Baadhi ya madereva pikipiki (bodaboda) ni wezi, chukua tahadhari

wa stendi

JF-Expert Member
Joined
Jul 7, 2016
Posts
25,190
Reaction score
27,434
Yaani wanapaki pembeni na barabara au karibu na kituo cha daladala wakipata abiria mnaelewana vizuri tuu na anakupeleka lakini akifika sehemu iliopo bar anasimama anatoa simu yake kujifanya anampigia mtu halafu anairudisha mfukoni kisha anakuambia "naomba simu yako nimcheki jamaa"hapo anataja jina la mhudumu mojawapo wa hiyo bar.

Ukimpa simu anapiga halafu anashuka kwenye boda yake anazima kabisa na ufunguo anachomoa halafu anaenda na simu yako mle ndani bar yeye anakuacha na boda yake sasa hapo ukijichanganya umfuate mle ndani yeye kumbe ameshakusoma unaingiaje yeye anatoka fasta anaenda washa pikipiki yake anapotea na simu yako wewe unabaki unaulizia lile jina alilotamka.

Nimeoana niwaambie maana jamaa yangu juzi tuu leo siku ya 3 simu yake imeondoka kwa style hiyo .

Ukipanda pikipiki jitahidi upande kwa unayemjua au kama yuko kijiweni kwake hakikisha kavaa reflector ile yenye namba ya kijiwe hata ikitokea tatizo inakuwa rahisi kulitatua.

Jumapili ikiwe njema kwenu.
 
Noted

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wengine hutumia dawa kupumbaza

Tusimlaumu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wengine hutumia dawa kupumbaza

Tusimlaumu

Sent using Jamii Forums mobile app
Basi katika mambo ambayo huwa nayapinga na kusema ni ujinga ni hili la kusema wanatumia dawa kupumbaza! Hakuna dawa ya kupumbaza. Matapeli siku zote hucheza na ubongo wako na kukufanya uamini kwa muda kile wanachokuambia ni kweli japo baadae ukija kutafakari utajiona ulikuwa mjinga kupita maelezo. Unachotwa kiakili tu na hakuna la zaidi.
 
Kama una appointment na demu, katika kukuelekeza alipo anakwambia mpe simu bodaboda
 
sijakutuma uniquote mkuu. Ligi unaipenda mwenyewe
Hua unapenda ligi za kipumbavu sana,bila shaka una stress za maisha zinakusumbua,hutaki kurekebishwa? unataka uendelee kufuga ujinga? simu yako halafu hupendi kuazima? utaazimaje kitu ambacho ni mali yako? kingine ukisha weka thd au comment hapa JF inakua sio mali yako tena na kila mtu anayo haki ya kuquote na kucomment,ukitaka mtu asikuquote acha kuandika chochote humu.
 
Gazeti lote hili povu la nini wakati sijaona sehemu nilipokukosea. ulitamani nikupe likes nyingi ama.

Mkuu stress zako pelekea Bwana ako. Daima chizi hudhani kila amuonae ni chizi mwenzie. Pole shosti
 
Poleni sana, na kwa nini umpe simu yako aitumie...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…