?

Hajabambikiziwa kesi?

Pls, explain tujiepushe na feke news kuhusu lipi au nini juu ya huyu mtu Erick Kabendera....
 
Ni sakata la Ndugu Erick Kabendera
Kila mtu ana lake...Wengine watatunga ili kufurahisha nafsi zao na watu wao.Tafadhali ukipata habari yoyote kuhusu hii ishu ni vema ukaihakiki kabla ya kuiweka humu... Na wewe uliyeikuta humu ihakiki pia kabla ya kuisambaza kwa wengine.
Nimeandika sababu nimeshazishuhudia habar kadhaa za hivyo mpaka sasa na pia ni kutokana na kasumba ya baadhi ya wanajf hasa kwa matukio yanayotrend nchini mfano ni ile ishu ya Pompeo na Makonda.
Ni hayo tu.
POMPEO BABA LAO.
 
Maumivu aliyoyapitia Kabendera hayaelezeki,pascal umekimbilia kujisafisha kwanza pasipo kuwa na UTU , huna uchungu kabisa nilitegemea ungeenda kwa kabendera kumtia moyo kwa kufiwa na mama yake pili kwa adha iliyompata ya kukaa mahabusu kwa kubambikiwa kesi...PASCAL UMEACHA FANI YAKO SASA UMEKIMBILIA SIASA, ,ITAKUMALIZA!

hivi Kabendera kama angefungwa, ungekuja tena kujisafisha???
 
Fake kivipi sasa?

Hajaachiliwa toka jela?

Hajalipa ama kutakiwa kulipa Tshs. 273M ili kununua Uhuru wake?

Mama yake hajafa?

Hajabambikiziwa kesi?

Pls, explain tujiepushe na feke news kuhusu lipi au nini juu ya huyu mtu Erick Kabendera....
Nadhani hatujaelewana boss
 
Pole sana! Nakushauri uendelee kuusema ukweli hata kama utapingwa na watu wote, ilmradi ujue kuwa Mungu atakuwa upande wako.

Kumbuka kuwa ni aheri kuwa peke yako na Mungu kuliko kuungwa mkono na umati wa watu - wanafiki, vigeugeu na waovu!
Wanabodi,

Kwa vile sisi binadamu tuna uwezo tofauti, na sio watu wengi wanajitambua uwezo wao katika kitu kinachitwa "self realization", ikitokea unajitambua, na unapokasirika kwa kutotendewa haki, kwa kutwishwa misalaba ambayo sio yako, na ukiumia na kulaani watesi wako, na unajua nini kitawatokea pale Mungu anapoamua kukutua msalaba huo, then sauti ya Mungu inakuingia, na hapo hapo unakumbuka na kuwasamehe watesi wako, kabla karma haijaanza kuwafanyia kazi.

Baada ya mwandishi wa habari za uchunguzi, Erick Kabendera kukamatwa na polisi na kushikiliwa mahabusu kwa miezi 7, msalaba wa kukamatwa nilibebeshwa mimi. Eti ni mimi Pascal Mayalla ndiye niliyesababisha kukamatwa kwa Erick Kabendera, kwasababu ya zile makala zangu za uzalendo humu JF.
Hizi ni Baadhi ya Makala Zangu Kuhusu Uzalendo, wale wenye muda, pitieni halafu mnieleze wapi nimemponza mtu yoyote?


Japo nilijifanya mgumu na sijali, kwasababu kiukweli kabisa, makala zile wakati zinaandikwa hazikuwa na lengo la kumchomea mtu yoyote, popote, na wala sikuwahi kuwafahamu waandishi wa makala hizo. Na mpaka sasa ninapoandika leo, bado siwafahamu waandishi wowote wa makala hizo, lakini kwa upande mwingine, kwa vile kuna mwandishi wa habari, Erick Kabendera, amekamatwa katika mazingira ya kutatatisha. Baada ya askari waliotumwa kumkamata kukataa kujitambulisha, hivyo kudhaniwa ni wasiojulikana na Erick akawagomea kuwafungulia, ndipo wakamfanyia utekaji kwanza; kwa kutekwa na kufichwa kusikojulikana kwa muda siku mbili za mwanzo, huku serikali wakitupiana mpira, mara ni polisi, mara ni immigration, na kosa lake mara ni uraia ila full kujiuma uma!.

Ila baada ya kufikishwa mahakamani ndipo kukaibuka uhujumu, utakatishaji fedha na magenge ya uhalifu. No one was sure axactly what is it, hivyo any reasonable man lazima ujiulize, "what if ni kweli mwandishi ni yeye?", "what if ni kweli zile makala zangu ndizo zimeiamsha serikali na kuichochea kumtafuta anayeandika?", "what if ni kweli mwanzo alitumiwa wasiojulikana ili wampoteze kama Azory Gwanda na Ben Saanane lakini baada ya Erick kuunguza picha, ndipo ikashindikana, na kuamua kumtafutia mashitaka yoyote ya kumbambikia just to silence him? Then japo nilikuwa najikaza kisabuni, lakini automatically nilianza kujihisi, na kila siku Erick alipokuwa akifikishwa mahakamani naumia, "what if sababu ni mimi?".

Kila uzi wowote kumhusu Erick Kabendera ukipandishwa humu JF lazima humo ndani ya uzi, lazima nilikuwa natajwa as a "snitch". Kila mateso aliyokuwa anakutana nayo Erick Kabendera, na mimi yalikuwa yananiumiza psychologically. Kwanza nikawa sichangii uzi wowote kuhusu jambo lolote kwa Erick Kabendera.

Mimi ni story teller, kwa wapenda nyuzi fupi, ishieni hapa, na kwenda kule kwenye hitimisho, wapenda mastory ya JF, tuendelee hapa

Sisi Wakristu wa kweli, tunaofuata mafundisho ya Mungu wa Kweli, na kufuata mafunzo ya Bwana wetu Yesu Kristo wa Kweli, tumefundishwa kusamehe hata saba mara sabini, hivyo mimi kwa upande wangu, niliisha kusamehe toka siku ile ya kwanza ulipopandisha bandiko hili kwa kulipuuza, kwasababu ulikuwa hujui utendalo. Pia nimewasamehe wale wote walionituhumu ni mimi kwa kuamini kuwa kweli ni mimi.

Hitimisho:
Hivyo kwa uzi huu, baada ya ukweli wa mashitaka ya Erick Kabendera kubainika, mimi nimewasamehe "Wale Wote walionituhumu mimi kuhusika na kukamatwa kwa Erick Kabendera, na kufuatia msamaha huo, pia "Mungu nae, amewasamehe" Hakuna tena adhabu ya karma kwenye kunisingizia mimi issue ya Kabendera, ila tafadhalini sana, msirudie tena kumtuhumu mtu mwingine yoyote kwa tuhuma ambazo hamna hakina nazo! Kauli huwa zinaumba, sisi wengine tunajijua kauli zetu na madhara yake, hivyo mkituudhi tusiposamehe.


Hivyo kwa upande wangu, uwe na amani kabisa, na wote mlionituhumu humu na kungine kote, muwe na amani, nimekusamahe na kuwasamehe wengine wote kwa roho safi na roho nyeupe, lakini ili karma isikushughulikie na wewe kwa upande wako, baada ya kuujua ukweli huu, do the right thing, hata kimoyo moyo tu, inatosha Mungu anasikia kila kitu hata usipozungumza, ile kuwaza tuu, is enough!

Ubarikiwe sana.

Paskali.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom