Baadhi ya ndugu wauza nyumba ya familia Kariakoo iliyokuwa na waqfu. Mapanga yatembea nje nje

Baadhi ya ndugu wauza nyumba ya familia Kariakoo iliyokuwa na waqfu. Mapanga yatembea nje nje

Mkinga hajui hilo
Inapaswa afahamu, kama mali inamilikiwa na warithi kwa pamoja ambapo wanachukua tu kodi kwa kugawana, ni lazima kipindi cha kuuza warithi wote wakubali kuuza, haweza akaamua mmoja kuuza kwa niaba ya wenzake bila makubaliano, huo utakuwa mgogoro mzito sana
 
Nipo Kariakoo, anaesimamia hiyo nyumba ni dd yao. Ishu ni kua anawapiga ndugu zake. Mfano frem ni 1,000,000 anawaambia wenzake kodi ni 600,000. Hiyo ndo shida
Kwa hiyo ni sawa ilivyouzwa bila hata yeye kuhusishwa?
We mtu una akili inayofanyakazi kweli?

Dhuluma ya Kodi ndo inampora mtu uhalali wa urithi?
 
Nimeona video inatrend ya ugomvi mkubwa wa nyumba ya urithi Kariakoo mtaa wa Manyema.

Nyumba hiyo ya ghorofa 5 ilijengwa na mzee anaeitwa Mohammed Alidina ambae alifariki miaka kazaa iliyopita.

Mzee huyo wakati akiwa hai alitoa sehemu ya nyumba hiyo. Floor ya juu itumike kama madrassa na kufanya taratibu za kukabidhi kwa msikiti ambazo waislamu wanaziita waqfu. Ghorofa zilizobaki aliendelea kuzitumia kuishi na zingine kupangisha appartments na fremu kwa wafanyabiashara Kariakoo.

Baada ya huyo mzee kufariki aliacha watoto 11, ambao watoto wao waligawana hizo appartments na fremu na kuendelea na maisha.

Mbeleni watoto wachache wa kiume wa marehemu mzee huyo wakapendekeza wazo la kutaka nyumba hiyo iuzwe kila mtu akajenge kwake. watoto wengine wakapinga kwamba hawataki nyumba iuzwe maana baba yao enzi za uhai alisema nyumba isiuzwe na akatoa sehemu ya nyumba iwe madrassa inayomilikiwa na waislamu wote. sasa watauzaje nyumba yenye wakfu ambayo ni mali ya waislamu wote.

Watoto wenye wazo la kuuza wakaona hapa kuuza ngumu. wakaamua kwenda kumshirikisha imamu wa msikiti ambao ulipewa wakfu sehemu ya nyumba hiyo. maana msikiti ulikuwa na documents za wakfu walizopewa na marehemu baba yao.

Kimya kimya wakashirikiana na imamu wa msikiti uliopewa hizo documents. wakatafuta mteja Mkinga mmoja wakamuuzia nyumba bila watoto wengine kujua.

Mbeleni mkinga huyo ambae ni mnunuzi aliyonunua hiyo nyumba akaenda kuchukua mali yake. Ndipo watoto wengine wakagundua nyumba imeuzwa. Ndipo ugomvi mkubwa ukaibuka na mapanga juu.



View attachment 2928225
Mkinga ameyakanyaga. Kama alienda bila utaratibu wa kisheria ana kesi kadhaa hapo za jinai zikiwemo za, Uvamizi, Kuvunja, Kuiba, Kuharibu mali, Shambulizi la maungoni na kadhalika....

Tatizo la Tannzania ni jeshi la polisi kushirikiana na wahalifu wanaosumbua jamii. Na kibaya zaidi tuna mkuu wa Jeshi la Polisi ambaye hajawahi kuwa na huruma kwa raia zaidi ya kuwalinda viongozi na kutiii amri zao hata kama ni za kindezi ndezi.

Hapo ni halali kabisa Rais kuingilia kati hili suala.
 
Nimeona video inatrend ya ugomvi mkubwa wa nyumba ya urithi Kariakoo mtaa wa Manyema.

Nyumba hiyo ya ghorofa 5 ilijengwa na mzee anaeitwa Mohammed Alidina ambae alifariki miaka kazaa iliyopita.

Mzee huyo wakati akiwa hai alitoa sehemu ya nyumba hiyo. Floor ya juu itumike kama madrassa na kufanya taratibu za kukabidhi kwa msikiti ambazo waislamu wanaziita waqfu. Ghorofa zilizobaki aliendelea kuzitumia kuishi na zingine kupangisha appartments na fremu kwa wafanyabiashara Kariakoo.

Baada ya huyo mzee kufariki aliacha watoto 11, ambao watoto wao waligawana hizo appartments na fremu na kuendelea na maisha.

Mbeleni watoto wachache wa kiume wa marehemu mzee huyo wakapendekeza wazo la kutaka nyumba hiyo iuzwe kila mtu akajenge kwake. watoto wengine wakapinga kwamba hawataki nyumba iuzwe maana baba yao enzi za uhai alisema nyumba isiuzwe na akatoa sehemu ya nyumba iwe madrassa inayomilikiwa na waislamu wote. sasa watauzaje nyumba yenye wakfu ambayo ni mali ya waislamu wote.

Watoto wenye wazo la kuuza wakaona hapa kuuza ngumu. wakaamua kwenda kumshirikisha imamu wa msikiti ambao ulipewa wakfu sehemu ya nyumba hiyo. maana msikiti ulikuwa na documents za wakfu walizopewa na marehemu baba yao.

Kimya kimya wakashirikiana na imamu wa msikiti uliopewa hizo documents. wakatafuta mteja Mkinga mmoja wakamuuzia nyumba bila watoto wengine kujua.

Mbeleni mkinga huyo ambae ni mnunuzi aliyonunua hiyo nyumba akaenda kuchukua mali yake. Ndipo watoto wengine wakagundua nyumba imeuzwa. Ndipo ugomvi mkubwa ukaibuka na mapanga juu.



View attachment 2928225
WAISIHARAMU SIKU HIZI NDIYO WAMEJIVISHA NGOZI YA UISLAMU
 
Kwani mzazi alisema isiuzwe? Kwa nini wasitumie mahakama kupata ufafanuzi wa kisheria? Hii tabia ya baadhi ya wanandugu kuuza Mali halafu wanageukiana ili kumtapeli aliyenunua lazima wanasheria waliangalie vizuri.

Mke na mume wanakubaliana kukopa hela kwa dhamana ya nyumba yao, hela zikiisha mume anamtuma mke mahakamani kudai eti nyumba imeuzwa bila ridhaa ya familia, lengo kuwaibia wakopeshaji, hata wanandugu wa kariakoo ndio mchezo wao
Hacha kupotosha watu,Mke na mume wakienda kukopa hela kupitia Nyumba ya Familia lazima wakopeshaji waje kuulizia kama kweli familia imekubaliana na maamuzia ya Mkopoaji,lazima baba na mama wapige picha nje ya Nyumba na kama anawatoto pia watapiga picha kukubaliana na ilo swala tena mbele ya nyumba na sahihi kuwekwa na vidole Gumba juu.
 
Nipo Kariakoo, anaesimamia hiyo nyumba ni dd yao. Ishu ni kua anawapiga ndugu zake. Mfano frem ni 1,000,000 anawaambia wenzake kodi ni 600,000. Hiyo ndo shida

Sasa wao wanashindwa kuwauliza wapangaji wao?! Mbona ni jambo dogo tu?!!
 
Imagine baunsa umekodishwa unalipwa elfu 30 kwa siku. Unaenda kwenye kazi unakutana na mapanga watu wanalinda mali yao.

Baunsa Unapigwa mapanga kwenye mali isiyo kuhusu
Yaani watu wanapiganua mabillion
Wewe unarisk maisha kwa ajili 30k
 
Nyumba ya mirathi ina taratibu zake kuuza.Huwezi kuuza kitu cha watu wengi,kijanja janja.Huyo Sheikh,na huyo mnunuzi wakamatwe,ni wezi hao na ni matapeli,na kama yupo wakili,kahusika na huu utapeli,pia akamatwe.
Nani awakamate,polisi ndiyo hao waliahidi usalama na baadaye kuonekana pamoja Mkinga.
 
Back
Top Bottom