Baada ya vifo vya Said Oswayo na mkewe, Swalha Salum mali zinatakiwa kwenda katika Familia ya Mke au Mume?

Baada ya vifo vya Said Oswayo na mkewe, Swalha Salum mali zinatakiwa kwenda katika Familia ya Mke au Mume?

Mleta mada, unakuja jamiiforum kutafuta ushauri!! Sio kwamba hawapo waislamu wanaozijua sheria za mirathi. Allah a'lam!

Ushauri wangu, mtafute sheikh aliesoma, anajua haya mas'ala ya urithi wa mali, na sio wadau wa sheria.

Tafuta sheikh, usifikiri hiki kitu rahisi rahisi tu kupata jibu. Hao wanasheria wanajua nini taratibu za kiislamu!!! Tusomeni dini ndugu zangu waislamu, haya ndio madhara yake mnaangukia kwa wadau wa sheria. Haijulikani ni dini gani hao watu.
 
Mleta mada, unakuja jamiiforum kutafuta ushauri!! Sio kwamba hawapo waislamu wanaozijua sheria za mirathi. Allah a'lam!

Ushauri wangu, mtafute sheikh aliesoma, anajua haya mas'ala ya urithi wa mali, na sio wadau wa sheria.

Tafuta sheikh, usifikiri hiki kitu rahisi rahisi tu kupata jibu. Hao wanasheria wanajua nini taratibu za kiislamu!!! Tusomeni dini ndugu zangu waislamu, haya ndio madhara yake mnaangukia kwa wadau wa sheria. Haijulikani ni dini gani hao watu.
Hivi mfano ikitokea upande mmoja unataka sheria ya kiislam itumike kwenye mirathi na upande mwingine unataka sheria za kiserikali zitumike. Hapo inakuwaje?
 
Mi tangia mwanzo nilikuwa nawaza mashemeji kujazana nyumbani ndoa haina hata miezi sita, ndomana mimba haingii, itaingiaje mmejazana ndani ya nyumba ya wanandoa wapya [emoji1787]
Mimi wabongo mmenichosha[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Hivi mfano ikitokea upande mmoja unataka sheria ya kiislam itumike kwenye mirathi na upande mwingine unataka sheria za kiserikali zitumike. Hapo inakuwaje?
Mwisho wa yote katiba na sheria za nchi ndo zitaamua.Hayo mambo ya dini yatapigwa chini kesi ikifika mahakamani.Kwenye dini Kuna ubaguzi ambao unavunja katiba na sheria za nchi.Mtoto wa nje ya ndoa kwenye dini anachukuliwa kuwa haramu lakini katiba inalinda usawa na sheria ya mtoto ya 2009 inatambua watoto wote kuwa sawa na sheria za urithi zinawapa watoto wote haki ya kurithi.Mahakama ilishaliweka wazi swala hili.
 
Mleta mada, unakuja jamiiforum kutafuta ushauri!! Sio kwamba hawapo waislamu wanaozijua sheria za mirathi. Allah a'lam!

Ushauri wangu, mtafute sheikh aliesoma, anajua haya mas'ala ya urithi wa mali, na sio wadau wa sheria.

Tafuta sheikh, usifikiri hiki kitu rahisi rahisi tu kupata jibu. Hao wanasheria wanajua nini taratibu za kiislamu!!! Tusomeni dini ndugu zangu waislamu, haya ndio madhara yake mnaangukia kwa wadau wa sheria. Haijulikani ni dini gani hao watu.
Umasikini mbaya Sana unaweza ukauza mwanao wa kike kisa njaa. Ama unafurahi mwanao akiiba
 
Hivi mfano ikitokea upande mmoja unataka sheria ya kiislam itumike kwenye mirathi na upande mwingine unataka sheria za kiserikali zitumike. Hapo inakuwaje?
Sheria za serikali huwa zimeakisi dini rules I think hazitofautiani sana
 
Hivi mfano ikitokea upande mmoja unataka sheria ya kiislam itumike kwenye mirathi na upande mwingine unataka sheria za kiserikali zitumike. Hapo inakuwaje?

Ndoa ilifungwa kiserikali au kidini? Kama ilifungwa Kwa dini ya kiislam basi ni wazi taratibu za sheria za kiislam zitafuatwa. Kama Walifunga Bomani basi sheria za nchi zitafuatwa
 
Mtu unafungua uzi kabisa kujadili mali za marehemu ambao hawakuhusu!
 
Umasikini mbaya Sana unaweza ukauza mwanao wa kike kisa njaa. Ama unafurahi mwanao akiiba

Sikiliza mkuu, waliofiwa familia zao ni waislamu, Sasa, kinachokuleta humu ni nini!! Halafu unaongea viyu havina mantiki yoyote!! Sheria za mirathi huzijui, acha wenyewe walishughulikie kupitia kwa masheikh.

Wadau wa sheria/serikali, mahakamani, polisi, hapa sio mahali pao.
 
Hivi mfano ikitokea upande mmoja unataka sheria ya kiislam itumike kwenye mirathi na upande mwingine unataka sheria za kiserikali zitumike. Hapo inakuwaje?

Mkuu wenger, mimi cna elimu, ndio maana nikashauri wamuone sheikh, waachane na hao wadau wa sheria/serikali.

Au wawasiliane na masheikh wa zanzibar, kuna sheikh mmoja amesoma sana anaitwa Shaaban Albattashi. Wengi watakua humu watakua wanamjua
 
Sikiliza mkuu, waliofiwa familia zao ni waislamu, Sasa, kinachokuleta humu ni nini!! Halafu unaongea viyu havina mantiki yoyote!! Sheria za mirathi huzijui, acha wenyewe walishughulikie kupitia kwa masheikh.

Wadau wa sheria/serikali, mahakamani, polisi, hapa sio mahali pao.
Okay mkuu.
 

Tukio la Said Oswayo kumuua mkewe, Swalha Salum kisha na yeye kuuawa ikidaiwa amejiua bado ni gumzo Nchini Tanzania.

Wivu wa mapenzi ndio unatajwa na wengi kuhusu matukio hayo yaliyotokea ndani ya mwezi huu Mei 2022, lakini hoja yangu hapa siyo kuhusu walivyouawa, nina kitu tofauti kabisa.

Tayari kumeanza kelele kuhusu urithi wa mali, upande wa mwanamke inadaiwa wanaamini wao wana haki ya msingi, wakati huo ndugu wa mume nao wameanza kuonesha ishara kuwa wanataka kuwa sehemu ya mali hizo.

Marehemu walifunga ndoa Desemba 2021, ikiwa na maana kuwa ndoa yao ilikuwa na miezi mitano tu lakini mwanaume alikuwa vizuri kiuchumi na wadau wengi wa Mwanza wanaamini hicho ndicho kilichompeleka kwa mwanaume huyo, inasemekana lakini, hatuwezi kuusemea moyo wa mtu.

Inadaiwa mwanaume ana mtoto ambaye alimpata kabla hajamuoa huyo bibie.

Nimezungumza na wataalam wawili wa sheria na haya ndio yalikuwa maelezo yao:

MDAU WA KWANZA WA SHERIA:
Cha kwanza kabisa itaangalia kama marehemu aliacha wosia ambao unaweza kutaja mgawanyo wa mali zake na mengine yote.

Kama hakuna wosia, na wawili hao hawakuwa wamefanikiwa kupata mtoto, hapo mrithi halali ni mtoto wa huyo mwanaume hata kama alimpata nje ya ndoa.

Kinachotakiwa kufanyika ni kikao cha familia ambacho kitamchagua msimamii wa mirathi. Kama mtoto ana miaka chini ya 18 basi huyo msimamizi wa mirathi atatakiwa kusimamia mali za marehemu hadi mtoto atakapofikisha miaka 18.

Lakini kabla ya kufika huko msimamizi wa mali akishateuliwa na familia, anatakiwa kwenda Mahakamani kuapa, baada ya hapo ndani ya siku 14 atatakiwa kutafuta mali zote za marehemu ziwe kwenye orodha yake na zijulikane.

Nikirudi nyuma kama hivyo wawili hao hawakuwa na mtoto, kwenye urithi kawaida sheria inasema mtoto au watoto wanatakiwa kupata 80%, wazazi wa mume 10% na wazazi wa mke ni 10%

Mtoto akifikisha miaka 18 anatakiwa kwenda Mahakamani kuapa kuwa ametimiza umri huo na yuko tayari kuchukua mali kutoka kwa msimamizi na kuziendesha mwenyewe, au anaweza kuandika barua ya kutaka msimamizi aendelee kusimamia kwa muda atakaopendekeza yeye.

MDAU WA PILI WA SHERIA
Hapo baada ya taratibu za vikao vya familia na kumteua msimamizi wa mirathi, mali zote zitakuwa mali ya mtoto au watoto, kama hawana basi mali zitaenda kwa wazazi wa mwanaume.

Hiyo itafanyika kama marehemu hakuacha urithi wowote, mfano hao wanandoa (Swalha na Said) ndoa yao ilikuwa changa, hawakuwa na mtoto, hapo mwenye haki ya mali ni mtoto.

Mali ambazo walizipata ndani ya ndoa hizo wanaweza kugawana na upande wa mwanamke, mfano nimeona familia ya mwanamke inataka kung’ang’ania nyumba, ile siyo mali yao, labda kama wakati wanajenga walikuwa pamoja na nyaraka zipo wakati wa ujenzi kuwa mwanamke alishiriki.

Pia mali ambazo zitakuwa na jina la mwanamke pia zinaweza kuchukuliwa na upande wa familia ya mwanamke

HITIMISHO
Baada ya wadau hao, kuna yeyote ambaye anaona kisheria imekaaje kuhusu mali za marehemu Said? Kwani najua mgogoro mkubwa utaibuka muda si mrefu.... Mwenye uelewa atuelezee
Kifupi walifunga ndoa ya Bakwata ambayo hamrithishi mwamamke mali. Hivo pointi ya msingi ni moja tu wosia na warangi lazima wafoji ndo maana hawataki kufungua nyumba.
 
NATAKA NISEME KIDOGO.
HAPA KUNA MASUALA MENGI YA KUZINGATIA.
1, YALITOKEA MAUAJI KWANZA
KATIKA QURAN SURATUL NISAA
'Na haiwi Muumini kumuuwa Muumini ila kwa kukosea. Na mwenye kumuuwa Muumini kwa kukosea basi amkomboe mtumwa aliye Muumini, na atoe diya kuwapa jamaa za maiti, isipo kuwa waache wenyewe kuwa ni sadaka. Na akiwa ni jamaa wa maadui zenu, hali yeye ni Muumini, basi ni kumkomboa mtumwa aliye Muumini. Na akiwa ni miongoni wa watu ambao pana ahadi baina yenu na wao basi wapewe diya watu wake na akombolewe mtumwa Muumini. Na asiye pata, basi afunge miezi miwili mfululizo, kuwa ni toba kwa Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi na Mwenye hikima. (92) Na mwenye kumuuwa Muumini kwa kukusudia, basi malipo yake ni Jahannamu humo atadumu, na Mwenyezi Mungu amemkasirikia, na amemlaani, na amemuandalia adhabu kubwa.'

KWA HIVYO SAID (ALIYEFARIKI),
MOJA KATIKA ALIYOTAKIWA KUFANYA NI , ALITAKIWA KULIPA FIDIA KWA FAMILIA YA MWANAMKE KAMA ALIMUUA SIO KWA KUSUDI, ILA IKIWA FAMILIA YA MWANAMKE IMESAMEHE HAMNA NENO.

2. SAID (ALIYEFARIKI) JEE WATOTO WALIOWAZAA ALIWAZAA NJE YA NDOA , AU ALIWAPATA WAKATI AMESHAOA? IKIWA ALIWAPATA BAADA AMESHAOA WANA FUNGU LAO, IKIWA ALIWAPATA KABLA YA KUOA HAWANA KITU HAPO.

3. IKIWA KUNA WATOTO WA NDOA, MKE ATAPATA CHAKE 1/8 AMBACHO KITAKWENDA KWA FAMILIA YAKE, LA IKIWA HAKUNA WATOTO WA NDOA MKE ATAPATA CHAKE 1/4.

4. MALI ZOTE AMBAZO SAID ( ALIEFARIKI) ALIMUANDIKIA MKEWE HIZO ZOTE HAZITOINGIA KWENYE MIRATHI.
MALI AMBAZO SAID AMEACHA WASIA APEWE MKEWE, HAITOWEZEKANA KUPEWA KWA SABABU KILA MWENYE KURITHIWA HAACHIWI URITHI.
KWENYE UISLAM SHERIA ZOTE ZIMEWEKWA HAZIFUATWI SHERIA ZA TWAAHUUTW.
 
Back
Top Bottom