Baadhi ya nyimbo za WASAFI zapigwa marufuku, Diamond ashutumiwa kutolipa kodi anapofanya kazi Kenya

hawa vijana wanatukana sana nowdays itabidi media za Tanzania zianzishe kampeni ya "tokomeza matusi kwenye nyimbo" ndo watashtuka ujinga wanaoufanya.
Vipi kuhusu nyimbo za nje au kwa vile watu wengi hawajui kiingereza?
Ushaona nyimbo ya Dj Khalid ft Chris Brown, Nick Minaj ya Do you mind?
 
Vile hatuzielewi za wakongo ndo poa coz matusi hatuyasikii
Nakumbuka kipindi tunakula tupo familia pamoja na mshua. Ikapigwa nyimbo ya Koffi Olomide. Kum@ inauma. Watu tukajifanya hatujaisikia mpaka ikaisha. Hii nyimbo ilipigwa sana enzi zile
 
Siasa imehusika pia si ajabu ukasikia kampun iliyo wapeleka wasanii wa bongo kufanya shows za mwisho wa mwaka kupelekwa mahakamani kwa kukwepa kulipa kodi.Ikumbukwe kuwa kampuni hiyo inamilikiwa na mwanasiasa hassan joh sultan.
 
kenya watoto wachanga kabisa wanaimba inama inama...balaaa tupu hili....
 
Mbona ni hoja mbili tofauti?
Kwahiyo issue ni kodi au maadili?
Mbona kama chuki ya kibaguzi tu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…