DOKEZO Baadhi ya Wahudumu wa Treni ya SGR (Dar) wanalangua tiketi kisha wanaziuza kwa bei ya juu

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Wahindi walishapewa Hilo shirika la reli wakashidwa kuliendesha
Kwao India kwenyewe shirika lao la Reli.choka mbaya
Hao hao Wahindi ndiyo wanaendesha Google, Microsoft, World Bank n.k. inategemea na wahindi. Lakinj kwenye management ni the best. Kama hakuna Wahindi wawape hata Wachina. Ila wamatumbi lazima waliue hilo shirika
 
Hao hao Wahindi ndiyo wanaendesha Google, Microsoft, World Bank n.k. inategemea na wahindi. Lakinj kwenye management ni the best. Kama hakuna Wahindi wawape hata Wachina. Ila wamatumbi lazima waliue hilo shirika
Kwenye IT wako vizuri kwenye Reli hamna kitu

Kwao Reli Yaowahindi India mahututi Hizo management skills za Reli wameokota wapi wakati Reli Yao Tu marehemu
 
Dadek! Washafanya yao.
Na hapo utakuta mbinu nyingine kama buku hivi zipo kwenye mafaili. Ni bandika, bandua.
Hiyo ndio Tanganyika halisi
 
Waajiri Wahindi ndiyo wasimamie kila kitu. Hao Waswahili ni watu wa hovyo kabisa hawawezi kuwa na maadili na mwisho wataiua kabisa hiyo huduma
Wala pilipili waliwahi pewa reli ya kati, hali ndio ikawa mbaya zaidi.
Tanganyika ni special mzee!
Wakianzisha Olympic ya Ujanja Ujanja tungeweza kuambulia hata dhahabu.
 
Hii inafanyika Duniani kote, sijui Kwa Nini walichelewa.
 
Watanzania badilikeni. Nunua tiketi yako mtandaoni kabla ya kwenda station. Mambo ya kwenda station huna tiketi unabahatisha ndio mwisho wa siku mnalialia.
Weekend hizo treni zinajaa kweli. Sasa mnaleta mazoea ya hovyo huna tiketi unaenda kichwa kichwa station kubahatisha. Anatokea mtu na tiketi yake anataka akuuzie kwa bei yake unaanza kulialia. Tuache mazoea ya Magufuli bus terminal, kata tiketi mapema uone kama utakazimishwa kuuzowa tiketi mara tatu ya bei.
 
Umeelewa alichoandika lakini?

Hata ukifika pale na cheti Cha ubatizo utaambiwa tren imekaa hivyo jiongeze Kuna abiria kaghaili kusafiri ndo unapigwa Cha juu

Hivyo vitambulisho havitasaidia lolote
Kama ni hivyo inabidi uzuiwe kuondoka hadi umtaje aliyekuuzia tiketi ili huo mchezo ubainike na wahusika uwataje wachukuliwe hatua.

Tukiendelea kununua hizo tiketi za magendo ndivyo tutakavyoendelea kuimarisha huo mtindo mchafu.

Nashauri mtego uwekwe ili hao watumishi wakamatwe na kupewa kesi ya Uhujumu uchumi.
 
Nakubaliana nawewe lkn je nani atamfunga paka kengele Ili Hali waliambiwa hadharani wale kulingana na urefu wa kamba zao?
 
Hii ndio bongo nyoso ..dar hakuna mashamba wala mazizi ya kufuga....bila ya ujanjaujanja hutoboi
 
bongo kila kitu dili.
 
Au kama majina ya kwenye ticket yanatofautiana na majina ya kwenye kitambulisho chako hakuna kusafiri, na inatakiwa ihesabike kama vile umeiba ticket ya mtu mwingine!!
 
Hawana uwezo wa kununua tiketi zote 4,000 kwa siku 2 au. 3 mfululizo. Ticket unaaweza. Kuilipia kwa Tigo pesa hapo hapo ulipo, siku ukienda ni kupanda tu..
 
Au kama majina ya kwenye ticket yanatofautiana na majina ya kwenye kitambulisho chako hakuna kusafiri, na inatakiwa ihesabike kama vile umeiba ticket ya mtu mwingine!!
Nakubaliana na hili maana kujisajili kwenye mfimo wa e ticket huwa tunaweka namba ya NIDA ambapo lazima majima yako yaonekane, so kitambulisho inabidi kiwe lazima.

Kama tunafanya check in mapema, hili linawezekana kufanyika
 
Kwa sisi flight catcher shii kawaida sana dunia nzima. Akili mukichwa mzee.

Hata mabasi, ndege, uwanja wa taifa kuangalia match nk hukosi madalali wao hawana nia ya kusafiri lakini hufanya hayo mambo.

So just get used to it. Ile sio daladala panga safari yako mapema otherwise kama una emergency kubali upigwe tu. Dunia tambara bovu no chance for the innocents.
 
Kama waliweza kuharibu mfumo wa kulipia kwa kadi wa brt na hawakufanywa chochote kwanini wasiharibu mfumo wa sgr
 
Mtoto anasafiri Kwa dhamana ya mzazi ambae tayari ana kitambukisho, sasa mtoto mdogo wa miaka 4 mpaka 6 hata bila cheti anajulikana tu ni mtoto hivyo nusu tiketi inamhusu, angalau wale wa miaka 10 au 12 hapo forgery ya umri inaweza ikawepo maana hata wa miaka 14 anaweza kujifanya ana miaka 12
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…