Baada ya ukweli wa Erick Kabendera kubainika, wote walionituhumu kuhusika nimewasamehe kwani Mungu amewasamehe. Msirudie tena!

Baada ya ukweli wa Erick Kabendera kubainika, wote walionituhumu kuhusika nimewasamehe kwani Mungu amewasamehe. Msirudie tena!

Kwa juhudi zako hizi za kuja JF kujitetea...
Nimekuelewa; lakini naomba niiache akili yangu ifanye maamuzi yake!!
 
Pascal Mayalla,
kuna "voluntary confession and a confession by inducement" A confession by inducement may result to the untrue admission of guilt" Ikiwa facts zipo wazi kwa nini upelelezi haukamiliki? Unahitaji Barua ya mtuhumiwa kama ilivyoelekezwa na mfalme au lengo ni kutaka ukweli ujulikane mbele ya ulimwengu kwa kutolewa ushahidi?

Tunajua the pre Bargaining yetu kuwa haiko transparent na ipo kwenye makosa yaliyo kwenye committal proceedings /hatua za awali na upelelezi usiokamilika,Hakuna anayependa uhuru wake upotee?Hivyo hata dukani mtu ataingia kununua uhuru kama amabavyo mkolooni alaivyotamani kutunyima uhuru nasi tulitamani kuwa huru.

Anayejua ukweli wa yote ni DPP tu maana yeye ndiye pilato mkuu wetu japo hanawi mikono kama pilato wa Kirumi. Hili Pandora la "detain" and "pre bargain" kuna siku walioanzisha watatamani mbingu zifunuke waingie moja kwa moja bila kufa.what comes around goes around.
 
Pascal Mayalla, Mayalla: Sept 2018, nikiwa naelekea Moshi kwa shuhuli ya Muhimu sana, nilikamatwa na trafic sehemu za Same kwa sababu ya walidai tyre zimechoka. Ukweli tyre Ilikuwa bado nzima kabisa. Baada ya majadiliano ya muda mrefu trafic walinipa option mbili.

Ya kwanza kulipa faini ya sh. 30,000, ya pili nisilipe nisilipe lakini wazuie gari na kesi iende mahakamani. Nili opt kulipa faini. Na tyre hizo mpaka leo nazitumia. Suala la Kabendera kulipa faini haina maana alikuwa na makosa hayo. Ndio maana serikali imesema hakuana ruhusa kukata rufaa. Kabendera ameamua kikiri, kulipa ili arudishiwe uhuru wake.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
I was undefined
Petro mtu huwezi kukiri makosa usiyoyafanya alafu ukubali kulipa mamilioni ya pesa acheni kudanganya umma. Kama kweli kaonewa basi wakili wake ni mzigo. Nikujulishe mimi nimesoma agreement yake. Mtani ukiisoma hasa page ya pili utabadilisha mawazo.

Nilikua namuonea huruma lakini sasa nikisikia karudishwa jela nitafurahi sana. Jamaa ni mav* kabisa. Subirini mtaona mengi huyoo kakubali kuwa snitch. Sababu hii doc ni nyeti ningeianika hadharani kusingetokea yeyote ws kumuonea huruma. Wote mnajiita rafiki zake subirini tu kugongewa hodi na mapolisi kama mlishirikiana naye katika maongezi yeyote

NAWAOMBEENI PITIENI KESI YA KUBAMBIKWA YA ISAACK WRIGHT JR aliyepewa hukumu ya kwenda jela maisha kwakesi ya kubambikiwa na serikali na kukaa jela miaka 7. Akiwa jela akasomea sheria na kujiwakilisha mwenyewe. Katika rufaa serikali ilikubali atoke baada ya hiyo miaka na yeye afute kesi. Jamaa alikataa na kusema bora afie jela kuliko kukubali makosa ambayo hakuyatenda. Mwishoni akashinda kesi na kufutiwa criminal record.

Petro wewe mwsnasheria tatizo lenu mnafanya biashara zaidi ya kusaidia watu baadhi yenu

[/URL]
 
Halafu huo mkataba wa kukiri umekaa kikandamizaji sana:
  1. Ukishakiri kosa unapoteza haki ya kukata rufaa, isipokuwa tu kama rufaa hiyo ni dhidi ya adhabu
  2. Mkurugenzi wa Mashitaka bado ana haki ya kukata rufaa
  3. Kwa kukiri makosa unafutiwa pia mashitaka mengine yaliyoshitakiwa pamoja na hayo uliyokiri, lakini ukikiuka makubaliano makosa hayo yote yatafufuliwa (yaani hii iko kimafia kabisa, mfano kama Eric alivyokiri kosa la kutakatisha fedha amefutiwa pia shitaka la kuratibu kundi la kihalifu, lakini akikiuka makubaliano shitaka hili litafufuliwa, maana yake msoto wa jela na kauli za 'upelelezi haujakamilika' zitaendelea indefinitely)
Hii ni sheria ya ajabu sana.
Hii siyo mkataba kamili mkuu. Aliyekupatia kaweka nusunusu kasome ujurasa wa pili. Aliwekewa bunduki kuusaini? Wakili wake alikua wapi?
 
Pascal, wewe ndie ulienifanya mimi nikajiunga JF na nlikuwa nakuheshimu sana. Ila natangaza tena kama nlivyowahi kutangaza hapo kabla, sikuheshimu kamwe na nlidhani kweli wewe ni mtu Bora ila hufai kutokana na mengi uliyoyaandika humu.
Sema wewe mkuu wakati unamsubilia le mutuz, afikishe wachangiaji mia moja, unatililika na dogo pasikaliii, sijui kilichomsibu nini, sijui hizi teuzi za kujipendekeza ama vyuma ila jamaa nondo za maana zipo ila tu utawala.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kuna watu humu wanataka watu waandike kile wanachokoamini au kukipenda lakini ikija hoja inayotofautiana na mtazamo wao badala ya kutoa hoja ya kuipinga wanakimbilia nkutoa matusi na kashifa kwa mtoa hoja hivi wao watajisikiaje siku wanabambikiziwa tuhuma ambazo hawakuzitenda? ila wakumbumbuke malipo huwa hapahapa duniani.
 
Ni ukweli upi tumeujua mzee? Ni mpuuzi na mpumbavu tu ndie atakaeamini mashtaka ya Eric. Ukweli unajulikana na hata watoto wadogo wanalijua hilo. Unahusika na tabu zote alizopitia Eric hata kama ni kwa asilimia 0.1

Sent using Jamii Forums mobile app
Tatizo unatetea mtu ambaye hata maisha yake ya kila huyajui. Unawezaje kumtetea mtu ukiwa hata hufahamiani naye naye pia hakufahamu, bedroom yake hamko pamoja!
 
Wanabodi,

Kwa vile sisi binadamu tuna uwezo tofauti, na sio watu wengi wanajitambua uwezo wao katika kitu kinachitwa "self realization", ikitokea unajitambua, na unapokasirika kwa kutotendewa haki, kwa kutwishwa misalaba ambayo sio yako, na ukiumia na kulaani watesi wako, na unajua nini kitawatokea pale Mungu anapoamua kukutua msalaba huo, then sauti ya Mungu inakuingia, na hapo hapo unakumbuka na kuwasamehe watesi wako, kabla karma haijaanza kuwafanyia kazi.

Naomba nitoe pole sana kwa mwandishi wa habari za uchunguzi, Erick Kabendera kwa anayopitia, na hayuko peke yake katika hayo, kuna wengi wengine pia wanapita katika mapito kama hayo japo ni kwa njia tofauti tofauti, yote haya ni mapito tuu na kuna siku yatafika mwisho na yatapita.

Toka kukamatwa kwake na polisi na kushikiliwa mahabusu kwa miezi 7, msalaba wa kukamatwa huko nilibebeshwa mimi. Eti ni mimi Pascal Mayalla ndiye niliyesababisha kukamatwa kwa Erick Kabendera, kwasababu ya zile makala zangu za uzalendo humu JF.

Hizi ni Baadhi ya Makala Zangu Kuhusu Uzalendo, wale wenye muda, pitieni halafu mnieleze wapi nimemponza mtu yoyote?


Japo nilijifanya mgumu na sijali, kwasababu kiukweli kabisa, makala zile wakati zinaandikwa hazikuwa na lengo la kumchomea mtu yoyote, popote, na wala sikuwahi kuwafahamu waandishi wa makala hizo. Na mpaka sasa ninapoandika leo, bado siwafahamu waandishi wowote wa makala hizo, lakini kwa upande mwingine, kwa vile kuna mwandishi wa habari, Erick Kabendera, amekamatwa katika mazingira ya kutatatisha. Baada ya askari waliotumwa kumkamata kukataa kujitambulisha, hivyo kudhaniwa ni wasiojulikana na Erick akawagomea kuwafungulia, ndipo wakamfanyia utekaji kwanza; kwa kutekwa na kufichwa kusikojulikana kwa muda siku mbili za mwanzo, huku serikali wakitupiana mpira, mara ni polisi, mara ni immigration, na kosa lake mara ni uraia ila full kujiuma uma!.

Ila baada ya kufikishwa mahakamani ndipo kukaibuka uhujumu, utakatishaji fedha na magenge ya uhalifu. No one was sure axactly what is it, hivyo any reasonable man lazima ujiulize, "what if ni kweli mwandishi ni yeye?", "what if ni kweli zile makala zangu ndizo zimeiamsha serikali na kuichochea kumtafuta anayeandika?", "what if ni kweli mwanzo alitumiwa wasiojulikana ili wampoteze kama Azory Gwanda na Ben Saanane lakini baada ya Erick kuunguza picha, ndipo ikashindikana, na kuamua kumtafutia mashitaka yoyote ya kumbambikia just to silence him? Then japo nilikuwa najikaza kisabuni, lakini automatically nilianza kujihisi, na kila siku Erick alipokuwa akifikishwa mahakamani naumia, "what if sababu ni mimi?".

Kila uzi wowote kumhusu Erick Kabendera ukipandishwa humu JF lazima humo ndani ya uzi, lazima nilikuwa natajwa as a "snitch". Kila mateso aliyokuwa anakutana nayo Erick Kabendera, na mimi yalikuwa yananiumiza psychologically. Kwanza nikawa sichangii uzi wowote kuhusu jambo lolote kwa Erick Kabendera.

Mimi ni story teller, kwa wapenda nyuzi fupi, ishieni hapa, na kwenda kule kwenye hitimisho, wapenda mastory ya JF, tuendelee hapa

Sisi Wakristu wa kweli, tunaofuata mafundisho ya Mungu wa Kweli, na kufuata mafunzo ya Bwana wetu Yesu Kristo wa Kweli, tumefundishwa kusamehe hata saba mara sabini, hivyo mimi kwa upande wangu, niliisha kusamehe toka siku ile ya kwanza ulipopandisha bandiko hili kwa kulipuuza, kwasababu ulikuwa hujui utendalo. Pia nimewasamehe wale wote walionituhumu ni mimi kwa kuamini kuwa kweli ni mimi.

Hitimisho:
Hivyo kwa uzi huu, baada ya ukweli wa mashitaka ya Erick Kabendera kubainika, mimi nimewasamehe "Wale Wote walionituhumu mimi kuhusika na kukamatwa kwa Erick Kabendera, na kufuatia msamaha huo, pia "Mungu nae, amewasamehe" Hakuna tena adhabu ya karma kwenye kunisingizia mimi issue ya Kabendera, ila tafadhalini sana, msirudie tena kumtuhumu mtu mwingine yoyote kwa tuhuma ambazo hamna hakina nazo! Kauli huwa zinaumba, sisi wengine tunajijua kauli zetu na madhara yake, hivyo mkituudhi tusiposamehe.


Hivyo kwa upande wangu, uwe na amani kabisa, na wote mlionituhumu humu na kungine kote, muwe na amani, nimekusamahe na kuwasamehe wengine wote kwa roho safi na roho nyeupe, lakini ili karma isikushughulikie na wewe kwa upande wako, baada ya kuujua ukweli huu, do the right thing, hata kimoyo moyo tu, inatosha Mungu anasikia kila kitu hata usipozungumza, ile kuwaza tuu, is enough!

Ubarikiwe sana.

Paskali.
Ukweli upi umebainika?Kwa ushahidi upi?Je imethibitishwa bila shaka yoyte kwamba kweli ana makosa au amelazimishwa kukiri ama asotee rumande?
 
Pascal, wewe ndie ulienifanya mimi nikajiunga JF na nlikuwa nakuheshimu sana. Ila natangaza tena kama nlivyowahi kutangaza hapo kabla, sikuheshimu kamwe na nlidhani kweli wewe ni mtu Bora ila hufai kutokana na mengi uliyoyaandika humu.
Hapo ndio unamfanya Pascal Mayalla aendelee kuwa bora zaidi na zaidi. Ili ukubalike sehemu yoyote, lazima wengine wakupende na wengine wakuchukie. Ndio unakuwa mkamilifu. Na uchangiaji wako unamfanya wasiomjua waanze kumjua vizuri. Nao wanaibuka wa kumpenda na wa kumchukia. Yeye tayari ana jina. Tengeneza la kwako tena uwe "verified user" kama yeye.
 
Ndugu Paskali pole sana, nakupongeza kwa kuwasamehe dhidi ya karma maana ile ya Dr.Slaa bado inawatandika. Nimalize kwa kusema pole sana kwa kuchafuliwa hadhi yako humu jamvini na vizabizabina.

aende zake uyo snitch wako, amekalia kujipendekeza tu kuusaka ukuu wa wilaya, watakupa tu hicho cheo ila huache kujipendekeza ata ukawaCOST wengine, au uliumia mwenzio kuupiga mpunga through magazeti ya wazungu, hacha hizo watu kama nyie wakati nasoma tuliwaita mandata pia wanafiki
 
Pasco katika utetezi wako huu ndio umeharibu. Mmoja wa watu walio sema kwa nguvu kuwa makala zako hazikuwa za kumharibia Kabendera ni mie, lakini wote tulijua kuwa kesi alizofunguliwa ni za kutunga hazina uhusiano na yeye maana watesi wake wamesimamia msimamo kuwa Kabendera amekuwa akiichafua nchi nje.

Kwa makala yako nikama unataka tuamini kuwa kilichomtesa sio kazi yake bali ni utakatishaji fedha ndio maana amelipa 100M na atalipa mamilioni mengine for six month.

Pasco, Kabendera kalipa 100M? Au ni mchezo unachezwa kuipa serikali advantage kuwa mashtaka yetu yalikuwa sahihi?

Wewe ni Investigative Journalist, hebu ingia chimbo utuambie hela hizo zilizolipwa kwa DPP zilikuwa zimehifadhiwa bank gani? Na zimepokelewa na kuingizwa account gani ya serikali? Fuatilia kwa wakili wake akupe risiti ( ERV) ya mapokezi ya fedha hizo. TUANZIE HAPO.

Hili shinikizo la wafadhili lingekwepeshwaje kama sio kutumia hadaa? Na Kabendera bado alikuwa anauhitaji Uhuru wake hivyo sio ajabu kukubali maelekezo ya mchezo ili akakae na mkewe!

Anyway, naweza kuwa wrong kiasi Fulani. Lakini kuachiwa kwake sio sababu ya kufuta tuhuma zako dhidi yake bali tuhuma zako juu ya yaliyompata Kabendera zilisha futika siku nyingi kwa ukweli uliouweka hadharani kwa kauli zako. Achana na vibaka waliokuwa wanaendelea kukushikia bango kwa ushabiki.

Sent using Jamii Forums mobile app
Unacholeta mezani ni dhana. Kwamba kulikuwa na shinikizo lililopelea kuachiwa
Na kwa vile labda aliachiwa kwa shinikizo basi hizo hela hazikulipwa.
That's fine, kama hiyo ni dhana yako sawa tuambiwe kwa nini unaamini hivyo na ututhibitishie. Usimpe kazi tena pasco, eti yeye ndio akatafute ukweli sijui benki, mara risiti kuthibitisha dhana yako ambayo yeye haiamini na anayo ya kwake... Kaka huo ni ufala mkubwa.
Kwa kukusaidia kidogo
Kitendo cha Kabendera kukiri kuna madhara yafuatayo;
1. Hatokata rufaa milele
2. Anatambulika kitaifa na kimataifa kama mhalifu
3. Atapoteza haki za kuajiriwa kwenye utumishi wa umma, mwandishi wa serikali mkurugenzi etc.
4. Hawezi kuteuliwa nafasi yoyote ya umma kama ubalozi, Rc, msemaji wa Rais Zitto nk
5. Hawezi kugombea nafasi yoyote ya kisiasa kama ubunge urais au udiwani.
Kumbuka adhabu yake amepewa full kwa maana ya kulipa deni la kodi 170mls na fine ya 100mls sambamba na kifungo/au fine ya 250000.
Katika kutekeleza adhabu hiyo amelipa hela badala ya kifungo, amelipa 100mls na ameahidi kumalizia 170 ndani ya siku 180.
Katika uhalisia, hii ni 'maximum sentence' kwa mtu aliye fanya plea bargain.
Kama kungekuwa na shinikizo la hao mabeberu basi kungekuwa na UAHUENI ktk adhabu na wasingeruhusu achafuliwe na apoteze haki zake kiasi hiki achilia mbali mafedha aliyotoa ambayo hata hao Armnesty International wanasikitika.
Nakushauri, wajibu wa kuthibitisha kuwa Kabendera hajalipa ni wako wewe unayeamini hivo. Sio Pasco hasa ikizingatiwa mwenyewe amekiri kalipa.
Kwa vile yuko uraiani muulizeni hela alitoa wapi, muulizeni mkewe kweli walifungua kampuni, kweli walihamisha hela.
Serikali hoi ni wapumbavu sana maana hata mkewe alipaswa akamatwe kama mshiriki mwenza katika majimbo sambamba na lile genge lote.
 
Pascal, wewe ndie ulienifanya mimi nikajiunga JF na nlikuwa nakuheshimu sana. Ila natangaza tena kama nlivyowahi kutangaza hapo kabla, sikuheshimu kamwe na nlidhani kweli wewe ni mtu Bora ila hufai kutokana na mengi uliyoyaandika humu.
Akili kama zako ni za kipumbavu kabisa..
Hvi usipomheshimu ww unafikiri atapungukiwa nini? Ww umejiunga jf umemkuta na ubora wake na ndio maana ukashawishika naye kwahyo kutokumheshimu kwako ni kazi bure maana atabaki na ubora wake tu..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom