Baada ya vifo vya Said Oswayo na mkewe, Swalha Salum mali zinatakiwa kwenda katika Familia ya Mke au Mume?

Tanzania ya Leo ina katiba na sheria vinavyosimamia usawa wa watoto na haki zao.Ikitumika sheria ya kidini kuwanyima urithi watoto shauri likienda mahakamani watoto watapata urithi.
Mirathi ya kiislamu inatambulika kisheria labda kama familia ina mchanganyiko wa waislamu na wakristo kwa huku bara.
 
Kifupi walifunga ndoa ya Bakwata ambayo hamrithishi mwamamke mali. Hivo pointi ya msingi ni moja tu wosia na warangi lazima wafoji ndo maana hawataki kufungua nyumba.
Bakwata wanafuata sheria ya mirathi ya kiislamu ambayo wazazi, watoto wanawake na wanaume wote wanarithi kwa kutumia formula inayoeleweka.
 
Bakwata wanafuata sheria ya mirathi ya kiislamu ambayo wazazi, watoto wanawake na wanaume wote wanarithi kwa kutumia formula inayoeleweka.
mkuu niko unguja mwaka wa 20 jamaa wanaoa kila siku na kuacha na wala hawana wasi
 
mkuu niko unguja mwaka wa 20 jamaa wanaoa kila siku na kuacha na wala hawana wasi
Kupeleka kesi ya mirathi Bakwata au kwa Mali ya Wakf kwa Zanzibar inategemea wenyewe familia kwani kuna commission kubwa pale wanachukua - niliwahi kusikia zaidi ya asilimia ishirini ya thamani ya mirathi. Asilimia kubwa ya akina sisi huwa hatupendi kwenda mpaka pale iwapo lazima (hasa unapokuwa na wanafamilia watata au wengi kama vile matumbo tafauti).

Mirathi ya kiislamu ni taaluma na siyo kila sheikh anaweza kurithisha ipasavyo, pia calculations zake zinahitaji umakini kidogo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…