Baba afungwa jela Maisha kwa Kubaka Wanae Wakike wawili na kumlawiti wa Kiume

Baba afungwa jela Maisha kwa Kubaka Wanae Wakike wawili na kumlawiti wa Kiume

Wakati mwingije haya mambo yanatokana na ugomvi wa mke na mume , mama anaamua kumkomoa mzazi mwenzie ..
Kwenye malezi mama zetu huwa wanatengeneza Jeshi kubwa sana linalotokama na watoto mnaozaa. Jeshi hili siku zote huwa lipo upande wa mama , ndo ile inatokea unasokesha watoto hadi wanapata kujielewa na kazi , halafu ,uzeeni unakuta watoto wanaamua kumchukua mama yao na kujengea kijumba mhini. .
Kuna uwezekano pia hao watoto kuwa wamepangwa na mama ili kumuangamiza baba yao, ilishawahi kutokea Kenya , Baba alitiwa hatiani kwa kesi ya kubaka mwanae akakaa jela kwa miaka kadhaa , binti alishikwa na roho ya huruma akaenda mahamani kuomba kuema ukweli kuwa hakuwahi kubakwa ila aliongopa ili kumkomoa baba yake kwa maelekezo ya mama yake
 
Mahakama ya Hakimu Mkazi Singida imemhukumu kifungo cha maisha mkazi wa Mtaa wa Majengo, Fabiano Dubabe kwa kosa la kuwabaka na kuwalawiti watoto wake watatu.

Dubabe, aliyekuwa akijishughulisha na kazi ya ulinzi anatuhumiwa kutenda makosa hayo kati ya mwaka 2018 na 2022 kwa nyakati tofauti.

Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo, Robert Oguda alisema Mahakama imeridhishwa bila kuacha shaka kuwa, mtuhumiwa alitenda makosa hayo kinyume na sheria ya adhabu.

Alisema ushahidi uliotolewa na upande wa mashtaka umethibitisha bila kuacha shaka kwamba, mshtakiwa ana hatia kama alivyoshitakiwa.

“Mshitakiwa, Mahakama hii inakutia hatiani kwa makosa mawili ya kubaka watoto wako wawili wa kike kwa nyakati tofauti na kila kosa utatumikia jela miaka 30.

“Lakini unatiwa hatiani kwa makosa matatu ya kumwingilia kinyume na maumbile mtoto wako wa kiume, kila kosa utatumikia jela maisha yako yote,” alisema Hakimu Oguda.

Mwanasheria wa Serikali na Mwendesha Mashitaka, Nuru Chiwalo alisema mbele ya Mahakama hiyo kuwa mshitakiwa alitenda makosa hayo kati ya mwaka 2018 na 2022.

Chiwalo alisema jumla ya mashahidi 18, akiwamo mke wa mshitakiwa kwa nyakati tofauti walitoa ushahidi dhidi ya Fabiano.

Wakati akijitetea, mshitakiwa aliomba kupunguziwa adhabu kutokana na hatia aliyokutwa nayo kwa kuwa ana familia inayomtegemea.

MWANANCHI
Ametenda makosa hayo kati ya mwaka 2018 na 2022

Ametenda makosa hayo ndani ya miaka 4.muda wote huo walikuwepo wapi kumshitaki??

Mimi nina wasiwasi sana na hayo mashitaka. Inawezekana wamemuona hamnazo wakamfanyia figisu wampoteze
 
Ni kweli inatia shaka, lakini mbona nae kajitetea kwa kuomba kupunguziwa adhabu?
Huoni kama hapo inakuwa kama amekubali kosa?
Ukishakutwa Na hatia mahakamani ukaombwa ujitetee huna namna nyingine ya kusema zaidi ya hiyo sababu tayari umeshakutwa na hatia hata usiposema hivo adhabu ipo pale pale
 
Ukishakutwa ba hatia mahakamani ukaombwa ujitetee huna namna nyingine ya kusema zaidi ya hiyo sababu tayar umeshakutwa na hatia hata usiposema hivo adhabu ipo pale pale
Kujitetea kwake ingekuwa, sijatenda kosa ila.

Hukumuni mtakavyo, kama hujatenda kosa kataa mpaka mwisho wa uhai wako
 
Ni kweli inatia shaka, lakini mbona nae kajitetea kwa kuomba kupunguziwa adhabu?
Huoni kama hapo inakuwa kama amekubali kosa?
sasa ukishatoa utetezi wako mwisho ukatiwa hatiani unadhani kinachobaki nini kama sio kuomba upungizowe adhabu ?
 
Back
Top Bottom