Baadhi ya wanaume wakimbia familia zao kutokana na hali ngumu ya maisha

Baadhi ya wanaume wakimbia familia zao kutokana na hali ngumu ya maisha

Bushmamy

JF-Expert Member
Joined
Aug 18, 2019
Posts
9,140
Reaction score
15,963
Kutokana na hali ya ukame inayoendelea nchini na hivyo kusababisha upungufu wa chakula. Kwenye baadhi ya maeneo baadhi ya wanaume wamekimbia nyumba zao na kuwaacha wanawake na watoto pekee katika familia.

Baadhi ya wanawake Wamekuwa wakijitaftia ridhiki kwa kwa kutembea umbali mrefu kuelekea maeneo ya mjini kwenda kuuza kuni, mkaa au kuomba chakula

Wanawake hao jamii ya kimaasai wamesema huondoka majumbani kwao alfajiri ya saa kumi na hutembea kwa miguu hadi saa tatu au nne za asubuhi hadi kufikia kata za mjini ambapo hupeleka kuuza mkaa na kuni na hufika nyumbani usiku wa saa tatu hadi saa nne.

Baadhi ya wanawake hao kutoka kata za mirongo na Mbuyuni mkoani Arusha wamesema kuwa wanapitia changamoto nyingi za kimaisha kutokana na Kuwa wababa wamekimbia familia zao na hivyo hupambana wenyewe kwa kila kitu.

Pia baadhi ya wanawake wa kimaasai kutoka vijiji vya olkomoro wilaya ya Siha mkoani Kilimanjaro wamesema kutokana na ukame na Kukosekana kwa Mavuno familia zimekuwa zikishindia uji na hivyo wababa wa familia kukimbia familia zao. Na hivyo watoto nao kukosa afya iliyo bora kutokana na kukosekana kwa mlo kamili
 
Watu wako buzzy kupinga ushoga, njaa na majanga ya asili sio vipaumbele vyao.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Feminists walituambia hao ni wanawake wa shoka wanachokifanya wanaume, wao watakifanya zaidi

Nilitegemea kuona Feminists wakiitangaza hiyo habari kama hamasa kwa wanawake wengine ambao bado wanasubiri mume ndio alete hela ya chakula ndani
 
Kutokana na hali ya ukame inayoendelea nchini na hivyo kusababisha upungufu wa chakula. Kwenye baadhi ya maeneo baadhi ya wanaume wamekimbia nyumba zao na kuwaacha wanawake na watoto pekee katika familia.

Baadhi ya wanawake Wamekuwa wakijitaftia ridhiki kwa kwa kutembea umbali mrefu kuelekea maeneo ya mjini kwenda kuuza kuni, mkaa au kuomba chakula

Wanawake hao jamii ya kimaasai wamesema huondoka majumbani kwao alfajiri ya saa kumi na hutembea kwa miguu hadi saa tatu au nne za asubuhi hadi kufikia kata za mjini ambapo hupeleka kuuza mkaa na kuni na hufika nyumbani usiku wa saa tatu hadi saa nne.

Baadhi ya wanawake hao kutoka sehemu za mirongo wamesema kuwa wanapitia changamoto nyingi za kimaisha kutokana na Kuwa wababa wamekimbia familia zao na hivyo hupambana wenyewe kwa kila kitu.

Pia baadhi ya wanawake wa kimaasai kutoka vijiji vya olkomoro wilaya ya Siha mkoani Kilimanjaro wamesema kutokana na ukame na Kukosekana kwa Mavuno familia zimekuwa zikishindia uji na hivyo wababa wa familia kukimbia familia zao. Na hivyo watoto nao kukosa afya iliyo bora kutokana na kukosekana kwa mlo kamili
Ah safi wacha tuwaone superwoman sasa
 
Kuna walamba 🍯 wananunua v8 tu kama mchuzi daaah

Kila mtu ana shida zake asee 😒
 
Naonaga washua Kula winga ni kama Tabia ya asili.
 
Feminists walituambia hao ni wanawake wa shoka wanachokifanya wanaume, wao watakifanya zaidi

Nilitegemea kuona Feminists wakiitangaza hiyo habari kama hamasa kwa wanawake wengine ambao bado wanasubiri mume ndio alete hela ya chakula ndani
Interesting 😅
 
Watu wako buzzy kupinga ushoga, njaa na majanga ya asili sio vipaumbele vyao.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Wazungu ni smart kichwani wao huwa wbnapambana kutafuta suluhisho la matatizo magumu kama njaa, magonjwa , climate change n.k
Sisi huku tunakomaa na ushoga halafu wala hatuna suluhisho ya matatizo yanayotukabili, . Mtu anakimbia nyumba na watoto halafu tunategemea hao watoto wawe smart .
Ushoga ni kama fupa analopewa mbwa mjinga adeal nalo wakati watu wanafanya vitu vingine kabisa vyenye impact kwa jamii!
 
Back
Top Bottom