KERO Baadhi ya Wafanyabiashara Soko la Soweto na Uyole (Mbeya) wanauza Samaki walioharibika kwa makusudi

KERO Baadhi ya Wafanyabiashara Soko la Soweto na Uyole (Mbeya) wanauza Samaki walioharibika kwa makusudi

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
Kiufupi Mbeya yote imekaa kimagumashi magumashi kila kitu ni uhuni uhuni tu alafu wa kishamba..
 
Habari Wana jukwaa la JamiiForums, leo nimekuja na jambo hili linalowahusu hawa Wafanyabiashara wa Samaki katika masoko ya Soweto na Uyole jijini Mbeya.

Baadhi ya hao watu hawajali kabisa afya za watu, maana wamekuwa na utaratibu wa kuuza Samaki ambao tayari wameharibika na hawafai kwa matumizi.

Mimi ni mhanga wa hao Wafanyabiashara hasa wa Soko la Uyole maana ndiyo lipo karibu na kwangu, hivyo huduma muhimu nazipata pale.
Kuna wale Samaki Wakavu, mwanzo nilikuwa najua wale ndiyo salama kuliko Samaki wa Bichi kumbe nilikuwa najidanganya.

Kuna siku Mwanongwa wa watu nikajichanganya nikanunua Samaki aina ya Kambale ambaye amekaushwa kwa kutumia Moshi, nilivyofika nyumbani na kumuweka kwenye maji ya Moto nikaona wadudu aina ya funza wakitoka kwenye Samaki.

Kesho yake nikaenda sokoni na yule Samaki na kumuonesha muuzaji, alichonijibu ni kuwa yupo tayari kunibadilishia Samaki na siyo kurudisha fedha, nikaachana naye na kuondoka.
Baada ya muda nikaamua kufanya uchunguzi kangu kuhusu Wafanyabiashara wenye tabia kama hizo, nikampata kijana mmoja ambaye ameajiriwa kwenye duka la Samaki (Fresh food).

Huyo kijana alinisimulia jinsi ambavyo Wafanyabiashara hao wa Samaki wanavyofanya, anadai wale Samaki wabichi wakianza kuharibika baada ya kukaa muda mrefu kwenye majokofu wanaamua kuwakaanga kwenye mafuta na kuwauza.

Hivyo, wanafanya huku wakijua kabisa kwamba Samaki hao hawafai kwa matumizi ya binadamu, ila kwa kuogopa hasara wanaamua kuwauzia watu Samaki waliyoharibika.

Ukiachana na hao Samaki wa bichi, kuna hawa Samaki wa kukaushwa kwa Moshi, hawa ni vigumu sana kutambua kama wameharibika mpaka ukifanikiwa kuwaweka kwenye maji ya Moto ndiyo utaona wadudu wanavyotoka.

Wafanyabiashara wa Samaki hawa wakavu mara nyingi huwa wanachukua blashi na mafuta ya kupikia, kisha wanaanza kuwapaka Samaki hao ili waonekane wanahali nzuri lakini kumbe ni balaa.

Hivi kama kitu kimekudodea mpaka kimeharibika kuna haja gani ya kuendelea kukiuza na kupelekea kuziweka hatarini afya za watu? Si bora ukatupe tu.

Na ninyi ma bwana afya mliopo sokoni, hivi kazi yenu mnaijua kweli au ndiyo kutwa kuchukua rushwa na kushindwa kusimamia misingi ya kazi zenu.

Wafanyabiashara wa Soko la Soweto na Soko la Uyole hiyo tabia mnayoifanya ni sawa sawa na uchawi, hivi unawezaje kumlisha binadamu mwenzio kitu kilichooza na mkiambiwa mnakuwa wakali.

Serikali ifuatilieni watu wenu mliowapa dhamana ya kusimamia na kukagua maduka ya vyakula, wanashindwa kuzifanya kazi zao kwa weledi matokeo yake kutwa wanarudi na vifungashio nyumbani vimejaa rushwa za Samaki, kuku na vitu vingine vingi ili wawe kimya.

Tunakoelekea tutatoana ngeu kwa kweli maana hii sasa imezidi hata kama ni kutafuta pesa ila siyo kwa staili hii.

Mwanongwa nawakumbusha tu kuwa hii tabia siyo nzuri ipo siku mtaua binadamu wenzenu kwa kuwauzia chakula kilichooza.
Kwani ni lini Mtanzania akawa mwadilifu na mkweli?

Wanauza nyama zilizolala buchani

Wanauza mbegu fake

Wanauza Mchanga wanasema mbolea

Wanachanganya vumbi kweybidhaa ili.kuongeza uzito na upuuzi mwingine kama huo.

So na hao ni sehemu ndogo tuu ya uhuni so hakuna Cha kushangaa maana hata waliopewa jukumu la ulinzi kulinda Afya wanasubiria tamko.la Rais,twende hivyo hivyo.
 
Funza kama anatoka ndani ya Kambare poa tu,unamchanganya na Kambare unawala mbona ni protini za kutosha.Mbaya funza atoke kwenye kinyesi.
Labda samaki awe ananuka tu, ila kama hanuki nawala wote yeye na hao funza wake.
Sema ubaya tu ni kua huenda wale wapuuzi huenda wanapuliza madawa ili wasitoe harufu ambayo labda yana madhara, hiyo ndo shida.
 
Kiufupi Mbeya yote imekaa kimagumashi magumashi kila kitu ni uhuni uhuni tu alafu wa kishamba..
Hakuna sehemu isiyo na wafanyabiashara wahuni hii nchi.

Nenda Ilala, nenda karume, nenda kariakoo uone kila bidhaa inafanyiwa kanjanja labda hizi za viwandani.

Ila mbogamboga, hao samaki, matunda, nguo, viatu kote huko kuna kanjanja.
 
Kiufupi Mbeya yote imekaa kimagumashi magumashi kila kitu ni uhuni uhuni tu alafu wa kishamba..

Sehemu gani TZ hakuna magumashi? Nchi yote hii imeoza.
 
Kwani ni lini Mtanzania akawa mwadilifu na mkweli?

Wanauza nyama zilizolala buchani

Wanauza mbegu fake

Wanauza Mchanga wanasema mbolea

Wanachanganya vumbi kweybidhaa ili.kuongeza uzito na upuuzi mwingine kama huo.

So na hao ni sehemu ndogo tuu ya uhuni so hakuna Cha kushangaa maana hata waliopewa jukumu la ulinzi kulinda Afya wanasubiria tamko.la Rais,twende hivyo hivyo.
Hatari
 
Watu wameweka maslai mbele ndomana magonjwa kama saratani yamezidi kwenye jamii
 
Habari Wana jukwaa la JamiiForums, leo nimekuja na jambo hili linalowahusu hawa Wafanyabiashara wa Samaki katika masoko ya Soweto na Uyole jijini Mbeya.

Baadhi ya hao watu hawajali kabisa afya za watu, maana wamekuwa na utaratibu wa kuuza Samaki ambao tayari wameharibika na hawafai kwa matumizi.

Mimi ni mhanga wa hao Wafanyabiashara hasa wa Soko la Uyole maana ndiyo lipo karibu na kwangu, hivyo huduma muhimu nazipata pale.
Kuna wale Samaki Wakavu, mwanzo nilikuwa najua wale ndiyo salama kuliko Samaki wa Bichi kumbe nilikuwa najidanganya.

Kuna siku Mwanongwa wa watu nikajichanganya nikanunua Samaki aina ya Kambale ambaye amekaushwa kwa kutumia Moshi, nilivyofika nyumbani na kumuweka kwenye maji ya Moto nikaona wadudu aina ya funza wakitoka kwenye Samaki.

Kesho yake nikaenda sokoni na yule Samaki na kumuonesha muuzaji, alichonijibu ni kuwa yupo tayari kunibadilishia Samaki na siyo kurudisha fedha, nikaachana naye na kuondoka.
Baada ya muda nikaamua kufanya uchunguzi kangu kuhusu Wafanyabiashara wenye tabia kama hizo, nikampata kijana mmoja ambaye ameajiriwa kwenye duka la Samaki (Fresh food).

Huyo kijana alinisimulia jinsi ambavyo Wafanyabiashara hao wa Samaki wanavyofanya, anadai wale Samaki wabichi wakianza kuharibika baada ya kukaa muda mrefu kwenye majokofu wanaamua kuwakaanga kwenye mafuta na kuwauza.

Hivyo, wanafanya huku wakijua kabisa kwamba Samaki hao hawafai kwa matumizi ya binadamu, ila kwa kuogopa hasara wanaamua kuwauzia watu Samaki waliyoharibika.

Ukiachana na hao Samaki wa bichi, kuna hawa Samaki wa kukaushwa kwa Moshi, hawa ni vigumu sana kutambua kama wameharibika mpaka ukifanikiwa kuwaweka kwenye maji ya Moto ndiyo utaona wadudu wanavyotoka.

Wafanyabiashara wa Samaki hawa wakavu mara nyingi huwa wanachukua blashi na mafuta ya kupikia, kisha wanaanza kuwapaka Samaki hao ili waonekane wanahali nzuri lakini kumbe ni balaa.

Hivi kama kitu kimekudodea mpaka kimeharibika kuna haja gani ya kuendelea kukiuza na kupelekea kuziweka hatarini afya za watu? Si bora ukatupe tu.

Na ninyi ma bwana afya mliopo sokoni, hivi kazi yenu mnaijua kweli au ndiyo kutwa kuchukua rushwa na kushindwa kusimamia misingi ya kazi zenu.

Wafanyabiashara wa Soko la Soweto na Soko la Uyole hiyo tabia mnayoifanya ni sawa sawa na uchawi, hivi unawezaje kumlisha binadamu mwenzio kitu kilichooza na mkiambiwa mnakuwa wakali.

Serikali ifuatilieni watu wenu mliowapa dhamana ya kusimamia na kukagua maduka ya vyakula, wanashindwa kuzifanya kazi zao kwa weledi matokeo yake kutwa wanarudi na vifungashio nyumbani vimejaa rushwa za Samaki, kuku na vitu vingine vingi ili wawe kimya.

Tunakoelekea tutatoana ngeu kwa kweli maana hii sasa imezidi hata kama ni kutafuta pesa ila siyo kwa staili hii.

Mwanongwa nawakumbusha tu kuwa hii tabia siyo nzuri ipo siku mtaua binadamu wenzenu kwa kuwauzia chakula kilichooza.
Chukua hatua binafsi, mnyororo wa chakula hapa nchini hauna usimamizi madhubuti.
 
Back
Top Bottom