Baada ya walimu walio kuwa wamejificha kwenye Ofisi za Elimu Msingi, Sekondari na TSD ndani ya Halmashauri kutimuliwa sasa Idadi ya walimu Waongezeka

Baada ya walimu walio kuwa wamejificha kwenye Ofisi za Elimu Msingi, Sekondari na TSD ndani ya Halmashauri kutimuliwa sasa Idadi ya walimu Waongezeka

Hapo kwenye mkuu wa mambo ya elimu kwenye halmashauri ndo umechemka yaani PhD holder badala ya kwenda kufundisha awe desk office. Mmh
Masters elimu hawaitambui, Sasa wanataka na PhD awe mkuu wa idara.

Kwenye sekta nyingine hao PhD wamedeliva nn Cha maana?
 
Nianze kwa kumpongeza Prof Adolf Mkenda kwa kazi nzuri aliyoifanya Baada ya walimu walio kuwa wamejificha kwenye Ofisi za Elimu msingi, sekondari na TSD ndani ya Halmashauri kutimuliwa sasa Idadi ya walimu wa kufundisha madarasa ni Waongezeka .

Hii ni baada ya malalamiko mengi kuandika Jf sasa Hali imetulia na walimu wa kufundisha darasani msingi na sekondari wameongezeka na Hata serikali ikiajiri itaajiri walimu wachache .

Kazi iliyobakia ni kupunguza Idadi ya maafisaelimu waliopo imara ya Elimu msingi na sekondari ikiwa ni pamoja na kufunganisha hizo idara na kuunda idara moja ya Elimu ndani ya Halmashauri moja.

Prof Mkenda kasi unayokwenda nayo inaridhisha na Uko vizuri.

Pili muundo mpya wa Elimu mkuu wa idara aside na kiwango cha chini ya PhD Ili aweze kusimamia Elimu ipasavyo.

Kuna walimu walikuwa wamefichwa kwa afisaelimu Mkoa ambao walikuwa hawana barua Za uteuzi nao warudishwe madarasani haraka iwezekanavyo.
Rais aliposema kwamba watabadili muundo wa Elimu hukumpongeza ila Waziri anapofafanua utaratibu ndio unampongeza 😆😆😆.

Ukipenda boga ..............
 
Unajifichaje Halmashauri ofisini kufanya kazi bila kupangiwa. Hii mada ni usanii.
 
Mkuu tafadhali leta habari kamili ni nini Prof kafanya na kwa namna ipi. Habari yako umeileta kama mwendelezo hivi,si kila mmoja yuko huko kwenye masuala ya walimu?.
 
Kweli kabisa,km history,Mambo ya wangoni nk,tuachane navyo sasa
Taifa lolote ambalo watu wake hawajui historia ya Nchi yao na nchi nyingine basi ni Taifa mfu.
Taifa kama la marekani somo la historia ni lazima kama ilivyo kwa mathematics na Biology kwa hapa kwetu (O-LEVEL).

UZALENDO amabao Mh. Rais anasisitiza bila watu kujua historia ya Nchi yao ni bure.
Kiufupi historia ni maisha ya kila siku it's inevitable to escape.
 
Mkuu tafadhali leta habari kamili ni nini Prof kafanya na kwa namna ipi. Habari yako umeileta kama mwendelezo hivi,si kila mmoja yuko huko kwenye masuala ya walimu?.
Amewafukuza ofisini na kuwa Rudisha darasani, walimu wote ambao walikimbia kufundisha darasani wakiwa wajiriwa wa serikali wakaende kufanya kazi kwenye Ofisi Za maafiselimu msingi, sekondari na TSD bila kuwa na barua Za uteuzi kutoka kwa Katibu mkuu Tamisemi,
 
Duu, nimeamini adui wa walimu ni mwalimu mwenyewe.
 
Kuna jambo moja lilinishangaza sana kuhusu fedha za uviko zilizotumika kujenga madrasa. Kuna shule hazikuwa zinahitaji madarasa, walimu hawana ofisi, shule haina jengo la maabara, Kuna shule changa hazina hata vyumba viwili vya kulala walimu. Kwanini matumizi ya hizi fedha hayakuangalia mahitaji ya msingi ya shule? Siyo kila shule ilikuwa inahitaji madarasa. Mfano Kuna maeneo ya mkoa wa Kilimanjaro wanaoandikishwa darasa la la kwanza hawazidi 15. Unakuta shule ina mikondo 8 na Ina vyumba vya madarasa 12,Wana ziada ya vymba 4,halafu bado wanajenga mengine 2 au matatu.

Siasa inaathiri Sana MAENDELEO ya nchi hii.
Na kuna shule toka uhuru hazijawahi kupata darasa jipya au kufanyiwa ukarabati ukionyeshwa hizo shule unaweza sema hii sio tanzania
 
Unashangaa unajifunza eti Zao la Buni Ghana au ulimaji wa mahindi Tennessee ili inisaidie nini. Mtu unaulizwa Umri wa Juma ni mara 3 ya umri wa Sofia je miaka sita iliyopita walikua na umri gani, kwann usimuulize maswali ambayo application yake ndo hizo saundi. Kuna vitu katika elimu ni vya kutoa kabisa. Elimu ya kilimo na ufundi iwe kuanzia darasa la 5
 
Eti serikali itaajiri walimu wachache. Kwamba walimu sasa wamepatikana. Ni kichekesho. Inaonekana mleta mada hujui kwa kina tatizo la upungufu wa walimu lilivyo.

Pili, Waziri Kama ana uthubutu na anataka shule ziwe na uwiano mzuri wa walimu maeneo ya vijijini basi AHAMISHE WALIMU WALIOLUNDIKANA MAENEO YA MIJINI awapeleke vijijini. Kwa hili utaona jinsi ambavyo nchi hii haina upungufu mkubwa wa walimu, Namaanisha tatizo siyo kubwa km tunavyodhani.

Mara nyingi upungufu unaoimbwa references inayotumika Ni shule za vijijini wakati mijini unakuta mwalimu ana vipindi 6 KWA wiki Kati ya vipindi 40. Baadhi ya maeneo Vijijini walimu wana vipindi hadi 60.

Waziri aangalie suala la walimu kupangwa vijijini na baada ya muda mfupi wanahama kinyemela kwenda mijini, kwa barua zinazotoka moja kwa moja TAMISEMI. TAMISEMI imekuwa sehemu ya tatizo.

Serikali iangalie kwa kina na kuboresha mazingira ya kufundisha na kujifunza bila kusahau stahiki za walimu zilizoko kisheria.

Mimi bado naona uhitaji wa afisa elimu kuwa wawili kwasababu mtu mmoja kudili kwa mfano na shule 160 za msingi na pengine 40 za sekondari ktk halmashauri moja Ni kazi nzito tofauti na mtazamo wa watu nje ya ufahamu wa jinsi elimu inavyoendeshwa.

(Nimewahi kufundisha sekondari kwa miaka 15 saba kati ya Hiyo nikiwa Mkuu wa shule)
Kumbe hiki kinachoonekana kama upungufu wa walimu ni kwa sababu walimu wengi wamelundikana shule za mijini........serikali sasa iweke uwiano sawa wa walimu kwenye shule za mijini na vijijini ili iweze kuajiri pia watu wa kada nyingine..........maana kelele zimekuwa nyingi kwamba kuna uhaba wa walimu na kupelekea serikali kutoa ajira za walimu wakati kimsingi uhaba huo haupo, bali walimu wamelundikana kwenye shule za mijini.
 
Kurudishwa Walimu waliokuwa ofisini kwenda kufundisha mashuleni bado hakutatui Sana changamoto ya upungufu Wa Walimu.Idadi Yao ni ndogo sana ukilinganisha na idadi ya shule na upungufu Wa Walimu uliopo.Dawa ya upungufu Wa Walimu ni kuajiri Walimu wapya.Hata hivyo endapo hizo ofisi za halmashauri zina upungufu Wa maafisa elimu, watateuliwa tu Walimu Wa kujaza hizo nafasi.
 
Amewafukuza ofisini na kuwa Rudisha darasani, walimu wote ambao walikimbia kufundisha darasani wakiwa wajiriwa wa serikali wakaende kufanya kazi kwenye Ofisi Za maafiselimu msingi, sekondari na TSD bila kuwa na barua Za uteuzi kutoka kwa Katibu mkuu Tamisemi,
Hayo yote uliyopongeza wala sio waziri wa elimu ni waziri wa tamisemi

teuzi nyingi za halmashauri zinatoka tamisemi kasoro zile chache ambazo wanateuliwa na wizara husika.

kwa sasa wizara ya elimu inateua wathibiti ubora wa elimu halmashauri wengine wengi teuzi zao zinatoka tamisemi.
 
Ushauri

Hebu jaribu kusoma majukumu ya wizara ya elimu na wizara ya tamisemi,,,kwenye mada zako unachanganya haya majukumu.
 
Back
Top Bottom