Kuna watu bado hawajaelewa namna PUTIN alivyowachezea mchezo nchi za magharibi na kulazimisha kuwa gesi na mafuta yake yatalipiwa kwa rouble tu. Iko hivi:
Benki ambayo imekuwa ikifanyakazi kama wakala wa Urusi wa kupokea malipo kwa ajili ya gesi ya Urusi ni GAZPROMBANK. Kwa kuwa nchi za magharibi bado zinahitaji gesi na mafuta toka Urusi HAWAKUIWEKEA VIKWAZO BENKI HII. Kwa sababu hiyo hii bank haikuondolewa kwenye mfumo wa SWIFT. Kwa hiyo Urusi ikasema, nchi inayotaka kununua gesi LAZIMA ifungue akaunti mbili hapo Gazprombank. Akaunti moja ni akaunti ya rouble. Akaunti ya pili ni ya EURO au dola. Mnunuzi akija na dola au Euro itabidi aziweke kwenye akaunti yake hiyo ya pili. HALAFU kwa niaba ya mnunuzi benki ya Gazprombank itatumia hizo pesa za Euro au Dola kununua Rouble kisha kuziweka hizo rouble kwenye akaunti ya kwanza ya mteja. Hatua ya mwisho ni kuwa benki ya Gazprombank itapeleka hizo pesa zikiwa katika hali ya rouble kwa akaunt ya dealers wanaouza gesi na mafuta kwa mujibu wa mkataba. Wale dealers wakipokea hizo pesa (roubles) ndio wanaruhusu mteja apewe gesi au mafuta.
Kwa maelezo ni kama mchakato mrefu lakini kiutendaji kwa kutumia mifumo hilo ni tendo la dakika chache sana. Mwisho wa siku muuzaji wa gesi (Urusi) atapokea Rouble hata kama mteja alitoa Euro. Maajabu ya mfumo huu ni kwamba mteja hawezi kudai kuwa mkataba wa kulipa kwa euro umekiukwa kwa kuwa bado pale Gazprombank atapeleka Euro. Lakini mwisho wa siku Urusi ataingiza Rouble.
Maana yake ni kwamba thamani ya Rouble kwenye soko la fedha itapanda maana itahitajiwa sana kwa ajili ya kulipia gesi.
Hapo awali mnunuzi wa gesi au mafuta alikuwa anaweza kulipia moja kwa moja kwenye akaunti ya nje ya benki kuu ya Urusi. Kwa sasa hizo akaunti zimefungiwa. Unaweza kuingiza euro au dola lakini huruhusiwi kutoa!!! Mabeberu walitaka waendelee kulipa kwenye akaunti za Urusi zilizofungiwa!! Ndiyo maana Urusi kasema hapana.
Lakini pia urusi imewekewa vikwazo kufanya miamala kwa kutumia euro au dola. Kwa hiyo hata kama hiyo dola ukiipata huna jinsi ya kuitumia. Ndio hapo PUTIN alipochemsha bongo akaja na utaratibu wa kupokea malipo kwa Rouble hata kama mteja atalipa kwanza kwa euro au dola.
Unaweza kufuatilia mwenyewe maelezo hapa:
If they do switch, how will it work?
Putin’s order makes Gazprombank the intermediary in the gas trade.
A foreign buyer is now obliged to transfer foreign currency to one special, so-called “K”, account at the lender. Gazprombank would then buy roubles on behalf of the gas buyer to transfer roubles to another special “K” account, the order said.
Britain put Gazprombank on its list of banned entities earlier this month. It was not included in the European Union’s order excluding some Russian banks from the SWIFT messaging system.
“Potentially, the Kremlin is acting from a fear that Gazprombank will soon be sanctioned too, amid a wider bid by the European Union to cut energy ties with Russia completely,” analysts at Fitch Solutions said.